Hii ngumu kumeza

Hii ngumu kumeza

Status
Not open for further replies.
Ni miezi kama miwili imepita tangu nimalize chuo na kurudi nyumbani.....lakini hata hivyo nilikuwa narudi kipindi cha likizo kuonana na familia.

Kwanza niseme tu wazi,,,sina desturi ya kukagua simu ya mkewangu lakini baada ya kumtilia mashaka ilibidi nifanye hivyo.

Nikweli nilichokikuta inbox ya Facebook ni hiyo conversation kati ya wife(chati ya bluu)

na jamaa ambae namjua na ni mfanyakazi mwenzangu pia na nlikuwa namheshim sana.
Hiyo conversation inaonesha watu hawa ni wapenzi wala haihitaji nguvu ya ziada kugundua hilo.

Wadau hii kitu nilikuwa nasikia tu kwa watu kumbe ni kweli aisee inauma sana usiombe yakukute....

Imagine mtu tuko nae over ten years sasa pamoja na watoto wawili Leo hii ananifanyia hichi kitu..

Afadhali hata ningekuwa na tabia ya kuchepuka nisingeumia sana.....ningejisemea tu moyoni kwamba malipo ni hapahapa duniani , muosha huoshwa.

Lakini kinachoniuma Mimi nimekuwa mwaminifu tangu nilipomuoa sijawahi msaliti hata Siku moja.

Wakuu embu nisaidieni experience kwa wale mliopata maswahibu kama haya au hata kama hayajakupata nishauri tu kabla sijaharibu Niko na hasira sio ya kawaida ingawa sijionyeshi kwake.....View attachment 897325
Hawa wanatiana kabisa tena wamemisiana kama miez miwili hawajadinyana
 
My broo kweli mkeo anafanya makosa ok lakini japo na hilo analofanya kwani hana mazuri anayokufanyia yanayokurahisha ukiachia na hilo analofanya kabla ya kuamua kuachana nae chunguza hilo,kama asilimia kubwa ana maudhi hakufurahisha unaweza kuamua unavyotaka kama anakufurahisha asilimia nyingi si vema kumuacha haijalisha hata kama anatembea na rafk yako,kaa nae mueleze makosa yake akikubali na akiomba msamehe,hiyo pia ni changamoto za ndoa sio mazuri kila siku,ww ungemchiti hata na ndugu yake wa damu na uhakika angekusamehe,hivyo tu kama utajal
 
Mkuu pole sana;penzi lako kwa mkeo linahitaji 'restoration' kama unaweza kumtoa 'out' fanya hivyo na mkiwa huko jaribu kujadiliana hilo suala kwa upole....nadhani utapata muafaka.
Mkuu una roho ngumu sana. Kwa kipi hasa? Mtu ambaye amelelewa na wazazi wake,ukakutana kwenye mahusiano na baadae ndoa,kamwe siyo ndugu yako na kamwe hafai kumng'ang'ania. Atakuliza. Kipee namshauri kama jambo hilo ni kweli amuache mara moja.
 
Mkuu una roho ngumu sana. Kwa kipi hasa? Mtu ambaye amelelewa na wazazi wake,ukakutana kwenye mahusiano na baadae ndoa,kamwe siyo ndugu yako na kamwe hafai kumng'ang'ania. Atakuliza. Kipee namshauri kama jambo hilo ni kweli amuache mara moja.
Ni wazo jema,ila nikiangalia watoto wanaweza kupata shida huko mbeleni;wengine huwa wanatengana vyumba kwa muda huku wakiangalia kama mhusika amejirekebisha.
 
Mungu aniepushe mbali na mke msaliti maana dunia itashangaa kitakachotokea.

Pole sana mkuu.
Fanya tu kumuambia ukweli juu ya anachokifanya na ukupe maelezo yanayoeleweka.
Siwezi kushauri zaidi ya hapo maana kama ingekuwa kwangu huyo msela angezindukia ICU wakati huo mke yupo kwao kuepusha mauaji.
 
Maamuzi sahihi unayoweza kufanya bila mazara wala majuto kwako na yatakayo onesha kuwa "you are psychologically matured enough ni ama kumuacha mazima au kumsamehe mazima baada ya kuzungumza nae Kwa kirefu!
Hili la kumsamehe linahitaji kiwango chako cha imani ukibusti Kwa kwenda kuonana na watumishi wa Mungu watakaokueleza faida ya kusamehe na kusahau na hasara za ktutosamehe na kusahau!
Kwa hiyo nakushauri Kabla ya kumuuliza chochote kawaone watumishi wa Mungu wakushauri kutokana na imani yako !
Kama hutaweza kumuachilia Moyoni mwako na kumtamgazia msamaha toka ndani ya kina cha moyo wako basi afadhali umuache Kwa amani bila Shari wala visasi!
Ukijichukulia sheria mkononi kibao kitakugeukia 🏻🏻 Jamhuri itakuhusu!
Kuna Watu wengi wako jera wanasubiri kunyongwa !
Ustaarabu/uungwana wako, ukomavu wako wa kisaikolojia, imani yako inapimwa Kwenye Mitihani Kama hiyo!
Utavukaje hapo salama bila kuharibu upande wako au wake ?!
Tafakali Kwa usahihi na mapana Yake !
 
Pole Ndugu ni vizuri ukawashirikisha Wazazi wa pande zote mbili ikibidi uwashirikishe na viongozi wa Dini.
 
Mkuu muache huyo mwanamke, kuna mengi sana ya kufanya inatakiwa ujikite ili uyakamilishe hakuna haja ya kukumbatia vitu vinavyoumiza moyo, hata maandiko yameruhusu kumuacha mke ambaye ni mzinzi (ukimfumania kwa uzinzi), ukiendekeza utakuja lia sana na kuumia moyo sana. Huo ni mtazamo wangu, yaani mimi mke wangu achepuke lakini nisijue hapo sawa ila nikija kujua namuacha hapo hapo asije akanimaliza. But all in all Mke anauma sana mkuu.
Nahisi wewe ni ndugu yangu ila tumbo tofauti... Ni kweli kuna mambo mengi sana yakufanya
 
Hili swala lilintokea mkuu inauma sana akajibu kirahisi ni amezoea matani nililfikisha kwao but yakaisha mpaka leo cna imani nae .pole jikaze kiume
 
Ningedili sana na huyo mfanyakazi mwenzangu mpk angeona dunia chungu.. Ndoa miaka kumi halafu kuteteleshwa na wanafiki haikubaliki hata kidogo...

Usimwache mkeo kwa sasa fanya maandalizi ya namna mtakavyoweza kuwalea watoto katika kipindi hiki cha mikwaruzano ya nafsi..
 
Wewe nahisi umenielewa......inauma sana Braza!!! Inaniumaaa
Huu ndyo ushauri pekee ambao utauelewa kwa kuwa ndyo maamuzi uliyokwisha yafanya. Naamini ushauri mwingine wowote hutauona kama unafaa.
Ila tu ujue watu hawafanyi maamuzi katika hasira na hatuoani ili tuachane kwa kuwa hatuko wakamilifu
 
Kwa kifupi picha siipati .

Hata nikiomba uhamisho ---Ok hivi sasa ntatizamanaje na wife......... Mtu ambae tulizoea kufurahi pamoja , tuna enjoy maisha., kumbe tunachekeana kinafiki........ behind ananisaliti
Life is everywhere mkuu! umejilimit sana na kuona huyo mwanamke ni kila kiyu kwako...
Chaa kuwa independent and unlimited kwaba you can be anywhere and at any time vinginevyo nyinyi ndio mnaojiua.
I know what I am talking about! badilisha mentality wapo wanawake wengi watakufariji huyo achana nae kama maandiko yanavyosema kwenye Mathayo 19:7-8

Toka kifungoni mkuu hilo jambo ni gumu sana lakufanya hapo tuu ni kumuacha huyo mwanamke! watoto utale mwenyewe au tafuta ndugu zako au dada mwema awalee naamini MUNGU ni mwema atakufungulia njia nyingine baada ya hiyo kufunga.
Mkumbie sana huyo mwanamke mzinzi kwani atakuletea ukimwi akuwahishe kaburini uwaache watoto na wapendwa wako wakiteseka kwa sababu ya tatizo dogo ambalo ulishindwa kuswitch kwa kuoa mwanamke mwingine eti kisa hutamsahau eti umemzoea chaa wapo wengi wamepitia situation kama yako ila wana matumaini kwa sababu the world is endless through the power of GOD we do a lot of things.
Huyo mwingine utakae muoa atatengeneza tena historia kwako na kufuta ya zaman! This is how life it is man.

President Donald Trump ana wake wangapi? is he doing well or not?
Ment wake up sky is he limit.
 
Cheki afya zenu kama ziko poa,toa onyo kali kwa mkeo na huyo mdhalimu.Ili maisha yaendelee...kwa kujifunza angalia kipindi cha 'cheaters tv-youtube' mtu anamkuta mkewe analiwa live na anaamua kusamehe,kutokana na muda walioishi inakuwa si rahisi kuachana.
Afadhali ww umeshauri kikubwa kama mtu mwenye familia wengine wanaongelea kirahis sabbu hawako kwenye situation kama hyo.

Wanawake hua wanavumilia mengi ndan ya ndoa lkn sabbu tu ya watoto wao wanaamua kusamehe na kusonga mbele
Ukiangalia ndoa ina miaka mingi sana..
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom