Hivi kuna ubalozi hata mmoja umeanza kujenga ofisi za ubalozi Dodoma?

Tangu serikali itangaze kuhamia Dodoma na baadae kuwagawaia bure viwanja mabozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini,kuna nchi hata moja imeonyesha ni ya kujenga ubalozi kue mkoani Dodoma?

Ni kweli kila nchi ina taratibu zake za kutekeleza jambo kama hili, ila kwa muda wote huu, nilitarajia kusikia kuna nchi wala mbili au tatu zimeanza kuonyesha dalili za kujenga ubalozi mkoani Dodoma ila pale katika Mji wa Serikali sioni dalili ya ubalozi unaojengwa.

Kwa ukimya huu,inawezekana hizi nchi haziko tayari kuhamia Dodoma ikiwemo hata kufungua ubalozi ndogo kama walivyofanya China na Ujerumani.

Baada ya Mheshimiwa kutangaza kuhamia rasimi Dodoma,labda tutaona mabadiliko/jitihada za balozi hizi nazp kuhamia Dodoma.

Serikali inatakiwa kufanya mengi ya kushawishi nchi hizi kujenga balozi zao ikiwemo kujenga na kuboresha miundombinu katika eneo husika pamoja na huduma nyingine za kijamii kama vile mahospitali ya kisasa,iweke mazingira ya kushawishi na kuvutia watu kujenga shule za kimataifa,n.k vinginevyo itachukua zaidi ya miaka 10 hili jambo kutimia.
Salary Slip kuna mambo ambayo huyajui. Uwe unaulizaGA!
Kigogo 2014 anaemaje kwani
Kama kuna kitu nyumbus hawataki kusikia ni jina la KIGOGO2014!
 
Come please
Asante ila nisikusumbue nauliza hapahapa, samahani niliambiwa eti kujenga Ihumwa ni lazima uwe na building permit ambayo nasikia ni kazi sana kuipata, ni kweli mkuu? Namimi Nina plot huko next year nitaanza ujenzi, asante sana
 
Hizi nyumba zifikishwe na hiyo meli Dodoma port pale ndiyo zitawahi kuwasili kuliko kupitia Dar port.
 
Asante ila nisikusumbue nauliza hapahapa, samahani niliambiwa eti kujenga Ihumwa ni lazima uwe na building permit ambayo nasikia ni kazi sana kuipata, ni kweli mkuu? Namimi Nina plot huko next year nitaanza ujenzi, asante sana

Kwa mujibu wa taratibu Za miji yetu ujenzi unahitaji vibali,lakini Kwa Dodoma ni rahisi kuliko Dar lakini unaweza kuanza uku ukishughulikia kibali
 
Uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma huenda ukasaidia kuifanya Dar ipumue kidogo walau maana imejaa almost!
Kila siku maingizo mapya yanaingia Dar imagine msongamano wa watu unaweza kuwa mkubwa zaidi kiasi gani?!

Vinginevyo Kuwe na mikakati mingine ya kukuza miji mingine ili kulifanya juju la Dar kupumua

Ni mtazamo tu
 
Usiwe na haraka. Hata wizara za serikali bado hazikalamilisha ujenzi wa majengo yao pale mji wa serikali. Miundombinu hususani za lami bado pia hazijakamilika. Haya si masuala ya kukamilika ndani ya muda mfupi, tuwe na subira. Ni suala la muda tu balozi nyingi zitafungua makao yake makuu Dodoma. Kumbuka kwa sasa Dom hata international airport bado haina.
Si mlisema december 2018 mtakua mmehamia Dodoma? Kwanini bado hamtaki kuacha mkoa wetu?
 
Kwa ukimya huu,inawezekana hizi nchi haziko tayari kuhamia Dodoma ikiwemo hata kufungua ubalozi ndogo kama walivyofanya China na Ujerumani.
Hujui kitu
Kama nchi ina ubalozi kamili,lazima ofisi iwepo kwenye .mji wa makao makuu ya serikali
Ni suala la muda tu,watajenga wengine hawakua na bajeti hiyo,na nchi zingine hazipo vizuri kifedha
 
Kwa mujibu wa taratibu Za miji yetu ujenzi unahitaji vibali,lakini Kwa Dodoma ni rahisi kuliko Dar lakini unaweza kuanza uku ukishughulikia kibali
SAWA NASHUKURU SANA, NGOJA NIPATE HATI KWANZA MAANA TULIONUNUA KUTOKA MANISPAA MPAKA UPATE HATI NDIO UNARUHUSIWA KUJENGA, ASANTE SANA
 
Mbona serikali ishahamia huko ila foleni haipungui
Uamuzi wa Serikali kuhamia Dodoma huenda ukasaidia kuifanya Dar ipumue kidogo walau maana imejaa almost!
Kila siku maingizo mapya yanaingia Dar imagine msongamano wa watu unaweza kuwa mkubwa zaidi kiasi gani?!

Vinginevyo Kuwe na mikakati mingine ya kukuza miji mingine ili kulifanya juju la Dar kupumua

Ni mtazamo tu
 
Mbona serikali ishahamia huko ila foleni haipungui

Inaonekana kana kwamba haijapungua kwakuwa msongamano ulikuwa mkubwa sana kiasi kwamba hata badiliko dogo la serikali kuhamia Dodoma linakuwa halipelekei kule kupungua kwa foleni kuweza kuonekana moja kwa moja!

Nazani itakuwa imepungua lakini kwa kiasi kidogo sana !

Na mambo ya kuboresha ili kupunguza msongamano ni pamoja na kuboresha miundombinu kwa kuongeza ukubwa wa barabara mfano kutoka double road kwenda Tripple road , kuongeza barabara za pembezoni/mitaani kutengenezwa na kutumika, Halmashauri ya Jiji kuacha kutoa vibali vya ujenzi maeneo ya mijini na barabara kuu, miji ya mikoa mingine kuendelezwa kimkakati n.k
 
Twende Dodoma,
Dodoma haina mvuto,ilitakiwa tu kujenga mji mdogo wa shughuli za Bunge.
Hadi leo hawajui wanataka Didoma iwe nini?
Ila wakiweza kuweka miundo mbinu ya kisasa kuunganisha Dodoma na mikoa mingine barabara ,reli,na anga harafu wakaweza kutatua swala la maji,wakapanda miti yenye kivuli kwa wingi yenye uwezo wa kukinga vumbi.Labda baada ya miaka 20 kutokea sasa inaweza ikapata hadhi ya kuitwa mji mkuu.Lakini akija Raisi mwenye msimamo tofauti,Dodoma itabakia center ya shughuli za madini tu kama ilivyokuwa huko nyuma.
 
Back
Top Bottom