Hiki kikombe kina umri wa miaka 20+

Hiki kikombe kina umri wa miaka 20+

Noma sana! Kuna glasi moja hivi ya kunywea maji mshua, inakuwa kama gamba la kobe, naona bimkubwa alishaiweka kama kumbukumbu pale home.
Nipo shule ya msingi glasi ipo.

Mshua wangu pia bado anayo saa ya AJANTA ya ukutani, inatumika mpaka leo. 😊
Ni kumbukumbu nzuri sana.
 
Miaka ya 1980, baba yangu alinunua redio casette player. Kpindi hicho kila mtu alikuwa anaishangaa. Tulikuwa tunaona ni kama ina ''vidude'' vingi sana vya kubonyeza, mtu hujui ubonyeze kipi. Alikuwa anaitumia wakati yupo nyumbani tu, kusikiliza redio na kanda za dini. Ilikuwa inafungiwa ndani muda wote. Fast foward baada ya sisi kukua na kuondoka nyumbani na wazazi kufariki, bado iko, mpya kwa sababu haikuwa inatumika au sahihi kila mtu alikuwa anaogopa kutumia asije kuharibu.
Saafi, kipengele ni kupata kanda zake zinazofanya kazi
 
Meza ya tv home ina miaka takribani 22-25 hivi.. ilipokuja teknolojia ya tv za ukutani, ipo ipo tu.. mbao ngumu sana ile
 
Watoto ndio wanapukutisha vitu cha mchina siku hizi. Kila baada ya muda utasikia unaambiwa vikombe vimepungua. Madogo wanavibamiza.
Zamani vya udongo pamoja na uimara wake vilikuwa vinadumu sana sababu vilikuwa vilitunzwa kwa ajili ya wageni, familia inatumia plastiki. Halafu kama familia zetu mfano Kagera wakati wa kula tulikuwa tukitumia sinia moja familia nzima
 
Meza ya tv home ina miaka takribani 22-25 hivi.. ilipokuja teknolojia ya tv za ukutani, ipo ipo tu.. mbao ngumu sana ile
Kuna meza fulani hivi ilikuwa na partition tatu, ya tv, deki na chini kuweka mikanda, ilikuwa kama hii sema haikuwa mbao kama hii

Stand.jpg
 
Back
Top Bottom