Bora Kama Serikali kupitia TAMISEMI ingetoa tamko kuwa likizo za mwezi Machi na Septemba kuwa hazipo

Dig the EA

JF-Expert Member
Dec 7, 2017
279
270
Ni utaratibu wa kitaalamu, kitaaluma na ujifunzaji kisaikolojia wanafunzi na walimu kupata muda wa kupumzisha akili. Lengo la mapumziko hayo ni kuipa akili muda wa kupata nguvu za kusoma na kuelewa masomo yaliyo mbele.

Kitu cha ajabu na kinachoendelea miaka ya hivi karibuni ni likizo hizo za mwezi wa tatu na wa tisa kutokufungwa. Shule nyingi katika mikoa mingi nchini wanafunzi na walimu hawafungi Shule. Wako busy madarasani wakisoma kama vile si likizo. Pressure ya kusoma likizo inatoka mikoani (Elimu) na Halmashauri ya wilaya husika( idara ya Elimu).

Pressure hiyo inasukumwa na hofu ya matokeo ya mitihani ya mwisho iwe ni kwa darasa la nne, darasa la Saba, kidato cha pili, kidato cha nne au kidato cha sita. Kwa maneno mengine Kuna kutokuamini kuwa kilichofundishwa miezi au miaka yote hakitoshi hadi uhitaji wa kufundisha likizo. Hiyo ni hofu. Pia mfumo wa Elimu yetu unathamini mitihani kuliko kujifunza, hali hiyo hufanya viongozi hao kufanya chochote ili mradi waone matokeo mazuri.

Matokeo yake ndo hayo ya Shule kutokufungwa na kazi zinaendelea. Madhara ya hali hiyo wanafunzi wanachoka akili na mwili kiasi cha kutokujifunza wala kuelewa. Upande wa walimu wamejaa vinyongo na malalamiko sababu ya vitisho na kulazimishwa kufundisha kipindi cha likizo.

Ni Bora Kama serikali kupitia TAMISEMI ingetoa tamko kuwa likizo za mwezi March na September kuwa hazipo na zimefutwa, kuliko kuziweka harafu hazizingatiwi.
 
Mi kama mwalimu huwa nafuata azimio la kazi nimeazimia nini katika kufundisha mwaka mzima. Sipendi sifa kufundisha muda wa ziada. Hizo terms ni lazima wanafunzi wapumzike na hakuna mkuu wa shule au ofisa yeyote wa elimu au mwanasiasa wa ngazi yeyote atakayenilazimisha nifundishe wakati wa likizo za wanafunzi, sifundishi na hawana jeuri ya kunifukuza kazi. Siwezi kukiuka taratibu za ufundishaji zilizopangwa kitaalamu. Likizo zote wanafunzi wanapaswa kupumzika ili ku refresh mind tayari kupokea maarifa mapya
 
Yote uliyoandika ni kisingizio Cha walimu

Ila ukweli ni alosto mbaya zawalimu ,zinapelelekea hayo mtoto lakwanza kilasiku lazima aende na 300 na nilikizo
 
Kufululiza kufundisha bila kujali mapumziko hakufanyi wanafunzi wafaulu kwa wingi kama dhana ndiyo hiyo, huko ni kuchosha wanafunzi. Siku hizi mpaka darasa la sita wanawekwa bize muda wote eti kujiandaa na la saba. Kuna la nne nao hawafungi wako bize na maandalizi ya mitihani yao. Shuleni kwangu sitaki ujinga huo na ofisa elimu wa ngazi yeyote hadi waziri wa elimu haniambii kitu nje ya utaratibu wa ufundishaji uliopangwa kitaalamu katika misingi ya elimu na saikolojia ya ufundishaji.
 
Kwanza tuanze na hawa walio weka mitihani ya taifa kipindi cha likizo. Next week kuna mtihani WA taifa WA lasaba je ulitaka watoto wafunge shule ilhali wanamtihani WA taifa.
 
Ni utaratibu wa kitaalamu, kitaaluma na ujifunzaji kisaikolojia wanafunzi na walimu kupata muda wa kupumzisha akili. Lengo la mapumziko hayo ni kuipa akili muda wa kupata nguvu za kusoma na kuelewa masomo yaliyo mbele.

Kitu cha ajabu na kinachoendelea miaka ya hivi karibuni ni likizo hizo za mwezi wa tatu na wa tisa kutokufungwa. Shule nyingi katika mikoa mingi nchini wanafunzi na walimu hawafungi Shule. Wako busy madarasani wakisoma kama vile si likizo. Pressure ya kusoma likizo inatoka mikoani (Elimu) na Halmashauri ya wilaya husika( idara ya Elimu).

Pressure hiyo inasukumwa na hofu ya matokeo ya mitihani ya mwisho iwe ni kwa darasa la nne, darasa la Saba, kidato cha pili, kidato cha nne au kidato cha sita. Kwa maneno mengine Kuna kutokuamini kuwa kilichofundishwa miezi au miaka yote hakitoshi hadi uhitaji wa kufundisha likizo. Hiyo ni hofu. Pia mfumo wa Elimu yetu unathamini mitihani kuliko kujifunza, hali hiyo hufanya viongozi hao kufanya chochote ili mradi waone matokeo mazuri.

Matokeo yake ndo hayo ya Shule kutokufungwa na kazi zinaendelea. Madhara ya hali hiyo wanafunzi wanachoka akili na mwili kiasi cha kutokujifunza wala kuelewa. Upande wa walimu wamejaa vinyongo na malalamiko sababu ya vitisho na kulazimishwa kufundisha kipindi cha likizo.

Ni Bora Kama serikali kupitia TAMISEMI ingetoa tamko kuwa likizo za mwezi March na September kuwa hazipo na zimefutwa, kuliko kuziweka harafu hazizingatiwi.
Serikali haitoi vifaa stahiki vya kufundishia, walimu wanapikwa kiujanjaujanja, vipindi darasani siyo timilifu mwisho wa mwaka wanafunzi wamefeli, lawama kwa walimu, ufaulishaji haulengi competency ila pass hata kwa kuiba mitihani alimradi waonekane wamefaulu na kupata sifa, nje ya ukweli ukiwapima watoto hawajui kitu na ndiyo maana ya hiyo fundisha ya zimamoto ya kukaririsha

Haileti maana kama muda wa kusoma hautoshi halafu unawatumia walimu kwenda mkesha wa mwenge, kusimamia uchaguzi, na kazi zingine zisizo majukumu yao halafu mwisho wa siku uwaambie hamna likizo na likizo hiyohiyo umewapa week mbili
 
Mi kama mwalimu huwa nafuata azimio la kazi nimeazimia nini katika kufundisha mwaka mzima. Sipendi sifa kufundisha muda wa ziada. Hizo terms ni lazima wanafunzi wapumzike na hakuna mkuu wa shule au ofisa yeyote wa elimu au mwanasiasa wa ngazi yeyote atakayenilazimisha nifundishe wakati wa likizo za wanafunzi, sifundishi na hawana jeuri ya kunifukuza kazi. Siwezi kukiuka taratibu za ufundishaji zilizopangwa kitaalamu. Likizo zote wanafunzi wanapaswa kupumzika ili ku refresh mind tayari kupokea maarifa mapya
Safi sana kwa msimamo huo. Ingawa walimu wengi hawana ujasiri huo. Wakuu wa Shule na walimu wakuu nao huungana na Maafisa Elimu kuwatisha walimu ili wafundishe kipindi cha likizo..... mwanafunzi hapendi asome likizo na walimu hawapendi wafundishe likizo. Sijui kujifunza huko kunakuwaje
 
Yote uliyoandika ni kisingizio Cha walimu

Ila ukweli ni alosto mbaya zawalimu ,zinapelelekea hayo mtoto lakwanza kilasiku lazima aende na 300 na nilikizo
Hapa hoja si walimu kupenda tuition au hizo 300 sijui 500. Hoja ni ulazima kutoka kwa viongozi kulazimisha kufundisha kipindi cha likizo kama siku za kawaida za masomo
 
Mfumo wa elimu katika nchi hii ni kinyaa, Wizara ya elimu pamoja na tamisemi wana miongozo lakini haifuatwi.

