SimbaMpole123
JF-Expert Member
- Apr 23, 2023
- 5,240
- 4,376
Story ya Yesu
Mathayo anataja vizazi 26 Kati ya Yesu na Daudi, Luka hutaja vizazi 41. Mathayo anaanza kwa mtoto wa Daudi Solomon, wakati Luka anaanza kwa mtoto wa Daudi Nathan. Mathayo anasema Babu yake Yesu anaitwa Yakobo wakati Luka anasema babu yake Yesu Ni Heli. Cha kushangaza zaidi wamefuatilia vizazi vya Yosefu wakati Hana uhusiano na Yesu Kama kweli kazaliwa kwa bikira Mariam.
Mathayo 2:13-15 inasema Yesu alipelekwa Misri baada ya kuzaliwa. Luka 2:22-40 inasema walibaki Bethlehem, wakaenda Jerusalem na kurudi Nazareth, bila kutaja kwenda Misri.
Kifo Cha Yuda kinasemwa na Mathayo 27:5 kuwa alijinyonga Ila Matendo ya Mitume 1:18 inasema alianguka shambani na akafa.
Yohana 19:17 inatuambia alibeba msalaba wake, Marko 15:21-23 inasema Simoni alimbebea msalaba.
Kila kitabu Cha injili kinasema maneno ya Yesu ya mwisho tofauti Kila injili inachanganya tukio la kufufuka kwa Yesu. Marko 16:2 inasema ilikuwa asubuhi, Yohana 20:1 inasema ilikuwa usiku.
Mathayo 28:2 inasema alionekana malaika mmoja, Yohana 20:11-12 inasema malaika wawili. Marko 16:5 inasema mwanaume mmoja Luka 24:4 inasema wanaume wawili.
Hitimisho: Story ya Yesu inasemekana imeibiwa kutoka dini za kihindi, kipersia, kimisri, kigiriki na kirumi. Miungu yao mingi ilizaliwa December 25, ilizaliwa kutoka kwa Bikira, ilifanya miujiza, ilikufa na kufufuka.
Ina maanisha story ya Yesu sio original na iliundwa na watu tofauti tofauti ndo maana hata vitabu vya dini kuhusu yeye vinajichanganya kuhusu maisha yake yalivyokuwa. Kama ukristo mzima unategemea story hii na Ina makosa kihivi, je Biblia litakuwa neno halisi kutoka kwa Mungu au utunzi wa Binadamu?
Mathayo anataja vizazi 26 Kati ya Yesu na Daudi, Luka hutaja vizazi 41. Mathayo anaanza kwa mtoto wa Daudi Solomon, wakati Luka anaanza kwa mtoto wa Daudi Nathan. Mathayo anasema Babu yake Yesu anaitwa Yakobo wakati Luka anasema babu yake Yesu Ni Heli. Cha kushangaza zaidi wamefuatilia vizazi vya Yosefu wakati Hana uhusiano na Yesu Kama kweli kazaliwa kwa bikira Mariam.
Mathayo 2:13-15 inasema Yesu alipelekwa Misri baada ya kuzaliwa. Luka 2:22-40 inasema walibaki Bethlehem, wakaenda Jerusalem na kurudi Nazareth, bila kutaja kwenda Misri.
Kifo Cha Yuda kinasemwa na Mathayo 27:5 kuwa alijinyonga Ila Matendo ya Mitume 1:18 inasema alianguka shambani na akafa.
Yohana 19:17 inatuambia alibeba msalaba wake, Marko 15:21-23 inasema Simoni alimbebea msalaba.
Kila kitabu Cha injili kinasema maneno ya Yesu ya mwisho tofauti Kila injili inachanganya tukio la kufufuka kwa Yesu. Marko 16:2 inasema ilikuwa asubuhi, Yohana 20:1 inasema ilikuwa usiku.
Mathayo 28:2 inasema alionekana malaika mmoja, Yohana 20:11-12 inasema malaika wawili. Marko 16:5 inasema mwanaume mmoja Luka 24:4 inasema wanaume wawili.
Hitimisho: Story ya Yesu inasemekana imeibiwa kutoka dini za kihindi, kipersia, kimisri, kigiriki na kirumi. Miungu yao mingi ilizaliwa December 25, ilizaliwa kutoka kwa Bikira, ilifanya miujiza, ilikufa na kufufuka.
Ina maanisha story ya Yesu sio original na iliundwa na watu tofauti tofauti ndo maana hata vitabu vya dini kuhusu yeye vinajichanganya kuhusu maisha yake yalivyokuwa. Kama ukristo mzima unategemea story hii na Ina makosa kihivi, je Biblia litakuwa neno halisi kutoka kwa Mungu au utunzi wa Binadamu?