Kati ya vitu vilivyonisikitisha katika mchakato wa uchukuaji fomu za kuelekea Magogoni mwaka huu wa 2015, ni kitendo cha Ofisi ya CCM Makao Makuu kuchukua fedha za mwananchi wa Kigoma (Tshs. 1,000,000.00) wakati tayari walishaweka vigezo 13 na kimojawapo kikisema mgombea lazima awe na elimu kiwango cha chini iwe ni Chuo Kikuu au elimu inayoendana na kiwango hicho.
Ushauri wangu Chama kimrejeshee fedha yake kwa nia njema tu, kwani inaonekana walipiwa pande zote mbili(Waandaa vigezo na mchukua fomu), labda kama vigezo vile vilitajwa kumaanisha kitu kingine. Nachelea kusema huu sasa ni utapeli