Hii ndoto inamaanisha nini?

Hii ndoto inamaanisha nini?

Ebana eeh wiki kama moja nyuma pia niliota kitu inataka fanana na hii ila mimi niliota sehemu ambayo nilishawahi kuipita sasa ajabu ni kwamba hiyo sehemu sio route yangu ya kila siku na niliwahifika kwa mara moja tu.

Ajabu ni pale kesho yake nikiwa nimesahau kabisa si ni kajikuta nipo sehemu ile ile sasa nikawa naona kabisa hiyo sehemu nilikuepo ila sikumbuki vizuri, wakati navuta kumbukumbu nikaiona picha kamili ya vile niliota na ndio sehemu nilipo, nilistaajabu kwa muda.
aisee
 
amina kwahiyo haina maana yoyote hii? sikumbuki kuwa na ndoto ya aina hii inanifikirisha mana ndoton naumiza kichwa hapa n wapi uhalisia hivyohivyo tena nikasema kabisambona kama hapa sio pageni machoni mwangu
Hiyo Haina maana yoyote,

Ni uthibitisho kuwa wewe uliwahi kuwa hapo kabla katika mwili wa kiroho katika Ulimwengu wa Roho wa NDOTO.

Uitishwe,

Ila zipo ndoto za kumtilia maanani, usipuuze ndoto, ni HALISI,

Mfano, mtu akikuendea Kwa mganga, katika Roho lazima upate taarifa Kwa kuota ndoto, sababu wewe ni ROHO,ingawa ndoto itakuwa Kwa mafumbo ambayo utahitaji kufungua codes.
 
Ulikuwa unayaelekea mafanikio…sijui yapi sasa….maadui ni hao minazi mitatu kukuzuia….lakini mbali na vizuizi umeyafikia ila bado maadui hawajachoka kukuharibia….ndiyo maana mbali na kuifikia nyumba lakini bado minazi haijapotea….ni alert kuwa makini
 
Ukifundishwa,

Au ukiamua, unaweza kuchunguza ya sirini Kwa kuomba kabla ya kulala Ili uende katika Roho kufahamu Siri au taarifa Fulani,

Mfano, limetokea tukio la wizi nyumbani kwako, unaweza kuomba kabla ya kulala Ili uonyeshwe ni ni kilitokea uwajue wezi,

Ndoto ni kama tu CCTV camera, unarudisha nyuma na kuona matukio yote.
kuna namna inafundishwa?? naitajuaje nataka kujua
 
Ulikuwa unayaelekea mafanikio…sijui yapi sasa….maadui ni hao minazi mitatu kukuzuia….lakini mbali na vizuizi umeyafikia ila bado maadui hawajachoka kukuharibia….ndiyo maana mbali na kuifikia nyumba lakini bado minazi haijapotea….ni alert kuwa makini
duh shukran
 
Hiyo Haina maana yoyote,

Ni uthibitisho kuwa wewe uliwahi kuwa hapo kabla katika mwili wa kiroho katika Ulimwengu wa Roho wa NDOTO.

Uitishwe,

Ila zipo ndoto za kumtilia maanani, usipuuze ndoto, ni HALISI,

Mfano, mtu akikuendea Kwa mganga, katika Roho lazima upate taarifa Kwa kuota ndoto, sababu wewe ni ROHO,ingawa ndoto itakuwa Kwa mafumbo ambayo utahitaji kufungua codes.
bora umenitoa mawazo kwa hii reply yako
 
Siku kama nne nyuma niliota nipo napita njia ambayo kiuhalisia naijua hiyo njia lakini sikuwahi kuipita, yaani unaiona njia inaelekea huko ila sijajua inaishia wapi nasjawah kujishughulisha kisha nikajikuta nimefikia kwenye kitongoji nimekaa kibarazani nje.

Mbele yangu kuna minazi kwa idadi ni mitatu nikishtuka kulipokucha sikuifatilia sana nikaendelea na shughuli zangu, kimbembe ni leo nimeipita hiyo njia na hiyo nyumba pia ndio nilipofikia na idadi ya minazi ipo vilevile kama nilivyoota sasa nimekuwa najiuliza hii sehemu niliiona wapi nikagundua niliota jaman inanitatiza inawezekanje na inamaanisha nini?
Kila mmoja anaweza kuja na tafsiri yake lakini mwisho wa siku wewe utachagua mbivu au mbichi.
Kuna vyanzo vitatu vya ndoto! Kutoka kwa Mungu! Kutoka kwa shetani! Kutokana na shughuli zetu za kila siku!
Ndoto inayotoka kwa Mungu mara nyingi hujirudiarudia mpaka haakikishe umepata ujumbe na umeelewa na hizo ndoto huwa kama ishara ya onyo au tahadhari! Ndoto za shetani huwa ni dhahiri hakuna kulemba unachokiota kitatokea vilevile au tayari kimeishatokea! Ndoto zinazotokana na mishemishe zetu za kujitafutia riziki huwa sio ngeni zinakuwa zinalenga uhalisia wa shughuli zako za kila siku!
Sasa tafsiri ya ndoto yako na imetokea kama ulivyoota ni mambo ya nguvu za giza (wachawi) ambao wanakupangia cha kufanya kila kukicha unafuata ratiba yao kama ilivyotokea leo! Kama ni Mungu kakuonyesha basi jitahidi kuomba kabla ya kulala wachawi na ulimwengu wa giza wasiingilie ratiba ya maisha yako. Watu wengi siku hizi uenda kwa waganga wa Kienyeji kutaka kufanikisha kila jambo lao kama ni kuoa, kuolewa, kupata jazi, wengine hata kukuamsha usiku na kukufanyisha kazi au kukuingilia kimwili! Kwahiyo leo kama ni Mungu au subconscious ya ubongo imerekodi hiyo ndo hali halisi! Nakushauri omba sana kabla ya kulala
 
Aisee,

Natamani kufahamu kwenye maisha yako mambo unayoyafikiria sana huwa yanatokea kama ulivyoyaona kwenye fikra?

Umeshawahi kutaka kufanya maamuzi fulani ila kukawa na nguvu ya ndani inakuzuia au kukuruhusu? Kama ni ndio hii hali inajitokeza mara kwa mara? Nini kinatokea ukiitii hiyo nguvu na nini kinatokea usipoitii hiyo nguvu?
 
Aisee,

Natamani kufahamu kwenye maisha yako mambo unayoyafikiria sana huwa yanatokea kama ulivyoyaona kwenye fikra?

Umeshawahi kutaka kufanya maamuzi fulani ila kukawa na nguvu ya ndani inakuzuia? Kama ni ndio hii hali inajitokeza mara kwa mara? Nini kinatokea ukiitii hiyo nguvu na nini kinatokea usipoitii hiyo nguvu?
sasa hivi nimeacha kuipatiliza hio sauti lakini naweza kua nawaza jambo kichwan ikaja sauti ndani yangu inanishauri usifanye au fanya hivi au achana nayo nikiitii hua na matokeo mazuri nikipuuzia hua matokeo yake sometimes najutiwa why sikifanya vile ninayofikiria hayatokei kabisaa ninaweza pia tukawa tunaongea jambo nikikuambia hili jambo hatutoboi ujue hatutoboi na hatufiki poppte tena tukijikwamua ndio mbaya zaidi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom