hii ni ya kienyeji

hii ni ya kienyeji

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2006
Posts
4,192
Reaction score
680
juzi kati nilikuwa na jamaa yangu mmoja akanihadithia mkasa wa kweli ambao nilicheka sana, na nnaona ni jambo jema kizuri kula na wenzio. sasa wacha niimwage hapa





anasema kuna jamaaa mmoja alitembelewa na baba toka kijijini kwao hapo kwake da re salam, sasa alikaa kama wiki moja, siku ya baba kurudi kijijini, mtoto alimchukua baba yake na kupita nae kwenye ATM machine na kutoa kama laki tatu na kumkabidhi baba kwa ajili ya nauli na matumizi kule kijijini, kisha akampeleka Ubungo kwa safari

kama baada ya siku mbili, akapokea simu kutoka kwa Baba Mdogo akitaka amtumie kama shilingi laki mbili, jamaa akamtumia. kama siku tatu hivi shangazi nae akataka atumiwe mapeni. na kila siku zikienda waombaji wanaongezeka na wanaomba dau kubwa.


mtoto akampigia simu mama yake kumsikitikia kuhusu hio tabia iliozuka, mama akamwambia mwanawe kuwa yote hayo baba yako huyo, amewaambia watu wewe mjini uko na kibanda cha pesa unaenda kuchukua tu
 
Alichemsha kweli,madingi si wa kwenda nao huko.
 
hizi ndo komed, manake inasound ukweli na inachekesha.
 
Mbona wa hivyo wapo wengi, kuna mwingine anaombwa elfu tano anatoa pochi nzima na minoti ya buku kumi anaanza kuchanmbua mbele ya mtu then ana mpa elfu kumi. Inaonyesha huna mahesabu katika maisha.
 
Back
Top Bottom