Hivi kwanini hununui na kusoma vitabu?

Hivi kwanini hununui na kusoma vitabu?

Uzi mzuri sana huu. Mimi napenda kusoma vitabu na pia huwa nanunua pale bajeti yangu inaporuhusu. Ila naweza kuchangia kidogo juu hii mada.

Kwanza kabisa ubongo wa mwanadamu unapenda mambo husisimua na kumfanya mtu ajisikie furaha. Mambo hayo huhifadhiwa na ubongo hukufanya uyarudie over and over. Mfano ni kufanya ngono, kutumia madawa ya kulevya, kuscroll social media n.k

Kusoma vitabu hasa nonfiction books ni kazi kama zilivyo kazi nyingine na tena huuchosha ubongo. Inahitaji commitment kuweza kufanya hii kazi. Sababu kubwa ni kwamba tunapenda kuwa kwenye comfort zone that's why unaweza kuscroll newsfeed hata saa nzima but unashindwa kusoma kitabu cha financial management kwa nusu saa.
Nadhani sababu kubwa ni hiyo, then chini yake zitafuata uvivu, kuwa busy n.k
 
Kusoma vitabu ni hobby kama zilivyo hobbies nyingine tu. Binafsi sikuwaga na hiyo hobby kabisa nlikua kila kitabu nnachosoma naishia katikati

Ugonjwa wangu mkubwa ulikua ni movie, nlikua natumia muda mwingi kwenye movies na ukizingatia mi sio mshabiki wa mpira

Huu uraibu wa kusoma vitabu ulianza mwaka juzi tu na hii ni baada ya kukutana na kitabu cha jamaa mmoja anaitwa James Clear (Atomic Habits), hiki ndo kitabu cha kwanza kufanikiwa kukimaliza chote bila kuishia katikati, kilikua na pages 680+

Hiki kitabu kwa kiasi flani kilianza kubadilisha lifestyle yangu, baada ya hapo nikaanza kutafuta vitabu vingine... nasoma vitabu vya aina zote...fiction na non fiction, kwa mwaka jana pekee nimefanikiwa kumaliza vitabu 7

Niko selective kwenye kuchagua vitabu vya kusoma maranyingi huwa naangilia vile ambavyo vimekua recommended na watu wengi kwenye magroup ya wanaopenda kusoma vitabu hata humu jf kuna nyuzi kibao za vitabu

Vitabu vyote huwa nadownload kutoka torrent sites kwa format ya .epub afu navitumia kwa app ya Media365 sijawahi nunua hardcopies

Kuhusu muda wa kuvisoma hii kwangu ni rahisi ukizingatia natumia simu so naweza ku visomea popote pale, wakati mwingine hata niko kwenye foleni ndani ya bank nimeboreka nafungua tu app napitia hata page 10 fasta, huwa natenga dakika 20 - 30 asubuhi na jioni karibu kila siku nasoma page za kutosha, siku hizi ule muda wa kuchek movies nimeuhamishia kwenye vitabu

Nimekuja kugundua vitabu vina fantasy flani kama movies tena naweza kusema kwangu imekua zaidi ya movie kwasabu na-enjoy na pia naongeza maarifa ya kutosha, Vitabu vinatoa maarifa in detail. Hata kingereza changu cha kuandika naona kabisa kime improve, siku hizi zile memo za kiofisi naziandika kiufundi sana naona mpaka boss wangu ame notice hii kitu ameniambia

Hapa kilichobaki ni kuwa develop tu wanangu na hii tabia ya kupenda kujisomea najua watajifunza mengi sana
Kuna kitabu kimoja cha huyu mwamba anaitwa Mark Manson - The Subtle Art Of Not Giving A Fu*k natamani kama kila mtu angekisoma ili tuishi kwa kuheshimiana
Kusoma vitabu kunaweza kukuketea uraibu pia. Unasoma hiki unamaliza, unashika kingine ila ukiangalia hakuna hatua uliyopiga zaidi ya kujiaminisha kwamba umebadilika. Tunaita illusion of progress. Kimawazo unaona umetoboa ila kiuhalisia kuna bills kama zote za kulipa.
Hiyo haimaanishi kwamba tusisome, la, kikubwa ni kusoma na kufanyia kazi yale unayosoma.
Kwa mfano hicho kitabu cha Atomic habits ni kizuri sana. Baada ya kukisoma inabidi ujifanyie assessment je, umeweza kubreak zile bad habits kwa kiasi gani?
 
make money boss, achana na vitabu unapoteza muda.

mimi muda unaosoma kitabu mimi natengeneza hela
 
Kusoma vitabu kunaweza kukuketea uraibu pia. Unasoma hiki unamaliza, unashika kingine ila ukiangalia hakuna hatua uliyopiga zaidi ya kujiaminisha kwamba umebadilika. Tunaita illusion of progress. Kimawazo unaona umetoboa ila kiuhalisia kuna bills kama zote za kulipa.
Hiyo haimaanishi kwamba tusisome, la, kikubwa ni kusoma na kufanyia kazi yale unayosoma.
Kwa mfano hicho kitabu cha Atomic habits ni kizuri sana. Baada ya kukisoma inabidi ujifanyie assessment je, umeweza kubreak zile bad habits kwa kiasi gani?
Uko sahihi mkuu, kusoma ni jambo moja na ku impliment ni jambo jingine ila mi kuna habit moja nilishajiapiza lazima niifanyie kazi na nimefatisha methodology ya kwenye hicho kitabu ni ngumu lakini ile habit cheat sheet imenirahisishia kiasi chake
 
Halafu wengi ni choka mbaya, watu wa fantasies. Yaan nitoke kibaruan nmechoka nisilale nisome kitabu? Vitabu nilivyosoma toka darasa la kwanza mpaka namaliza chuo kikuu miaka mi4 vinatosha sana kwa maarifa.
Shida inaanzia hapa. Mnadanganywa na Motivesheni Spikaz kuwa ujisoma vitabu sijui mia kwa mwaka unakuwa tajiri. Ni ujinga huo. Kazi ya vitabu ni kushirikishana ujuzi na maarifa. Unaweza kusoma vitabu kujifunza namna ya kupika, njia za kupata wateja katika biashara, namna ya kuwa na huduma bora kwa wateja, malezi ya watoto, mada mbali mbali za imani, mambo ya kisayansi, Teknolojia, au burudani.

Acha kusoma na kusikiliza mambo ya motivesheni spikaz. Soma vitabu vitakavyokuongezea maarifa sio kukujaza ujinga na kujiona tajiri wakati umetia viraka na umesaga soli...
 
Kwanini ninunue wakati online unaweza kuvipata bure?
Ili kuwawezesha waandishi waweze kuandika zaidi. Kuandika kitabu ni kazi ngumu na ina gharama. Kama unampenda mwandishi basi mtie joto kwa kununua kazi yake!
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Salaam,

Tunaendelea kutatua changamoto na kutoa elimu kwa umma katika nyanja mbalimbali.

Uzi huu tutautumia kujua sababu za watu kutosoma vitabu hasa hapa nchini Tanzania. Lazima kuna shida mahali!

Wataalamu wameshaeleza na kuthibitisha kuwa usomaji wa vitabu husaidia kunoa ubongo, kubadilisha tabia za mtu/jamii, kumsaidia kudhibiti mazingira, biashara na faida nyingine lukuki ikiwemo burudani na kusafiri kimawazo, kihisia na kujifunza.

Pia mtu anayesoma na asiyesoma vitabu utofauti wao mkubwa upo kwenye namna ya kufikiri na kutatua changamoto.

Labda tukuulize wewe ambaye huna utaratibu wa kujisomea vitabu; Kwanini hununui kitabu na kusoma? Je, hupendi au basi tu? Nini kifanyike upate ari ya kusoma vitabu?

Funguka, tuzungumze.
Binafsi situmii pombe, sivuti sigara, ugoro, mpira, betting. Siyo mtu wa outing sana.

Kwasasa at 31, nilitaka nitafute hobby mpya, nikaona ni vitabu lakini kununua lundo la hardcopy nianze kusoma imekuwa ngumu.

Hata Book clubs au Maktaba za maana kwaajili ya kusoma hakuna.

Kwahiyo bado ni Dilemma.
 
Binafsi situmii pombe, sivuti sigara, ugoro, mpira, betting. Siyo mtu wa outing sana.

Kwasasa at 31, nilitaka nitafute hobby mpya, nikaona ni vitabu lakini kununua lundo la hardcopy nianze kusoma imekuwa ngumu.

Hata Book clubs au Maktaba za maana kwaajili ya kusoma hakuna.

Kwahiyo bado ni Dilemma.
Wee utakuwa mgegedaji papuchi
 
Binafsi situmii pombe, sivuti sigara, ugoro, mpira, betting. Siyo mtu wa outing sana.

Kwasasa at 31, nilitaka nitafute hobby mpya, nikaona ni vitabu lakini kununua lundo la hardcopy nianze kusoma imekuwa ngumu.

Hata Book clubs au Maktaba za maana kwaajili ya kusoma hakuna.

Kwahiyo bado ni Dilemma.
Wee utakuwa mgegedaji papuchi
 
Halafu wengi ni choka mbaya, watu wa fantasies. Yaan nitoke kibaruan nmechoka nisilale nisome kitabu? Vitabu nilivyosoma toka darasa la kwanza mpaka namaliza chuo kikuu miaka mi4 vinatosha sana kwa maarifa.
Wewe utakuwa umesoma sana ila hujaelimika, hakuna msomi aliyeelimika akasema eti vitabu alivyosoma vinatosha huku akijua kuwa kila siku mambo mapya huzaliwa na mawazo mbadala huibuliwa kutoka sehemu mbalimbali za ulimwengu. Bora ungesema huna hobby ya kusoma vitabu hivyo unajifunza kwa njia nyingine.
 
Salaam,

Tunaendelea kutatua changamoto na kutoa elimu kwa umma katika nyanja mbalimbali.

Uzi huu tutautumia kujua sababu za watu kutosoma vitabu hasa hapa nchini Tanzania. Lazima kuna shida mahali!

Wataalamu wameshaeleza na kuthibitisha kuwa usomaji wa vitabu husaidia kunoa ubongo, kubadilisha tabia za mtu/jamii, kumsaidia kudhibiti mazingira, biashara na faida nyingine lukuki ikiwemo burudani na kusafiri kimawazo, kihisia na kujifunza.

Pia mtu anayesoma na asiyesoma vitabu utofauti wao mkubwa upo kwenye namna ya kufikiri na kutatua changamoto.

Labda tukuulize wewe ambaye huna utaratibu wa kujisomea vitabu; Kwanini hununui kitabu na kusoma? Je, hupendi au basi tu? Nini kifanyike upate ari ya kusoma vitabu?

Funguka, tuzungumze.
Vitabu nilivyosoma kwa zaidi ya miaka 20 sijaona misaada wowote kwenye kupata hela, tena bado nihangaike na mavitabu tu jamani niacheni mimi
 
Nasoma kitabu kimoja kila week iwe hard copy Au soft copy. Kitabu kikiwa kizuri sana naweza soma hata masaa 10 non stop. Kupitia vitabu thamani yangu imeongezeka, vitabu vimenifanya kukubalika kupitia mawazo yangu kubadilika.
 
Back
Top Bottom