Salih
JF-Expert Member
- Jan 31, 2013
- 619
- 401
Kwanza hizo zawadi mnazopokea kila siku nanyi muwe unatuonea huruma hivi hamchoki tu kupokea zawadi zawadi, na baada ya mchezo tunapunguza kwakuwa hata kwenye kula kasi ya tonge la kwanza ni tofauti na tonge la pili na kuendelea....tuvumiliane tuMwanaume anaweza akawa anamfukuzia mwanamke kabla hajampata,ataonyesha anakupenda sana,atakuwa anaongea na hisia kali sana
Kabla hujamkubalia kila baada ya lisaa anakupigia sim,SMS kila wakati,zawadi hazihesabiki
Ila ukishampa mchezo tu hali hubadilika ,sim alizokuwa anapiga kila lisaa atakuwa anakupigia baada ya masaa 12,SMS zinakata,zawadi zinaisha
Na cha ajabu mwezi mzima alikuwa anakufukuzia bila kukata tamaa,spidi zile zile lakini baada ya mchezo mambo hubadilika
Je wanaume kwa nini unaonyesha kumpenda mwanamke kwa hisia kali kabla ya kukupa mchezo na akisha kupa tu kwa nini hisia zako zinapungua?
Ni kweli wanaume huwa wanatamaa tu au ni kuprend kupenda kumbe ni kuzuga mwanamke aingie 18 apate anachotaka na kupotea?
Na mwanamke hupenda zaidi pale anapokutana kimwili na mwanaume ambaye anaonekana kumpenda
Na baada ya hapo humuachia mzigo wa mawazo mwanamke baada ya kutoa mzigo
Wanaume tuambieni kwa nini huwa na tabia hii lakini sio wote ila asilimia kubwa kabla na baada ya kukutana kimwili huwa ni tofauti