Hivi huu mchezo bado upo?

Hivi huu mchezo bado upo?

Ukichanganya michezo yote hiyo ya utotoni na mfumo wa maisha tulipotea ndio maana bongo za kizazi hicho zilikuwa safi katika umeri mdogo yaani mtu ana miaka 8 anatumwa mjini kununua vitu na anarudi bila wasiwasi.

sasa hivi toto la miaka 12 ukimtuma dukani anasahahu ametumwa nini?
 
Aisee, chini ya umri huo watu tulikuwa tunatoka Dar to Mwanza kwa train japokuwa upo na mtu mzima lakini humo ndani ya behewa ni struggle for existence mnaonana wakati wa kula Salanda

ha haha ha umenifurahisha .. kumbe we kakubwa eeeh?
 
kuna hii kioo kioo ..................sijui sijui..............wa mwisho akamatwe atiwe gerezani
 
midako, esta esta banda shuzi, kuruka kamba, banchikicha, iki na oko, yai bovu, tulinge bayoyoyo mingine nimesahau jamani tuliifurahia sana na hasa kucheza kwa nafasi siyo sasa hivi watoto wetu wanafungiwa ndani kama kuku wa kisasa.
 
...ingia upepo watetema ingia upepo watetema... enzi zetu hizo
 
Watoto wa touchscreen siku hizi laini laini tu si ajabu mabwabwa wanazidi kuongezeka.
 
hawa watoto wa katuni hawajacheza

Hahahaaaaaa. Watoto wa sasa ni kizazi cha play station,na nyinyi wazazi wao wa sasa ni kizazi cha kuendekeza date na michepuko na kushinda bar/grocery na pia kwenda misibani na madira badala ya kanga huku mkiwa mmejikwatua/jiremba vya kutosha.
 
Ule mtende unachanua,x2 wakati wa kuchanua huchanua chanu chanu chanu..............cha aaaaaaaaa
 
Hivi nani kaona watoto sasaivi wakitengeneza magari ya waya na makopo? Tulikuwa na vyama watoto wa kiswazi na wakishua tukionana ni vita
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom