MWANAHARAMU
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 5,171
- 13,231
Nilioa mnamo mwishoni mwa 2020 kwa ndoa ya kulazimisha.
Kifupi ndoa hii haikuidhinishwa kwa moyo mmoja na wazazi wake,
isipokuwa Babu yake na bibi yake ndio waliisimamia kidete, na kunisapoti nimuoe mjukuu wao.
Wazazi wake waliapa kuwa hawatoshiriki kwenye hii ndoa, hivyo ikabidi ifungwe nyumbani kwa Babu yake.
Sherehe kubwa ilifanyika kwao na kwetu, kabla ya kuelekea ukumbini siku ya jumapili ila wazazi wake hawakuhudhuria zaidi ya bibi na babu yake na ndugu wengine.
Mtu niliyemuoa hakuwa mpya kwenye maisha yangu, kwani nilianza nae mahusiano nikiwa kidato Cha sita wakati yeye akiwa form III.
Hivyo mwaka 2012 wakati yupo kidato Cha nne, alijigundua ni mjamzito kipindi wanajiandaa na mtihani wa Taifa.
Akaja kwangu akiomba pesa atoe, nami nikamkatalia nikimwambia akitoa ajue Mapenzi yetu yameishia hapo, ila kabinti kakang'ang'ania Kutoa hivyo kuachana bila kukubaliana.
Mimi nilikuwa kwenye kipindi Cha kujiandaa ili nikajiunge chuo kcmc Kilimanjaro.
Ila baada ya Ile Taarifa ikabidi nikamshirikishe baba yangu mzazi anipe ABC nini Cha kufanya.
Mzee akanambia tunabadilisha program Yale masuala ya chuo weka kando, nenda kajiunge kule kunakoogopwa na wengi, ili uweze kumlea mwanao halafu baada ya miaka mitatu nitakufanyia mpango uludi chuo.
Hivyo basi kupotea mtaani ila kosa nililofanya kutomuaga bibie na Mimi kutojuwa msimamo wake kama atatoa au atalea.
Kifupi ndoa hii haikuidhinishwa kwa moyo mmoja na wazazi wake,
isipokuwa Babu yake na bibi yake ndio waliisimamia kidete, na kunisapoti nimuoe mjukuu wao.
Wazazi wake waliapa kuwa hawatoshiriki kwenye hii ndoa, hivyo ikabidi ifungwe nyumbani kwa Babu yake.
Sherehe kubwa ilifanyika kwao na kwetu, kabla ya kuelekea ukumbini siku ya jumapili ila wazazi wake hawakuhudhuria zaidi ya bibi na babu yake na ndugu wengine.
Mtu niliyemuoa hakuwa mpya kwenye maisha yangu, kwani nilianza nae mahusiano nikiwa kidato Cha sita wakati yeye akiwa form III.
Hivyo mwaka 2012 wakati yupo kidato Cha nne, alijigundua ni mjamzito kipindi wanajiandaa na mtihani wa Taifa.
Akaja kwangu akiomba pesa atoe, nami nikamkatalia nikimwambia akitoa ajue Mapenzi yetu yameishia hapo, ila kabinti kakang'ang'ania Kutoa hivyo kuachana bila kukubaliana.
Mimi nilikuwa kwenye kipindi Cha kujiandaa ili nikajiunge chuo kcmc Kilimanjaro.
Ila baada ya Ile Taarifa ikabidi nikamshirikishe baba yangu mzazi anipe ABC nini Cha kufanya.
Mzee akanambia tunabadilisha program Yale masuala ya chuo weka kando, nenda kajiunge kule kunakoogopwa na wengi, ili uweze kumlea mwanao halafu baada ya miaka mitatu nitakufanyia mpango uludi chuo.
Hivyo basi kupotea mtaani ila kosa nililofanya kutomuaga bibie na Mimi kutojuwa msimamo wake kama atatoa au atalea.