Hii ndo tatu bora ya wagombea wa CCM

Hii ndo tatu bora ya wagombea wa CCM

Status
Not open for further replies.
Hakuna kazi kama ambao wana ahueni kwenye kashfa za rushwa na ufisadi ni Mwandosya na Mahiga hawa wanaweza kupitishwa, wakitaka kurudia uchafu uliofanywa 2005 na Kikwete na mtandao wake ambapo mabilioni ya pesa za kifisadi yalihongwa kwa wajumbe hakuna wa kushindana na fisadi Lowassa na fisadi Magufuli. Wote hawa hakuna atakayefua dafu kwa mgombea wa UKAWA Dr Slaa.

Hakuna kazi ngumu kama kutabiri top 3 ya CC ya CCM.
 
Mpaka kufikia jana jioni tar. 10/06/2015, takriban wanachama 29 wamechukua fomu au kutangaza nia ya kugombea urais wa nchi hii.

Hii ni idadi kubwa sana ya watu kutangaza kutaka urais wa nchi yetu, nadhani kiti cha rais sasa kimeonekana cha kawaida sana, kiasi kwamba kuna ambao wana elimu ya msingi pekee lakini nao wamechukua fomu, kuna ambao wamejiuzulu kwa kashfa za wizi nao wamechukua fomu.

Maoni yangu ni kwamba peformance ya kiwango cha chini iliyooneshwa na rais aliyepo sasa imesababisha hali hii.

Kwa maoni yangu, kati ya wote waliokwishacukua fomu au kutangaza nia; watu watatu wanaoweza kupitishwa na CCM kufikia fainali (mkutano mkuu) ni
1. Mark Mwandosya,
2. Mwigulu Nchemba na
3. John Magufuli
,


Na huenda John Magufuli akawabwaga wenzie katika hatua hiyo na kupewa fursa ya kupeperusha bendera ya CCM. Mpambano kati ya Dr. Magufuli na Dr. Slaa utakua na msisimko wa aina yake.

Tupia maoni yako, unadhani ni nani wana nafasi ya kupitishwa na CCM?

Huyu Gorimahiya wanaemsifu eti anaitwa "the poch boy", vp hafai kweli! Nasikia atachukua form dk za mwisho kabisa! Eti "The Posh Boy", hii Nchi ina vituko kuliko akina sokomoko!
 
Hakuna kazi kama ambao wana ahueni kwenye kashfa za rushwa na ufisadi ni Mwandosya na Mahiga hawa wanaweza kupitishwa, wakitaka kurudia uchafu uliofanywa 2005 na Kikwete na mtandao wake ambapo mabilioni ya pesa za kifisadi yalihongwa kwa wajumbe hakuna wa kushindana na fisadi Lowassa na fisadi Magufuli.

Mkuu sipingi mtizamo wako lakini umetumia kigezo kimoja tu, nchi kila mtu ni fisadi ila tunatofautiana viwango na umaarufu. Hata kwa kigezo hicho bado kupata top 3 ni ngumu maana wapo wengi nao (6, mwezi wa kwanza, mwigulu et al)
 
Acha kuweweseka ww...Lowassa ndio mpango wa CCM...labda uko mbali sana na CCM insiders...as well labda hufautilii wanapokwenda kutafuta udhamini uone NGUVU ZAO KUKUBALIKA NA WANANCHI, Lowassa hata
uunganishe wagombea wengine wooooote CCM hawafikii nusu ya Nguvu na influence za
Lowassa kwa wananchi...!!

Lowasa utamchagua wewe lkn sio mtanzania mwenye akili zake timamu.hana jipya yani.
 
mkoa wa kigoma una watu wa maajabu!!!
hii ni ajabu nyingine baada ya zitto na kabour

duh huyo mzee kweli katia fora hivi aliaga kweli nyumban?? kwamba anaenda kuchukUa fomu?????? jamn yote Tisa ila haka kamzeee kamenichekesha sana
 
Hao uliowaweka kwenye brackets kwa maoni yangu hata kwenye top 5 hawastahili kuwemo, kwa kifupi ni kwamba ni lazima MACCM wampitishe mgombea wao kutoka kwenye huu utitiri kama tukiangalia sifa za kiongozi bora wa kuliongoza Taifa letu katika huu utitiri hakuna hata mmoja. Wote hawa walikaa kimya wakati nchi inaangamia kwa mika kumi ili kulinda maslahi yao ya siku za usoni badala ya yale ya Tanzania na Watanzania na hivyo kuacha ufisadi ukishamiri, rushwa ikishamiri, ujangili ukishamiri, utendaji na uongozi mbovu ukishamiri n.k. hadi kufikia nchi kutoswa na Wafadhili. Walikuwa wapi wote hawa kwa miaka kumi huku nchi ikiangamia!? Mbona hatukuwasikia kukemea madudu mbali mbali nchini yaliyofanywa katika kipindi hicho.

Mkuu sipingi mtizamo wako lakini umetumia kigezo kimoja tu, nchi kila mtu ni fisadi ila tunatofautiana viwango na umaarufu. Hata kwa kigezo hicho bado kupata top 3 ni ngumu maana wapo wengi nao (6, mwezi wa kwanza, mwigulu et al)
 
Hao uliowaweka kwenye brackets kwa maoni yangu hata kwenye top 5 hawastahili kuwemo, kwa kifupi ni kwamba ni lazima MACCM wampitishe mgombea wao kutoka kwenye huu utitiri kama tukiangalia sifa za kiongozi bora wa kuliongoza Taifa letu katika huu utitiri hakuna hata mmoja. Wote hawa walikaa kimya wakati nchi inaangamia kwa mika kumi ili kulinda maslahi yao ya siku za usoni badala ya yale ya Tanzania na Watanzania na hivyo kuacha ufisadi ukishamiri, rushwa ikishamiri, ujangili ukishamiri, utendaji na uongozi mbovu ukishamiri n.k. hadi kufikia nchi kutoswa na Wafadhili. Walikuwa wapi wote hawa kwa miaka kumi huku nchi ikiangamia!? Mbona hatukuwasikia kukemea madudu mbali mbali nchini yaliyofanywa katika kipindi hicho.

Ndo maana nilisema ni vigumu sana kutabiri top 3 ya ccm kutokana na sifa na sababu mbalimbali. Ulianza na ufisadi sasa umekuja na kufumbia macho mambo mengi. I still believe that the screening process isn't an easy job for cc
 
1, Mkuu mwaka huu tunapata rais kiongozi na mchapa kazi P MAGUFULI, hatutaki rais
2,tutapata baraza la mawaziri makini na wachapa kazi,sio urafiki wa kijinga husio na tija,
3 akiwa rais naona watumishi wote wakipewa viapo vya uhadirifu kama alivyofanya kwa wakandara wasio waaminifu.
 
Kufumbia macho uozo wa miaka kumi nchini ndiyo yale yale ya ufisadi na rushwa, hawa walioamua kufunga macho nao wana madhambi yao kwa hiyo wakaamua ili kulinda maslahi yao ni bora tu wafunike kombe. Kumbuka ile kauli ya Kikwete ya "kulivua gamba" kwa kutaka kuwafukuza CCM ""wachafuzi" wa CCM mafisadi Lowassa, Rostam, Chenge na wengineo wengi lakini baada ya kutishwa kwamba yeye akianza wao watamaliza na "Ikulu hakutalalika" kauli ile ikaanza kukimbiwa na wengine ndani ya CCM hata kukanusha kauli ile ilimaanisha nini. Ndiyo sababu nilihitimisha kwamba katika huu utitiri hakuna mwenye sifa hata mmoja ndio sababu wakajaribu tena kumshawishi SAS ili abadili msimamo wake na hata Augustino Ramadhan, ila hilo la CCM kuwa na mgombea wao ni lazima walikamilishe pamoja na kuwa kwenye huu utitiri hakuna anayestahili.

Ndo maana nilisema ni vigumu sana kutabiri top 3 ya ccm kutokana na sifa na sababu mbalimbali. Ulianza na ufisadi sasa umekuja na kufumbia macho mambo mengi. I still believe that the screening process isn't an easy job for cc
 
Wrong analysis...ili hao wafike Mkutano mkuu inategemea NEC watakuepo na watu gani...Labda useme hao 3 watafika NEC not otherway around
 
Kumbuka ile kauli ya Kikwete ya "kulivua gamba" kwa kutaka kuwafukuza CCM ""wachafuzi" wa CCM mafisadi Lowassa, Rostam, Chenge na wengineo wengi lakini baada ya kutishwa kwamba yeye akianza wao watamaliza na "Ikulu hakutalalika" kauli ile ikaanza kukimbiwa na wengine ndani ya CCM hata kukanusha kauli ile ilimaanisha nini. Ndiyo sababu nilihitimisha kwamba katika huu utitiri hakuna mwenye sifa hata mmoja ndio sababu wakajaribu tena kumshawishi SAS ili abadili msimamo wake na hata Augustino Ramadhan, ila hilo la CCM kuwa na mgombea wao ni lazima walikamilishe pamoja na kuwa kwenye huu utitiri hakuna anayestahili.
This makes a lot of sense ukifuatilia siasa za kutafuta raisi na kauli za makada wenye nafasi za juu lakini si presidential aspirants na wanaowania kikubwa ni agenda ya kuvua gamba kama imeibuka tena.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom