Hili ni taifa la wajinga

Nafurahi mno tupo pamoja katika kuweza kuona na kupinga MAANGAMIZI ya Watanzania huku wakishangilia kama mazuzu!
Hata hivyo ukombozi wa kifikra unaanza kwa wachache, tuuendeleze kwa namna tunavyoweza.
Tunahitaji mawazo ya namna hii yaingie kwa kichwa cha kila mtanzania.

Thank you, keep it up.
 
Najaribu kutoa darsa baada ya kupata phd yangu nikiwa mitaani Bongo..Mkuu Bongo shule!

Hongera Mkandara kwa PHD, ila unaweza kuishi bongo bila shule mkuu.
Pili hongera kwa maoni yako maana yote ni ya kweli kabisa, sasa je nani wa kumfunga mbuzi kengere? nani atakayetuongoza ili atufumbue macho kuondokana na huu ujinga? kuna watu wengi tu hawajui chochote kinachoendelea katika taifa letu kwanza wanakushangaa kutamka kuwa hili taifa ni la wajinga - mfano mdogo ni wale wazee sidhani wanaelewa chochote wao walishangilia tu ushabiki wa ki-chama wakati hata hawajui madai gani yanaongelewa kwa ujumla wake.

Bila elimu ya uraia kwa watanzania wetu hatutaweza kuwaondoa hawa watwana madarakani waliojipa hati miliki ya nchi yetu, na wataendelea kutukandamiza, Unyonge wetu na kutoelewa elimu ya uraia (wewe unaita ujinga) itatufanya tuonewe, tupuunzwe na kunyanywaswa.
 
Tanzania yetu imegeuka kuwa uwanja wa fisi.. Tanzania ni nchi pekee ambayo kila kitu kinauzika utafikiri nchi iko vitani. Hakuna standard yoyote wala ramani ya Tanzania ya kesho (blueprint).

I liked this one!!!!!!!! Cha kustaajabu watu wengi tu wameridhika na hali hiyo and some do think ndiyo utaratibu all around ther globe!
 
Kuna msemo wa kwetu kwamba " NAFUU UMASIKINI WA MALI KULIKO UMASIKINI WA AKILI, KWA KUWA UKIWA NA AKILI BILA MALI UTATAFUTA MALI NA UPATE, LAKINI UKIWA NA MALI BILA AKILI UTAIPOTEZA HIYO MALI NA KUANGAMIA"

Tujiulize tuna kipi kwa ujumla kama taifa na kipi hatuna kulingana na busara za wazee wetu wa zamani!
 
Najaribu kutoa darsa baada ya kupata phd yangu nikiwa mitaani Bongo..Mkuu Bongo shule!

Dah mkuu hongera zako, Mjini shule kweli kabisa.
Unajua kazi ya kuelimisha ndugu na jamaa zetu yatupasa tuianze sasa ukielimisha kumi na hawa nao wakaenda kuelimisha wenzao kumi basi elimu ya uraia inakuwa inasambaa kwa mtindo huo, ni kweli waTZ wengi hatujui haki zetu.
 
Ni kweli kabisa tumekuwa wajinga kupiliza. Na nafikiri makuwadi wa ukoloni mamboleo waliona tatizo letu. Wakaanza kwanza kuvunja ile mihimili ya uwepo wa Taifa lolote lile ambayo ni elimu na uzalendo. Leo hii tunategemea nini kwa hawa vibaraka wa ukoloni mamboleo wasiiona haya kudaganya ili mradi tu waendelee kukaa madarakani bila kujari kesho kuna nini? Kweli tuanze kufuta ujinga na kutumia vichwa vyetu kama individuals ili tufikie ukomo wa upuuzi huu unaoendelea ndania ya nchi yetu.

