Ni kweli maneno hayo yanaumiza sana wala si rahisi kwa mtu yeyote asikie neno au jambo baya anaambiwa hususani mzazi/wazazi.
Kwanza nianze kwa kukupa pole mno maana hiyo ni moja ya changamoto katika maisha ya mwanadamu.
Kwa ushauri wangu ambao kidogo itakuweka sawa kisaikolojia, ni kwamba unapaswa kuvumilia na hali ambayo unayo kwa sasa na vizuri ukaenda kwa mama yako mzazi mkawa na maongezi yenu binafsi tena ya kina.
Onesha furaha pindi unapoenda kuongea na mama yako, hata kama bado unaumia lakini ni vyema uachie tabasamu pindi upo na mama yako,
Anza kuongea naye kwa udadisi wa kina ili kujua zaidi chanzo cha yeye kusema na kuonesha kitendo cha kutaka wewe ungetangulia kuaga dunia.
Pia naamini utakuwa na hisia kali pale mtakapo kuwa na maongezi wenu unaweza kumhoji kwa maswali haya,
1. Mama unajua nakupenda na nimetimiza wajibu wangu wa kukupenda wewe kama mwanao, na ni haki yako kupendwa zaidi neno upendo, lakini kwa jambo ambalo limetokea msibani mpaka kwenye mazishi kusema kuwa " bora ningekufa mimi na isiwe mdogo wangu" ulikuwa na maana gani hasa kuongea maneno mazito tena mbele za watu, huoni ya kwamba nimedhalilika na kuonesha tatizo/ utofauti katika familia yetu....??
2. Ni kitu gani hasa nimekukosea mama yangu mpaka ukaamua kufikia kutamka maneno mazito kama hayo, au nimekukwaza kwa jambo gani mama yangu, najua thamani ya upendo wako na napenda uwe na amani moyoni, nitaacha kufanya jambo ambalo limekukera, ( atoe sababu za msingi kama anazo na wewe uzipitie kwa makini ukiridhia nazo acha kabisa )
Aghalabu wazazi wanapenda watoto wao kwa namna moja ama nyingine lakini si mbaya na wewe ukamwambia maoni yako juu ya maamuzi yako uliyofikia.
( mfano )
Mueleze kuhusu mahusiano yako, mambo yako ambayo unataka yaende vipi kwa misingi yako/ sababu zako, msimamo wako katika mambo yako kwa ujumla,
Mweleze nafasi uliyonayo kwa sasa ni kuamua maisha yako yaende vipi, wala mwingine hana haki ya kukulazimisha zaidi ya ushauri/maoni.
Mueleze mama yako mzazi kila kitu akifahamu kuhusu misimamo yako na haki zako, endapo atakuewelewa haina shida,
Pia kama hutopenda kuwa na mambo mengi na kuzuia jambo hili lisiwe kubwa katika familia na hata kwa ndugu zenu, fanya jambo gumu kidogo.
Mfuate mama yako mzazi ikiwemo na ndugu kama wataweza kufika uwaambie kuwa umeamua kumsamehe mama yako kwa yote yaliyo tokea na awe na amani moyoni, kisa Fanya mambo yako mengine, kwa hakika mama yako kama mtu mzima ataweza kufikiria vyema atakuwa karibu na wewe maana hawezi kuwa mpweke kwa sasa.
Fanya kama hakuna kilichotokea na ufanye mambo mengine ya muhimu, kwa haya ni maisha tu yanapita na yana mwisho wake wala usiumie sana na jaribu kutowaza sana suala hili angalau kidogo upunguze maumivu.
Pole sana kwa msiba, pole mno kwa mazito yaliyokukuta, nakutakia maisha mema....