Hivi Geita kuna mbunge?

Hivi Geita kuna mbunge?

Huyo jamaa huwa haji mara kwa mara huku, na akija huwa anajificha, ukibahatika saana unaweza kumkuta kwenye baa moja inaitwa ambassador akiwanywa ngumu kumeza.Mimi kwa mawazo yangu ni kwamba jamaa anarudisha pesa zake za kampeni halafu apate na kafaida kidogo,kisha harudii tena kugombea.Huyu jamaa alichukua hili jombo kwa manufaa yake yeye mwenyewe, mimi nipo huku tangia januari 2011 but sijawahi kumuona akihamasisha shughuli za maendeleo hata mara moja, walomchagua ndio wa kulaumiwa cause suluhisho lilikuwepo, Rodgers Ruhega alikuwepo, aliwaambia mambo mengi ambayo Magamba walipaswa kufanya lakini hakuna, aliwaambia ni kitu gani atafanya akipewa kura kuwa mbunge kupitia CHADEMA ila wao wakaamua kuchagua historia ambayo hadi leo inawatesa.
 
Alipigwa mkwara mapema na magamba akaambiwa Geita ni shamba lao afunge mdomo wake, jamaa akaenda kukaa kwenye stuli ndefu na kuanza kujiburudisha kwa kinanah baridi!
 
Hawa wana Geita hawajifunzi kabisa! Eti sasa hivi wanamuandaa Vicky Kamata for 2015! Wanaruka mkojo watakanyaga ma.vi!
 
Huyu jamaa si alikuwa na mke wa kutoka Russia? Au wameachana? Mrusi anakubali atanue na vimwana?

Jamaa nasikia huwa anaponda sana CCM. Anasema wazi kabisa aliingia ili apate Ubunge na anawashangaa vijana kwa kuishabikia CCM wakati hawana faida yoyote kutoka humo ndani. Yaani kwa upande fulani nilimpenda kwa sababu anawaambia watu moja kwa moja kuwa "niliwanunua na mkanunulika, tulishamalizana." Sasa hivi yeye hata hajali na anasubiri tu kila mwezi hela yake ya bunge. Wananchi wamebaki kucheka tu Ujinga wao walioufanya.
Walimchagua Donald Max wakawa wanamwita jembe,sasa jembe limelima kwenye rami limeishiwa makali!
Kazi yake imebaki kunywa pombe na kutanua na walembo hili ni funzo kubwa kwa wanageita 2015 msifanye tena kosa hakuna jembe ndani ya ccm.
 
Lohh, yaani umenivunja mbavu. Ukimuona msalimie "Dobri din..."
Alipigwa mkwara mapema na magamba akaambiwa Geita ni shamba lao afunge mdomo wake, jamaa akaenda kukaa kwenye stuli ndefu na kuanza kujiburudisha kwa kinanah baridi!
 
Hahahaaa, jamaa halitaki Wapambe. Anakupa za usoni moja kwa moja.

CC: FirstLady1

Nimekaa Geita Tangu mwaka 2000 mwezi wa Pili,nimeshiriki uchaguzi wa mwaka huo,katika jimbo la Geita akapatikana Mbunge anaitwa Ernest Mabina,kwenye Jimbo la Busanda alipatikana Mbunge anaitwa Faustine Rwilomba Kabuzi (Marehemu),na Jimbo la Nyang'hwale alikuwepo James Musalika.

Wabunge hawa walifanya kazi kubwa sana ya kujaribu kuijenga Geita,lakini walikuwa wakibebwa sana na Marehemu Kabuzi ambaye hadi leo hii bado anakumbukwa kutokana na juhudi zake katika kuwapelekea wananchi wa Jimbo lake maendeleo pamoja na Wilaya yote ya Geita wakati huo kabla haijapata Mkoa,lakini Pia Mabina alikuwa akijitahidi sana ingawa yeye ni mtu wa Ground hakuwa na maneno mengi sana mitaani,kuongea sana alikuwa hajui isipokuwa alikuwa mtekelezaji,nadhani hii huenda ilisababishwa kwake na shughuli yake za Usalama wa Taifa,kwa sababu mara nyingi ni watu wakimya sana mfano mwingine ni Mbunge wa jimbo la Mbogwe Augustine Masele,naye mkimya mkimya lakini mambo yake chinichini sana.

