Hiyo scania ya Sauli weka mbali na watoto imekaa vizuri hata ikipita kwenye matuta inaunafuu mkubwa kuliko basis lolote kwasasa
LC Hardtop ni gari ya kazi sio ya mashindano[emoji28][emoji28][emoji28] kuna kipindi flan nilipanda gari moja ya tour, kutoka Ngorongoro pale getini kuja Arusha town, jamaa alinipa lift kiroho safi!! Nahisi alikuwa amevuta bangi kidogo, kwasababu alikuwa rafu sana.
Ameshuka kwenye ule mlima kutoka Karatu kuingia mto wa Mbu kama kichaa, kutoka Mto wa mbu to Makuyuni kuna vizibiti mwenda vya chini (downs). Huyu jamaa alikuwa anazipiga balaa, aisee!! Nilivumilia sana kwa kweli.
Hizi gari za kijapani sio comfortable cars especially hizi Land cruiser hardtop
Ameishia kusema ni grand sijui nini kama V8 hata sijaelewa.asante maana nilijua sentensi ya mwisho atatujuza aina ya gari yake
Mkuu tumtag @KIDUKULILO atupe uzoefu wake.kwani kidukulilo anasemaje kuhusu kushindana na vyombo vya usafiri barabarabi ilhali wewe una gari tena ford escape...najua unapitia nyuzi zake hapa daily;hukuwapa hata ofa ya nyama choma njiani??
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] mkuu post picha ukiwa unacheza mziki.Nakumbuka nilifanya ligi moja Matata na nisoyemjua barabarani siku niliyotoka kupiga kura, mwaka 2015....
Barabara iliyohusika ni Ali Hassan Mwinyi kuanzia hapa mataa ya Serena hadi Bagamoyo Road maeneo ya Tegeta.
Mida ilikuwasaa kumi jioni.
Chanzo cha ligi, alinichomekea kiboya bin kibabe halafu akanioneshea like, nshakuchomekea utanifanya nini sasa.... mmaamaaeee nilimkanyagia mafuta nahisi alienda kumeza cofta kwa vumbi nililomuachia. Shida yangu niko mbishi sana...
Siku husika ilikuwa jumapili watu sio wengi barabarani na siku ya uchaguzi hivo barabara ilikuwa nyeupeee.
Gari alilotumia mleta ligi mwenzangu kama sijasahau ilikuwa Altezza maana ilikuwa hizi gari za chini. Mimi nilikuwa na Grand Car (yaani gari ya juu halafu iko branded grand uchomaji wake wa mafuta uko sawia na V8 hukoo).
Siku hizi nimekua kiasi nimepunguza ukorofi na ubishi, ligi za barabarani almost nimeziacha.
Ligi niliyobakia nayo ni ya Mahaba na Mziki tuu. Mtu akiwa tayari tufanye ligi ya kucheza mziki kuanzia saa nne usiku hadi jogoo la saa kumi alfajiri linawika bila kupumzika.....
Kasinde Platinum Matata.
[emoji3][emoji3][emoji3] mkuu siyo walikuwa wanaendesha tudude!!?[emoji28][emoji28][emoji28] wenye vyombo vya usafiri wanazingua sana
Hii ni kweli kabisa mkuu.Siyo ligi, mimi binafsi huwa napenda kumark gari moja na kutembea nyuma yake na huwa sipendi aniache sana, mkitembea kwa pamoja muda mrefu mnakuwa kama ndugu kiasi kwamba akikuacha muda hasikuone hujikuta akijiuliza yule jamaa kapata shida gani, na husishangae anakusubiri na ukipata shida husishangae mnakesha wote barabarani, so huu ni urafiki wa magari unaojijenga automatically. Magari yanafahamiana bwana!
Gari ni ishu kubwa sana barabarani mkuu.Kukimbia kwa gari sio Sababu unatumia gari gani!
Mbio ni Moyo wa mtu, kuna watu wana roho ngumu sanaaaa.
Safari za usiku sitaki hata kusikia maana unakuwa Kwenye wasiwasi muda wote sasa hiyo shida yote ya niniUsiku sio salama kwa ligi.
Si rahisi kuona zaidi ya 200M, ukiwa speed zaidi ya 100kph, ni ngumu kukwepa hatari ya ghafla.
Usishindane na watu wa magazeti, hao wanapita hiyo njia kila siku tena usiku. Wanaifahamu vizuri sana.
Na usiku kuna ajali nyingi sana za uzembe na kukosa umakini.
Kuwa makini, usishindane na usiemjua.
Mkuu tungis agusi kwa ndege ya ardhini kisbolicha ya changamoto za barabarani, kwa upande wa ligi za mabasi ya abiria nasikia kwa sasa anayesumbua route ya dar - mwanza ni tungis express na anayesumbua route ya dar - mbeya ni sauli express. imefika kipindi mpaka watu wanabet kuhusu haya mabasi.
View attachment 1222485View attachment 1222488
STI ni kelele tupu.STI unaifahamu lkn?
Ukiachana na Vw polo R hebu tuweke hapa records wa gari za Germany nyingine kwny WRC tulinganishe na Subaru.
Napenda sana ila nikiwa peke yangu,nikishakuwa na familia nyie piteni tu kwa raha zenu...
Kweli cc zinachangia mkuu lkn not a must,nilikua na mazda rx 8 ina cc 1300 ila hio Ford Escape uliyokua nayo nakupita kama umesimama vile mkuu.Gari ni ishu kubwa sana barabarani mkuu.
Nikuambie tu kama una gari yenye engine capacity below 1900cc. Wewe ligi waachie wengine kabisa!! Hata uwe una moyo wa mbio.
Hii ni nzuri.Siyo ligi, mimi binafsi huwa napenda kumark gari moja na kutembea nyuma yake na huwa sipendi aniache sana, mkitembea kwa pamoja muda mrefu mnakuwa kama ndugu kiasi kwamba akikuacha muda hasikuone hujikuta akijiuliza yule jamaa kapata shida gani, na husishangae anakusubiri na ukipata shida husishangae mnakesha wote barabarani, so huu ni urafiki wa magari unaojijenga automatically. Magari yanafahamiana bwana!