Hili jambo limeniumiza sana

Hili jambo limeniumiza sana

Kila siku hayo hayo hivyo viwanda vitajengeka kwel
Wabongo tukiisha karirishwa inakuwaga ni shida tupu......haka ka msemo ka Nchi ya Viwanda hadi kanaleta kichefu chefu unataka kuniambia hata huko kwenye nchi zenye viwanda hakuna watu wana matatizo ya kifamilia kisa ni nchi za viwanda?
Kujenga viwanda kuna husiana vipi na matatizo yake ya familia?

Sent from my Compaq desktop-1997 Using Jamiiforums desktop app
 
Kama ni wakiume kweli ni suala lA kisaikolojia zaidi...Mdgo ako akiwa kama kitinda mimba na wakiume unconscious amebeba taswira ya Baba mbele ya mama...Msamehe mama bure hata ingekuwa kinyume chake kabaki Baba we ungekuwa taswira ya mama kwa Mzee wako.....hii inaanzia tangia umri wa utotoni wanasaikolojia wanaita Oedipus Complex....Katika kipindi cha Msiba kulia kule ni mama kadhihilisha kilicho ndani yake Kwa mwanae......sasa namna ya kushinda hiyo sababu ni Mzazi Mungu wako mwingine Kama umeolewa Mme wako anaweza play part hyo au Mjukuu akiwa wa kiume......Msamehe Bure na hiyo ni psychological treatment kubwa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Najiulizaga kwa nini mzazi ampende huyu kuliko yule zaidi wakati wote ni watoto wake,cha ajabu utakuta baba na mama wamejigawia watoto Wa kuwapenda..huyu baba hampendi na huyu mama hampendi hua nachanganyikiwa kwa kwel.ili tatizo nimeliona kwingi sijui tatizo ni nn.
Pole sana ndugu ndio dunia yetu ilivyo,piga moyo konde acha maisha yasonge,pia kumbuka kusamehe.
 
Haaaaaa haaaaaa haaaaaa , naona Mungu anawekewa madaraja then soon atawekewa "makaravati"
Atachimbiwa na mitaro,dini nyingine unaambiwa mume ni mkuu sana,ni BWANA kabisa...ndio maana wanasema acheni Mungu aitwe Mungu.

Mzazi ana uwezo mkubwa wa kuchangia kukuumiza mno nafsi na akili na kukuchanganya kabisa.Wazaz wengine ukicheka nao wanakutoa undondocha.

Wazazi tuwapende na kuwaheshimu mnooo ila HAPANA wao sio Mungu.
 
Mama naye ni binadamu. Ana damu na mwili wa nyama. Ana mapungufu kama binadamu. Ongeza upendo kwake naye bila hiana atajirudi.
 
Wabongo tukiisha karirishwa inakuwaga ni shida tupu......haka ka msemo ka Nchi ya Viwanda hadi kanaleta kichefu chefu unataka kuniambia hata huko kwenye nchi zenye viwanda hakuna watu wana matatizo ya kifamilia kisa ni nchi za viwanda?
Kujenga viwanda kuna husiana vipi na matatizo yake ya familia?

Sent from my Compaq desktop-1997 Using Jamiiforums desktop app
 
Wabongo tukiisha karirishwa inakuwaga ni shida tupu......haka ka msemo ka Nchi ya Viwanda hadi kanaleta kichefu chefu unataka kuniambia hata huko kwenye nchi zenye viwanda hakuna watu wana matatizo ya kifamilia kisa ni nchi za viwanda?
Kujenga viwanda kuna husiana vipi na matatizo yake ya familia?

Sent from my Compaq desktop-1997 Using Jamiiforums desktop app
Kwakweli hata Mimi nimemshangaa
 
Kama ni wakiume kweli ni suala lA kisaikolojia zaidi...Mdgo ako akiwa kama kitinda mimba na wakiume unconscious amebeba taswira ya Baba mbele ya mama...Msamehe mama bure hata ingekuwa kinyume chake kabaki Baba we ungekuwa taswira ya mama kwa Mzee wako.....hii inaanzia tangia umri wa utotoni wanasaikolojia wanaita Oedipus Complex....Katika kipindi cha Msiba kulia kule ni mama kadhihilisha kilicho ndani yake Kwa mwanae......sasa namna ya kushinda hiyo sababu ni Mzazi Mungu wako mwingine Kama umeolewa Mme wako anaweza play part hyo au Mjukuu akiwa wa kiume......Msamehe Bure na hiyo ni psychological treatment kubwa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Nitauzingatia sana labda inatokana na hayo mambo uliyoyaainisha hapo juu
 
Najiulizaga kwa nini mzazi ampende huyu kuliko yule zaidi wakati wote ni watoto wake,cha ajabu utakuta baba na mama wamejigawia watoto Wa kuwapenda..huyu baba hampendi na huyu mama hampendi hua nachanganyikiwa kwa kwel.ili tatizo nimeliona kwingi sijui tatizo ni nn.
Pole sana ndugu ndio dunia yetu ilivyo,piga moyo konde acha maisha yasonge,pia kumbuka kusamehe.
Shukrani ndugu
 
Ni na
Najiulizaga kwa nini mzazi ampende huyu kuliko yule zaidi wakati wote ni watoto wake,cha ajabu utakuta baba na mama wamejigawia watoto Wa kuwapenda..huyu baba hampendi na huyu mama hampendi hua nachanganyikiwa kwa kwel.ili tatizo nimeliona kwingi sijui tatizo ni nn.
Pole sana ndugu ndio dunia yetu ilivyo,piga moyo konde acha maisha yasonge,pia kumbuka kusamehe.

Ndio maana hata watoto wanaweza zaliwa familia moja lakini kila mmoja akawa na tabia tofautitofauti muhimu tu kuelewa wazazi ni wanadamu so as watoto nao wanaweza mpenda mzazi mmoja kuliko mwingine
 
Habari zenu jamani


Katika familia yangu tumezaliwa wawili Mimi nikiwa ndiye mtoto wa kwanza alafu akafwata midogo wangu ambaye tayari ni marehemu mwezi sasa umepita.....nimebaki Mimi na mama yangu baba alishafariki miaka imepita.

Kabla ya mdogo wangu kufariki alikuwa ni kipenzi cha mama sana hilo halikuwa linanisumbua niliona kawaida sana pia hiyo ilitokana na mahusiano ya mpenzi niliekuwa nae mama hakumpenda sana jambo hilo lilifanya Mimi na mama yangu tusiwe na maelewano.
Kitu kilichokuja kuniumiza na nimuone mama tofauti ni siku mdogo wangu alipofariki mama alikuwa akilia wa nguvu na huku akilitaja jina la mdogo wangu na Mimi.......nanukuu( BORA USINGEONDOKA WW KIPENZI CHANGU ANGEONDOKA DADA YAKO (yani mimi)INGEKUWA AFADHARI.
Maneno hayo halikuwa akiyarudia kuanzia mwanzo wa msiba mpaka anazikwa jambo hili liliwashangaza wengi na liliniumiza sana mpaka Leo nikikumbuka Yale roho inaniuma sana nashindwa hata kumuangalia mama yangu naishia kulia.
Pengine nimemkosea mama yangu sana lkn sikutegemea kama anaweza kuombea Mimi kufa imeniumiza sana.
Amekuja leo na baadh ya ndugu akiomba msamaha sijasema chochote nimeishia kulia.nataman niende mbali kwasababu nimejua Mimi si chochote kwake.





Mwenye ushauri au mawazo yoyote kisaikolojia siko sawa.
Duu Mama yako kavuka mipaka sana lakini samehe...songa mbele huyo ndiyo Mama yako.
Kwanza nenda kamuombe msamaha mama yako mzazi kwa yote...
Mama yako ana sababu zaidi ya hii ulio tuambia ya kumkataa mtu wako...na pia wewe unaweza chagua kati ya Mama yako au huyo mchumba wako.
Ukweli ni kwamba kamwe usidanganywe wala kudanganyika kuwa utaweza kuwa huna maelewano na mama yako na bado ukapata baraka,,,,, sahau kabisa..
Halafu hutoweza kuolewa na mtu ambaye Mama yako hamkubali....
Badilika na uende umuombe mama yako msamaha....pia hilo jina ambalo umejipa nalo ni tatizo zaidi
 
watu wengine sijui mkoje! ulichoandika ni upumbavu mtupu! na unakeraa, kama ni kweli alikuomba msamaha halafu wewe ukajifanya eti umeumia sana kwa yaliopita, jua mama sio kama mwalimu" mtafute muombe msamaha mama yako! ningekuwa ndo mjomba wako ningekupiga marufuku kufika kwangu mpaka mamaako akuridhie. eti HILI JAMBO LIMENIUMIZA SANA! mangapi we uliomuumiza mamaako!? kama una akili weka mabaya ya mamaako aliokufanyia na mazuri aliokufanyia kwenye mizani sahihi, yapi yanazidi! kitendo cha mamaako kukuomba msamaha haitakiwi uendelee kumsikiliza bali ni kumzuia na badala yake wewe ndo umuombe msamaha yeye! baraka zinkufuata ulipo unazipiga teke!?
wewe na we kapimwe mkojo
 
kitu kingine hujasema kama umeolewa au kama una mwanaume ambaye ni mpenzi/ mchumba wako huyo ndo wa kuwa nae karibu akusaidie kisaikolojia utulie.
 
We unadhani akupendi ila u kweli anakupenda sana isupokuwa shetani mara nyingi anatafuta sababu angekuwa hakupendi asingekulea mpaka hapo ulipo wenda kuna kitu kinamsumbua ambacho ashidwa kukusamehe ongeza upendo kwake
 
We unadhani akupendi ila u kweli anakupenda sana isupokuwa shetani mara nyingi anatafuta sababu angekuwa hakupendi asingekulea mpaka hapo ulipo wenda kuna kitu kinamsumbua ambacho ashidwa kukusamehe ongeza upendo kwake
 
Habari zenu jamani


Katika familia yangu tumezaliwa wawili Mimi nikiwa ndiye mtoto wa kwanza alafu akafwata midogo wangu ambaye tayari ni marehemu mwezi sasa umepita.....nimebaki Mimi na mama yangu baba alishafariki miaka imepita.

Kabla ya mdogo wangu kufariki alikuwa ni kipenzi cha mama sana hilo halikuwa linanisumbua niliona kawaida sana pia hiyo ilitokana na mahusiano ya mpenzi niliekuwa nae mama hakumpenda sana jambo hilo lilifanya Mimi na mama yangu tusiwe na maelewano.
Kitu kilichokuja kuniumiza na nimuone mama tofauti ni siku mdogo wangu alipofariki mama alikuwa akilia wa nguvu na huku akilitaja jina la mdogo wangu na Mimi.......nanukuu( BORA USINGEONDOKA WW KIPENZI CHANGU ANGEONDOKA DADA YAKO (yani mimi)INGEKUWA AFADHARI.
Maneno hayo halikuwa akiyarudia kuanzia mwanzo wa msiba mpaka anazikwa jambo hili liliwashangaza wengi na liliniumiza sana mpaka Leo nikikumbuka Yale roho inaniuma sana nashindwa hata kumuangalia mama yangu naishia kulia.
Pengine nimemkosea mama yangu sana lkn sikutegemea kama anaweza kuombea Mimi kufa imeniumiza sana.
Amekuja leo na baadh ya ndugu akiomba msamaha sijasema chochote nimeishia kulia.nataman niende mbali kwasababu nimejua Mimi si chochote kwake.





Mwenye ushauri au mawazo yoyote kisaikolojia siko sawa.
Pole sana kwa hili.
Machozi yako yametosha kuwa adhabu kwa mama yako mpaka amekutaka radhi na kuhitaji muishi kama zamani.
Usiiwaze sana kauli ya kilio chake, tambua kwamba kwa sasa yeye ni mama yako hana mbadala kwako na yeye hana mbadala kwa upande wako pia.
Ujumbe wa machozi hueleweka mapema sana,msamehe mama yako.
Mama amempoteza mtoto anmbaye ni kipenzi kwake na aliyebaki hana maelewano naye ,kama wewe ndo ungekuwa mama ungejiweka kwenye kundi lipi?
Tafadhali msamehe mama yako haraka iwezekanavyo ili nafsi yake iwe huru akutizamapo.
Hii ni itilafu ya kibinadamu isikufanye umuhukumu mama daima na kutoishi kwa furaha na amani.
Ipumzishe roho yako na roho ya MAMA YAKO kwa kumsamehe.
Ni wakati wako kumuonesha mama kuwa vile akufikiriavyo sivyo.
Prove your mother wrong for lovely words during this trying time.
Be like a strong wall.
Strong wall shake but don't collapse!
 
Back
Top Bottom