Hivi, jirani kwanini hununui gari?

Hivi, jirani kwanini hununui gari?

Acha umasikini Jeuri kupewa wazo unajifanya umesahau simu
Na hiyo ofisi yenu wote mnamtegemea huyo jamaa mmoja hata aibu hamuoni?
Umepewa ushauri tu ulipaswa kuutumia
 
wako watu wanadai gari sio muhimu bora kujenga nyumba, ukiwa unakaa nyumba ya kupanga ukanunua gari wanakuona mwehu tu, sasa mvua ikinyesha unapandisha vioo hadi juu , walewale walio kucheka wananuna na kukuona una roho mbaya , si wapande nyumba zao sasa.
 
sasa kwanini hununui gari? hadi amesema ina maana anakuona una uwezo. sasa kwanini hununui gari?
 
'Kupanga ni kuchagua' ila unapotimiza slogan hii hakikisha usije ukamkwaza mwenzio maana unaweza ukaamua kuchagua B ili A akutimizie mwenzio hilo ni kosa la wabongo!!!!
Halafu raha ya lift uombe siku moja kisha mwenye gari ndo atambu uhitaji wako! maana kama ulishaomba mara moja ilibidi yeye ndo awe anakustua.. kwa hiyo wakati mwingine ungekuwa hautokei sehemu aliyokuwa anakupa lift then kama alikuwa anapenda kukupa lift lazima angekupigia simu kukuuliza 'upo wapi jirani twende bwana'
 
Labda ulikuwa unamchafulia, unaingia na matope au mchanga....
Kavumilia akaona ngoja akupe ukweli wake...
MUNGU atakupa lako Mhishimiwa sana...
 
Mtegee misumari anapotoka kwake au mahali anapokuoea lift halafu usipande yeye na wapambe wake uwapite njiani uwahi ofisini kuwaonyesha hata yeye anahitaji msaada kwani atazikwa nalo
vidole vya mkono havilingani na si wote tutakufa siku moja ww msubiri tu atajileta

Kwa gear hiyo wala hamtapata, yaani kuna watu wanaroho ya kwanini
 
mmm ! mshikaji huyo jirani kakuchoka punguza kumwomba lift tena pateza mawasiliano kabisa anakusumanga huyoo!
 
Jamani leo naona jirani yangu niliyezoea kumuomba 'lift',
nadhani huenda baada ya 'kunichoka' kutokana na katabia
kangu ka kumuomba lifti wakati wa kwenda kazini.

Huenda aliamua kunitolea uvivu, au pengine nilikuwa namboa, au pengine
kwa mtazamo wake, anadhani ninao uwezo au labda ni ubahili
wangu.......hata sijui why....ila kifupi mara baada ya kupanda, akionekana
hana furaha, neno lake la kwanza likawa 'Hivi jirani kwa nini hununui
gari likusaidie usafiri wa kwenda na kurudi ofisini? Abiria wengine wawili walokuwa
ndani ya gari walibaki kuangaliana tu, maana nao kama wasaidiwa
huenda walihis hilo 'dongo' linawahusu pia

Kwa kuhisi huenda jamaa kanichoka, nililoweza kufanya ni
kuguna tu, mhhhhhh bila kujibu kitu huku nikiwa na aibu tele usoni.
Baada ya kwenda kama mita 70 hivi, nikajidai nimesahau simu na kumuomba jamaa
anishushe niirudie simu yangu nyumbani. Baada ya kushuka
nikapanda zangu daladala na kuelekea job.

Hapa kazini hii stori imekuwa gumzo kwani abiria wale wengine waliifikisha
hii skendo ofisini na imekuwa gumzo la siku. Kila mtu 'ananitania' kwa kurudia
kauli ya mshikaji, 'Hivi jirani kwa nini hununui gari'? Nabaki nacheka tu hapa
ofisini!

pole ila mkomeshe kakodishe hata ka vitz halafu unamvizia akipita wewe unakuwa mbele yake...leo kakwo kesho kwangu....
 
Ungekuwa unachangia hata mafuta haya yasinge kukuta
We kila siku unamlia timing jirani akupe lift ameamua kukutolea uvivu
 
Gharama za kutunza au kuwa na gari.1. Ununuzi (capital tied up)2.Bima3. motor vehicle licence4. service ya kila mara5. Ununuzi wa matairi6. ununuzi wa vipuri7. mafuta ya gari8. gharama za maegesho9. n.kJe wewe unamsaidiaje mwenzako katika gharama hizi?Ungekuwa muungwana unajaza hata mafuta ya wiki moja kwa mwezi angekuwa anakupitia nyumbani kwako mwondoke.Acha kupendelea KITONGA ( MITEREMKO)

Mkuu kama sisi waomba lift wote tungekuwa na mtizamo kama huu, wala hili swali la '' Hi jirani kwanini hununui gari?'' lisingekuwepo. Yaani kabisa jamaa anakuafuata nyumbani mnawahi ofisini... usafiri jamii unatimia... tatizo watu mteremko.. anakuachia mamichanga tu... yaani acha bana...
 
wako watu wanadai gari sio muhimu bora kujenga nyumba, ukiwa unakaa nyumba ya kupanga ukanunua gari wanakuona mwehu tu, sasa mvua ikinyesha unapandisha vioo hadi juu , walewale walio kucheka wananuna na kukuona una roho mbaya , si wapande nyumba zao sasa.

hili dongo nalo
 
kakuambia jambo jema nawe tia hasira ununue lako
kuna watu kweli hata wakipewa lifti hata viatu hawakunguti mchanga unakuta umejpinda asbh au mke kaamka mapema kasafisha gari la mumewe na kutoa michanga watu wengine kazi yao lift za kila siku na kujaza michanga.hata mm iliniboa sana hii kitu
naona ulimboa labda kwa hilo.

Ni kweli aisee

Au jamaa mwenyewe asubuhi anataka wawe wanaongea mambo yao na wife wanaona wewe umewakodelea.
 
Mwenye gari hana kosa lolote! Mpaka akuambie hivo maana yake amehisi unataka kulazimisha usafiri wake uwe wako! Kila mtu ana taratibu zake za kuishi na amenunua gari kwa matumizi yake kwanini umlaumu? Kama mnafanya kazi sehemu moja hio sio hoja ya yeye kukupa ride kila siku, kama anataka kupitia sehemu nyingine before work je? Watz tuna tabia kama mnafanya kazi sehemu moja na mtu na ana gari unataka kila siku anakupe ride tena bureee hata mafuta huchangii na wala hujui garama ya matengenezo ikiharibika! Wewe unafurahia tu kukaa na kukenua meno! Watu kama hao ndo tunaowahitaji ili wakupe gadhabu na uongeze juhudi ununue yako! Tena isitoshe anakufahamu fika kama ungekuwa wewe walahi hata asingejaribu kupanda hio gari
 
Jirani pesa ni ngumu sana uchumi unapanda kila siku kwa mshahara huu serikali ikiniongezea ni 5% kwa mwaka Inflation
12% ..nakuna kichwa kwa mawazo.
Jirani naomba unipe mbinu wewe ulifanyaje mpaka ukapata gari ?
 
Ndokyo, huyo jirani yako mpuuze. Hivi kwenye mji kama Dar kama mwenye uwezo anunue gari hayo magari yatapita barabara ipi. huyu jirani ni limbukeni wa gari si ajabu anaendesha ki vitz halafu ni 'dereva automatic' kwa sababu lazima gari yake itakuwa ni automatic. Haya mascrap ya kutoka Japa sasa hivi asilimia 98 ni automatic wengi waendeshao magari hayo hawawezi kuendesha gari yenye gia za kubadili (manual).
Usiumie kwa jambo dogo tu.
 
Gari ni kitu muhimu sana. Lakini si LAZIMA kuwa nalo. Kwasababu usipokuwa na gari lako, magari ya umma (daladala) yapo. Ila mambo mengine kama nyumba ni muhimu zaidi kadiri yangu. Kwasababu sidhani kama kuna nyumba za umma, na hivyo hata kama tunapanga laikini tunapanga kwa mtu binafsi na ndio maana hata kodi zipo holela sana. Asikuumize sana huyo jamaa, kama vipi we panda zako daladala.
 
Mkuu ukiishi mjini ka-vitz muhimu!pole kwa kunyanyapaliwa...:A S embarassed:
 
pole sana bora amekuambia mapema,Mungu atakujalia bila ufisadi wala damu ya mtu utanunua lako tu.Hehehehehe leo usiku utaota umenunua gari.
 
Mkuu, naona kwenye avatar yako unakunywa mkojo wa nyani...kwa style hiyo utaweza kununua gari kweli?inaelekea wewe ni mbahili hata wa maji ya kunywa!
 
Back
Top Bottom