Du hamwishi manung'uniko. Kila kitu manunguniko. alikuwepo twiga mkanungu'nika, kweli ni kisiwa cha wanung'unikao.Naona Wazanzirabi Walisahauliwa Kabisa Kwenye Hizo Pesa
Picha Ya Nyerere Imekuwa Ya Kudumu Lakini Maalim Abein Amani Karume Haimo Sasa Haya Ndiyo Mamabo Yanayopelekea Muungano Kuonekana Ni Wabara Tuuuu
Nichukieni Sasa Kwa Kusema Hilo
Du hamwishi manung'uniko. Kila kitu manunguniko. alikuwepo twiga mkanungu'nika, kweli ni kisiwa cha wanung'unikao.
Mzee Mtei,Wanasahau kuwa nchi yao ina uchumi ambao ni asilimia 5 tu ya uchumi wa Tanzania; hata kwa eneo ni chini ya 5%.
Wiki chache zilizopita niliwaletea historia ya fedha ya sarafu hapa nchini kwetu nikaahidi kumalizia na historia ya noti. Kwa bahati mbaya majukumu yamenizidi nikashindwa kupata nafasi ya kuiandika ingawa nilikuwa nimeshaifanyia utafiti wa kutosha. Leo hii nimeamua kulivalia njuga ili niikamilishe, samahani sana kwa wanachama kwa vile historia hii ni ndefu kidogo kuliko ile ya sarafu kwa vile noti zilipitia mabadiliko mengi sana kuliko sarafu.
Kwa muda mrefu fedha zilizotumia katika nchi hii zilikuwa ni sarafu. Noti za karatsi zilianza kutumiaka mwaka 1905 wakati wa utawala wa mjerumani kwa upande wa bara. Noti hizo zilitolweka katika thamani ya Rupie 5, 10, 50, 100 na rupie 500 kama ionekanavyo hapa chini. Noti za rupie 500 zilikuwa chache sana na sikufanikiwa kupata picha yake
Rupie 5
Rupie 10
Rupie 50
Rupie 100
Kwa upande wa zanzibar, mwaka huo huo wa 1905, noti za Rupee za kizanzibari zilitolewa katika thamani za Rupee 5, 10, 20, 50, 100 na rupee 500 pia. Kwa bahati mbaya sikuweza kupata picha zake zote, naonyesha mfano wa noti za rupee 5 tano tu niliyofanikiwa kupata.
5 Zanzibari rupee
Wakati wa vita ya kwanza ya dunia, serikali ya kijerumani ilitoa noti za dharura ambazo zilikuwa ni za karatasi ya kawaida kabisa. Noti hizi zilikuwa katika thamani za Rupie 1, 5, 10, 20, 50 and Rupie 200 ingawa hizi za Rupie 200 zilikuwa adimu sana na sikufanikiwa kupata picha yake
1 Rupie
5 Rupien
10 Rupien
20 Rupien
50 Rupien
Noti hizi za dharura zilikuwa hafifu sana na wakati mwingine zilikuwa zinafyatuliwa kwa muhuri tu kama hii hapa chini ya Rupie 1.
Inaelekea kuwa mji wa Tabora ulikuwa na umuhimu wa pili kwa dar es salaama wakati wa serikali ya kijerumani kwa vile unaonyeshwa katika Noti zote. Kama mtakumbuka, ile sarafu ya dhahabu ya Rupie 15 ilikuwa inaitwa "Tabora Pound."
.....INAENDELEA
Mzee Edwin Mtei, wewe ndiwe uliyekuwa Gavana wa kwanza wa Benki kuu ya tanzania ilipoundwa baada ya kuvunjika kwa East African Currency Board; je unaweza kutusaidia kuelewa chanzo cha kuvunjika kwa EACB na ni namna gani mlivyoamua kusanifu pesa zetu mpya? Yaani ni nani aliyepewa jukumu la kusanifu pesa zetu mpya na ni vigezo gani vilivyotumika katika usanifu huo. Wewe unajua mengi kuhusu historia ya pesa hiyo kwani tangu mwaka 1966 hadi 1980 ulikuwa kenye nafasi inayohusu pesa hizo. Ni wewe peke yake ambaye sahihi yake inonekana pande zote mbili za pesa hiyo: upande wa waziri na upande wa gavana. Wengine wote ama walikuwa magavana tu (Nyirabu, Rutihinda, Idrisa Rashid, Balali na Benno) au Mawaziri tu ( Amil Jamal, CD msuya, Kighoma Malima, Steven Kibona, Mbilinyi, na waliofuatia)Wanasahau kuwa nchi yao ina uchumi ambao ni asilimia 5 tu ya uchumi wa Tanzania; hata kwa eneo ni chini ya 5%.
Iko wapo pesa ya Tanganyika kabla ya kuchapishwa hizo hela za kijerumani? Sitaki pesa ya Dola ya zanzibar, pesa ya Dola la Tanganyika please??????
Pesa ya Tanganyika ilikuwa ikiitwa vipi kabla ya Pesa hizo za Kijerumani na kizanzibar?
Jee, munayo picha ya pesa hizo za Tanganyika?