Nimekuwa nikifuatilia kwa muda mrefu hali ya kisiasa nchini na kile kinachoitwa maridhiano. hali hii imenifanya nitafakari jambo hili kwa muda mrefu na kuona nitoe maoni yangu kwenye forum hii ili waungwana mpime na mjiridhishe kabisa kwamba Chama Cha mapinduzi hakitaki maridhiano na hakina nia ya dhati kutekeleza hayo yanayoznungumzwa kama majadiliano.
Mwanzoni kabisa katika kipindi cha awamu ya kwanza ya muhula huu tuliambiwa kwamba kuna 4R ambazo ndio muongozo wa mama katika kuleta muafaka wa kitaifa na kulikuwa na kila dalili kwamba tunakoelekea kama taifa tulikuwa tunaelekea kuzuri; hizi 4R ziliishia wapi?
Baadae ikasemekana kwamba kuna mazungumzo kati ya CCM na chama kimojawapo lakini mazungumzo hayo wakati yanataka kufikia mwisho CCM wakaweka ngumu kwa maana ya kwamba hawakutaka yaingie kwenye maandishi.
Hata hivyo wadau mbalimbali walitka maridhiano hayo yafanyike kabla ya uchaguzi na walienda mbali kwa kusema mfumo wetu wa kuchaguana haujakaa vizuri;sio ndani ya vyama lakini hata vyama kwa vyama uwanja haujakaa sawa;vi vema siku zikasogezwa hata kama ni miaka mitatu mbele utengenezwe mfumo bora wa uchaguzi lakini hoja hiyo ikakataliwa.
Dhana kubwa ya maridhiano ni katiba mpya,tume huru ya uchaguzi,haki na kwa sasa yanaongezeka mengine kulingana na wadu wanavyotoa hoja zao
Kinachoshangaza Makamu wa rais siku za hizi karibuni alitoa maoni yake juu ya issue ya katiba;kejeli anazozipata kutoka kwa wana ccm wenzake zina ashiria kweli kwamba kuna maridhiano
Sasa hivi kuna ushawishi mkubwa wa kutaka watu waingie kwenye maridhiano;lakini kuna mambo ya kujiuliza hapa;
1. Maridhiano hayo ni ya nini?
2. Wanaridhiana nani na kwa nini?
3. Kuridhiana ili iweje?
HITIMISHO: CCM HAITAKI MARIDHIANO;wangekuwa wanataka maridhiano wangeyafanya tu hata bila kutaka vyama ambavyo havitaki maridhiano kushiriki na kiufupi maridhiano sahihi yalipaswa kwa kuanza mchakato wa katiba mpya na kuweka mfumo mzuri wa kuchaguana kitu ambacho ccm hawawezi na wala hawataki.
kwa maana nyingine issue ya maridhiano ni dhana tu na kujazana uongo.
Mwanzoni kabisa katika kipindi cha awamu ya kwanza ya muhula huu tuliambiwa kwamba kuna 4R ambazo ndio muongozo wa mama katika kuleta muafaka wa kitaifa na kulikuwa na kila dalili kwamba tunakoelekea kama taifa tulikuwa tunaelekea kuzuri; hizi 4R ziliishia wapi?
Baadae ikasemekana kwamba kuna mazungumzo kati ya CCM na chama kimojawapo lakini mazungumzo hayo wakati yanataka kufikia mwisho CCM wakaweka ngumu kwa maana ya kwamba hawakutaka yaingie kwenye maandishi.
Hata hivyo wadau mbalimbali walitka maridhiano hayo yafanyike kabla ya uchaguzi na walienda mbali kwa kusema mfumo wetu wa kuchaguana haujakaa vizuri;sio ndani ya vyama lakini hata vyama kwa vyama uwanja haujakaa sawa;vi vema siku zikasogezwa hata kama ni miaka mitatu mbele utengenezwe mfumo bora wa uchaguzi lakini hoja hiyo ikakataliwa.
Dhana kubwa ya maridhiano ni katiba mpya,tume huru ya uchaguzi,haki na kwa sasa yanaongezeka mengine kulingana na wadu wanavyotoa hoja zao
Kinachoshangaza Makamu wa rais siku za hizi karibuni alitoa maoni yake juu ya issue ya katiba;kejeli anazozipata kutoka kwa wana ccm wenzake zina ashiria kweli kwamba kuna maridhiano
Sasa hivi kuna ushawishi mkubwa wa kutaka watu waingie kwenye maridhiano;lakini kuna mambo ya kujiuliza hapa;
1. Maridhiano hayo ni ya nini?
2. Wanaridhiana nani na kwa nini?
3. Kuridhiana ili iweje?
HITIMISHO: CCM HAITAKI MARIDHIANO;wangekuwa wanataka maridhiano wangeyafanya tu hata bila kutaka vyama ambavyo havitaki maridhiano kushiriki na kiufupi maridhiano sahihi yalipaswa kwa kuanza mchakato wa katiba mpya na kuweka mfumo mzuri wa kuchaguana kitu ambacho ccm hawawezi na wala hawataki.
kwa maana nyingine issue ya maridhiano ni dhana tu na kujazana uongo.
