Hivi ATCL kufanya safari za ndege Chato, hakutaliletea hasara kibiashara Shirika hilo?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Siku chache zilizopita tulimsikia Mtendaji Mkuu wa shirika la ndege la ATCL, Ladislaus Matindi akiutangazia Umma wa watanzania kuwa shirika lake la ndege, kuanzia tarehe 9/01/2021 litaanza safari zake za ndege za kwenda kijijini Chato.

Ninavyojua Mimi ni kuwa unapokuwa kwenye biashara ni lazima kwanza ufanye "feasibility study" kujua kama mpango wako utakuletea faida kabla ya kuanza kuutekekeza.

Ninajiuliza hivi hao ATCL wamefanya kweli hiyo "feasibility study" kabla ya shirika hilo kujitumbukiza kufanya safari za ndege kuelekea huko kijijini Chato?

Nina uhakika kuwa safari hizo za shirika za ndege la ATCL kuelekea Chato zitaliingizia hasara shirika hilo, sasa ni kwanini wajitumbukize kwenye huo mradi utakaowaletea hasara?

Je, shirika hilo la ATCL kufanya safari huko Chato ni katika "kujikomba" kwa Rais wa nchi hii, John Pombe Magufuli, ambaye ni nyumbani kwake huko Chato?

Kwa kuwa tunafahamu kuwa CAG wala Bunge halitakuwa na "ubavu" wa kulihoji shirika hilo kama limekula hasara, kwa kuwa shirika hilo limehamishiwa shughuli zake kwenye ofisi ya Rais, ambapo ni "marufuku" kufanya uchunguzi kwenye shughuli zozote ambazo ziko chini ya ofisi hiyo ya Rais!

Ninavyofahamu Mimi ni kuwa shirika hilo likipata hasara ya uendeshaji wake, litapata ruzuku kutoka serikalini, ambazo ni pesa za walipa kodi wa nchi hii, za kwako na za kwangu, kwa hiyo tuna haki ya kuhoji uendeshaji wa shirika hilo.

Nimekuwa nikijiuliza hivi huo ndiyo utawala bora unaozingatia sheria za nchi hii?

Tunamuomba Mtendaji Mkuu wa shirika hilo la ATCL, Stanslaus Matindi ajitokeze hadharani na kutujibia maswali haya kama shirika lake limefanya "feasibility study" ya kutosha na kujiridhisha kuwa kupeleka safari za ndege huko kijijini Chato, kutaliletea faida shirika hilo.
 
Kimei aliwahi kusema wkt anafungua branch ya CRDB kule chato 'kutokana na utafiti alioufanya mh. No.1 imeonekana Chato panafaa kuwekwa bank'.

So kwa sasa hivi hatujajua 'feasibility study' ya kupeleka ndege huko ilifanywa na nani.
Kama ulivyosema wakati ule CRDB kabla ya kufungua tawi lake huko, Mkurugenzi mkuu wa enzi hizo. Kimei alisema"feasibility study" ya kupeleka tawi la CRDB hapo Chato lilifanywa na raia no 1 nchini, kuwa kungeleta manufaa kwa benki yake.

Hebu tujiulize hivi Jiwe ndiye amekuwa CEO wa benki ya CRDB?

Tunataka kujua je ATCL imefanya hiyo "feasibility study" au nao wanategemea maamuzi yafanywe na Jiwe, kabla ya kufanya maamuzi ya kurusha ndege zake huko Chato?
 
Kama ulivyosema wakati ule CRDB kabla ya kufungua tawi lake huko, Mkurugenzi mkuu wa enzi hizo. Kimei alifanya "feasibility study" na kutueleza wananchi kuwa kutaleta manufaa kwa benki yake.

Tunataka kujua je ATCL imefanya hiyo "feasibility study" kabla ya kufanya maamuzi ya kurusha ndege zake huko Chato?
'Mkurugenzi mkuu wa enzi hizo. Kimei alifanya "feasibility study" na kutueleza wananchi kuwa kutaleta manufaa kwa benki yake.'

Kimei hakufanya yeye feasibility study ila anasema ilifanywa na mzee baba mwenyewe.
 
102011131.jpg
 
Kama ulivyosema wakati ule CRDB kabla ya kufungua tawi lake huko, Mkurugenzi mkuu wa enzi hizo. Kimei alifanya "feasibility study" na kutueleza wananchi kuwa kutaleta manufaa kwa benki yake.

Tunataka kujua je ATCL imefanya hiyo "feasibility study" kabla ya kufanya maamuzi ya kurusha ndege zake huko Chato?
Pesa ya Chato inathamani zaidi ya yakwenu.
 
Kama ulivyosema wakati ule CRDB kabla ya kufungua tawi lake huko, Mkurugenzi mkuu wa enzi hizo. Kimei alifanya "feasibility study" na kutueleza wananchi kuwa kutaleta manufaa kwa benki yake...
Mkuu nakupongeza kwa huu uzi, hata ukitaka aseme hivyo, atajitokeza na atasema hivyo. Lakini haimaanishi ni lazima awe anasema ukweli. Kwa sasa serikali kusema uongo ni jambo la kawaida kabisa.
 
Mleta mada
Siku chache zilizopita tulimsikia Mtendaji Mkuu wa shirika la ndege la ATCL, Ladislaus Matindi akiutangazia Umma wa watanzania kuwa shirika lake la ndege, kuanzia tarehe 9/01/2021 litaanza safari zake za ndege za kwenda kijijini Chato.
Ujinga wako ni hapo ulipoandika kijijini Chato

Chato sio kijiji ni Mji
Naona hujawahi hata fika unaandika upumbavu wako hapa
 
5 mingine,sisi tuendelee kupiga kelele mitandaoni huku Kenya Airways,Ethiopian Airways,Rwandaair,Emirates etc etc wakipiga pesa na kufanya biashara kubwa sana huku SADC.tuendelee kulala and i almost forget please keep voting kuhusu kiongozi bora Africa maana sisi kwenye keyboard tumebobea!!
 
5 mingine,sisi tuendelee kupiga kelele mitandaoni huku Kenya Airways,Ethiopian Airways,Rwandaair,Emirates etc etc wakipiga pesa na kufanya biashara kubwa sana huku SADC.tuendelee kulala and i almost forget please keep voting kuhusu kiongozi bora Africa maana sisi kwenye keyboard tumebobea!!
Tumepiga kwa Rais wa Ghana Nana Addo
 
Uongo unaongelea Chato ya Leo au ya miaka ipi? Hii ya sasa yenye hadi mahoteli ya Kitalii?
Mtalii gani mwenye akili zake timamu aende akatalii chato.

Hata wewe mwanalumumba na mfia magufuli ukiulizwa kati ya chato kilimanjaro au Arusha unapenda ukatalii wapi utachagua Arusha au Kilimanjaro na siyo chato.
 
Back
Top Bottom