Salaam, Shalom!
Palikuwepo manabii wengi Katika agano la kale, mfano Adam, Nuhu, Musa, Elia, Nehemiah, Daniel nk nk.
NABII katika Agano la kale na kuishia kwa Yohana Mbatizaji,waliishi maporini kujitenga na UOVU kuepuka kuona, kusikia UOVU Katika mikusanyiko ya watu, ingawa SI wote, manabii hawakuoa ingawa baadhi walioa, hawakujenga au kuanzisha makanisa kama sasa, ukiona mtu anajenga nyumba ya ibada na kuhudumia watu, huyo ni mchungaji mwenye karama ya unabii, Mungu akimwita nabii akafungue kanisa, huyo ni mchungaji lakini ndani ana karama ya unabii.
TAFSIRI YA NABII.
Nabii ni mtu aliyeteuliwa na Mungu , mtu huyo, kinywa chake, Mungu hukitumia kunena yatokayo kwa Mungu, kuelekea nchi na JAMII husika.
Nabii Musa kwa Mfano, aliongea na Mungu direct, au kwa maono au kupitia ndoto Kisha akaja kuleta ujumbe wa Mungu kwa watu wa Mungu.
Uandishi pia wa Biblia, wote, ni manabii walipokea neno kwa njia ya kusikia,maono au ndoto Kisha wakaandika walichosikia Katika gombo na vitabu mbalimbali ambavyo ndivyo vilivyokusanywa kupata Biblia.
NABII WA MWISHO NI NANI.
Yesu Kristo ameweka wazi, nabii wa Mwisho ni Elia/ Yohana Mbatizaji, na hakuna mwingine baada yake kwa sababu baada ya Yesu kuja, akazaliwa, kufa na kufufuka, hapatatokea nabii mwingine yoyote atakayeleta unabii wowote kinyume na INJILI YA AGANO JIPYA YA KUZALIWA ,KUFA, KUZIKWA NA KUFUFUKA KWAKE YESU KRISTO.
Hivyo ukisikia nabii mwingine yeyote amekuja na kuleta habari tofauti na injili ya ufalme ya YESU KRISTO aliyezaliwa,aliyekufa,akazikwa na kufufuka, huyo ni nabii wa uongo aongozwaye na Roho ya mpinga Kristo.
TAFSIRI YA NABII KATIKA AGANO JIPYA.
Nabii katika Agano jipya ni mtumishi wa Mungu anayehubiri Neno la Mungu kwa nguvu za Roho mtakatifu. Ni aliletaye neno kutoka kuandikika, likatamkika na kuwa hai na kuleta matokeo halisi.
Nabii katika Agano jipya ni yule anayeliamini neno na kuhubiri injili kwa Imani na watu wanaamini na kupokea nguvu na neema ya wokovu.
Kwa Tafsiri hiyo, nabii anaweza kuwa Mchungaji kwa maana, kuhubiri injili kwa kuongozwa na Roho mtakatifu ni sharti kwanza usikie sauti iliyo ndani ya neno la Mungu lililoandikwa, Kisha uipokee Katika Roho Kisha uilete kuwa neno ambalo utalitamka kwa kinywa Kisha likasikiwa na watu kwa sikio la Roho na likapokelewa kwa Imani.
Nabii na unabii Katika Agano jipya ni mtu ndani ya kanisa aliye chini ya mchungaji aliyepewa karama ya unabii, na kama nilivyoeleza hapo juu,
Nabii mwenye karama ya unabii( prophecy) ataena kwa lugha, Mungu atatumia kinywa chake kunena injili na ufunuo juu ya Injili, Kisha atatafsiri alichokisema kwa lugha aliyonena kama ni lugha ya malaika au lugha za wanadamu Ili kulijenga kanisa.
TAFSIRI POTOFU YA NABII KATIKA AGANO JIPYA.
Kuna watu wanapotosha nabii na tafsiri ya Nabii kwa kuchanganya na kitu kiitwacho " Jicho/mwonaji" au "macho ya kinabii/ mwonaji".
Ukisikia mtu anawaambia watu akiwaambia Jana ulikula Nini, au kesho utaenda wapi, au ulizaliwa sehemu Fulani, Umesoma Shule Fulani, au jina la mama yako ni Fulani bila kumwambia, huyo SI nabii, ni sehemu tu ya office ya unabii iitwayo uonaji./ Mwonaji./ Macho ya Roho, sasa huyo SI nabii kamili.
PROPHECY:Is to preach the Gospel with power of The Holly spirit/ spirit of JESUS.
Note: WEWE pia unisomaye Katika thread hii ni nabii ikiwa tu Umeokoka, unaye Roho mtakatifu,na unahubiri injili kwa nguvu za Roho mtakatifu.
Mungu awabariki.
Ikiwa hujampa Yesu maisha Yako fuatisha sala hii:
Ee Mungu katika jina la Yesu Kristo, nina kukiri wewe kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yangu, ninatubu dhambi zangu zote, ninaomba unisamehe, ulifute jina langu katika kitabu cha hukumu, uliandike jina langu katika kitabu cha uzima, nipe uwezo wa kuishi maisha matakatifu, dhambi isinishinde, uovu usinishinde, ulevi usinishinde, uzinzi usinishinde, uchawi usinishinde, ninaomba hayo kupitia jina la Yesu Kristo aliye Bwana na Mwokozi wa maisha yangu. Aamin
Palikuwepo manabii wengi Katika agano la kale, mfano Adam, Nuhu, Musa, Elia, Nehemiah, Daniel nk nk.
NABII katika Agano la kale na kuishia kwa Yohana Mbatizaji,waliishi maporini kujitenga na UOVU kuepuka kuona, kusikia UOVU Katika mikusanyiko ya watu, ingawa SI wote, manabii hawakuoa ingawa baadhi walioa, hawakujenga au kuanzisha makanisa kama sasa, ukiona mtu anajenga nyumba ya ibada na kuhudumia watu, huyo ni mchungaji mwenye karama ya unabii, Mungu akimwita nabii akafungue kanisa, huyo ni mchungaji lakini ndani ana karama ya unabii.
TAFSIRI YA NABII.
Nabii ni mtu aliyeteuliwa na Mungu , mtu huyo, kinywa chake, Mungu hukitumia kunena yatokayo kwa Mungu, kuelekea nchi na JAMII husika.
Nabii Musa kwa Mfano, aliongea na Mungu direct, au kwa maono au kupitia ndoto Kisha akaja kuleta ujumbe wa Mungu kwa watu wa Mungu.
Uandishi pia wa Biblia, wote, ni manabii walipokea neno kwa njia ya kusikia,maono au ndoto Kisha wakaandika walichosikia Katika gombo na vitabu mbalimbali ambavyo ndivyo vilivyokusanywa kupata Biblia.
NABII WA MWISHO NI NANI.
Yesu Kristo ameweka wazi, nabii wa Mwisho ni Elia/ Yohana Mbatizaji, na hakuna mwingine baada yake kwa sababu baada ya Yesu kuja, akazaliwa, kufa na kufufuka, hapatatokea nabii mwingine yoyote atakayeleta unabii wowote kinyume na INJILI YA AGANO JIPYA YA KUZALIWA ,KUFA, KUZIKWA NA KUFUFUKA KWAKE YESU KRISTO.
Hivyo ukisikia nabii mwingine yeyote amekuja na kuleta habari tofauti na injili ya ufalme ya YESU KRISTO aliyezaliwa,aliyekufa,akazikwa na kufufuka, huyo ni nabii wa uongo aongozwaye na Roho ya mpinga Kristo.
TAFSIRI YA NABII KATIKA AGANO JIPYA.
Nabii katika Agano jipya ni mtumishi wa Mungu anayehubiri Neno la Mungu kwa nguvu za Roho mtakatifu. Ni aliletaye neno kutoka kuandikika, likatamkika na kuwa hai na kuleta matokeo halisi.
Nabii katika Agano jipya ni yule anayeliamini neno na kuhubiri injili kwa Imani na watu wanaamini na kupokea nguvu na neema ya wokovu.
Kwa Tafsiri hiyo, nabii anaweza kuwa Mchungaji kwa maana, kuhubiri injili kwa kuongozwa na Roho mtakatifu ni sharti kwanza usikie sauti iliyo ndani ya neno la Mungu lililoandikwa, Kisha uipokee Katika Roho Kisha uilete kuwa neno ambalo utalitamka kwa kinywa Kisha likasikiwa na watu kwa sikio la Roho na likapokelewa kwa Imani.
Nabii na unabii Katika Agano jipya ni mtu ndani ya kanisa aliye chini ya mchungaji aliyepewa karama ya unabii, na kama nilivyoeleza hapo juu,
Nabii mwenye karama ya unabii( prophecy) ataena kwa lugha, Mungu atatumia kinywa chake kunena injili na ufunuo juu ya Injili, Kisha atatafsiri alichokisema kwa lugha aliyonena kama ni lugha ya malaika au lugha za wanadamu Ili kulijenga kanisa.
TAFSIRI POTOFU YA NABII KATIKA AGANO JIPYA.
Kuna watu wanapotosha nabii na tafsiri ya Nabii kwa kuchanganya na kitu kiitwacho " Jicho/mwonaji" au "macho ya kinabii/ mwonaji".
Ukisikia mtu anawaambia watu akiwaambia Jana ulikula Nini, au kesho utaenda wapi, au ulizaliwa sehemu Fulani, Umesoma Shule Fulani, au jina la mama yako ni Fulani bila kumwambia, huyo SI nabii, ni sehemu tu ya office ya unabii iitwayo uonaji./ Mwonaji./ Macho ya Roho, sasa huyo SI nabii kamili.
PROPHECY:Is to preach the Gospel with power of The Holly spirit/ spirit of JESUS.
Note: WEWE pia unisomaye Katika thread hii ni nabii ikiwa tu Umeokoka, unaye Roho mtakatifu,na unahubiri injili kwa nguvu za Roho mtakatifu.
Mungu awabariki.
Ikiwa hujampa Yesu maisha Yako fuatisha sala hii:
Ee Mungu katika jina la Yesu Kristo, nina kukiri wewe kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yangu, ninatubu dhambi zangu zote, ninaomba unisamehe, ulifute jina langu katika kitabu cha hukumu, uliandike jina langu katika kitabu cha uzima, nipe uwezo wa kuishi maisha matakatifu, dhambi isinishinde, uovu usinishinde, ulevi usinishinde, uzinzi usinishinde, uchawi usinishinde, ninaomba hayo kupitia jina la Yesu Kristo aliye Bwana na Mwokozi wa maisha yangu. Aamin