Historia ya mtandao wa YouTube

Kasomi

JF-Expert Member
Sep 3, 2014
11,036
20,337
Historia ya mtandao wa YouTube

YouTube ilianzishwa na Chad Hurley, Steve Chen na Jawed Karim ambao awali wote walikuwa wafanyakazi wa PayPal. Hurley alisomea urasimu katika Chuo Kikuu cha Indiana ya Pennsylvania, huku Chen na Karim wakisomea kompyuta sayansi pamoja katika Chuo Kikuu cha Illinois huko Urbana-Champaign.

Kulingana na hadithi inayorudiwa mara nyingi katika vyombo vya habari, Chad Hurley na Steve Chen waliibua wazo la YouTube wakati wa miezi ya mwanzo ya 2005, baada ya kukabiliana na matatizo ya kugawa video zilizochukuliwa kweye chakula cha jioni nyumbani kwa Chen huko San Francisco. Jawed Karim hakuhudhuria sherehe hii na alikana kwamba sherehe ilikuwepo, na Chad Hurley alisema kuwa, wazo kuwa YouTube lilianzishwa baada ya chakula cha jioni" pengine lilitiwa nguvu sana na mawazo ya matangazo ili kuunda hadithi yenye kueleweka zaidi."

YouTube ilianza kama teknolojia ya kufadhiliwa, hasa kutoka kwa uwekezaji wa dola za Marekani milioni 11.5 kutoka kwa Sequoia Capital kati ya Novemba 2005 na Aprili 2006. Hapo awali makao makuu ya YouTube yalikuwa upande wa juu wa Pizzeria na mkahawa wa Kijapani katika San Mateo, California. Jina la kikoa chake kilianza kutumika tarehe 15 Februari 2005, na tovuti iliundwa miezi kadhaa iliyofuata. Video ya kwanza kwenye Youtube ilikuwa Me at the Zoo, na mwanzilishi wa onyesho Jawed Karim kwenye San Diego Zoo. Video hii ilipakiwa mnamo tarehe 23 Aprili 2005, na bado yaweza kutazamwa kwenye tovuti.

YouTube iliupatia umma toleo la kwanza la tovuti Mei 2005, miezi sita kabla ya uzinduzi rasmi mnamo Novemba 2005. Tovuti ilikua haraka, na Julai 2006 kampuni ilitangaza kwamba zaidi ya video mpya 65,000 zilikuwa zikipakiwa kila siku, na kwamba tovuti ilikuwa ikipokea watazamaji wa video milioni 100 kwa siku. Kulingana na tarakimu zilizochapishwa na kampuni ya utafiti wa masoko comScore, YouTube inaongoza katika utoaji wa video kwenye mtandao katika Marekani, ikiwa na mgawo wa soko wa karibu asilimia 43 na zaidi ya video bilioni sita zilizotazamwa mnamo Januari 2009. Inakadiriwa kuwa video mpya za jumla ya masaa 20 hupakiwa kwa tovuti kila dakika, na kwamba karibu robo tatu ya nyenzo hizi hutoka nje ya Marekani. Pia inakadiriwa kwamba katika mwaka 2007 YouTube ilitumiwa kipimo data sawa na kiasi kilichotumika kwenye wavuti mzima wa mwaka 2000. Mwezi Machi 2008, kipimo data cha YouTube kiligharimu dola milioni 1 za Marekani kwa siku. Alexa ameipa nafasi ya nne YouTube kama tovuti iliyotumiwa kwa wingi kwenye wavuti, nyuma ya Google, Yahoo! na Facebook.

Uchaguzi wa jina Youtube ulisababisha matatizo kwa vile jina hili lilikuwa likitumika kwa tovuti, ya Yotube Mmiliki wa tovuti, Universal Tube & Rollform Equipment, aliandikisha kesi mahakamani dhidi YouTube Novemba 2006 baada ya kupokea idadi kubwa ya watu waliokuwa wakitafuta YouTube. Universal Tube kwa sasa imebadilisha jina la tovuti yake na kuwa www.utubeonline.com.

Mnamo Oktoba 2006, Google Inc ilitangaza kwamba ilikuwa imeipata YouTube kwa dola bilioni 1.65 katika hisa za Google, agano hili lilikamilishwa tarehe 13 Novemba 2006. Google huwa haitoi tarakimu za kina za gharama ya kutunza YouTube, na mapato ya YouTube ya mwaka 2007 yalibainishwa kuwa "siyo kitu" katika uwekaji jalada. Juni 2008 nakala katika gazeti la Forbes lilitoa makadirio ya mapato ya 2008 kuwa dola milioni 200 za Kimarekani, huku likibaini mafanikio katika mauzo ya matangazo.

Mnamo Novemba 2008, YouTube ilifikia makubaliano na MGM, Lions Gate Entertainment na CBS ambazo ziliruhusu makampuni kutuma filamu nzima na maonyesho ya televisheni kwenye tovuti, yakiandamana na matangazo. Hatua hii imekusudiwa kutoa ushindani kwa tovuti kama Hulu, ambazo huwa na nyenzo kutoka kwa NBC, Fox, na Disney.

Tarehe 9 Oktoba 2009, wakati wa ukumbusho wa tatu kutoka kuchukuliwa na Google, Chad Hurley alitangaza katika chapisho la blogu ya kwamba YouTube ilikuwa inatumiwa na "zaidi ya watazamaji bilioni moja" duniani kote.

Mnamo Novemba 2006, YouTube, LLC ilununuliwa na Google Inc kwa Dola bilioni 1.65, na sasa huendeshwa kama shirika dogo la Google. Kampuni hii ipo San Bruno, California na inatumia teknolojia ya Adobe Flash kuonyesha aina mbalimbali za video zilizotengenezwa na watumiaji, pamoja na vijisehemu vya sinema, vijisehemu vya maonyesho ya runinga, na video za nyimbo, vilevile maudhui ambayo hayajakomaa kama vile video za kublogu na video za asili zilizo fupi.

Maudhui mengi yaliyomo kwenye YouTube yametumiwa na watu binafsi, ingawa vyombo vya habari pamoja na makampuni yakiwemo CBS, BBC, UMG na mashirika mengine hutoa baadhi ya habari zao, kama sehemu ya mpango wa ushirikiano na YouTube.

Watumiaji ambao hawajasajiliwa wanaweza kutazama video, wakati watumiaji waliosajiliwa wanaruhusiwa kutumia na kunakili idadi isiyo na kipimo ya video. Video ambazo zanaweza kuwa na maudhui yaliyo na ujumbe wenye lugha isiyoruhusiwa zinapatikana kwa watumiaji waliosajiliwa tu na wenye umri zaidi ya miaka 18. Kunakili kwa video zenye lugha ya kukashifu, mambo ya ngono, ukiukwaji wa hakimiliki, na habari zinazohimiza uhalifu kumepigwa marufuku katika mkataba wa masharti ya huduma ya YouTube.

Akaunti za watumiaji waliosajiliwa hujulikana kama "channels"

Pia soma Jinsi ya kutengeneza You Tube channel

Mtandao wa Yotube haupatikani baadhi ya Nchi
Nchi kadhaa zimezuia upatikanaji wa YouTube tangu kuanzishwa kwake, ikiwemo Jamhuri ya Uchina, Morocco, na Thailand. YouTube sasa imezibwa nchini Uturuki baada ya utata juu ya video iliyoonekana kuwa yenye matusi kwa Mustafa Kemal Atatürk. Licha ya kuzuiwa huku, Waziri Mkuu wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan alikubali kwa waandishi wa habari kwamba angeweza kupata YouTube, kwani tovuti bado inapatikana huko Uturuki kwa kutumia mbadala wa wazi.

Tarehe 3 Desemba 2006, Iran ilizuia kwa muda upataji wa YouTube, pamoja na tovuti zingine kadhaa, baada ya kuzitangaza kama zinazokiuka maadili ya kijamii na kanuni za vitendo. YouTube ilizibwa baada ya video iliyopakiwa kwenye wavuti kujaribu kumwonyesha Mwajemi/Mwirani anayeiigiza katika filamu za mapenzi akishiriki katika ngono. Kuzuia huku baadaye kuliondolewa na kisha kukarejeshwa Uajemi baada ya uchaguzi wa rais 2009.

Mnamo 23 Februari 2008, Pakistan ilizuiliwa YouTube kutokana na "nyenzo za kukera" kwa imani ya Uislamu , pamoja na kuonyeshwa kwa katuni ya Kideni ya nabii Muhammad. Hii ilisababisha karibu kuzimwa kimataifa kwa tovuti ya YouTube karibu masaa mawili, kwa vile kuzibwa huko kwa Pakistan kulichukuliwa na nchi nyingine. Pakistan iliondoa kizibo chake tarehe 26 Februari 2008. Wapakistani walizunguka kizibo hicho cha siku tatu kwa kutumia programu mtandao wa kibinafsi.

Shule katika baadhi ya nchi zimeziba upatikanaji wa YouTube kutokana na wanafunzi wa kupakia video zenye tabia ya uchokozi, vita vya shuleni,tabia ya ubaguzi wa rangi, na nyenzo zingine zisizofaa.

YouTube kwa sasa ni mtandao wenye watumiaji wengi na vijana wengi wamejiajiri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom