Hii ofa mpya ya airtel ikoje

Hii ofa mpya ya airtel ikoje

Hercule Poirot

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2011
Posts
1,770
Reaction score
1,555
Wakati watumiaji wa Airtel modem tukiwa ktk janga la kushuka kwa speed yake toka HSPDA hadi EDGE , huku wao wakitangaza kuwa wana speed kali ya 3,75 g na sasa wametoa/wanatangaza kama wanajf mnavyoona hio banner yao hapo juu kuwa NUNUA MODEM YAO KWA TSH 30,000/= NA UPATE INTERNET YA BURE KWA MIEZI 6 INA UKWELI WOWOTE ....KWA AMBAYE AMESHANUNUA KUPITIA HII OFA TAFADHALI TUNAOMBA ATUPE FEEDBACK KUHUSU OFA HIO NA UWEZO/SPEED YA HIZO MODEM MAANA TUNAKARIBIA KUWAKIMBIA HAWA JAMAA
 
Miezi 6 bure?lugha za biashara 2 hizo yan utakuta kila mwezi wanakupa 400mb ila wanavyoongea utadhani ni unlimited for 6 months..ngoja walionunua watujuze
 
hata mim siwaelew kwa sasa maana hata ile ofa ya kuanzia saa tano usiku wameitoa, hiyo promotion sijajua inakuaje labda anaejua atujuze tafadhali.
 
Tekiniki za bizna hizo,kwani hzo modem ni za 4G? Mitambo ya 4g wamefunga lini na nani aliwapa hyo lisence?
 
Wezi tu hao hawana lolote wameshindwa kazi bora walale mbele tu.
 
Wadau leteni feedback au hakuna aliyenunua hio modem ya ofa....ndo kusema jamaa Airtel wanafulia
 
Hakuna lolote labda walionunua leo, ila bado tuna 3G, TTCL ile ya Fiber Optic ndo wakweli
 
Ntanunua kesho.. Ntawajulisha leo mvua nkashndwa.. Bt swala la speed mbona Airtel iko mwake sana.. Uku naona inapta wk speed haijashuka
2.5mbps au 280KBps tena iko safi sana ktk kustream hd hazigandi kabisaa!!
 
Mkuu huko kwako tu....sisi huku tunachezea kitu cha EDGE wiki ya pili sasa....kesho tutacikilizia feedback toka kwako.
 
Hamna ki2 spidi ya kawaida sana kuna rafiki yangu kanunua jana,ila kuna muda ilikuwa inamsumbua maana network iko down na anakaa town!
 
mkuu tony tuambie kuhusu hicho wanachosema ni ofa ya miezi sita kikoje....ishu ya speed twaijua
 
Hercule jaribu kuforce ikamate 3G Only! Kama umeset auto.. All the time EDGE minara iko full so inapewa first piorty.. Kitu hku ni swafi kabisa baadae nataka nweke tena Airtel nwotch epl.
 
jaribu kuforce ikamate 3G Only! Kama umeset auto.. All the time EDGE minara iko full so inapewa first piorty.. ..baadae nataka nweke tena Airtel nwotch epl.

Dah! Kwa akina sie hizo teminology na technical settings tutaweza kweli??

Mwisho wa siku watumiaji wote wa Modems tutakua mafundi wa IT sasa. Mweee.....!!??
 
Miezi 6 bure?lugha za biashara 2 hizo yan utakuta kila mwezi wanakupa 400mb ila wanavyoongea utadhani ni unlimited for 6 months..ngoja walionunua watujuze

inaanza saa sita mkuu...nadhani wanatoa mb 200
 
mkuu.....mimi nimekinunua leo hii....
ki ukweli kina speed fulani ambayo sielewi sana lakini ukikiweka kwenye laptop kinajiset chenyewe na speed ni nzuri.....
tatizo linakuja......hii free internet ya miezi 6 inatoka wapi....?....wabongo na bure unatujua tena......
wakati nakinunua kulikuwa na watu wengi so nikaona muuzaji kachanganyikiwa kwa maswali....nikaona isiwe tabu nitauliza customer care.....
kupiga customer care kuuliza....muhudumu wa kwanza akanipotezea akakata simu.....
wa pili alikiri kwamba.....kweli sijui hiyo free internet inakujaje kujaje naomba unisamehe jaribu kuuliza tena kesho.....
binafsi nimebaki kwenye mataa.....naendelea nayo kwa bundle yangu ya kawaida......
ila speed mwanakwetu.....iko mwake.....
 
Dah! Kwa akina sie hizo teminology na technical settings tutaweza kweli??

Mwisho wa siku watumiaji wote wa Modems tutakua mafundi wa IT sasa. Mweee.....!!??
Mkuu nivizuri kusema haujaelewa wap kuliko kulalamika..
 
Back
Top Bottom