Tatizo la nchi hii upumbavu ni mwingi sana.
Mifumo ya Elimu imeparaganyika sana
 
Kufululiza kufundisha bila kujali mapumziko hakufanyi wanafunzi wafaulu kwa wingi kama dhana ndiyo hiyo, huko ni kuchosha wanafunzi. Siku hizi mpaka darasa la sita wanawekwa bize muda wote eti kujiandaa na la saba. Kuna la nne nao hawafungi wako bize na maandalizi ya mitihani yao. Shuleni kwangu sitaki ujinga huo na ofisa elimu wa ngazi yeyote hadi waziri wa elimu haniambii kitu nje ya utaratibu wa ufundishaji uliopangwa kitaalamu katika misingi ya elimu na saikolojia ya ufundishaji.
Hongera sana kwa kulikataa hilo shuleni kwako, nadhani utakuwa mkuu wa Shule au Mwalimu Mkuu. Kwenye vikao vyenu na viongozi jaribu kulisemea hilo. Si walimu, si wanafunzi wanapenda kusoma likizo. Likizo watu wapumzike, Kama wanaona ulazima na umhimu kusoma likizo, basi wazifute hizo likizo
 
Mi kama mwalimu huwa nafuata azimio la kazi nimeazimia nini katika kufundisha mwaka mzima. Sipendi sifa kufundisha muda wa ziada. Hizo terms ni lazima wanafunzi wapumzike na hakuna mkuu wa shule au ofisa yeyote wa elimu au mwanasiasa wa ngazi yeyote atakayenilazimisha nifundishe wakati wa likizo za wanafunzi, sifundishi na hawana jeuri ya kunifukuza kazi. Siwezi kukiuka taratibu za ufundishaji zilizopangwa kitaalamu. Likizo zote wanafunzi wanapaswa kupumzika ili ku refresh mind tayari kupokea maarifa mapya
Nimesoma Mara tatu nikadhani huenda aliyendika hapa ni mimi, ujue baadhi ya walimu hawajitambui kabisa,mimi siwezi na sitaweza kufundisha wakati wa likizo,sisi walimu ndo chanzo cha matatizo ya watoto kutopumzika,ila hii inachangiwa na wengi ya walimu kutokuwa na shughuli mbadala za kutuingizia vipato,hivyo watoto hubaki kama faraja kwetu.Shuleni kwangu Wapo wanafundisha sana ila sijaona mkuu wala mtaaluma ananitafuta kwa kutoingia kwenye vipindi vyangu
 
Nimesoma Mara tatu nikadhani huenda aliyendika hapa ni mimi, ujue baadhi ya walimu hawajitambui kabisa,mimi siwezi na sitaweza kufundisha wakati wa likizo,sisi walimu ndo chanzo cha matatizo ya watoto kutopumzika,ila hii inachangiwa na wengi ya walimu kutokuwa na shughuli mbadala za kutuingizia vipato,hivyo watoto hubaki kama faraja kwetu.Shuleni kwangu Wapo wanafundisha sana ila sijaona mkuu wala mtaaluma ananitafuta kwa kutoingia kwenye vipindi vyangu
Hongera sana na una bahati kuwa na Mkuu wa Shule au mtaaluma anayejitambua. Hakuna mwalimu miaka hii asiyejitambua ndugu; shida kubwa hapa ni ubabe, vitisho na nguvu nyingi zinazotumiwa na Maafisa Elimu na wakuu wa Shule kiasi cha kuzua ugomvi na kutokuelewana, ili tu walimu wafundishe kipindi cha likizo
 
Hongera sana na una bahati kuwa na Mkuu wa Shule au mtaaluma anayejitambua. Hakuna mwalimu miaka hii asiyejitambua ndugu; shida kubwa hapa ni ubabe, vitisho na nguvu nyingi zinazotumiwa na Maafisa Elimu na wakuu wa Shule kiasi cha kuzua ugomvi na kutokuelewana, ili tu walimu wafundishe kipindi cha likizo
Hata aje afisa elimu taifa,siwezi fundisha,ninao waraka unaozuia kufundisha wakati wa likizo
 
Hata aje afisa elimu taifa,siwezi fundisha,ninao waraka unaozuia kufundisha wakati wa likizo
Digba Sowey! Nimeipenda hiyo! Waraka huo wengine hawana...... ingefaa watu waupate.
Digba Sowey ni mmoja wa character matata kwenye novel iitwayo "Unanswered Criei" cha mwandishi aitwaye Osman Konteh......novel nzuri sana.
Hoja na msimamo wako vinafaa visambae kwa walimu wengi
 
Back
Top Bottom