Hili la Diamond Kutumbuzia AFCON

Kwangu mimi Diamond kugewa bendera kuipeperusha ni swala la kiushindani zaidi kati yake na hasimu wake kimuziki.
Karibuni tu mashabiki wake watasema unaona tumegewa mpaka bendera? Nyinyi mmegewa nini?
 
Kitendo cha Diamond kuchagulia kutumbuiza AFCON ni cha kupongezwa sana ila hakiachi tusifanye tafakuri jadidi

  1. Kwamba Mtanzania amefuzu kwenda kutumbuiza huku TIMU YA TAIFA IKISHINDWA KUFUZU kucheza soka
  2. Kwamba kwa kuwa tumeshindwa mguuni walau tumefikiriwa mdomoni
  3. Kwamba huenda soka letu ni la maneno zaidi na ndio maana tunaambiwa wacha maneno weka MUZIKI
  4. Kwamba Waziri anakabidhi bendera ya TAIFA la Tanzania kwa Diamond kwa kuwa anakwenda KUWAKILISHA TAIFA nalo ni la kupongezwa pia maana tutapata kodi
  5. ...........................................................ongeza.
  6. Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye, akimkabidhi bendera msanii wa Bongofleva Nasib Abdul(Diamond Platnum) anayekwenda kutumbuiza katika ufunguzi wa mashindano yatakayofanyika Januari 14 nchini Gabon iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Joti nae anaenda?
 
Hili jipu sema basi tu..nape shule nae naskia ndogo na majukumu ya nafasi yake hayajui
 
Acheni kulalamika wa hovyo nyinyi. Kuchagulia kwa D kwenda Gabon shida nini sio kila kitu mnalalamika tuu nyambavu zenyu. Dogo amejipanga ndiyo maana mambo yanamwendea powa. Kwa mpila gani unaochezwa bongo! mm naona ni wakati sasa wa serikali kuwekeza kwenye mziki kwa maana ndiyo unafanya powa kuitangaza Tanzania lakini sina maana ya kuacha kufanya mikakati thabiti ya kukuza soka bongo I hope tutafika tuu God willing!! Big up diamond big up Mbwana Samatha....!!!
 
Back
Top Bottom