Hassan Mambosasa
JF-Expert Member
- Aug 2, 2014
- 3,350
- 4,485
Habari zenu, hebu rejeeni kichwa cha uzi hapo juu. Naamini mpo vyema kiafya, hata mimi nipo hivyohivyo na shukrani zote kwa Muumba.
Kilichonifanya nikafungua uzi huu, ni kuhusu huu mfumo wa ufaulu ambao umewekwa na baraza la mitihani hapa nchini. Ambao umekuwa wa kutoeleweka kabisa, ili utumike kwa vizazi vyote vitakavyopitia hatua za kielimu hapa nchini.
Siku hizi huu mfumo wa upangaji wa madaraja na alama za ufaulu umekuwa kama rangi ya kinyonga, Kila kukicha ni wenye kubadilika hovyohovyo, mara mwaka huu watumie huu. Uje mwingine itumike vingine, hadi inakuwa haieleweki.
Mfano, unakuta hawa kidato cha pili wametumia mtindo wa DIVISION mwaka fulani, mara unakuja mwingine wanatumia GPA, mara wastani na hata ule wa DISTINCTION. Hata kidato cha nne haya yanatokea pia, si huko chini tu.
Hivi baiwezekani zile alama za kizamani zikaendelea kutumika kama mwanzo, ila kufanyike maboresho tu kuendana na teknolojia ya sasa ilivyo?
Kushuka kwa thamani ya elimu hapa nchini, hadi mtu akifaulu kidato cha nne anaonekana kama kavuka mtihani wa kujipima wa darasa la nne. Hakutokani na huku kubadilika kwa hii mifumo?
Sasa hivi imekuwa kama ni mchezo yaani, akija kiongozi huyu atabadilisha na kuweka hivi. Mara mwingine aweke vile, ilimradi aonekane naye alipita kwenye uongozi na kufanya kitu. Pasipo kukumbuka wanatuharibia elimu na kutyletea mkanganyiko kwenye vyeti tu.
Kilichonifanya nikafungua uzi huu, ni kuhusu huu mfumo wa ufaulu ambao umewekwa na baraza la mitihani hapa nchini. Ambao umekuwa wa kutoeleweka kabisa, ili utumike kwa vizazi vyote vitakavyopitia hatua za kielimu hapa nchini.
Siku hizi huu mfumo wa upangaji wa madaraja na alama za ufaulu umekuwa kama rangi ya kinyonga, Kila kukicha ni wenye kubadilika hovyohovyo, mara mwaka huu watumie huu. Uje mwingine itumike vingine, hadi inakuwa haieleweki.
Mfano, unakuta hawa kidato cha pili wametumia mtindo wa DIVISION mwaka fulani, mara unakuja mwingine wanatumia GPA, mara wastani na hata ule wa DISTINCTION. Hata kidato cha nne haya yanatokea pia, si huko chini tu.
Hivi baiwezekani zile alama za kizamani zikaendelea kutumika kama mwanzo, ila kufanyike maboresho tu kuendana na teknolojia ya sasa ilivyo?
Kushuka kwa thamani ya elimu hapa nchini, hadi mtu akifaulu kidato cha nne anaonekana kama kavuka mtihani wa kujipima wa darasa la nne. Hakutokani na huku kubadilika kwa hii mifumo?
Sasa hivi imekuwa kama ni mchezo yaani, akija kiongozi huyu atabadilisha na kuweka hivi. Mara mwingine aweke vile, ilimradi aonekane naye alipita kwenye uongozi na kufanya kitu. Pasipo kukumbuka wanatuharibia elimu na kutyletea mkanganyiko kwenye vyeti tu.