Nakubaliana na dhana ulioweka ya hawa makuwadi au white elephant anayeitwa 'serikali'. Kuhusu utaifa wanapigia chapuo hili dudu linaloitwa EAC, na utanzania taratibu utafutika. Kuhusu suala la elimu nadhani sote tunajua majuzikati hapa matokeo ya vijana wa Form 4 zaidi ya asilimia 70 WAMEFELI..hii sio coincidence kwangu na sitaki kuwa optimistic wakati naona mkondo wa maji unapoelekea. It is a consistent, systematic scehme ya kutengeza taifa la wajinga, hohehahe, kimwili kiroho na kiakili kaa magullible zombie ambayo yatapoteza in totality the control of their lives. I hope this makuwadi die of cancer, seriously wanakera sana.
 
Tatizo kubwa ni hili OMBWE LA UONGOZI....tunahitaji viongozi wazalendo na wenye ujasiri wa kusimamia rasilimali zetu kwa maendeleo ya taifa letu na vizazi vyetu vijavyo....hata mabadiliko ndani ya CCM yanawezekana, sio wote ni mafisadi au hawana uzalendo,ila wachache wenye nguvu ndio wanaotuharibia nchi.....na hawa wengye nguvu tunawapa sisi kwani sisi ndio tunaowachangua, mabadiliko hataletwa na sisi kusemea kwenye majukwaa yasiyowafikia wananchi wa kawadia kama JF lazima tutoke na kujitoa kwa ajiri ya maendeleo ya nchi na kuimplement kile tunachoamini.
I call upon all members of JF to come out and show the ways and help develop this nation.
 
Yaliyotokea jana na leo bila shaka yametuonyesha jinsi nchi yetu inavyopelekwa.. hatuhitaji mwanasayansi kutufumbua macho. Hii ndio hali halisi ya utawala wa CCM. tena basi JK amekuwa akifanya mengi kinyume cha matakwa ya wengi ndani ya chama. Leo hii maswala ya Richmond hayaruhusiwi kuzungumziwa TENA bungeni.
Watu kama Mgaya tayari wamekwisha pachikwa majina na nina hakika kabisa kwamba toka leo hii TUCTA watakuwa ktk wakati mgumu sana kujiendesha na upo uwezekano wa kufutiwa liseni ama kuvunjika...Maneno ya rais JK hayakuwa na mzaha wowote bali ndio mwanzo wa wakati mgumu sana kwa kitengo hicho unless wao wasujudu kwa Uadilifu.

Nchi inatisha, utawala unanuka na hakika cheche za mapinduzi ya kweli zimewashwa na hawa wafanyakazi na pengine wanaeleweka vizuri kwa sababu hili swala linawagusa moja kwa moja. Hali ya wafanyakazi nchini inatisha. Toka waajiriwa wa Ikulu, Majeshi yetu hadi ofisi za mitaa wote hawa wamedhalilishwa kwa miaka mingi sana pasipo kuona manufaa ya ajira zao. Miaka ya 60 hadi 70 ilikuwa jambo la kawaida kabisa kwa mfanyakazi kuweza kujenga nyumba ya vyumba sita..uwezekano ulikuwepo ingawa sii mkubwa lakini leo hii huyo mfanyakazi hata kupanga nyumba ya kumtosha yeye na familia yake ni kasheshe.
Leo hii sehemu zote za starehe nchini ni sehemu za kuendesha Umalaya. Wanawake wenye heshima zao hawagusi sehemu hizi..Kila ofisi ya serikali na mashirika wafanyakazi wote wanategemea umalaya na hongo la aina yeyote ile kuendesha maisha yao..NITOE ndio maneno ya karibu hutumika kupokea hongo na haina kificho tena. Hata barua ya utambulisho toka kwa katibu kata inatakiwa honga ipatikane yaani hata sijui kutolea mfano. Machungu haya ndio yaliyonisukuma mimi kuanzisha mada hii na bahati nzuri swala la wafanyakazi limejitokeza.

Nchi inauzwa kwa mikakati isiyojenga kabisa. wakati India wanarudi ktk ukulima wa Asili sisi ndio kwanza tumebeba mabango ya kutangaza ukulima wa kisasa. Nchi zote duniani ambazo zilikuwa zikitumia Ukulima wa kisasa wamerudi ktk ukulima wa Asili. Bora kidogo chenye Afya kuliko wingi usiokuwa na tija. India wamegundua kwamba kilimo cha kisasa kwa kutumia mbolea na madawa ya umwagiliaji imeongeza idadi kubwa ya maradhi ya cancer kwa wakulima. Ni jana tu nimekuwa nikiona kipindi hicho kinachohusu maradhi ya cancer na kilimo huko India ktk jimbo la Punjab. Kwa maelezo zaidi mtaalaam wa mazao ya tropical alizungumzia madhara makubwa ya mbegu za maabara, ikiwa ni pamoja na gharama kubwa za mbolea na madawa kisha hifadhi ya mazao haya ambayo huchukua muda mfupi sana kuharibika.. Kutokana na matatizo haya wananchi wa chini walishindwa kuendelea na kilimo. Faida kubwa huenda ktk mashirika makubwa ya Ulaya yanayotengeneza mbolea na madawa na sii mkulima.

Kisha mtaalam huyu hakuishia hapo tu alizitaja nchi kama sita za Asia na Amerika ya kusini zilizoathirika na kilimo hiki kiasi kwamba hata wao wamerudi ktk kilimo cha Asili (organic). Hii haina maana wananchi wanarudi ktk kilimo cha jembe la mkono, laahasa isipokuwa hawatatumia tena mbegu za maabala ambazo zinatazama tu wingi Quantity) na sii ubora wa mazao yenyewe (Quality).
Hivyo tuweni makini sana na kama nakumbuka vizuri Prof. Mwandosya akiwa waziri wa Kilimo alikataa kabisa kuingia ktk mkakati huu wa kilimo cha kisasa kwa kutumia mbegu za maabara. hatujaishiwa kiasi hicho wala sii kweli mbegu zetu za asili hazivumilii ukame. Mbegu zote zilizoletwa toka maabara zimeanzishiwa program ya umwagiliaji hii haiukuwepo zamani lakini baada tu ya sisi kukubali mpango wa IMF na vyombo vyake vya biashara ndipo tunaona mageuzi ya Ukulima toka mbegu hadi matunzo ya shamba.
Tazama Operation ya malaria... wizi mtupu kuuziwa vyandarua vya mama Bush kumpatia sifa za kimataifa. Vita ya mbu ni kujenga mifereji inayovuta maji yote baada ya mvua kunyesha, kuua Mbu wote ktk mazalio yao..lakini haya maswala ya rais kutangaza dawa moja tu ndio inafaa kutumiwa ina maana zaidi ya kuuza biashara kuliko ponya. Siwezi kumlaumu kwani ndivyo alivyoambiwa kusema baada ya kupewa msaada lakini pamoja na yote haya hizo dawa hazikupata kufanyiwa majaribio ndani na madaktari wetu kwanza kabla hatujaingia mkenge. Mimi nimezungumza na madaktari wengi tu baada ya mimi kuugua malaria. Na ushauri wao haukuwa mzuri kusifia dawa hizo kwani tayari madhara yamekwisha jitokeza kwa baadhi ya wananchi.
Nchi yetu imeuzwa, Nasikia hata jengo la Usalama wa Taifa linajengwa na Marekani. Habari hii kama ni ya kweli basi tumeuza nchi, jengo lenyewe ukilitazama kwa makini ni sawa na tai aliyetua (eagle has landed).. Hii ina maana kubwa sana kwa Wamerekani. na huko Mbeya pia nasikia tayari kambi ya Marekani imeanza kujengwa..Hizi zote ni habari zinazotisha kwani Marekani siku zote hutazama maslahi yake. Kama kuna nchi Marekani wangeijnga basi haiti ingekuwa ya kwanza.. Hawa jamaa wapo karibu na Marekani toka enzi ya vita baridi lakini Haiti hiyo hiyo hadi leo hii ni nchi ya mwisho duniani.
 
Back
Top Bottom