matunduizi
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 6,596
- 15,393
Sababu kubwa ni laana za kuwapa wanadamu wenzao nafasi ya au karibu na Mungu.
Hii laana husababisha wahusika kutoridhika na matunzo ya Mungu wao.
Hivyo kumkinai Mungu, kuwakinai wanaowafuata wakiujua ubinadamu wao na kugeukia atheism kama faraja mbadala. Yesu akija atakuta kundi hili kubwa sana makanisani.
Hii itatokea kwa dini zote.
Kwa waislam mtume mohammad anakuzwa katika hadhi almost sawa na Allah kiasi kwamba huwezi kumtaja Allah bila kumtaja na yeye wakati Allah alikuwa na mitume zaidi ya Laki.
Kwa wakristo na makundi yao karibu wote watamtaja Yesu lakini kuna mtu flani wa kati ambaye anajichotea sifa na hadhi karibu na Yesu (Mungu pamoja nasi).
Huku wako watumishi wanachukia na kuumia wakiona unamtajataja Mungu bila na yeye kumtambua. Hivyo wafuasi kwa kosa hili wanatembea chini ya laana.
Hii imepelekea watu wa dini kuishi katika laana itakayowapelekea kukinaishwa na dini na kubaki tu kwa sababu za kijamii na za kishabiki na sio za kiroho tena.
BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.
Yeremia 17:5
NINI UFANYE?
Anza mazoezi ya vitendo ya kumtegemea Mungu 100% bila kuchomeka mtume, nabii, mtu katikati ya fikra zako.
Hii itakupandisha hadhi juu ya kila mwanadamu na Mungu atakupenda sana. Janjajanja za wanadamu, wasomi, mavuguvugu ya uasi wa mamlaka ya Mungu ya kizazi hiki yatakukwepa.
Ufanye nini sasa
Ufunuo wa Yohana 14:7
... Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.
Ni hayo tu.
Yafanyie kazi upandishe hadhi ubinadamu wako.
Hii laana husababisha wahusika kutoridhika na matunzo ya Mungu wao.
Hivyo kumkinai Mungu, kuwakinai wanaowafuata wakiujua ubinadamu wao na kugeukia atheism kama faraja mbadala. Yesu akija atakuta kundi hili kubwa sana makanisani.
Hii itatokea kwa dini zote.
Kwa waislam mtume mohammad anakuzwa katika hadhi almost sawa na Allah kiasi kwamba huwezi kumtaja Allah bila kumtaja na yeye wakati Allah alikuwa na mitume zaidi ya Laki.
Kwa wakristo na makundi yao karibu wote watamtaja Yesu lakini kuna mtu flani wa kati ambaye anajichotea sifa na hadhi karibu na Yesu (Mungu pamoja nasi).
Huku wako watumishi wanachukia na kuumia wakiona unamtajataja Mungu bila na yeye kumtambua. Hivyo wafuasi kwa kosa hili wanatembea chini ya laana.
Hii imepelekea watu wa dini kuishi katika laana itakayowapelekea kukinaishwa na dini na kubaki tu kwa sababu za kijamii na za kishabiki na sio za kiroho tena.
BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.
Yeremia 17:5
NINI UFANYE?
Anza mazoezi ya vitendo ya kumtegemea Mungu 100% bila kuchomeka mtume, nabii, mtu katikati ya fikra zako.
Hii itakupandisha hadhi juu ya kila mwanadamu na Mungu atakupenda sana. Janjajanja za wanadamu, wasomi, mavuguvugu ya uasi wa mamlaka ya Mungu ya kizazi hiki yatakukwepa.
Ufanye nini sasa
Ufunuo wa Yohana 14:7
... Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu yake imekuja. Msujudieni yeye aliyezifanya mbingu na nchi na bahari na chemchemi za maji.
Ni hayo tu.
Yafanyie kazi upandishe hadhi ubinadamu wako.