Historia ya Yesu siyo halisi ilibuniwa na watu tofauti tofauti

SimbaMpole123

JF-Expert Member
Apr 23, 2023
5,240
4,376
Story ya Yesu

Mathayo anataja vizazi 26 Kati ya Yesu na Daudi, Luka hutaja vizazi 41. Mathayo anaanza kwa mtoto wa Daudi Solomon, wakati Luka anaanza kwa mtoto wa Daudi Nathan. Mathayo anasema Babu yake Yesu anaitwa Yakobo wakati Luka anasema babu yake Yesu Ni Heli. Cha kushangaza zaidi wamefuatilia vizazi vya Yosefu wakati Hana uhusiano na Yesu Kama kweli kazaliwa kwa bikira Mariam.

Mathayo 2:13-15 inasema Yesu alipelekwa Misri baada ya kuzaliwa. Luka 2:22-40 inasema walibaki Bethlehem, wakaenda Jerusalem na kurudi Nazareth, bila kutaja kwenda Misri.

Kifo Cha Yuda kinasemwa na Mathayo 27:5 kuwa alijinyonga Ila Matendo ya Mitume 1:18 inasema alianguka shambani na akafa.

Yohana 19:17 inatuambia alibeba msalaba wake, Marko 15:21-23 inasema Simoni alimbebea msalaba.
Kila kitabu Cha injili kinasema maneno ya Yesu ya mwisho tofauti Kila injili inachanganya tukio la kufufuka kwa Yesu. Marko 16:2 inasema ilikuwa asubuhi, Yohana 20:1 inasema ilikuwa usiku.

Mathayo 28:2 inasema alionekana malaika mmoja, Yohana 20:11-12 inasema malaika wawili. Marko 16:5 inasema mwanaume mmoja Luka 24:4 inasema wanaume wawili.

Hitimisho: Story ya Yesu inasemekana imeibiwa kutoka dini za kihindi, kipersia, kimisri, kigiriki na kirumi. Miungu yao mingi ilizaliwa December 25, ilizaliwa kutoka kwa Bikira, ilifanya miujiza, ilikufa na kufufuka.

Ina maanisha story ya Yesu sio original na iliundwa na watu tofauti tofauti ndo maana hata vitabu vya dini kuhusu yeye vinajichanganya kuhusu maisha yake yalivyokuwa. Kama ukristo mzima unategemea story hii na Ina makosa kihivi, je Biblia litakuwa neno halisi kutoka kwa Mungu au utunzi wa Binadamu?
 
Andika vizuri halafu pangilia hoja zako vizuri ,tutakujibu kwa ufasaha

Nikionacho Ni kwanza huna elimu ya biblia kabla hujaongozwa na Roho mtakatifu

je una elimu ya Biblia kuanzia Lugha zilizotumika ,Mwandishi alilenga nini

Mfano Luka anapoelezea Ukoo wa Yesu, na Mathayo aapoelezea Ukoo wa Yesu

Je una elimu ya Lugha mbalimbali kabla hujakimbilia kwenye Biblia zilizotafsiriwa kwa Kisawahili kinachokosa misamiati mingi.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Story ya Yesu

Mathayo anataja vizazi 26 Kati ya Yesu na Daudi, Luka hutaja vizazi 41. Mathayo anaanza kwa mtoto wa Daudi Solomon, wakati Luka anaanza kwa mtoto wa Daudi Nathan. Mathayo anasema Babu yake Yesu anaitwa Yakobo wakati Luka anasema babu yake Yesu Ni Heli. Cha kushangaza zaidi wamefuatilia vizazi vya Yosefu wakati Hana uhusiano na Yesu Kama kweli kazaliwa kwa bikira Mariam.
Mathayo 2:13-15 inasema Yesu alipelekwa Misri baada ya kuzaliwa. Luka 2:22-40 inasema walibaki Bethlehem, wakaenda Jerusalem na kurudi Nazareth, bila kutaja kwenda Misri.
Kifo Cha Yuda kinasemwa na Mathayo 27:5 kuwa alijinyonga Ila Matendo ya Mitume 1:18 inasema alianguka shambani na
Ukiondoa mbingu na dunia nionyeshe kitu ambacho Mwenyezi Mungu hufanya bila kumhusisha mwanadamu. Mfano, kuzaliwa kwa watoto - tunasema ni Mwenyezi Mungu ndiye anayetutia roho, lakini mtoto anatokana na muunganiko wa mume na mke au mwanaume na mwanamke.

Nyumba ya ibada tunaiita 'nyumba ya Mungu' lakini inajengwa na binadamu. Sadaka tunasema ni ya Mungu, lakini inatolewa na kupewa wanadamu. Vitabu vitakatifu tunasema ni neno la Mungu, lakini vimeandikwa na binadamu.

Hata neno linaposomwa kanisani au mskitini tunasema ni neno la Mungu, lakini linasomwa na mwanadamu. Hivyo, katika mambo mengi Mungu anawashirikisha wanadamu katika kuifanya dunia iwe mahali pema zaidi. Kuna lugha ya kiteolojia inasema: "God did not create a perfect world, but a perfectable world" na ndiyo maana hatuna budi kutunza mazingira kwa kupanda miti na kupunguza uchafuzi wa mazingira, hewa na maji.

Tofauti unazoziona kwenye Biblia ni za kibinadamu/kimaandishi, lakini neno la Mungu ni timilifu maana linahusu 'saving justice, love of God and neighbour, forgiveness, compassion, salvation' na katika haya hakuna kilichokosewa. Hivyo, msingi wa biblia au focus yake ni "ukombozi wa mwanadamu" na siyo makabila mangapi au majina ya akina nani au sehemu gani.
 
Kwanini vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.

Kwamfano tukisoma katika injili ya Mathayo, tunaona, mwandishi anaanza kueleza ukoo wa Yesu tangu Ibrahimu Mpaka Yusufu, lakini alipofika kwa Daudi, aliendelea na kusema Daudi akamzaa Sulemani, (Mathayo 1:6)..Lakini tukirudi tena kwenye Luka hapo hapo tunaona Daudi alimzaa Nadhani (Luka 3:31), Hiyo ni kuonyesha kuwa Yesu alipitia uzao wa Nathani na sio wa Sulemani, kulingana na Luka. Lakini Mathayo anasema alipitia kwenye uzao wa Sulemani, kwanini iwe hivyo?

Pia ukisoma tena mwishoni utaona kulingana na Injili ya Mathayo, baba yake Yusufu alikuwa ni Yakobo, lakini Luka anatuambia baba yake Yusufu alikuwa ni Eli (Luka 3:23).. Naomba ufafanuzi juu ya hili.

JIBU: Ni wazi kuwa ukisoma kitabu cha Mathayo na kile cha Luka utaona kuna tofauti kubwa kwenye vizazi vya ukoo wa Yesu. Luka anatuambia baba wa Yusufu alikuwa ni Eli, na Mathayo inasema babaye alikuwa ni Yakobo. Lakini je! Hilo linamaanisha biblia inajipinga?

Jibu ni la! Ikumbukwe kuwa zamani katika taifa la Israeli walikuwa na desturi ya mtu kumnyanyulia ndugu yake uzao, na mtoto huyo kuitwa kwa jina la marehemu ikiwa mtu huyo atakufa kabla hajapata mtoto.. Soma. Kumbukumbu 25:5-6,

Kwamfano, kama wewe ni mwanaume umezaliwa katika familia, na ukaoa, lakini kwa bahati mbaya ukafa bila kupata mtoto, basi anatafutwa ndugu yako wa karibu aidha katika familia au katika ukoo, Yule aliye karibu zaidi na wewe, kisha anakwenda kumuoa huyo mke wako uliyemwacha, kisha anamzalia mtoto, lakini huyo mtoto hataitwa kwa jina lake, bali ataitwa kwa jina lako wewe marehemu, haijalishi kuwa watoto huyo watakuwa wametoka katika viungo vya mtu mwingine. Na Wanafanya hivyo ili kulitunza jina lako lisipotee.

Na ndicho walichokifanya Israeli wakati ule, ndicho alichokifanya Boazi kwa Ruthu, (ukisoma Ruthu 4:6-9)

Sasa tukirudi katika Injili. Mathayo aliandika Uzao wa Yusufu (Babaye Yesu), akifuata ubaba wa kibaolojia, na Luka aliandika uzao wa Yusufu akifuata ubaba wa kijina.

Ikiwa na maana kuwa Eli pengine alikufa kabla ya kupata mtoto, hivyo Yakobo akamchukua mke wake, na kuzaa naye ili kumtunzia jina, ndipo akamzaa Yusufu. Hivyo kibaolojia Yusufu alikuwa ni mtoto wa Yakobo lakini kisheria alikuwa ni mtoto wa Eli.

Na ndio maana Yakobo hatajwi katika injili ya Luka, bali ni Eli.. Lakini Mathayo anamtaja Yakobo Kama baba wa Yusufu lakini kibaolojia. Hivyo maandiko yapo sawa.
 
YUDA ISKARIOTE ALIJINYONGA AU ALIANGUKA??????????????


Baadhi ya watu Kama wewe mto mada huona kuwa injili zinasigishana. Hii ni kutokana na utofauti wa utoaji taarifa juu ya jambo moja.


Kwa mfano Mathayo anasema YUDA ISKARIOTE ALIJINYONGA wakati Luka katika kitabu cha matendo ya mitume anasema YUDA ISKARIOTE ALIANGUKA.


Hebu tunukuu hivi vitabu:-
1. Mathayo 27:5 unasema "AKAVITUPA VILE VIPANDE VYA FEDHA KATIKA HEKALU, AKAONDOKA, AKAENDA AKAJINYONGA".


2.Matendo 1:18

inasema " BASI MTU HUYU ALINUNUA KONDE KWA IJARA YA UDHALIMU , AKAANGUKA KWA KASI AKAPASUKA MATUMBO YAKE YOTE YAKATOKA".


KWA NINI NI MUHIMU KUTATUA TOFAUTI KAMA HIZI???


Ni MUHIMU sana kwa sababu WAPINZANI WA INJILI NA BIBLIA huyatumia maeneo kama haya kuwapotosha watoto wachanga kiroho na kuwatoa kwenye imani. Mara nyingi huwaambia, ona!!! Biblia sio neno la Mungu, imetungwa tu na watu , huoni wanavyotofautiana katika kuripoti?
Nadhani umeshaelewa shabaha ya ufafanuzi wa maeneo tata katika biblia.



Sasa twende kwenye ufafanuzi. Kabla ya kufafanua tujihoji wenyewe, Je, Mathayo na Luka wanapingana???

JIBU NI HAPANA NA WOTE WAMEELEZA TUKIO MOJA KWA USAHIHI.


Kinachotofautisha utoaji taarifa wa Mathayo na Luka ni MTINDO TU WA UWASILISHAJI.

Mathayo ametoa taarifa ya tukio la kujinyonga au kujitundika mtini kama ilivyozoeleka enzi hizo. Lakini Luka ameeleza tukio lililofuata baada ya kujinyonga yaani kupasuka matumbo.

Ni hivi baada ya Yuda ISKARIOTE kujitundika mtini, hakutolewa ili azikwe bali aliachwa mtini kwa kuwa alionekana kuwa najisi.
Sasa baada ya muda Fulani kupita kamba aliyojitundikia ilikatika naye akaanguka kwa kasi na matumbo yake yakatoka. Kwa hiyo Luka ameripoti kilichotokea baada ya kujinyonga na Mathayo ameripoti tukio la kujinyonga.
Kwa ujumla hakuna msigishano ila kuna taarifa zenye utamu zaidi. Maana kama wote wangeripoti kujinyonga tusingejua kilichotokea baada ya kujinyonga.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanini vizazi vya ukoo wa Yesu vinajipinga katika Mathayo na Luka.

Kwamfano tukisoma katika injili ya Mathayo, tunaona, mwandishi anaanza kueleza ukoo wa Yesu tangu Ibrahimu Mpaka Yusufu, lakini alipofika kwa Daudi, aliendelea na kusema Daudi akamzaa Sulemani, (Mathayo 1:6)..Lakini tukirudi tena kwenye Luka hapo hapo tunaona Daudi alimzaa Nadhani (Luka 3:31), Hiyo ni kuonyesha kuwa Yesu alipitia uzao wa Nathani na sio wa Sulemani, kulingana na Luka. Lakini Mathayo anasema alipitia kwenye uzao wa Sulemani, kwanini iwe hivyo?

Pia ukisoma tena mwishoni utaona kulingana na Injili ya Mathayo, baba yake Yusufu alikuwa ni Yakobo, lakini Luka anatuambia baba yake Yusufu alikuwa ni Eli (Luka 3:23).. Naomba ufafanuzi juu ya hili.

JIBU: Ni wazi kuwa ukisoma kitabu cha Mathayo na kile cha Luka utaona kuna tofauti kubwa kwenye vizazi vya ukoo wa Yesu. Luka anatuambia baba wa Yusufu alikuwa ni Eli, na Mathayo inasema babaye alikuwa ni Yakobo. Lakini je! Hilo linamaanisha biblia inajipinga?

Jibu ni la! Ikumbukwe kuwa zamani katika taifa la Israeli walikuwa na desturi ya mtu kumnyanyulia ndugu yake uzao, na mtoto huyo kuitwa kwa jina la marehemu ikiwa mtu huyo atakufa kabla hajapata mtoto.. Soma. Kumbukumbu 25:5-6,

Kwamfano, kama wewe ni mwanaume umezaliwa katika familia, na ukaoa, lakini kwa bahati mbaya ukafa bila kupata mtoto, basi anatafutwa ndugu yako wa karibu aidha katika familia au katika ukoo, Yule aliye karibu zaidi na wewe, kisha anakwenda kumuoa huyo mke wako uliyemwacha, kisha anamzalia mtoto, lakini huyo mtoto hataitwa kwa jina lake, bali ataitwa kwa jina lako wewe marehemu, haijalishi kuwa watoto huyo watakuwa wametoka katika viungo vya mtu mwingine. Na Wanafanya hivyo ili kulitunza jina lako lisipotee.

Na ndicho walichokifanya Israeli wakati ule, ndicho alichokifanya Boazi kwa Ruthu, (ukisoma Ruthu 4:6-9)


Sasa tukirudi katika Injili. Mathayo aliandika Uzao wa Yusufu (Babaye Yesu), akifuata ubaba wa kibaolojia, na Luka aliandika uzao wa Yusufu akifuata ubaba wa kijina.

Ikiwa na maana kuwa Eli pengine alikufa kabla ya kupata mtoto, hivyo Yakobo akamchukua mke wake, na kuzaa naye ili kumtunzia jina, ndipo akamzaa Yusufu. Hivyo kibaolojia Yusufu alikuwa ni mtoto wa Yakobo lakini kisheria alikuwa ni mtoto wa Eli.

Na ndio maana Yakobo hatajwi katika injili ya Luka, bali ni Eli.. Lakini Mathayo anamtaja Yakobo Kama baba wa Yusufu lakini kibaolojia. Hivyo maandiko yapo sawa.



Sent using Jamii Forums mobile app
Sawa lakini kwa Nini kuwe na tofauti katika namba ya vizazi. Mmoja 26 mwingine 41. Elezea hapo. Na hayo maelezo yako Ni maelezo ya wakristo kujaribu kutetea Biblia. Kubali moja ujumbe wa Mungu umekosewa au hujaandikwa kwa kueleweka au umeandikwa na watu tofauti miaka mingi baada ya Yesu na hivyo inaonyesha kuwa hawajui story halisi. Haya hujaelezea kuhusu sehemu zingine zinazopingana umetetea majina tu
 
YUDA ISKARIOTE ALIJINYONGA AU ALIANGUKA??????????????


Baadhi ya watu Kama wewe mto mada huona kuwa injili zinasigishana. Hii ni kutokana na utofauti wa utoaji taarifa juu ya jambo moja.


Kwa mfano Mathayo anasema YUDA ISKARIOTE ALIJINYONGA wakati Luka katika kitabu cha matendo ya mitume anasema YUDA ISKARIOTE ALIANGUKA.


Hebu tunukuu hivi vitabu:-
1. Mathayo 27:5 unasema "AKAVITUPA VILE VIPANDE VYA FEDHA KATIKA HEKALU, AKAONDOKA, AKAENDA AKAJINYONGA".


2.Matendo 1:18

inasema " BASI MTU HUYU ALINUNUA KONDE KWA IJARA YA UDHALIMU , AKAANGUKA KWA KASI AKAPASUKA MATUMBO YAKE YOTE YAKATOKA".


KWA NINI NI MUHIMU KUTATUA TOFAUTI KAMA HIZI???


Ni MUHIMU sana kwa sababu WAPINZANI WA INJILI NA BIBLIA huyatumia maeneo kama haya kuwapotosha watoto wachanga kiroho na kuwatoa kwenye imani. Mara nyingi huwaambia, ona!!! Biblia sio neno la Mungu, imetungwa tu na watu , huoni wanavyotofautiana katika kuripoti?
Nadhani umeshaelewa shabaha ya ufafanuzi wa maeneo tata katika biblia.



Sasa twende kwenye ufafanuzi. Kabla ya kufafanua tujihoji wenyewe, Je, Mathayo na Luka wanapingana???

JIBU NI HAPANA NA WOTE WAMEELEZA TUKIO MOJA KWA USAHIHI.


Kinachotofautisha utoaji taarifa wa Mathayo na Luka ni MTINDO TU WA UWASILISHAJI.

Mathayo ametoa taarifa ya tukio la kujinyonga au kujitundika mtini kama ilivyozoeleka enzi hizo. Lakini Luka ameeleza tukio lililofuata baada ya kujinyonga yaani kupasuka matumbo.

Ni hivi baada ya Yuda ISKARIOTE kujitundika mtini, hakutolewa ili azikwe bali aliachwa mtini kwa kuwa alionekana kuwa najisi.
Sasa baada ya muda Fulani kupita kamba aliyojitundikia ilikatika naye akaanguka kwa kasi na matumbo yake yakatoka. Kwa hiyo Luka ameripoti kilichotokea baada ya kujinyonga na Mathayo ameripoti tukio la kujinyonga.
Kwa ujumla hakuna msigishano ila kuna taarifa zenye utamu zaidi. Maana kama wote wangeripoti kujinyonga tusingejua kilichotokea baada ya kujinyonga.


Sent using Jamii Forums mobile app
Aaah kudadeki acheni uwongo. Ni story mbili tofauti. Moja inahusu kurudisha fedha na kuninyonya, na nyingine inahusu kununua kiwanja kwa kutumia zile hela(ambazo hakuzirudisha) na kwenye hicho kiwanja akajikwaa akaanguka kwenye mimawe na kupasuka matumbo. Acha kutetea kwa kuunganisha story mbili tofauti.
 
Ukiondoa mbingu na dunia nionyeshe kitu ambacho Mwenyezi Mungu hufanya bila kumhusisha mwanadamu. Mfano, kuzaliwa kwa watoto - tunasema ni Mwenyezi Mungu ndiye anayetutia roho, lakini mtoto anatokana na muunganiko wa mume na mke au mwanaume na mwanamke. Nyumba ya ibada tunaiita 'nyumba ya Mungu' lakini inajengwa na binadamu. Sadaka tunasema ni ya Mungu, lakini inatolewa na kupewa wanadamu. Vitabu vitakatifu tunasema ni neno la Mungu, lakini vimeandikwa na binadamu. Hata neno linaposomwa kanisani au mskitini tunasema ni neno la Mungu, lakini linasomwa na mwanadamu. Hivyo, katika mambo mengi Mungu anawashirikisha wanadamu katika kuifanya dunia iwe mahali pema zaidi. Kuna lugha ya kiteolojia inasema: "God did not create a perfect world, but a perfectable world" na ndiyo maana hatuna budi kutunza mazingira kwa kupanda miti na kupunguza uchafuzi wa mazingira, hewa na maji. Tofauti unazoziona kwenye Biblia ni za kibinadamu/kimaandishi, lakini neno la Mungu ni timilifu maana linahusu 'saving justice, love of God and neighbour, forgiveness, compassion, salvation' na katika haya hakuna kilichokosewa. Hivyo, msingi wa biblia au focus yake ni "ukombozi wa mwanadamu" na siyo makabila mangapi au majina ya akina nani au sehemu gani.
Sasa mi nawezaji chukulia serious ujumbe ambao unamakosa. Afu kingine story yenyewe ya wokovu sijui haimake sense. Huwezi jitoa we mwenyewe kwa we mwenyewe ili uokoe watu uliowatengeneza waovu we mwenyewe na useme umewaokoa kwenda motoni ambapo umetengeneza we mwenyewe. Ni sawa nije na bunduki nikuambie toa hela zako na we ukatoa ukasema Bora umekubali na umeokoka kufa. Haimake sense jaribu kufikiria nje ya box.
 
UNAJIBIWA UNASEMA UONGO

INAONESHA TAYARI UNA MAJIBU YAKO MFUKONI

WENGINE HATUPO TAYARI KUBISHANA

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio.. 😂Sasa unaunganisha story ambazo hazifanani..kwa hiyo kajinyonga afu akaanguka shambani kwake akapasuka utumbo. Ehe zile hela vipi alirudisha au alinunulia kiwanja. Au waandishi walikuwa wapata story nusu nusu kutoka kwa wadau. Vyovyote vile inaonyesha story either imetungwa au haina ukweli. Coz vyote haviwezi kuwa sawa kimoja kimetokea au vyote havijatokea.
 
Sasa mi nawezaji chukulia serious ujumbe ambao unamakosa. Afu kingine story yenyewe ya wokovu sijui haimake sense. Huwezi jitoa we mwenyewe kwa we mwenyewe ili uokoe watu uliowatengeneza waovu we mwenyewe na useme umewaokoa kwenda motoni ambapo umetengeneza we mwenyewe. Ni sawa nije na bunduki nikuambie toa hela zako na we ukatoa ukasema Bora umekubali na umeokoka kufa. Haimake sense jaribu kufikiria nje ya box.
Ukombozi ni zaidi ya fikira zako. Of course, huwezi kuona sense kama hujaelewa kitu. Kama hujafika "Soho" - ni moja ya sehemu maarufu sana jijini London - huwezi kuelewa wala kuelezea shughuli zinazoendelea huko. Huu ni mfano ninaoweza kukupa. Na wewe kama hujafikia level ya kuelewa au hutaki kuelewa, huwezi kuelewa.

Uandishi wa biblia uko kama waandishi wa habari wanavyoweza kuripoti tukio fulani. Mfano, imetokea ajali ya gari na kuna majeruhi 10 na waliopoteza maisha 3. Mwandishi A akifika sehemu ya ajali ataripoti kuna ajali imetokea sehemu X na kuna majeruhi 10 na waliopoteza maisha 3.

Mwandishi B ambaye amefika sehemu ya tukio na kukuta majeruhi na miili ya waliofariki imepelekwa hospitalini ataripoti kuwa kuna majeruhi wengine 3 waliofariki njiani, atasema ajali imetokea sehemu X waliofariki ni 6 na walionusurika ni 7. Angalia namba zimebadilika siyo kimakosa, bali kuendana na habari ilivyo kwa wakati huo na kama kuna mwandishi mwingine wa tatu atakayeenda sehemu ya tukio na kisha hospitalini na kukuta majeruhi wamesharuhusiwa kwenda nyumbani na ndugu wameshachukua miili ya wapendwa wao, naye taarifa yake itakuwa tofauti.

Tofauti hizi za namba na majina baadhi husema "waandishi wetu hawako serious". Lakini ukiangalia kila mwandishi aliripoti tukio kikamilifu kwa jinsi alivyopata taarifa za tukio lenyewe. Mfano, mwandishi wa kwanza hataongelea hospitali, daktari na nesi na mortuary. Lakini mwandishi wa pili ataongelea hayo pia. Mwandishi wa tatu yeye atategemea taarifa yake kwa madaktari na manesi.

Na kama kuna mwandishi wa nne huenda source ya taarifa yake atakuwa mwandishi mwenzake aliyefika sehemu ya ajali na kukuta majeruhi na waliopoteza maisha wakiwa bado sehemu ajali ilipotokea. Kama itakuwa hivyo, mwandishi huyu atatoa taarifa karibu inayofanana na mwandishi wa kwanza - maana anaweza hata kutaja namba za gari na jina la dereva, ambavyo kwa mwandishi wa nne hivi vitu kwake havitakuwa muhimu kwake. Sana sana anaweza kusema alipofika wodini walipolazwa majeruhi alikuta wodi ya wagonjwa imejaa, taarifa ambayo waandishi wengine hawatakuwa nayo pia.

Lakini pia kama waandishi hao watapeleka habari - mfano mmoja kwa wanafunzi wa chuo kikuu, mwingine kwa wakulima, mwingine kwa wavuvi na mwingine kwa wasanii kila mmoja atatumia msamiati au lugha inayoeleweka kwa wale anaowapelekea habari. Huu ni mfano (ingawa siyo mkamilifu) wa namna biblia ilivyoandikwa na tofauti za waandishi katika kuelezea habari wanazowasilisha siyo kosa/tatizo lao, bali ni aina ya habari ilivyopokelewa kutoka kwa chanzo cha habari na kuiweka katika lugha inayoeleweka kwa wale wanaopelekewa habari husika.
 
Ukombozi ni zaidi ya fikira zako. Of course, huwezi kuona sense kama hujaelewa kitu. Kama hujafika "Soho" - ni moja ya sehemu maarufu sana jijini London - huwezi kuelewa wala kuelezea shughuli zinazoendelea huko. Huu ni mfano ninaoweza kukupa. Na wewe kama hujafikia level ya kuelewa au hutaki kuelewa, huwezi kuelewa.

Uandishi wa biblia uko kama waandishi wa habari wanavyoweza kuripoti tukio fulani. Mfano, imetokea ajali ya gari na kuna majeruhi 10 na waliopoteza maisha 3. Mwandishi A akifika sehemu ya ajali ataripoti kuna ajali imetokea sehemu X na kuna majeruhi 10 na waliopoteza maisha 3.

Mwandishi B ambaye amefika sehemu ya tukio na kukuta majeruhi na miili ya waliofariki imepelekwa hospitalini ataripoti kuwa kuna majeruhi wengine 3 waliofariki njiani, atasema ajali imetokea sehemu X waliofariki ni 6 na walionusurika ni 7. Angalia namba zimebadilika siyo kimakosa, bali kuendana na habari ilivyo kwa wakati huo na kama kuna mwandishi mwingine wa tatu atakayeenda sehemu ya tukio na kisha hospitalini na kukuta majeruhi wamesharuhusiwa kwenda nyumbani na ndugu wameshachukua miili ya wapendwa wao, naye taarifa yake itakuwa tofauti.

Tofauti hizi za namba na majina baadhi husema "waandishi wetu hawako serious". Lakini ukiangalia kila mwandishi aliripoti tukio kikamilifu kwa jinsi alivyopata taarifa za tukio lenyewe. Mfano, mwandishi wa kwanza hataongelea hospitali, daktari na nesi na mortuary. Lakini mwandishi wa pili ataongelea hayo pia. Mwandishi wa tatu yeye atategemea taarifa yake kwa madaktari na manesi.

Na kama kuna mwandishi wa nne huenda source ya taarifa yake atakuwa mwandishi mwenzake aliyefika sehemu ya ajali na kukuta majeruhi na waliopoteza maisha wakiwa bado sehemu ajali ilipotokea. Kama itakuwa hivyo, mwandishi huyu atatoa taarifa karibu inayofanana na mwandishi wa kwanza - maana anaweza hata kutaja namba za gari na jina la dereva, ambavyo kwa mwandishi wa nne hivi vitu kwake havitakuwa muhimu kwake. Sana sana anaweza kusema alipofika wodini walipolazwa majeruhi alikuta wodi ya wagonjwa imejaa, taarifa ambayo waandishi wengine hawatakuwa nayo pia.

Lakini pia kama waandishi hao watapeleka habari - mfano mmoja kwa wanafunzi wa chuo kikuu, mwingine kwa wakulima, mwingine kwa wavuvi na mwingine kwa wasanii kila mmoja atatumia msamiati au lugha inayoeleweka kwa wale anaowapelekea habari. Huu ni mfano (ingawa siyo mkamilifu) wa namna biblia ilivyoandikwa na tofauti za waandishi katika kuelezea habari wanazowasilisha siyo kosa/tatizo lao, bali ni aina ya habari ilivyopokelewa kutoka kwa chanzo cha habari na kuiweka katika lugha inayoeleweka kwa wale wanaopelekewa habari husika.
Bana hebu acheni... Sasa ujumbe wa gazeti unafananisha na Biblia. We Kuna mtu ushawahi muomba akutafsirie gazeti. Si unasoma na kulielewa. Basi inaonyesha either Mungu Hana nia nzuri na sisi ndo maana anatumia njia mbovu ya mawasiliano inayoleta Vita na kupotea au hayo maneno Ni ya watu tofauti kutokana na tamaduni zao.
 
Story ya Yesu

Mathayo anataja vizazi 26 Kati ya Yesu na Daudi, Luka hutaja vizazi 41. Mathayo anaanza kwa mtoto wa Daudi Solomon, wakati Luka anaanza kwa mtoto wa Daudi Nathan. Mathayo anasema Babu yake Yesu anaitwa Yakobo wakati Luka anasema babu yake Yesu Ni Heli. Cha kushangaza zaidi wamefuatilia vizazi vya Yosefu wakati Hana uhusiano na Yesu Kama kweli kazaliwa kwa bikira Mariam.

Mathayo 2:13-15 inasema Yesu alipelekwa Misri baada ya kuzaliwa. Luka 2:22-40 inasema walibaki Bethlehem, wakaenda Jerusalem na kurudi Nazareth, bila kutaja kwenda Misri.

Kifo Cha Yuda kinasemwa na Mathayo 27:5 kuwa alijinyonga Ila Matendo ya Mitume 1:18 inasema alianguka shambani na akafa.

Yohana 19:17 inatuambia alibeba msalaba wake, Marko 15:21-23 inasema Simoni alimbebea msalaba.
Kila kitabu Cha injili kinasema maneno ya Yesu ya mwisho tofauti Kila injili inachanganya tukio la kufufuka kwa Yesu. Marko 16:2 inasema ilikuwa asubuhi, Yohana 20:1 inasema ilikuwa usiku.

Mathayo 28:2 inasema alionekana malaika mmoja, Yohana 20:11-12 inasema malaika wawili. Marko 16:5 inasema mwanaume mmoja Luka 24:4 inasema wanaume wawili.

Hitimisho: Story ya Yesu inasemekana imeibiwa kutoka dini za kihindi, kipersia, kimisri, kigiriki na kirumi. Miungu yao mingi ilizaliwa December 25, ilizaliwa kutoka kwa Bikira, ilifanya miujiza, ilikufa na kufufuka.

Ina maanisha story ya Yesu sio original na iliundwa na watu tofauti tofauti ndo maana hata vitabu vya dini kuhusu yeye vinajichanganya kuhusu maisha yake yalivyokuwa. Kama ukristo mzima unategemea story hii na Ina makosa kihivi, je Biblia litakuwa neno halisi kutoka kwa Mungu au utunzi wa Binadamu?
 
Bana hebu acheni... Sasa ujumbe wa gazeti unafananisha na Biblia. We Kuna mtu ushawahi muomba akutafsirie gazeti. Si unasoma na kulielewa. Basi inaonyesha either Mungu Hana nia nzuri na sisi ndo maana anatumia njia mbovu ya mawasiliano inayoleta Vita na kupotea au hayo maneno Ni ya watu tofauti kutokana na tamaduni zao.
Sasa hata kama hujui maana ya mfano basi wewe ni impossible. Ngoja nisipoteze muda wangu.
 
Yesu au Jesus au Yeshua ni mhusika aliyepata kuishi wala sio hadithi za Fasihi.

Kuhusu Kutofautiana Kwa maandiko Hii inatokana na tabia ya Lugha za kiuandishi,
1. Waandishi tofauti wanaoelezea tukio moja.
Pia kuna Waandishi ambao walishuhudia matukio mubashara na wapo waliohadithiwa.

2. Udhaifu wa kusahau
Hata wewe ukiambiwa uandike tukio uliloliona sasa hivi, ukaambiwa uandike tena sehemu nyingine habari ileile kuna uwezekano wa asilimia kubwa kutoandika habari ileile kwenye andiko jipya.

3. Kuzaliwa kwa Yesu sio Jambo la kibilia, Ila ni utaratibu wa kanisa ili kuimarisha na kuboresha Huduma za kanisa na Dini.
 
Back
Top Bottom