Hivi huwa inakuwaje?

Hivi huwa inakuwaje?

Manyanza

Platinum Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
20,255
Reaction score
48,109
wadau huwa mimi nashindwa kuelewa utakuta mtu anaenda kutoa PESA kwenye ATM. Akishamaliza anaanza kuzihesabu. Hivi hata kama akizukuta zimepungua/ ongezeka atafanya nini wakati huo Bank inakuwa imeshafungwa.
Na huwa inakera zaidi maeneo ya mikoani yaani umesimama kwenye foleni halafu kila anayeingia anakuwa anafanya kamchezo hako bila kuzingatia kuna foleni kubwa inasubiri huduma.
Sijaelewa na huwa najiuliza bila majibu mtu kuanza kuhesabu pesa baada ya kutoa kwenye ATM.
Naomba wenzangu kama mna mawazo tofauti.
 
utandawazi wito ..........wanaogopa dhuluma wengi risiti hawaifadhi.
 
Hivi machine inaweza kutoa pesa chini/juu ya kiasi ulichoandika? Lol.....nimeona niulize mwaya, ila mi sijawahi shuhudia!

huwa mimi nashangaa sana, kama mtu ume command kutoa laki moja iweje ukishatoa uanze tenaa kuzihesabu?
 
Kwenye ATM zetu za bongo hua inatokea watu wanapata chini ya kiasi walichotaka kitoke kutokana na makosa ya kupanga pesa. Yani kama sh. 5000 ikiwekwa kwenye tray la sh.10000 lazima kuna mtu atapunjwa mashine itakapotoa ile 5000 kama 10000....kwahiyo binafsi siwezi kulaumu mtu akihesabu vijisenti vyake just to make sure hajapigwa changa la macho. Bongo si ATM wala watu usanii kila mahali....
 
wadau huwa mimi nashindwa kuelewa utakuta mtu anaenda kutoa PESA kwenye ATM. Akishamaliza anaanza kuzihesabu. Hivi hata kama akizukuta zimepungua/ ongezeka atafanya nini wakati huo Bank inakuwa imeshafungwa.
Na huwa inakera zaidi maeneo ya mikoani yaani umesimama kwenye foleni halafu kila anayeingia anakuwa anafanya kamchezo hako bila kuzingatia kuna foleni kubwa inasubiri huduma.
Sijaelewa na huwa najiuliza bila majibu mtu kuanza kuhesabu pesa baada ya kutoa kwenye ATM.
Naomba wenzangu kama mna mawazo tofauti.

Ukiingia kwenye chumba cha ATM kuna tangazo linasomeka 'HESABU FEDHA ZAKO KABLA HUJAONDOKA'. Kwahiyo waliloliweka ni wajinga?
 
Ukiingia kwenye chumba cha ATM kuna tangazo linasomeka 'HESABU FEDHA ZAKO KABLA HUJAONDOKA'. Kwahiyo waliloliweka ni wajinga?

hivi unaweza uka justify vipi kwamba pesa yako imepungua au imeongezeka once umeshaitoa kwenye mashine na ATM receipt inaonyesha imetoa fedha taslimu

ukikuta zimepungua utamhakikishiaje afisa wa benki kwamba pesa zimepungua kwa ATM na si janja yako

siyo rahisi kihivyo mkuu
 
nimesha shuhudia mtu kaomba hela ikamuhesabia na pesa haikutoka ikatoa risiti kuthibitisha kwamba pesa kesha chukua,mtu atakaye fuata hapo au hata baada ya watu kazaa akapewa pesa zaidi ya ile ailiyoomba
 
nimesha shuhudia mtu kaomba hela ikamuhesabia na pesa haikutoka ikatoa risiti kuthibitisha kwamba pesa kesha chukua,mtu atakaye fuata hapo au hata baada ya watu kazaa akapewa pesa zaidi ya ile ailiyoomba

Gosh!!! Kama benki imeshafungwa sasa hapo sijui ndo inakuwaje!!
 
ukienda siku za kazi huwa wanacheki sabab kuna taarifa huwa zina baki kama kweli hela ilitoka au la kama haikutoka baada ya 24hrs ile hela huwa inarudi kwenye akaunt automatically,kwa yule aliye chukua zaidi ya kiwango ailchokuwa anahitaji maana atm ilitoa accidentally huwa inakuwa deducted kwenye ac yake
Gosh!!! Kama benki imeshafungwa sasa hapo sijui ndo inakuwaje!!
 
Watu na wahesabu coz ilishawahi kunitokea nimekomand laki ikatoka elfu 50 na risiti iasoma nimetoa laki,ilinisumbua sana kufatilia kwenye tawi nililofungulia account ndio wakanirudishia,ni vizuri kuhesabu mashine nyingi zina mawenge na zinakosea.
 
utahesabia mbele ya safari kwani mara nyingi inakua too late...............
 
mkuu kuhesabu mbona kitu cha kawaida icho.
Si unahakikisha tu, kwani mashine unadhani haikosei?
 
hivi unaweza uka justify vipi kwamba pesa yako imepungua au imeongezeka once umeshaitoa kwenye mashine na ATM receipt inaonyesha imetoa fedha taslimu

ukikuta zimepungua utamhakikishiaje afisa wa benki kwamba pesa zimepungua kwa ATM na si janja yako

siyo rahisi kihivyo mkuu

Mkuu sure unachoongea kuna siku niliingia kwenye hizi Umoja Switch. badala ya 50,000 ilitoka 30,000.
na receipt ilikuwa inaonyesha nime withdraw 50,000. nili complain mpaka kwa Meneja lakini wapi.
na msimamo wao ulikuwa pale pale. receipt inaonyesha elfu 50 wewe unasema elfu 30, hawakunielewa nikakubali kula hasara maana ilikuwa hamna evidence yoyote.
 
Back
Top Bottom