Wabunge hawa wote walirudi kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 kwa kishindo lakini kwa bahati mbaya Kabuzi akafariki Dunia mwaka 2007,wakati wao walikuwa wakiitwa 'UTATU MTAKATIFU' hadi Bungeni na walikuwa wasumbufu,hata hivyo huyu Mbunge wa sasa Max alijitahidi sana kumsumbua Mabina wakati huo na hasa kwenye uchaguzi wa mwaka 2005 lakini alishindwa vibaya,wakati huo maxalikuwa na hela za Pamba kwa sababu alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni moja inaitwa Copcot ambayo ilikuwa ya shemeji yake mzungu ambayo pia iko huko Kampala.

kutokana na pesa hizo aliamua kupanda nyasi kwenye eneo la hospitali ya wilaya ya Geita,pamoja na pembezoni mwa barabara ya Geita mjini ukielekea Mwanza kama mita 400 hivi pamoja na kujenga Public Toilet inayotumika hadi sasa ila kwa kulipia,hapo watu wakaona kwamba yeye ni mwanamaendeleo wakamshauri kugombea ubunge kwamba ataleta maendeleo kwa wakazi wa Jimbo la Geita,lakini mwaka 2005 akashindwa na alimfanyia visa kweli kweli aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Mabina.

Miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na kuwanywesha vijana viroba na kwenda kumzomea Mabina kwenye mikutano yake ya hadhara yote na hasa mjini Geita(kwenye uwanja wa Kalangalala),lakini huko vijijini alikuwa akishindwa wanamtoa mbio,hali hiyo iliwashawishi hata viongozi wa ngazi ya Mkoa na Taifa wa CCM na kumuona Mabina kama mtu anayewaharibia chama na ilipofika uchaguzi wa mwaka 2010 akashinda lakini kwa kutumia mchezo mchafu sana wa kununua kadi 3500 na kuzisambaza kwa watu wake ambao walikuja kumpigia kura,ingawa mbinu hiyo pia ilikuwa imetengenezwa na CHADEMA wakijua kwamba akishinda yeye na kupita kwenye kura za maoni ndani ya ccm itakuja kuwa rahisi sana kumshinda kwenye uchaguzi mkuu.

Ndicho kilichotokea alishinda na baada ya hapo upepo ukageuka,alishambuliwa na almanusra CHADEMA ishinde jimbo hilo kama sio wizi wa kura kwenye baadhi ya maeneo lakini pia kuna uzembe CHADEMA walifanya nadhani ni kutokana na kutokuwa wazoefu wa uchaguzi na hasa Rogers mgombea wa chadema na kundi lake wakazidiwa ujanja kidogo,chadema alipata sapoti kubwa sana kutoka hadi kwa wanaccm wenyewe ambao walikuwa wakiamini kwamba huyo Max hafai kubwa Mbunge.

kwa hiyo hayo yanayotokea sasa hivi ni halali kwa wakazi wa Geita ili wajifunze wakiambiwa wawe wanasikia na sio kushabikia kila mtu,jamaa sasa hivi linatembea na viroba tu kwenye mifuko ya koti na suruali,halina time na mtu na halijawahi hata kufanya mkutano mmoja wa hadhara iwe ni kuwashukuru wananchi ama kuzungumzia shughuli za maendeleo,labda kama anadandia ile ya wakubwa ambao nao siku hizi wanamkataa kwenye mikutano yao wanamwambia ajifiche kwa sababu anazomewa LIVE yani ile yenyewe,na nasikia kwamba hagombei tena ndio maana ameamua kutumia pesa zake vizuri.

Kuna mengi sana ya kuelezea juu ya huyu Mbunge wa Geita lakini ndio hivyo tena nitawachosha.hafai jimbo liko wazi.
 
Habari za Mbunge wa Mkoa Mpya wa Geita ni Ngumu sana na hakuna asiyezijua
Mbunge anasema anajuuuta kujihusisha na siasa ameamua kuwa mlevi tu na hataki kusikia anaitwa Mbunge ,..anajifisha
,Ila nadhani Geita ikimpa tena Vicky Kamata ndio inaelekea kufa kifo cha Mende

Yuko Busy na kina mama nadhani anajua kura nyingi zinapatikana kwao
 
Acha watu wajifunze !maana tunatabia ya kutoamini mpaka tuone!kila aliye na macho ameona.
 
habari zenu wadau......!
Naomba kuuliza tuu jamani hivi yule mbunge wa geita mjini bado yu hai au alishatangulua mbele ya haki????? sijawai kumuona wala kumsikia toka alipochaguliwa mwaka 2010, cyo kwenye bunge la katiba wala lile bunge jingine, nia yangu cyo kumuombea mtu kifo ila amekaa kimya sana utadhani geita haina mbunge,
 
by Kifai;
Habari za jumapili wakuu, napenda kuchukua nafasi hii kutaka kujuzwa hasa na wakazi wa mkoa mpya wa geita ambao bado miundo mbinu yake ni mibovu....! Nauliza hivi huyu mbunge wa jimbo la geita yupo wapi? Mbona haeleweki hata kiduchu? Yani toka amechaguliwa mwaka 2010 hata kugeuka kusema asante wa wapiga kura wake hawezi au ndo dharau kwa vile alishapata??? Popote alipo mfikishieni salamu za wakazi wa geita, najua atajichanganya 2015 agombee tena ndipo atajua tumeshachoka au la




cc
WABHEJASANA njoo huku mbunge wenu anatafutwa haonekani!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom