Hivi Dr. Mpango amewahi kufanya biashara yoyote?

Hivi Dr. Mpango amewahi kufanya biashara yoyote?

Watatoka wale wenzangu na mie wanaosajili namba binafsi wakati si ma milionea..
Sidhani mtu kama Mo atakuwa affected kwa kulipia ushuru wa 10m plate namba yake...
Wengi wa wenye private numbers ni matajiri si mchezo...hiyo ni hela ya mboga tu
 
Watatoka wale wenzangu na mie wanaosajili namba binafsi akati si ma milionea..
Sidhani mtu kama Mo atakuwa affected kwa kulipia ushuru wa 10m plate namba yake...
Wengi wa wenye private numbers ni matajiri si mchezo...hiyo ni ela ya mboga tu
Ukitaka kupata hela ni vizuri ukawashawishi wengine kulipa kodi kuliko kuweka vigingi.
 
Hivi na wewe Copenhagen, umeisoma hotuba ya bajeti yote na ukaimaliza?

Mbona unaanza kunitia wasiwasi kwamba unaishi katika nchi ambazo suala la kodi hawaliletei mzaha, yaani namaanisha uwezo wako wa kuchambua mambo kama haya ya kodi bila kuweka siasa unatakiwa uwe kwenye level ingine kabisa.

Au upo Makambako mkuu

lol.
Heshima yako mkuu Richard. Huenda labda uchovu mkuu nalala masaa machache halafu elimu yangu ndogo ila kiingereza nafahamu sana weekdays ndio maana.

Mimi ni muumini mzuri sana wa kulipa kodi hapa nadhani hata kwenye system wananifahamu. Nalipa 36%. Na April waliniletea tax card return December watanirudishia karibu million moja laki nane za kibongo.

Kama ujuavyo hizi nchi they heavily tax ndio maana wakati wa winter barafu inasombwa kokokoto inamwagwa usiteleze. Wakati wa fall majani yanasombwa hizo zote tax. Nimebahatika kuwepo nchi zote za Nordic hadi Icelend ila nimejikita sana Denmark na Norway nimeishi pia na system nazifahamu. Wewe uko nchi gani mkuu nahisi hapo juu Sweden
 
Hapana mkuu usijali, lugha unatumia pale inapobidi na ndio maana wenzetu wanathamini sana lugha zao.

Mimi ni nimepitapita tu katika hizo nchi katika harakati zangu, lakini nilikuwa nataka kusema kwamba kuna watu wanajali zaidi faida kuliko kulipa kodi inavyostahiki.

Hivyo mashine zinazotoa stakabadhi ya malipo ni moja ya viashiria vitakavyotoa ishara kwamba nchi inapata kodi inavyotakiwa.

Hii mifumo ya kodi ikiwekwa sambamba na mifumo ya hawa wahisani (nchi za Ulaya) watu wengine si hawatafanya biashara kabisa?
 
heshima yako mkuu Richard. Huenda labda uchovu mkuu nalala masaa machache halaf elim yangu ndogo ila kiingereza nafaham sana weekdays ndio maana.

Mimi ni muumin mzur sana wa kulipa kodi hapa nadhan hata kwenye system wananifaham. Nalipa 36%. Na April waliniletea tax card return December watanirudishia karib million moja laki nane za kibongo.

Kama ujuavyo hz nchi they heavily tax ndio maana wakati wa winter barafu inasombwa kokokoto inamwagwa usiteleze. Wakati wa fall majani yanasombwa hizo zote tax. Nimebahatika kuwepo nch zote za Nordic hadi icelend ila nimejikita sana Denmark na Norway nimeish piano system nazifaham. Wewe huko nchi gan mkuu nahis hapo juu Sweden

Inakuwaje mkuu unalipa tax 36%?

Utakuwa unafanya kazi zaidi ya moja.

Rate yao Denmark si ni 8% ya kipato kabla ya kodi kwenye ajira moja?
 
sasa kama sio kitu muhimu huoni hapo serikali itapata hasara maana watu wataamua kuachana nacho,sasa hiyo pesa waliotegemea kuipata si wataikosa
Swali mbona mnalikwepa, huyu jamaa mleta mada kasema kuongezeka kwa hiyo kitu itawaathiri wafanya biashara, nauliza itawaathiri kivipi??
 
Nchi inatakiwa ijiongeze , kutegemea wafanyabiashara tu ili kuendesha nchi iko siku tutakwama .

Mkuu, usisahau TANZANIA YA MAGUFULI NI YA VIWANDA. Sasa vivyo viwanda vitakuwa vya serikali??
 
Mkuuu, haya ndio madhara ya wahisani kupunguza misaada kwenye uchumi wetu. Watu walikuwa wanambeza JK kuwa kila siku yuko nje, but ukiwa na hali kama hii ambapo 90% ya wana Dar hawana ajira, unakaaje pale ikulu? By now JK angekuwa kwa Obama anapigia chapuo misaada kwa kuwa kiukweli nchi yetu ni maskini na hata pia nchi kama Israeli au Egypty ambazo ni 'tajiri' bado nazo zinapokea misaada kutoka America.
Nimeiangalia bajeti yake kwa umakini na inaonyesha kama imewalenga hasa wafanyabiashara, sijui lengo lake nini, kuwakomoa? Hivi kuna nchi inaweza kusonga bila wafanyabiashara?

Kwa mfano kutoza VAT kwenye miamala ya simu pamoja na kumgusa kila mtu lakini wafanyabiashara ndio watakaoathirika zaidi, maana badala ya mtu kutuma hela mbagala kwa simu sasa atapanda daladala na kupeleka kwa mkono.Hili la kuendelea kutegemea bia na sigara kwenye kodi litaua viwanda ambavyo ni tegemeo kubwa la ajira.

Ifahamike kwamba hakuna mfanyakazi wa serikali ya Tanzania aliyewahi kusajili namba binafsi kwenye gari lake, sasa kupandisha ada hii kwa 100% yaani kutoka mil 5 hadi mil10 ni kuwakomoa wafanyabiashara bila sababu yoyote.

Mtu yeyote aliyewahi kupata uzoefu kwenye biashara ambaye anazijua changamoto zake hawezi kuleta bajeti inayokandamiza sekta hii kwa kiwango ambacho ni hakika kuna viwanda na biashara kadhaa hazitaweza kumudu.
 
Labda aliwahi kuhuza ubuyu pale cafeteria Manzese.
 
Nimeiangalia bajeti yake kwa umakini na inaonyesha kama imewalenga hasa wafanyabiashara, sijui lengo lake nini, kuwakomoa? Hivi kuna nchi inaweza kusonga bila wafanyabiashara?

Kwa mfano kutoza VAT kwenye miamala ya simu pamoja na kumgusa kila mtu lakini wafanyabiashara ndio watakaoathirika zaidi, maana badala ya mtu kutuma hela mbagala kwa simu sasa atapanda daladala na kupeleka kwa mkono.Hili la kuendelea kutegemea bia na sigara kwenye kodi litaua viwanda ambavyo ni tegemeo kubwa la ajira.

Ifahamike kwamba hakuna mfanyakazi wa serikali ya Tanzania aliyewahi kusajili namba binafsi kwenye gari lake, sasa kupandisha ada hii kwa 100% yaani kutoka mil 5 hadi mil10 ni kuwakomoa wafanyabiashara bila sababu yoyote.

Mtu yeyote aliyewahi kupata uzoefu kwenye biashara ambaye anazijua changamoto zake hawezi kuleta bajeti inayokandamiza sekta hii kwa kiwango ambacho ni hakika kuna viwanda na biashara kadhaa hazitaweza kumudu.
Kwani kuna kigezo kwamba ili fulani awe waziri wa fedha anatakiwa kuwa na biashara ama aliwahi kufanya biashara?
 
Kulipa kodi si lazima
Tutaikwepa hadi itavyowezekana
 
Nimeiangalia bajeti yake kwa umakini na inaonyesha kama imewalenga hasa wafanyabiashara, sijui lengo lake nini, kuwakomoa? Hivi kuna nchi inaweza kusonga bila wafanyabiashara?

Kwa mfano kutoza VAT kwenye miamala ya simu pamoja na kumgusa kila mtu lakini wafanyabiashara ndio watakaoathirika zaidi, maana badala ya mtu kutuma hela mbagala kwa simu sasa atapanda daladala na kupeleka kwa mkono.Hili la kuendelea kutegemea bia na sigara kwenye kodi litaua viwanda ambavyo ni tegemeo kubwa la ajira.

Ifahamike kwamba hakuna mfanyakazi wa serikali ya Tanzania aliyewahi kusajili namba binafsi kwenye gari lake, sasa kupandisha ada hii kwa 100% yaani kutoka mil 5 hadi mil10 ni kuwakomoa wafanyabiashara bila sababu yoyote.

Mtu yeyote aliyewahi kupata uzoefu kwenye biashara ambaye anazijua changamoto zake hawezi kuleta bajeti inayokandamiza sekta hii kwa kiwango ambacho ni hakika kuna viwanda na biashara kadhaa hazitaweza kumudu.

This Nonsense, hata kujibu thread ni kuipa umuhimu usiyostahili ...
 
Mimi sasa kwenye kabiashara kangu ka ukulima naweza kuajiri hata watu 100 na nikawalipa kima cha chini cha 170,000 au 200000 kwa mwezi na walisipe kodi.

Ntakachofanya ntawaongeza marupurupu kidogo.

Pili, sihitaji hiyo personalised number plate kwani ni anasa kwangu.

Tatu, ntatoa risiti kwa kutumia mashine kama serikali inavyotaka.

Nne, ntajikita zaidi kwenye kilimo maana ndiko wafanyabiashara wadogowadogo wanakotakiwa kuelekeza nguvu zao na hawataathika sana na masuala ya kodi kwa bidhaa zilizotajwa.

Wewe endelea kulialia lakini ukitaka hizo personalised plate numbers ulipe hiyo 10m au kuuza vouchers na ukitaka kupata faida ni lazima usajiliwe na uchangie kodi kidogo.
Mkuuu, haya ndio madhara ya wahisani kupunguza misaada kwenye uchumi wetu. Watu walikuwa wanambeza JK kuwa kila siku yuko nje, but ukiwa na hali kama hii ambapo 90% ya wana Dar hawana ajira, unakaaje pale ikulu? By now JK angekuwa kwa Obama anapigia chapuo misaada kwa kuwa kiukweli nchi yetu ni maskini na hata pia nchi kama Israeli au Egypty ambazo ni 'tajiri' bado nazo zinapokea misaada kutoka America.
Mlikuwa mmezoe kupewa misaada na ndo maana mliona maisha ni poa tu hata pasipo kulipa kodi lakini ukumbuke hiyo misaada inatoka kwenye nchi ambazo ni kodi pia. Sasa unatakaje kuendelea alafu usione umuhimu wa kukamliwa kodi? Uliona wapi? Tunahitaji kujitegemea ndio maana tunawajibika kulipa kodi na haya yanayofanyika sahivi ni taswira nchi yetu itakuwaje hapo baadae ili na watoto wetu wafurahie nchi yao lakini pia wakue wakijua kwamba kodi ndio msingi wa maendeleo
 
swali mbona mnalikwepa,huyu jamaa mleta mada kasema kuongezeka kwa hiyo kitu itawaathiri wafanya biashara,nauliza itawaathiri kivipi??

"Personalised number plates" zinanunuliwa na watu walio na uwezo wa kuzinunua.

Wanazinunua kwa sababu mbili, kwanza kujitambusha kwa jamii kwamba wao ni nani na pia wanafanya hivyo(bila kujua kwamba hiyo ni "investment" kwamba wanawekeza maana kuna siku utaweza kufanya mnada wa hiyo (number plate kama za baadhi ya watu maarufu) na ukaiuza kwa gharama kubwa sana.

Hivyo serikali inaweza kuboresha kabisa biashara hii kupitia SUMATRA na kuifanya ni biashara inayoshamiri.

Ila kwa kuanzia ni budi wenye uwezo wa kulipa hicho kiasi wakasaidia Zaidi kwa utengenezaji wa namba hizo.

Sidhani watu kama Diamond au Masanja na wafanyabiashara wakubwa wataathirika sana kama wanapata "spare change" ya kuweza kununua hizo namba.
 
0
Inakuwaje mkuu unalipa tax 36%?

Utakuwa unafanya kazi zaidi ya moja.

Rate yao Denmark si ni 8% ya kipato kabla ya kodi kwenye ajira moja?
Nafanya kazi tatu. Sheria hapa kazi moja usipitishe masaa arubaini kwa wiki. Kwa siku nafanya 14-15 hours except Sundays. Kodi ni kubwa mno.
 
0
nafanya kazi tatu. Sheria hapa kazi moja usipitishe masaa arubain kwa wiki. Kwa siku nafanya 14-15 hours xcept Sundays. Kodi ni kubwa mno.

Naelewa unafanya kazi zaidi ya masaa 40 kwa wiki hivyo unalipa kodi mbili za dharura kwa kazi mbili na ile ya kwanza unalipa rate yenyewe.

Usisahau kula na kupumzika mkuu du!

Cha msingi ujenge ghorofa ya maana Tanzania ya kuja kupumzikia na kula bata ukifikisha miaka 60

Lol
 
Back
Top Bottom