Hivi kwanini hununui na kusoma vitabu?

Kusoma vitabu ni hobby kama zilivyo hobbies nyingine tu. Binafsi sikuwaga na hiyo hobby kabisa nlikua kila kitabu nnachosoma naishia katikati

Ugonjwa wangu mkubwa ulikua ni movie, nlikua natumia muda mwingi kwenye movies na ukizingatia mi sio mshabiki wa mpira

Huu uraibu wa kusoma vitabu ulianza mwaka juzi tu na hii ni baada ya kukutana na kitabu cha jamaa mmoja anaitwa James Clear (Atomic Habits), hiki ndo kitabu cha kwanza kufanikiwa kukimaliza chote bila kuishia katikati, kilikua na pages 680+

Hiki kitabu kwa kiasi flani kilianza kubadilisha lifestyle yangu, baada ya hapo nikaanza kutafuta vitabu vingine... nasoma vitabu vya aina zote...fiction na non fiction, kwa mwaka jana pekee nimefanikiwa kumaliza vitabu 7

Niko selective kwenye kuchagua vitabu vya kusoma maranyingi huwa naangilia vile ambavyo vimekua recommended na watu wengi kwenye magroup ya wanaopenda kusoma vitabu hata humu jf kuna nyuzi kibao za vitabu

Vitabu vyote huwa nadownload kutoka torrent sites kwa format ya .epub afu navitumia kwa app ya Media365 sijawahi nunua hardcopies

Kuhusu muda wa kuvisoma hii kwangu ni rahisi ukizingatia natumia simu so naweza ku visomea popote pale, wakati mwingine hata niko kwenye foleni ndani ya bank nimeboreka nafungua tu app napitia hata page 10 fasta, huwa natenga dakika 20 - 30 asubuhi na jioni karibu kila siku nasoma page za kutosha, siku hizi ule muda wa kuchek movies nimeuhamishia kwenye vitabu

Nimekuja kugundua vitabu vina fantasy flani kama movies tena naweza kusema kwangu imekua zaidi ya movie kwasabu na-enjoy na pia naongeza maarifa ya kutosha, Vitabu vinatoa maarifa in detail. Hata kingereza changu cha kuandika naona kabisa kime improve, siku hizi zile memo za kiofisi naziandika kiufundi sana naona mpaka boss wangu ame notice hii kitu ameniambia

Hapa kilichobaki ni kuwa develop tu wanangu na hii tabia ya kupenda kujisomea najua watajifunza mengi sana
Kuna kitabu kimoja cha huyu mwamba anaitwa Mark Manson - The Subtle Art Of Not Giving A Fu*k natamani kama kila mtu angekisoma ili tuishi kwa kuheshimiana
Useful comment. Barikiwa sana
 
Ila wanaosoma vitabu wanajionaga wameyapatia kinoma maisha.Wengi wanaosoma citabu hawana mahangaiko ya kiamaisha hivi Nikisoma napata nn culture za wazungu hawana socilization ndo maana wanasoma mm Niko muda wote na watu vitabu vya nn
 
Salaam,

Tunaendelea kutatua changamoto na kutoa elimu kwa umma katika nyanja mbalimbali.

Uzi huu tutautumia kujua sababu za watu kutosoma vitabu hasa hapa nchini Tanzania. Lazima kuna shida mahali!

Wataalamu wameshaeleza na kuthibitisha kuwa usomaji wa vitabu husaidia kunoa ubongo, kubadilisha tabia za mtu/jamii, kumsaidia kudhibiti mazingira, biashara na faida nyingine lukuki ikiwemo burudani na kusafiri kimawazo, kihisia na kujifunza.

Pia mtu anayesoma na asiyesoma vitabu utofauti wao mkubwa upo kwenye namna ya kufikiri na kutatua changamoto.

Labda tukuulize wewe ambaye huna utaratibu wa kujisomea vitabu; Kwanini hununui kitabu na kusoma? Je, hupendi au basi tu? Nini kifanyike upate ari ya kusoma vitabu?

Funguka, tuzungumze.
Binafsi huw napenda sana kusoma maandishi mengi tofauti, ila kwa kweli waandishi wengi wa zama hizi hawana sifa za kuwa bora, wanakosa vitu vingi muhimu ambavyo mwandishi bora anatakiwa kuwa navyo:-
1. Wanakosa ule ufundi wa kuwasilisha kazi zao kwa janmii(sanaa), waandishi wengi hawana utamu kwenye maandishi yao, anaelezea kisa fulani hakina utamu, kipo wazi, yaani hadi mtu anachoka kusoma.
2. Lakini pia wanakosa kuwa na uwezo wa kufanya tafiti ili kugundua jamii inahitaji nini kwa wakati gani, .n.k n.k.

Kwa maana hiyo basi, baadhi ya waandishi ni sababu ya watu kutopenda kusoma vitabu
 
Binafsi huw napenda sana kusoma maandishi mengi tofauti, ila kwa kweli waandishi wengi wa zama hizi hawana sifa za kuwa bora, wanakosa vitu vingi muhimu ambavyo mwandishi bora anatakiwa kuwa navyo:-
1. Wanakosa ule ufundi wa kuwasilisha kazi zao kwa janmii(sanaa), waandishi wengi hawana utamu kwenye maandishi yao, anaelezea kisa fulani hakina utamu, kipo wazi, yaani hadi mtu anachoka kusoma.
2. Lakini pia wanakosa kuwa na uwezo wa kufanya tafiti ili kugundua jamii inahitaji nini kwa wakati gani, .n.k n.k.

Kwa maana hiyo basi, baadhi ya waandishi ni sababu ya watu kutopenda kusoma vitabu
Asante sana kwa maoni yako mazuri. Tunayachuku na kuwafikishia walengwa. Tafadhali pata nakala ya kitabu cha LOVE BOMBS, mtunzi ni Mzee Mabala, kina mvuto, kina maudhui mazuri, ni maisha ya kila siku tunayoishi. Utapata kitu cha kujifunza.
 
Hukukuzwa hivyo. Sababu nzuri na ina mashiko.

Kwahiyo unaamini mtoto akikuzwa na tabia ya kusoma vitabu atadumu nayo, siyo?

Na wewe ambaye angalau unanunua mara moja moja, unadhani unahitaji kusaidiwaje ili upate ari ya kusoma?

Namna unavojibu katika comments ni dhahiri ww ni msoma vitabu. Hata kama usingesema unasoma lakini mtiririko wa mawazo yako katika maandishu unaonesha hivo.

Me napenda kusoma vitabu. Nina magroup mawili whatsapp ya kutumiana vitabu. So nna soft copy ya kila kitabu. Zaid ya vitabu 400 ninavyo soft copy.

Lakini sijawahi maliza kitabu kusoma.. nmewahi fika nusu ya pages vitabu viwili tuu ‘who will cry when you die’ na 48 laws of life nadhan.

Vitabu vingi nmesoma soma ila 2-10 pages

Naingiwa na uvivu sijui shida nini. Nkajipa reason huenda nasoma softcopy. Nkatafuta hard copy kimoja yale yale. Nkaanza labda kusoma bible nimalize nikasoma mwanzo, kutoka, nkarukia mathayo nusu nkaacha.

So napenda vitabu ila siviwezi.

Sababu kubwa ya mie kupenda nisome vitabu natamani niwe fluent katika lugha.
 
Namna unavojibu katika comments ni dhahiri ww ni msoma vitabu. Hata kama usingesema unasoma lakini mtiririko wa mawazo yako katika maandishu unaonesha hivo.

Me napenda kusoma vitabu. Nina magroup mawili whatsapp ya kutumiana vitabu. So nna soft copy ya kila kitabu. Zaid ya vitabu 400 ninavyo soft copy.

Lakini sijawahi maliza kitabu kusoma.. nmewahi fika nusu ya pages vitabu viwili tuu ‘who will cry when you die’ na 48 laws of life nadhan.

Vitabu vingi nmesoma soma ila 2-10 pages

Naingiwa na uvivu sijui shida nini. Nkajipa reason huenda nasoma softcopy. Nkatafuta hard copy kimoja yale yale. Nkaanza labda kusoma bible nimalize nikasoma mwanzo, kutoka, nkarukia mathayo nusu nkaacha.

So napenda vitabu ila siviwezi.

Sababu kubwa ya mie kupenda nisome vitabu natamani niwe fluent katika lugha.
Kiongozi inaonekana una hazina kubwa ya maandishi, hongera sana kwa hilo.

OMBI LANGU: Naomba untumie nami hvyo vitabu ulivyo navyo kwenye soft copy, naamini ombi langu utalizingatia.
Shukrani.
 
NIANZE KWA KUMNUKUU DENIS MPAGAZE..

kwenye makala yaje AKILI YAKO HAIPIMWI KWA KIWANGO CHA ELIMU YAKO

"Elimu yetu imegandamizwa na kitu kinachoitwa CHETI na hii hupelekea wasomi wetu wakishahitimu na kuajiliwa huwa hawanaga kawaida ya kujisomea kwani huko kujisomea hakutawasaidia chochote kwa kuwa hamna mwenye kuwapatia cheti". mfano wa maneno yake.

Binafsi nikiri kuwa sababu kubwa ni misingi toka mashuleni kwetu na hilo hutupeleka hadi tuingiapo mtaani nikumbushe kidogo enzi zile za vijarida kama Bongo, Tabasamu n.k nakumbuka kipindi niko primary na kijijini lakini wazee wetu kila warudi mjini kwenye mshahara walikua wananunua na hiyo ilipelekea tukawa ni wadau sana wa hayo majarida ila tulipoanza kukua na yale majarida kupigwa stop ikawa tunajaribu kutafuta badari kwenye riwaya huku ikawa ni changamoto zikawa nyingi kutokana na aina ya waandishi unajikuta unapitia vitabu vi5 viwili vikawa safi na vitatu utopolo Ikumbukwe umetumia mkwanja ila ahueni ilikuja kwa mara ya kwanza napata kitabu cha Machozi na Damu na Rais anampenda mke wangu za Shigongo (wa enzi zile acha siku hizi riwaya zake page 10 hautamani kuendelea wabongo tunaishi ki BIG G)
Kuanzia pale kidooogo nikajua kuna vitu vikali kwenye Riwaya zaidi ya vile vijarida.
Changamoto ikaja ikawa ni kujaribu kufatilia waandishi wengine huko ikawa kama tunabahatisha unakuta kimoja kipo poa viwili hamna kitu.
Kwa sasa Ahueni naipata hapa JF kwa huyu jamaa HABIB ANGA kiukweli makala zake unasoma 6 itakuboa 1 kwangu ndo namuelewa na wapo wengine humu ndani ila kwa series ya story kali huyu kwangu namheshimu ijapokuwa sina kitabu chake hata nakala moja na hii ni kutokana na promo zake au uzalishaji wake nahisi utakuwa ni mdogo
wakipatikana kama hawa wakawa wengi naamini kizazi cha akina Shigongo wa zamani kitakuwa kimeboreka Zaid ya kile
 
Kuna app ya kupakua vitabu vya kiswahili maana niadimu kupitiliza
Jaribu hii hapa.

 
Mimi nasomaga BIBLIA tu,
hizo hadithi za akina Eric shigongo,
Wamesha paya umaarufu, WAKO KWENYE VIYOYOZI SAIZI.
Wewe wana baki wana kutia moyo kama akina MITIMINGI

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
 
Namna unavojibu katika comments ni dhahiri ww ni msoma vitabu. Hata kama usingesema unasoma lakini mtiririko wa mawazo yako katika maandishu unaonesha hivo.

Me napenda kusoma vitabu. Nina magroup mawili whatsapp ya kutumiana vitabu. So nna soft copy ya kila kitabu. Zaid ya vitabu 400 ninavyo soft copy.

Lakini sijawahi maliza kitabu kusoma.. nmewahi fika nusu ya pages vitabu viwili tuu ‘who will cry when you die’ na 48 laws of life nadhan.

Vitabu vingi nmesoma soma ila 2-10 pages

Naingiwa na uvivu sijui shida nini. Nkajipa reason huenda nasoma softcopy. Nkatafuta hard copy kimoja yale yale. Nkaanza labda kusoma bible nimalize nikasoma mwanzo, kutoka, nkarukia mathayo nusu nkaacha.

So napenda vitabu ila siviwezi.

Sababu kubwa ya mie kupenda nisome vitabu natamani niwe fluent katika lugha.

Pole sana mkuu. Naweza kukupa mbinu za kusoma kitabu ukamaliza, nitakuwekea utaratibu, kama utaweza kuufuata basi, utasoma vitabu bila kuruka kurasa. Njoo inbox.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom