Historia ya Noti na Sarafu za Tanzania

Naona Wazanzirabi Walisahauliwa Kabisa Kwenye Hizo Pesa

Picha Ya Nyerere Imekuwa Ya Kudumu Lakini Maalim Abein Amani Karume Haimo Sasa Haya Ndiyo Mamabo Yanayopelekea Muungano Kuonekana Ni Wabara Tuuuu

Nichukieni Sasa Kwa Kusema Hilo
Du hamwishi manung'uniko. Kila kitu manunguniko. alikuwepo twiga mkanungu'nika, kweli ni kisiwa cha wanung'unikao.
 
Kichuguu, Hongera sana kwa kumbukumbu zuri uliyotuletea, umenikumbusha mbali sana hasa nilipoiona noti ya sh. 20 second ver (Pound) ya Nyerere maana hapo ndiyo nilipoanzia kumiliki pesa yangu mwenyewe. Enzi zetu tulikuwa tunaanza kumiliki pesa ukiwa mtu mzima kuanzia miaka 20 na kuendelea ingawa kulikuwa na watu waliokuwa wakimiliki kuanzia miaka 16 lakini walikuwa wanatunziwa na wazazi wao. Na akitaka kuitumia anaomba kwa mzazi wake na iwe kwa matumizi mhimu sana, mzazi anaweza kuitumia na akakutaarifu tu kwamba ameitumia na siyo lazima akurudishie ingawa kuna wazazi wengine walikuwa wanawarudishia watoto wao. ....nakushukuru sana asante kwa kumbukumbu.
 
Du hamwishi manung'uniko. Kila kitu manunguniko. alikuwepo twiga mkanungu'nika, kweli ni kisiwa cha wanung'unikao.

Wanasahau kuwa nchi yao ina uchumi ambao ni asilimia 5 tu ya uchumi wa Tanzania; hata kwa eneo ni chini ya 5%.
 
Nimempigia Mzee Mtei simu akanieleza maoni yake ni kwamba Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ivunjwe na kwamba atapendekeza hivyo atakapopata fursa ya kutoa maoni katika Tume ya Katiba Mpya inayoongozwa na Jaji Warioba. Kwa hiyo wale Wazanzibari wanaotaka Muungano uvunjike wakiona hii assement wanaweza kuhimiza matakwa yao na ya Mtei pia.
 
Hongera sana mkuu, manake noti za miaka ya 1905 nilikuwa hata sijawahi kuona picha zake. Ni historia nzuri iliyotulia na kuelimisha kwa kweli.

Ila tu 1992 ndio hapo wenye mamlaka walipopotea kwa kuchapa noti mpya za TSh. 5,000 (elfu tano) na Tsh. 10,000 (elfu kumi). Kwa kweli walihamasisha sana kuporomoka kwa shilingi, mfumuko wa bei na usumbufu kwa kutafuta chenji hasa vijijini.
 
Wiki chache zilizopita niliwaletea historia ya fedha ya sarafu hapa nchini kwetu nikaahidi kumalizia na historia ya noti. Kwa bahati mbaya majukumu yamenizidi nikashindwa kupata nafasi ya kuiandika ingawa nilikuwa nimeshaifanyia utafiti wa kutosha. Leo hii nimeamua kulivalia njuga ili niikamilishe, samahani sana kwa wanachama kwa vile historia hii ni ndefu kidogo kuliko ile ya sarafu kwa vile noti zilipitia mabadiliko mengi sana kuliko sarafu.

Kwa muda mrefu fedha zilizotumia katika nchi hii zilikuwa ni sarafu. Noti za karatsi zilianza kutumiaka mwaka 1905 wakati wa utawala wa mjerumani kwa upande wa bara. Noti hizo zilitolweka katika thamani ya Rupie 5, 10, 50, 100 na rupie 500 kama ionekanavyo hapa chini. Noti za rupie 500 zilikuwa chache sana na sikufanikiwa kupata picha yake

Rupie 5
doa_5rupien.jpg

Rupie 10
doa_10rupien.jpg

Rupie 50
doa_50rupien.jpg

Rupie 100
doa_100rupien.jpg

Kwa upande wa zanzibar, mwaka huo huo wa 1905, noti za Rupee za kizanzibari zilitolewa katika thamani za Rupee 5, 10, 20, 50, 100 na rupee 500 pia. Kwa bahati mbaya sikuweza kupata picha zake zote, naonyesha mfano wa noti za rupee 5 tano tu niliyofanikiwa kupata.

5 Zanzibari rupee


zz10.jpg


Wakati wa vita ya kwanza ya dunia, serikali ya kijerumani ilitoa noti za dharura ambazo zilikuwa ni za karatasi ya kawaida kabisa. Noti hizi zilikuwa katika thamani za Rupie 1, 5, 10, 20, 50 and Rupie 200 ingawa hizi za Rupie 200 zilikuwa adimu sana na sikufanikiwa kupata picha yake

1 Rupie
doa_1rupiene_1.jpg

5 Rupien
doa_5rupiene.jpg

10 Rupien
doa_10rupiene.jpg

20 Rupien

doa_20rupiene.jpg

50 Rupien

doa_50rupiene.jpg

Noti hizi za dharura zilikuwa hafifu sana na wakati mwingine zilikuwa zinafyatuliwa kwa muhuri tu kama hii hapa chini ya Rupie 1.

doa_1rupiene_3.jpg


Inaelekea kuwa mji wa Tabora ulikuwa na umuhimu wa pili kwa dar es salaama wakati wa serikali ya kijerumani kwa vile unaonyeshwa katika Noti zote. Kama mtakumbuka, ile sarafu ya dhahabu ya Rupie 15 ilikuwa inaitwa "Tabora Pound."


.....INAENDELEA

Asante sana kwa taarifa ya historia ya Tanzania.
 
Kichuguu asante kwa shule nzuri, hii mada nilikuwa sijawahi kuiona, pia nashukuru mods kwa kutengeneza jukwaa la historia. kwa haraka haraka ukiangalia historia ya machapisho ya fedha yetu utaona ni nani aliyeharibu uchumi wa Tanzania.
 
Nikusahihishe mkuu Kichuguu. Hayo majengo nyuma ya noti ya shilingi 1000/= siyo kiwanda cha Tanganyika parkers. hayo ni mgodi wa makaa ya mawe Kiwira uliofunguliwa mwaka 1988 na Mwinyi. Picha hiyo iliwekwa ili kuenzi mafanikio ya kufunguliwa kwa mgodi huo. Hata leo ukienda Kiwira (alikojisevia Mkapa) ndivyo yanavyoonekana. Hilo jengo la kushoto linalofuka moshi ndipo kuna mtambo wa kuzalisha umeme. Pembeni yake kulia unaona kuna lundo la makaa ya mawe. Kakibanda kulia kabisa ni geti la kuingilia mgodini.
 
Wanasahau kuwa nchi yao ina uchumi ambao ni asilimia 5 tu ya uchumi wa Tanzania; hata kwa eneo ni chini ya 5%.
Mzee Edwin Mtei, wewe ndiwe uliyekuwa Gavana wa kwanza wa Benki kuu ya tanzania ilipoundwa baada ya kuvunjika kwa East African Currency Board; je unaweza kutusaidia kuelewa chanzo cha kuvunjika kwa EACB na ni namna gani mlivyoamua kusanifu pesa zetu mpya? Yaani ni nani aliyepewa jukumu la kusanifu pesa zetu mpya na ni vigezo gani vilivyotumika katika usanifu huo. Wewe unajua mengi kuhusu historia ya pesa hiyo kwani tangu mwaka 1966 hadi 1980 ulikuwa kenye nafasi inayohusu pesa hizo. Ni wewe peke yake ambaye sahihi yake inonekana pande zote mbili za pesa hiyo: upande wa waziri na upande wa gavana. Wengine wote ama walikuwa magavana tu (Nyirabu, Rutihinda, Idrisa Rashid, Balali na Benno) au Mawaziri tu ( Amil Jamal, CD msuya, Kighoma Malima, Steven Kibona, Mbilinyi, na waliofuatia)
 
Last edited by a moderator:
Iko wapo pesa ya Tanganyika kabla ya kuchapishwa hizo hela za kijerumani? Sitaki pesa ya Dola ya zanzibar, pesa ya Dola la Tanganyika please??????

Pesa ya Tanganyika ilikuwa ikiitwa vipi kabla ya Pesa hizo za Kijerumani na kizanzibar?

Jee, munayo picha ya pesa hizo za Tanganyika?
 
Iko wapo pesa ya Tanganyika kabla ya kuchapishwa hizo hela za kijerumani? Sitaki pesa ya Dola ya zanzibar, pesa ya Dola la Tanganyika please??????

Pesa ya Tanganyika ilikuwa ikiitwa vipi kabla ya Pesa hizo za Kijerumani na kizanzibar?

Jee, munayo picha ya pesa hizo za Tanganyika?

Zanzibar alikuwa anatawala sultani/mwarabu kwa hiyo kulikuwa na pesa ya zanzibar chini ya sultani/mwarabu. Tanganyika alikuwa anatawala Mjerumani hivyo pesa ya mjerumani ndio iliyokuwa ikitumika.
Ukumbuke pia pesa ya zanzibar haikuanzishwa na watu wa zanzibar kabla mwarabu kuitawala zanzibar, na wala zanzibar haikuwa ikiitwa zanzibar kabla ya sultan/mwarabu kufika pale.
Kwa kifupi si wabara wala wa visiwani, hakuna ambaye alikuwa na pesa yake kabla ya wavamizi wa kijerumani na ki arabu.
 
Andate,

Labda umesahau au hukulijuwa hili, zanaibar walikuwa na sarafu kabla ya kufika kwa sulat Sayyid said Al Saidi 1806 na kufunguwa second zenj empire 1832.

Nakuomba ufungue tena vitabu vya hostoria utaona hilo
 
Back
Top Bottom