Hii ndo tatu bora ya wagombea wa CCM

Hii ndo tatu bora ya wagombea wa CCM

Status
Not open for further replies.
Huyu ni mkulima mmoja mwenye elimu ya STD 7 ambaye kaomba fomu huku akisema kama JK kaweza hata yeye anaweza na pia hana kashfa yeyote ya rushwa wala ufisadi

Kazi kweli kweli .................................!!!
 
Nec top 3
1.Lowasa
2.Membe
3.j.makamba

Nec top 5
4.M.mwandosya
5.J.Magufuli

Nec top 10
6.Mwigulu nchemba
7.S.muhongo
8.Samweli sita
9.Ramadhan bilal
10.kigwangala
 
Watanzania tukoje, mtu akitoa hata statistics za uwongo tunamuona ndio anafaa. Muhongo hafai
Hahahaaa!
Tatizo la upinzani ndio hili.
Sema sasa yupi anastahili,
sio una crush bila points zako..
 
Hajapitishwa Slaa, ila nadhani kwa UKAWA, yeye ndo anapewa nafasi kubwa zaidi akifuatiwa na Lipumba. Kwa kweli huyu jamaa (Dr. Slaa) ndo anayewanyima usingizi watu wa ccm


Uko sawa kabisa. yaani ccm wakisikia Dr. Slaa ndio atakuwa mgombea wa Ukawa wanachanganyikiwa.
  1. Wanafahamu uwezo wake mkubwa wa kujenga hoja
  2. Upande wa ccm walio bora sio rahisi kupitishwa na chama chao kwani kimetekwa na wauza unga, wezi na mafisadi
  3. Kila mmoja wao anajua mwaka 2010 Slaa hata kama hakushinda basi JK alimshinda kwa kura ambazo hata ni aibu kizitaja hapa, na kile kitendo cha kutaka umma ujitokeze kupinga matokeo ya uchakachuaji ule lakini viongozi wa dini wakamsihi kwa maslahi mapana ya taifa. Wanajiuliza je safari hii na huu mwamko iwapo atachaguliwa na ukawa ni dhahiri atashinda na wao hawako tayari kuachia madaraka kwa hofu ya kuishia jela na kufilisiwa mali zao walizochuma kwa wizi. Na ukitaka kuamini hilo wewe anzisha uzi usemao Ukawa ili washinde lazima wampitishe Dr. Slaa, nakuambia hata zile ID zilizokuwa zimelala zitaamka kutoa mashambulizi ya personal attack bila hoja, hawatolala mpaka waone watu wameacha kuchangia kwani hiyo mada itachafuka na kejeli kibao, matusi mengi, huku udini na ukanda ikiwa ndio hoja ya msingi. Acha kabisa kitu inatwa Slaa kuelekea uchaguzi wa october, viongozi wa ccm wanaweza kufa kwa kihoro. Angalia hata tathmini yao kwa mgombea wao kila mmoja wanajiuliza atamuweza Dr. Slaa? Wote wanapata hofu ya ajabu kwani huko ccm wasafi hawawezi kupita kwani sasa ccm ni ccm maslahi na sio ccm uzalendo.
 
"mimi nawaomba watanzania waniamini na waone kuwa mimi ninekaa nikajifikiria sana kuwa nafaa kubeba jukum hili.

Pia rais wa mwaka huu awe na sifa zifuatazo
🌂asiwe mbabe
🌂asiwe na jazba
🌂awe mwenye kuwaunganisha watu
🌂awe mstahimilivu
🌂awe muadilifu kwa watanzania.
🌂asiwe mtu wa kulipiza visasi"
hayo ni maneno aliyoyasema william ngeleja akiwa anachukua form ya kuwania urais kupitia ccm
 
Nahisi huyu mzee ametumika kukacover something, ivi nani wengine walichukua fomu/tangaza nia siku moja na huyu mzee, lets thing a bit outside the box.
 
1. Dr A Mahiga
2. Prof Mark Mwandosya
3. Samwel Sitta
 
Tano bora
1. Pinda
2. Mwandosya
3. Magufuli
4. Nchimbi
5. Wasira

Tatu bora
1. Pinda
2. Mwandosya
3. Magufuli
 
Lowasa aliomba ridha ya chama chake mwaka 1995 alikosa, na mwaka 2015 anaomc tena sio uroho wa madaraka kakini pia amewahi kuwa waziri mkuu alijiudhulu kwa kashfa ya Richmond, leo tumpe urais mtu ambaye alidumu kwa miaka 2 tu nafasi ya uwaziri mkuu na kisha kutuibia shilingi milionh 152 kila siku, tukimpa urais itakuwaje ? Nyerere alimkataa. Kama wana CCM wanamuenzi mwl Nyerere waanze na kumshughulikia Lowasa
 
Kama wana CCM watampitisha Lowasa itadhirisha kuwa ni chama ambacho hakina nia ya dhati kuwakomboa watanzania kutoka kwenye lindi la umasikini linalo sababishwa na rushwa, ufisadi, mmomonyoko wa maadili na mengine mengi. Lowasa alipokuwa waziri mkuu alitumia madaraka vibaya hata akajianzishia Richmond, akiwa waziri wa kilimo na mifugo alijimilikisha sehemu ya mbuga. Je akiwa rais atatuacha ? anahubiri ajira kwa watanzania ili hali BOT akiwa waziri mkuu alijaza nafasi kwa watoto wa vibopa. Tanzania tusitegee rais bora kutoka CCM, CCM kwa sasa wamechoka hata akitokea mtu tunaeamini atafanya kazi vizuri atabanwa na mfumo mbovu wa CCM
 
Huyu atashindwa kupitishwa kwa kigezo cha elimu tuu, lakini sidhani kama anayo kashfa yeyote ya kimaadili kama hao uliowataja.
View attachment 259125

Huku nako ni kukurupuka kwa kijinga. Hivi hata huko Kasulu anakotoka haipo ofisi ya Wilaya au hata ya tawi lake la ccm? Ni kwanini wasimwambie na mapema kuwa kigezo cha elimu kitamrusha nje na kumwacha milioni yake ikaenda kuungulia Dodoma? Hivi kwa wakati tulio nao ni nafasi ipi kwenye jamii anayoweza gombea na darasa lake la saba zaidi ya balozi wa nyumba kumi?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom