Kwanza naomba nieleweke kwamba naposema hili ni Taifa la Wajinga SITUKANI isipokuwa Ujinga kwa kiswahili safi ni kutoelewa ama kutoelimika..Hivyo kama watu watafahamishwa ama kuelimishwa wataondokana na Ujinga huo. Ujinga sii tusi kwa mwenye kutaka kuelimika ila laweza kuwa tusi kwa yule anayefikiria - Anajua kumbe hajui.
Kwa muda wa miezi mitano niliyokaa Tanzania nimegundua mengi sana ambayo yanapelekea sababu nyingi sana za Taifa letu kuendelea kugubikwa ktk usingizi mzito wa ujinga na ushindi kwa viongozi wabovu kuendelea kuchaguliwa..
Kibaya zaidi ni kwamba sifa zote mbaya za Maendeleo ya uchumi na Uongozi ndizo hutukuzwa na kupongezwa na wananchi ikiwa ni pamoja na wasomi wetu... Hakika Adui mkubwa wa Tanzania ni UJINGA kabla hata ya UMASKINI..tusipofuta kwanza Ujinga hatuwezi futa Umaskini na ndio maana siku zote Mapinduzi ya kijamii hutanguliwa na siasa zenye malengo ya kufuta Ujinga waliolishwa wananchi wapate kutambua haki zao.
Ndivyo walivyofanya vyama vyetu vya TAA kumwondoa mkoloni, KANU Kenya, Zimbabwe, South Afrika na kwingineko ambako awali wananchi wake chini ya kutawaliwa walifikiri kwamba hili lilikuwa jambo la kawaida kabisa..Na huko South, miaka ya 70 Apartheid ilikubalika kuwa ni haki ya watawala.
Kwa Tanzania nadhani imefika wakati wananchi wanapaswa kuambiwa Ukweli, ukweli kwamba haki zao zinachukuliwa na kwamba nchi yetu imefikia mahala ambapo itakuwa vigumu sana kukomboleka. Tanzania imezama ktk dimbwi la Ukoloni mamboleo na hakika hoja za kurudishwa kwa Azimio la Arusha, zimepokelewa kwa upinzani mkubwa sana, kiasi kwamba hata wasomi wenye elimu ya juu wameshindwa kuchambua mchele toka ktk pumba kwa sababu Azimio kama hili litawagusa hata wao moja kwa moja.
Hakuna Mtanzania hata mmoja anayependa Azimio la Arusha lije kama lilivyokuwa kuturudisha ktk Ujamaa ambao serikali inatawala njia zote za Uchumi. Hakika swala hili limerudishwa tu kwa kuzingatia kwamba Azimio la Zanzibar liliondoa Miiko na Maadili ya viongozi. Miiko na maadili ambayo hata ktk serikali za kibepari iwe Uingereza ama Marekani ipo na inasimamiswa kwa uangalifu mkubwa sana. Leo sisi tunapozungumzia miiko na maadili ya viongozi tunashindwa kabisa kutoa maelekezo isipokuwa viongozi wanapaswa kuitaarifu serikali mali na mapato yao kila mwaka.
Nilisema wananchi wanakila sababu ya kuikataa CCM.. nilisema Watanzania wanakila sababu ya kutoichagua CCM lakini hakuna kitakachowezekana ikiwa hao hao wananchi hawafahamu baya ama nini ni haramu. CCM inatumia kila mbinu za utawala dhalimu kuwagawa wananchi ktk makundi ya ushabiki.. Hii ni sumu kali inayopandikizwa kiasi kwamba mustakabali wa nchi unageuzwa kuwa unazi na ushabiki wa mpira wa miguu, kina Simba na Yanga au Arsenal na ManU, hivyo kupoteza kabisa maana ya Utawala mzuri isipokuwa hoja kubwa inabadilika na kuwa Ushindi ndio muhimu. Kiongozi wa juu anatazamwa kama kocha wa mpira, hao kina Maximo, Phiri na Wenger ktk kutafuta Ushindi na hakika hawa ndio watu maarufu Tanzania kuliko kiongozi mwingine yeyote duniani ukiondoa Obama, rais wa Marekani ambaye weusi wake ndio imechukuliwa kuwa sababu kubwa ya ubora wake.
Leo nitazungumzia swala moja kubwa, kwa nini tunahitaji kuiondoa CCM madarakani. Kuna Ujinga gani unaendelea kuwadidimiza wananchi ktk Ujinga zaidi.
Wananchi wenzangu, Tanzania ni nchi maskini lakini umaskini wetu unatokana na Uongozi mbovu -Period. Uongozi mbovu ni ule usiokuwa na malengo, usiokuwa na jukumu la kutekeleza mazuri yenye kuiletea sifa na maendeleo nchi yao hata kama nchi yenyewe ni ya Wajinga. Kuwa na Uzalendo, uchungu kwa kila tukio ambalo linamdhalilisha mwananchi iwe ndani ama nje ya nchi. Kutambua nini thamani ya kujitawala,nini haki ya Uraia baada ya kugombea Uhuru toka kwa mkoloni. Uhuru ni pamoja na Umoja wa wananchi wake ktk haki zote za kujitawala pasipo kubaguliwa kama ilivyokuwa awali chini ya mkoloni.
Pamoja na hayo yote tuwaambie wananchi ukweli hata kama ukweli huu utaondoa uadilifu kwa wananchi ambao ni watumwa ndani ya Uhuru wao...
Tanzania yetu imegeuka kuwa uwanja wa fisi.. Tanzania ni nchi pekee ambayo kila kitu kinauzika utafikiri nchi iko vitani. Hakuna standard yoyote wala ramani ya Tanzania ya kesho (blueprint). Je, nikikwambia kwamba Dar- es- salaam mji wetu mkuu unanuka! -Utaamini? mathlan Ukiambiwa Dar es Salaaam ni mji wa tisa duniani kwa Uchafu utajisikiaje? pengine hutaamini takwimu hizi hadi ufahamu ni nani aliyezitoa. Akiwa mzungu kuna ukweli kidogo kuliko mtu mweusi..Mgeni ataambiwa ana chuki pasipo watu kujiuliza hivi kwa nini Dar imekuwa ktk nafasi hiyo.
Tuiondoe CCM kwa sababu ni chama kinachowapotosha wananchi. Hakina nia nzuri na wananchi wake zaidi ya kutafuta Ushindi ktk kila Uchaguzi. Agenda kubwa ya chama CCM ni kupata ushindi... kwao Ushiondi ni lazima utafikiri hii ni michuano ya soka kombe la dunia. Lakini Umaskini unatazamwa kama sii jukumu la chama ila mwenyezi Mungu akipenda. Na wapo wananchi wanaaamini kabisa kwamba maendeleo ya Tanzania ni hadi pale Mungu akipenda,zile siasa za kuenezwa ukoloni zinarudi kwa mbinu mpya kabisa wakitumia maamdiko ya dini kuhalalisha Umaskini wetu.
Hakuna kiongozi CCM nafahamu kwa nini sisi leo hii ni maskini bado... kama yupo hajajitokeza na sidhani kama ukimuuliza anaweza jibu hadharani. Kwa kutofahamu sababu ya umaskini wetu sijui tutaweza vipi kuondokana na umaskini wenyewe tukiwa chini ya viongozi wasiofahamu kwa nini sisi ni maskini.
Na ndio maana utaona mikakati yote ya kuondoa Umaskini nchini imeshindwa. MKUKUTA na program nyingine zote zimeshindwa kuzaa matunda kwani yameweza kutugawa zaidi ktk makundi. Katika sehemu zilipofanikiwa MKUKUTA, sehemu nyingine mbili zimeibuka kurudi chini zaidi..ni sawa na chura anayeruka hatua mbili nakuteleza hatua tatu nyuma ama sawa na kujenga Ukuta juu ya msingi uliochukuliwana maji..
Umaskini wetu haufanani kabisa na nchi tajiri inayofilisika..wala haufanani kabisa na umaskini unaotokana na kutojaliwa rasilimali, maliasili kama ardhi bali ni kutotambua makosa ya wazi yanayojitokeza chini ya uongozi mbaya. Mfano mkubwa ni viongozi wetu kutotambua kina cha umaskini wenyewe..kuna wakati ati tunajifananisha na nchi zilizofilisika kiuchumi hali sisi hatujawahi kutajirika. Na kibaya zaidi tunapata ushauri toka kjwa wataalam ambao hawajawahi kuwa maskini wala kusomea elimu inayo deal na nchi iliyopo ktk vita vya umaskini..
Hata wataalam wa uchumi wanaweza tu kutumia Free market economy pale pasipokuwa na vita ya umaskini. Mahitaji yanapokuwa bado ni mahitaji (demand) na sio ni Shida (neccesity). Mdumo wa kibiashara wa demand na supply utaonyesha tu mafanikio ikiwa hakuna vita. Kwa mfano leo hii huko Kongo kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe vitu muhimu ni adimu..Sukari na chunvi zinauzwa kwa dollar zisizopungua 10 kwa kilo. Sasa ukianza kujiuliza maswala ya purchasing power na kutumia mahesabu ya demand na supply kupata majibu ya maendeleo hapo ndipo utakwama.
Sasa tazama kwetu ambako uwezo wetu wa kuzalisha ni mdogo kulingana na mahitaji..imefikia hadi kila kitu ni shida kubwa isipokuwa kwa misaada ama kuagiza mali toka nje kukidhi pengo kubwa la mahitaji ya wananchi. Hivyo, market economy inaweza tu kutoa matunda ya kiuchumi ikiwa uzalishaji wa ndani unakidhi ama unafuata mahitaji ndani na nje na sii kuagiza mali toka nje kukidhi mahitaji ya ndani - uzalishaji hakuna na ndipo makosa yanapoanza kutumika..
Jambo jingine kuu la umaskini wetu ni ile imani kwamba Umaskini ni swala la baadhi ya watu na baadhi ya sehemu.. Kama ndivyo basi hapakuwa na sababu ya sisi kuitwa nchi maskini. Utajiri wa nchi yeyote ama mtu binafsi unategemea nguvu ya ununuzi wa huyo maskini. Lakini pia imani potovu ya kwamba maskini akipewa fursa ataweza kutajirika pasipo kuangalia neema za vipaji na elimu ambazo pekee ndizo zinamwezesha mbunifu kutazama mahitaji ya soko..
Leo Masai naye kaingizwa ktk kilimo kwanza akipewa ardhi kulima mahindi badala ya kumwendeleza mmasai kwa kumwagilia ardhi yake ipate mimea ya malisho ya ng'ombe wake. Ugonvi mkubwa unajitokeza ktk vipaumbele vya wizara mbili tofauti. Kilimo against Mifugo na Uvuvi nani mwenye haki na ardhi ya mwenzake ktk mpango huu wa kilimo kwanza.
Labda kwa leo nimezungumza ya kutosha kwa kuanzia nisije wachosha wasomaji ila nitamalizia kidogo kwa kusema hivi.. wananchi wenzangu hatuna sababu ya kuwachagua CCM ikiwa wao hawafahamu kwa nini bado nchi yetu ni Maskini.. Uchanga wa nchi hauwezi kuwa sababu hata kidogo wala Ujamaa wa mwalimu hauwezi kuwa sababu kwani tumeona Vietnam na rwanda wakitupita kama tumesimama. Hawa wote walitambua kwanza kina cha Umaskini wao, wakayafahamu makosa yao kiutawala, waka enzi utawala bora kwa kuwaadhibu wale wote waliokiuka miiko na maadili ya Uongozi. Na Mwisho, mustakabali wa nchi yao kuwa mbele ya viti vyao majumbani ama ktk vyama vyao vya siasa.
Dira ya Taifa ni lazima iwe na AZIMIO pasipo hivyo tutakwenda hovyo hovyo kama mji wa Dar unavyojengwa. Upimaji ramani ya mji hutokea baada ya watu kujenga nyumba zao.. Barabara na mifereji hujengwa baada ya kila kitu kwisha jengwa.. Hii ndio Tanzania ya CCM.
Kwa muda wa miezi mitano niliyokaa Tanzania nimegundua mengi sana ambayo yanapelekea sababu nyingi sana za Taifa letu kuendelea kugubikwa ktk usingizi mzito wa ujinga na ushindi kwa viongozi wabovu kuendelea kuchaguliwa..
Kibaya zaidi ni kwamba sifa zote mbaya za Maendeleo ya uchumi na Uongozi ndizo hutukuzwa na kupongezwa na wananchi ikiwa ni pamoja na wasomi wetu... Hakika Adui mkubwa wa Tanzania ni UJINGA kabla hata ya UMASKINI..tusipofuta kwanza Ujinga hatuwezi futa Umaskini na ndio maana siku zote Mapinduzi ya kijamii hutanguliwa na siasa zenye malengo ya kufuta Ujinga waliolishwa wananchi wapate kutambua haki zao.
Ndivyo walivyofanya vyama vyetu vya TAA kumwondoa mkoloni, KANU Kenya, Zimbabwe, South Afrika na kwingineko ambako awali wananchi wake chini ya kutawaliwa walifikiri kwamba hili lilikuwa jambo la kawaida kabisa..Na huko South, miaka ya 70 Apartheid ilikubalika kuwa ni haki ya watawala.
Kwa Tanzania nadhani imefika wakati wananchi wanapaswa kuambiwa Ukweli, ukweli kwamba haki zao zinachukuliwa na kwamba nchi yetu imefikia mahala ambapo itakuwa vigumu sana kukomboleka. Tanzania imezama ktk dimbwi la Ukoloni mamboleo na hakika hoja za kurudishwa kwa Azimio la Arusha, zimepokelewa kwa upinzani mkubwa sana, kiasi kwamba hata wasomi wenye elimu ya juu wameshindwa kuchambua mchele toka ktk pumba kwa sababu Azimio kama hili litawagusa hata wao moja kwa moja.
Hakuna Mtanzania hata mmoja anayependa Azimio la Arusha lije kama lilivyokuwa kuturudisha ktk Ujamaa ambao serikali inatawala njia zote za Uchumi. Hakika swala hili limerudishwa tu kwa kuzingatia kwamba Azimio la Zanzibar liliondoa Miiko na Maadili ya viongozi. Miiko na maadili ambayo hata ktk serikali za kibepari iwe Uingereza ama Marekani ipo na inasimamiswa kwa uangalifu mkubwa sana. Leo sisi tunapozungumzia miiko na maadili ya viongozi tunashindwa kabisa kutoa maelekezo isipokuwa viongozi wanapaswa kuitaarifu serikali mali na mapato yao kila mwaka.
Nilisema wananchi wanakila sababu ya kuikataa CCM.. nilisema Watanzania wanakila sababu ya kutoichagua CCM lakini hakuna kitakachowezekana ikiwa hao hao wananchi hawafahamu baya ama nini ni haramu. CCM inatumia kila mbinu za utawala dhalimu kuwagawa wananchi ktk makundi ya ushabiki.. Hii ni sumu kali inayopandikizwa kiasi kwamba mustakabali wa nchi unageuzwa kuwa unazi na ushabiki wa mpira wa miguu, kina Simba na Yanga au Arsenal na ManU, hivyo kupoteza kabisa maana ya Utawala mzuri isipokuwa hoja kubwa inabadilika na kuwa Ushindi ndio muhimu. Kiongozi wa juu anatazamwa kama kocha wa mpira, hao kina Maximo, Phiri na Wenger ktk kutafuta Ushindi na hakika hawa ndio watu maarufu Tanzania kuliko kiongozi mwingine yeyote duniani ukiondoa Obama, rais wa Marekani ambaye weusi wake ndio imechukuliwa kuwa sababu kubwa ya ubora wake.
Leo nitazungumzia swala moja kubwa, kwa nini tunahitaji kuiondoa CCM madarakani. Kuna Ujinga gani unaendelea kuwadidimiza wananchi ktk Ujinga zaidi.
Wananchi wenzangu, Tanzania ni nchi maskini lakini umaskini wetu unatokana na Uongozi mbovu -Period. Uongozi mbovu ni ule usiokuwa na malengo, usiokuwa na jukumu la kutekeleza mazuri yenye kuiletea sifa na maendeleo nchi yao hata kama nchi yenyewe ni ya Wajinga. Kuwa na Uzalendo, uchungu kwa kila tukio ambalo linamdhalilisha mwananchi iwe ndani ama nje ya nchi. Kutambua nini thamani ya kujitawala,nini haki ya Uraia baada ya kugombea Uhuru toka kwa mkoloni. Uhuru ni pamoja na Umoja wa wananchi wake ktk haki zote za kujitawala pasipo kubaguliwa kama ilivyokuwa awali chini ya mkoloni.
Pamoja na hayo yote tuwaambie wananchi ukweli hata kama ukweli huu utaondoa uadilifu kwa wananchi ambao ni watumwa ndani ya Uhuru wao...
Tanzania yetu imegeuka kuwa uwanja wa fisi.. Tanzania ni nchi pekee ambayo kila kitu kinauzika utafikiri nchi iko vitani. Hakuna standard yoyote wala ramani ya Tanzania ya kesho (blueprint). Je, nikikwambia kwamba Dar- es- salaam mji wetu mkuu unanuka! -Utaamini? mathlan Ukiambiwa Dar es Salaaam ni mji wa tisa duniani kwa Uchafu utajisikiaje? pengine hutaamini takwimu hizi hadi ufahamu ni nani aliyezitoa. Akiwa mzungu kuna ukweli kidogo kuliko mtu mweusi..Mgeni ataambiwa ana chuki pasipo watu kujiuliza hivi kwa nini Dar imekuwa ktk nafasi hiyo.
Tuiondoe CCM kwa sababu ni chama kinachowapotosha wananchi. Hakina nia nzuri na wananchi wake zaidi ya kutafuta Ushindi ktk kila Uchaguzi. Agenda kubwa ya chama CCM ni kupata ushindi... kwao Ushiondi ni lazima utafikiri hii ni michuano ya soka kombe la dunia. Lakini Umaskini unatazamwa kama sii jukumu la chama ila mwenyezi Mungu akipenda. Na wapo wananchi wanaaamini kabisa kwamba maendeleo ya Tanzania ni hadi pale Mungu akipenda,zile siasa za kuenezwa ukoloni zinarudi kwa mbinu mpya kabisa wakitumia maamdiko ya dini kuhalalisha Umaskini wetu.
Hakuna kiongozi CCM nafahamu kwa nini sisi leo hii ni maskini bado... kama yupo hajajitokeza na sidhani kama ukimuuliza anaweza jibu hadharani. Kwa kutofahamu sababu ya umaskini wetu sijui tutaweza vipi kuondokana na umaskini wenyewe tukiwa chini ya viongozi wasiofahamu kwa nini sisi ni maskini.
Na ndio maana utaona mikakati yote ya kuondoa Umaskini nchini imeshindwa. MKUKUTA na program nyingine zote zimeshindwa kuzaa matunda kwani yameweza kutugawa zaidi ktk makundi. Katika sehemu zilipofanikiwa MKUKUTA, sehemu nyingine mbili zimeibuka kurudi chini zaidi..ni sawa na chura anayeruka hatua mbili nakuteleza hatua tatu nyuma ama sawa na kujenga Ukuta juu ya msingi uliochukuliwana maji..
Umaskini wetu haufanani kabisa na nchi tajiri inayofilisika..wala haufanani kabisa na umaskini unaotokana na kutojaliwa rasilimali, maliasili kama ardhi bali ni kutotambua makosa ya wazi yanayojitokeza chini ya uongozi mbaya. Mfano mkubwa ni viongozi wetu kutotambua kina cha umaskini wenyewe..kuna wakati ati tunajifananisha na nchi zilizofilisika kiuchumi hali sisi hatujawahi kutajirika. Na kibaya zaidi tunapata ushauri toka kjwa wataalam ambao hawajawahi kuwa maskini wala kusomea elimu inayo deal na nchi iliyopo ktk vita vya umaskini..
Hata wataalam wa uchumi wanaweza tu kutumia Free market economy pale pasipokuwa na vita ya umaskini. Mahitaji yanapokuwa bado ni mahitaji (demand) na sio ni Shida (neccesity). Mdumo wa kibiashara wa demand na supply utaonyesha tu mafanikio ikiwa hakuna vita. Kwa mfano leo hii huko Kongo kutokana na vita ya wenyewe kwa wenyewe vitu muhimu ni adimu..Sukari na chunvi zinauzwa kwa dollar zisizopungua 10 kwa kilo. Sasa ukianza kujiuliza maswala ya purchasing power na kutumia mahesabu ya demand na supply kupata majibu ya maendeleo hapo ndipo utakwama.
Sasa tazama kwetu ambako uwezo wetu wa kuzalisha ni mdogo kulingana na mahitaji..imefikia hadi kila kitu ni shida kubwa isipokuwa kwa misaada ama kuagiza mali toka nje kukidhi pengo kubwa la mahitaji ya wananchi. Hivyo, market economy inaweza tu kutoa matunda ya kiuchumi ikiwa uzalishaji wa ndani unakidhi ama unafuata mahitaji ndani na nje na sii kuagiza mali toka nje kukidhi mahitaji ya ndani - uzalishaji hakuna na ndipo makosa yanapoanza kutumika..
Jambo jingine kuu la umaskini wetu ni ile imani kwamba Umaskini ni swala la baadhi ya watu na baadhi ya sehemu.. Kama ndivyo basi hapakuwa na sababu ya sisi kuitwa nchi maskini. Utajiri wa nchi yeyote ama mtu binafsi unategemea nguvu ya ununuzi wa huyo maskini. Lakini pia imani potovu ya kwamba maskini akipewa fursa ataweza kutajirika pasipo kuangalia neema za vipaji na elimu ambazo pekee ndizo zinamwezesha mbunifu kutazama mahitaji ya soko..
Leo Masai naye kaingizwa ktk kilimo kwanza akipewa ardhi kulima mahindi badala ya kumwendeleza mmasai kwa kumwagilia ardhi yake ipate mimea ya malisho ya ng'ombe wake. Ugonvi mkubwa unajitokeza ktk vipaumbele vya wizara mbili tofauti. Kilimo against Mifugo na Uvuvi nani mwenye haki na ardhi ya mwenzake ktk mpango huu wa kilimo kwanza.
Labda kwa leo nimezungumza ya kutosha kwa kuanzia nisije wachosha wasomaji ila nitamalizia kidogo kwa kusema hivi.. wananchi wenzangu hatuna sababu ya kuwachagua CCM ikiwa wao hawafahamu kwa nini bado nchi yetu ni Maskini.. Uchanga wa nchi hauwezi kuwa sababu hata kidogo wala Ujamaa wa mwalimu hauwezi kuwa sababu kwani tumeona Vietnam na rwanda wakitupita kama tumesimama. Hawa wote walitambua kwanza kina cha Umaskini wao, wakayafahamu makosa yao kiutawala, waka enzi utawala bora kwa kuwaadhibu wale wote waliokiuka miiko na maadili ya Uongozi. Na Mwisho, mustakabali wa nchi yao kuwa mbele ya viti vyao majumbani ama ktk vyama vyao vya siasa.
Dira ya Taifa ni lazima iwe na AZIMIO pasipo hivyo tutakwenda hovyo hovyo kama mji wa Dar unavyojengwa. Upimaji ramani ya mji hutokea baada ya watu kujenga nyumba zao.. Barabara na mifereji hujengwa baada ya kila kitu kwisha jengwa.. Hii ndio Tanzania ya CCM.