Historia Halisi yenye kusisimua kuhusu rapa Juice WRLD

Scars

JF-Expert Member
Apr 8, 2017
44,442
105,404
Whatsup!

Leo nimeona nije na Biography ya Marehemu Juice Wrld, kwa wasiomjua wapate kumjua na wenye kumjua waweze kuyajua zaidi ambayo hawakuweza kuyajua.

Lakini pia kupitia uzi huu tutaendelea kujuzana hata yale ambayo unayajua na humu sijaweza kuyaandika kwasababu sio rahisi maisha ya miaka 21 kuyaelezea siku moja.

Uzi huu nitauweka kwa vipande ili kuwaepusha wadau na ile kero ya kusoma uzi mrefu usioisha kwasababu hata mimi ni mmoja wa wavivu wakusoma makala ndefu.


*****************************

Juice Wrld alizaliwa tarehe 2 Disemba 1998, majina yake halisi aliyopewa na wazazi wake ni Jarad Anthony Higgins.

Alihitimu High School education kwenye shule ya Homewood-Flossmoor High School iliyopo Illinois Chicago mwaka 2017.
1659640834067.png


Juice Wrld alibahatika kulelewa na mzazi mmoja ambaye ni mama yake anayeitwa Carmella Wallace. Hiyo ni baada ya wazazi kupeana talaka wakati Juice akiwa na umri mdogo wa miaka mitatu.

Mama yake mzazi alikuwa ni mtu wa wa dini sana, alikuwa ni muumini wa dhehebu la kisabato na mara nyingi alikuwa akimkataza Juice Wrld kusikiliza Rap Song au Hip Hop na badala yake alitaka asikilize miziki aina ya rock na pop pekee.

1659640743494.png


Juice Wrld alijifunza kupiga piano akiwa na umri wa miaka minne baada ya kuwa inspired na mama yake mzazi, ambaye baadaye mama yake alimuendeleza kwa kumpa pesa ya ada kwa ajili ya kujifunza zaidi.
1659640699969.png


KWANINI ALIAMUA KUJIITA JUICE WRLD?

Mwaka 1992 Legend wa Hip Hop Tupac Shakur alicheza filamu inayoitwa "Juice" ambayo ilivuma ulimwenguni kote.

Juice Wrld alikuwa ni shabiki wa Tupac au tunaweza sema alikuwa ni role mode wa Pac na alikuwa inspired sana na filamu hiyo lakini pia hata katika style ya maisha alipenda kujifananisha na Tupac, ikiwemo hadi style ya unyoaji nywele.

1659641073817.png


Kupitia filamu hiyo ya Tupac, Juice Wrld akajitungia jina na kujiita Juice The Kidd. Hili ni jina ambalo alianza nalo katika kipindi cha udogoni wakati akirekodi nyimbo zake kwa njia ya simu na kuziweka SoundCloud.

Juice Wrld aliachia nyimbo yake ya kwanza inayoitwa 'Forefer' mwaka 2015. Baadaye alikuja kubadilisha jina na kujiita Juice Wlrd na kutoa ufafanuzi kuwa jina hilo linawakilisha "taking over the world" ambalo lilidumu mpaka siku ya mwisho ya uhai wake.
 
URAIBU WA MADAWA (DRUGS ADDITION)

Juice Wrld alianza kutumia madawa ya kulevya kwa mara ya kwanza aina ya Lean akiwa na umri mdogo kabisa wa miaka 11.

Hali iliyompelekea kupatwa na addiction na kuanza kutumia madawa yenye nguvu zaidi aina ya Percocet na Xanax akiwa na umri wa miaka 15.

Juice Wrld alikuwa ni mtu mwenye uraibu mkubwa wa madawa ya kulevya ilifika hatua hadi akawa anajutia na alifanya majaribio kadhaa ya kuacha lakini ilishindikana.

Siku chache baada ya kifo cha Juice Wrld aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Alexia Smith alihojiwa na kituo cha habari cha Daily Mail alidai kuwa Juice Wrld kwa siku alikuwa anameza vidonge vitatu vilivyo changanywa na madawa aina ya "syrup concoction" au kwa jina lingine "Lean".

July 9 mwaka 2019 Juice Wrld katika account yake ya twitter alipost akimuapia mpenzi wake Ally Lotti kuwa ataachana na matumizi ya madawa.
1659641309049.png


Lakini pamoja na ahadi hiyo bado Juice alikuwa anatumia madawa kisirisiri (ana-cheat). Kwenye wimbo aliomuimbia mpenzi wake uitwao "Blood on My Jeans" amemuelezea mpenzi wake namna alivyokuwa akimcheat kwenye matumizi ya madawa moja ya nukuu ya mashairi yake ni "I value my relationship, it's forever
But I've been cheatin' on the drugs "

Juice Wrld ni msanii ambaye ameelezea circle yake ya maisha kupitia mziki, yani ukitaka kumjua kiundani basi ukisikiliza mashairi ya nyimbo zake utamjua kiundani sana.

Swala la kuacha madawa kwa Juice Wrld lilikuwa ni swala gumu sana, wale watu waliojaribu kumshauri aachane na madawa, kupitia wimbo wake "To the grave" au kwa jina lingine "Feelings" aliwapa majibu kuonesha namna ambavyo sio rahisi kuacha

"They tell me that it's easy to quit it
Funny comin' from someone that's not dealing with it, it
Wait, I'm getting a call from my dealer again"
 
SAFARI YA MUZIKI NA UMAARUFU

Juice Wrld alikuwa na kipaji kikubwa cha kuimba na uwezo wa ku freestyle, alikuwa akifanya battle challenge na wanafunzi wenzake kipindi yuko shuleni.

Mwaka 2018 Juice Wrld alishika namba 2 katika chat ya billboard ya top 100 kwa kibao chake cha "Lucid dreams" kutoka kwenye album yake ya kwanza inayokwenda kwa jina la "Goodbye & Good Riddance" kilichopelekea kujipatia umaarufu na kujulikana sana.

juicewlrd999-20211202-0006.jpg


"All girls are the same" ni moja ya nyimbo zilizomuongezea zaidi umaarufu na kumfanya ajulikane pande tofauti tofauti za ulimwengu.
juicewlrd999-20211202-0003.jpg


Pia alijizolea umaarufu kupitia wimbo wake wa 'Legends" alioimba kwa ajili ya kuwaenzi XXXTENTACION na Lil Peep aliouachia June 19, 2018 yani siku moja baada ya kifo cha XXXTENTACION.
 
MAISHA YA KIMAHUSIANO

Juice Wrld huwenda alishawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanawake wengine kipindi ambacho hana umaarufu lakini mahusiano ambayo yana fahamika, aliwahi ku date na mabinti wawili katika nyakati tofauti tofauti.

Mwanamke wake wa kwanza alikuwa anaitwa Alexia Smith au Starfire kama alivyokuwa akijiita, huyu alianza naye mahusiano mwaka 2018 ambapo walikuwa wakiishi pamoja na baadaye Juice alikuja kuthibitisha kuwa Starfire ni mpenzi wake

Picha chini ikimuonesha Juice Wrld akiwa na Alexia Smith au starfire

1659688323917.png
.

Japokuwa Starfire alikuwa na ukaribu na Juice na kuwa na inspiration kwenye shughuli zake za kimuziki lakini kwa bahati mbaya mahusiano hayo yalivunjika Novemba 2018 na Juice kuanza ukurasa upya na mwanamke mwingine aitwaye Ally Lotti.

Ally Lotti alikuwa ndio mwanamke pekee aliyeweza kudumu naye mpaka dakika ya mwisho ya uhai wake.

Na huyu binti pichani ndio Ally Lotti
1659650634289.png



1659650547769.png

Ni mwanamke aliyeonekana kumpenda sana licha ya kumshirikisha kwenye video yake ya "Bandit" aliyomshirikisha NBA Young boy alimualika mpenzi wake kama video Queen lakini pia mara kadhaa alipokuwa aki perfom jukwaani alimuita na kuwatagazia mashabiki jinsi gani ana mpenda.
1659642216297.png
 
UMAUTI

Disemba 8, 2019 siku sita kupita baada ya kusherekea siku yake ya kuzaliwa, na miezi mitatu kupita tangu amzike baba yake mzazi. Rapper Juice Wrld alikodi ndege binafsi (private jet) akitoka Los Angels (LA) kuelekea Chicago.
1659642519660.png


Ndege ilipokuwa inakaribia kutua Chicago, inasemekana marubani wa ndege hiyo walitoa taarifa FBI na Federal Aviation Administration (FAA) kuwa abiria waliomo ndani wana silaha na madawa ya kulevya.

FBI na Federal Aviation walikuwa na mbwa wa kunusa (sniffing dogs) na vifaa vya kunasa silaha (metal detectors) walikuwa wameisha jiandaa na wanasubiri ndege itue tu waanze kusachi.

Juice Wrld alipoona ma afisa wa FBI na FAA ali panick baada ya kujua kuwa angekamatwa na madawa hayo basi angeenda kutumikia kifungo cha miaka mingi gerezani.

Alikuwa kwenye panic ya hali ya juu na wazo la haraka lililomjia akilini ni kumeza (swallow) zile pounds sabini tofauti tofauti za madawa. Ambazo zilikuwa ni aina ya Opioid Percocet, Codeine na lean.

Klikuwa ni kiwango kikubwa cha mno alicho meza kwa lengo la kuficha ushahidi ili hao ma ofisa wasiweze kumkuta na vidhibiti.

Lakini Juice Wrld baada ya kubugia hayo madawa alianza kuteseka na kupelekea kupatwa na cardiac arrest kabla ya kupelekwa hospitali.

Juice Wrld alikuwa akivuja damu masikioni, puani na mdomoni ambapo aliwaishwa kituo cha afya cha karibu kinachoitwa Advocate Christ Medical Center ambapo Jumapili majira ya saa 9:15 usiku aliripotiwa kuwa amefariki.

January 22, 2020 ilitolewa ripoti ya vipimo vya mwili wa Juice vikionesha kiwango kikubwa cha sumu itokanayo na codeine na oxycodone.

Na hii ndio report iliyotolewa kuonessha sumu iliyokutwa mwilini baada ya kuji overdose na madawa
1659650770950.png



Hili ndio kaburi lake
1659691212565.png
 
Hiki ni kipande cha Freestyle akipita na beats la loose it by Eminem

Freestyle hii aliigonga zaidi ya lisaa akipita na beats tofauti tofauti za Eminem

 
Mambo ambayo yanaweza kukushangaza kuhusu JUICE WRLD

Kupitia nukuu ya mashairi yake kutoka kwenye kibao cha Legends yanayosema

"What's the 27 Club? We ain't making it past 21
I be goin through paranoia
So I always gotta keep the gun"


Mashairi hayo yamekuwa yakihusianishwa moja kwa moja na kifo chake kwa madai alijitabiria kufa katika umri wa miaka 21.

Ikumbukwe kuwa 27 club inawakilisha kundi la watu maarufu waliofariki wakiwa na umri wa miaka 27

Ukiachana na hiyo pia kuna mashairi tata ambayo nayo ni tragically kuhusiana na kifo chake

Kutoka kwenye wimbo wake wa all girls are the same nanukuu mashairi yake

"All this jealousy and agony that I sit in
I'm a jealous boy, really feel like John Lennon"


Sasa ili upate concept vizuri ngoja nikuongezee na nukuu hii ya mashairi kutoka kwenye wimbo wake wa "Too many"

The drug-abusers, codeine users that been hurt by women (Yeah)
I'm a drug-abusing, codeine using, modern-day John Lennon


Ukiangalia hizo nukuu mbili utagundua kuna jina la mtu limetajwa mara mbili hapo John Lennon

Huyu John Lennon ni nani?

John Lennon ni muimbaji na muandishi wa nyimbo za kingereza alizaliwa October 9 mwaka 1940

1659647938676.png


Juice Wrld na John Lennon wote wana historia moja ya utotoni inayofanana.

Baba yake Juice Wrld yani Higgins alimpa talaka mke wake (mama mzazi wa Juice Wrld) wakati Juice Wrld ana miaka mitatu.

Baba yake na John Lennon naye alisimamisha uhusiano wake na mkewe miaka mitatu baada ya John Lennon kuzaliwa.

John Lennon aliiuwawa tarehe 8 Disemba mwaka 1980

Hapo ndio kwenye pointi yangu

Juice Wrld ambaye katika mashairi yake amemtaja mara nyingi John Lennon ukumbuke naye alikufa tarehe 8 Disemba kama John Lennon, je hiyo ni coincidence?
 
999

Ilikuwa ni a.k.a yake aliyoigeuza kutoka kwenye kitabu cha mwisho cha biblia kilipotaja chapa ya 666

Ambapo yeye aliigeuza na kuwa 999 na kuipa tafsiri mpya ikiwa na maana ya "kuchukua jambo lolote baya, hali yeyote ngumu unayopitia, na kuigeuza kuwa jambo chanya litakoweza kukusukuma ukasonga mbele zaidi"

666 ni ishara ya jambo baya so yeye akaipindua kuwa 999 na kuibariki kuifanya liwakilishe jambo zuri
 
Juice Wrld anatajwa kama msanii wakipekee ambaye alikuja na style yake ya kiutofauti katika industry ya emo rap

Ambapo awali ilizoeleka kuwa na waimbaji wanaozungumzia pesa na wanawake

Kupitia kibao chake cha "Wishing well" unaweza kuona picha inayoelezea maisha yake kiufupi pamoja na tatizo la msongo wa mawazo ambalo limekuwa likimsumbua tangu utotoni.
 
fame is the worst drug known to man It’s stronger than, heroin (jay z)

Jumlisha na umri mdogo halafu ana pesa.
Kupitia wimbo wake wa "Wishing Well" Juice Wrld anamjibu Jayz

If it wasn't for the pills, I wouldn't be here
But if I keep taking these pills, I won't be here

I just told y'all my secret,
It's tearing me to pieces
I really think I need them
I stopped taking the drugs and now the drugs take me
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom