Hii sms nimeikuta kwenye simu ya mpenzi wangu

saudari

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
2,655
2,779
Nimekuta sms hii iliyoandikwa na Polisi kwenye simu ya mpenzi wangu.

Unajua nakuthamini zaidi ya MSHAHARA, bila wewe siwezi kuishi ni sawa na kukosa BUNDUKI eneo la tukio,

nitakuheshimu kama ninavyoliheshimu LINDO, wewe ndio IGP wa moyo wangu, daima nitakuweka mbele kama

LIGHT MAKER kwenye gwaride, mbona uko kimya nijibu basi nipate kufungua JADALA ndani ya moyo wako.

Usinifante moyo ukaenda mbio kama DEFENDER MPYA, nitakuweka salama kama msafara wa RAIS, nina RB ya

penzi lako usiniweke ROHO juu juu kama yanavyoniweka maandamano ya CHADEMA.


Huyu Polisi anamsumbua sana mpenzi wangu.
Je nifanyajeeeeee???????
 
Kwa nini unapekua simu ya mpenzi wako?:becky:

Hujui kama simu ya mpenzi wako ni mali yake binafsi?

Ukome kabisa kupekua pekua simu ya mpenziyo. Utakuja kufa siku si zako. Jiaminishe tu kuwa mpenzi wako ni mkweli na mwaminifu kwako hata kama hayuko hivyo.:madgrin:
 
umenicopy hiyo sms nilitumiwaga na mpenzi wangu afande so ntamwambia unatumia maneno yake bila ridhaa yake

Nishauri sasa mimi nifanyaje au niende kutafuta dawa kama ile ya Temeke.
 
Kwa nini unapekua simu ya mpenzi wako?:becky:

Hujui kama simu ya mpenzi wako ni mali yake binafsi?

Ukome kabisa kupekua pekua simu ya mpenziyo. Utakuja kufa siku si zako. Jiaminishe tu kuwa mpenzi wako ni mkweli na mwaminifu kwako hata kama hayuko hivyo.:madgrin:
Ina maana wewe huwa haumpekui? Be honest!
 
Kwa nini unapekua simu ya mpenzi wako?:becky:

Hujui kama simu ya mpenzi wako ni mali yake binafsi?

Ukome kabisa kupekua pekua simu ya mpenziyo. Utakuja kufa siku si zako. Jiaminishe tu kuwa mpenzi wako ni mkweli na mwaminifu kwako hata kama hayuko hivyo.:madgrin:

Nashukuru Nyani Ngabu kwa ushauri wako.
Nimetafuta kitufe cha like nimekikosa iminibidi nikuLIKE hivi:A S thumbs_up:.
 
I normally dont. Ni tabia mbaya tu. Kwa nini upekue simu ya mpenzio ilhali unayo ya kwako?

kwani kuna ajabu gani huko kwenye simu hadi ilindwe kuliko hata mwili wake ambao nausasambua kama karanga? Kama anajiamini na hana siri ya kuficha, why not?
 
I normally dont. Ni tabia mbaya tu. Kwa nini upekue simu ya mpenzio ilhali unayo ya kwako?

Kwa mtaji huo huo hutakiwi kumdadisi wala kumhoji chochote kuhusu maisha yake kwa sababu na wewe unayo maisha yako. Jali ya kwako achana na ya kwake. Hakuna kuulizana unaenda wapi, ulikuwa wapi, huyo nani, na kadhalika.
 
Kwa mtaji huo huo hutakiwi kumdadisi wala kumhoji chochote kuhusu maisha yake kwa sababu na wewe unayo maisha yako. Jali ya kwako achana na ya kwake. Hakuna kuulizana unaenda wapi, ulikuwa wapi, huyo nani, na kadhalika.

Kwa hali hiyo mtaishije sasa kama watu ambao hamjuani, hata brother & sister sometime huulizana.
Hayo hayatakuwa maisha ya mtu na mpenzi wake bali ni mtu na maisha yake,
 
Kwa hali hiyo mtaishije sasa kama watu ambao hamjuani, hata brother & sister sometime huulizana.
Hayo hayatakuwa maisha ya mtu na mpenzi wake bali ni mtu na maisha yake,

Sasa kama hakuna kugusa simu yake kwa sababu ni 'yake kwake' kuna haja gani ya kugusa mambo mengine ilhali ni 'yake kwake'?
 
Usirudie tena upekuzi wa aina hiyo... Siku nyingine utakuta makubwa zaidi ya hayo halafu ukajikuta umeamkia ICU.....Trust her mkuu...
 
Back
Top Bottom