Hii ndio Iringa halisi na watu wake

Hii ndio Iringa halisi na watu wake

Ipogoro
 

Attachments

  • 1473840589682.jpg
    1473840589682.jpg
    44.9 KB · Views: 119
Mkuu Barbarosa umetembelea miji mingapi ya Tz, Mbona iringa kama kisarawe tu cjaona kinachokuvutia ww pamoja kuwa ni mji mkongwe, tughorofa twenyewe tunajengwa sasa. Ukifika stand watu/vijana wamelewa tu
 
Mkuu Barbarosa umetembelea miji mingapi ya Tz, Mbona iringa kama kisarawe tu cjaona kinachokuvutia ww pamoja kuwa ni mji mkongwe, tughorofa twenyewe tunajengwa sasa. Ukifika stand watu/vijana wamelewa tu

ukiondoa majiji itaje basi hiyo miji uliyoitembelea wewe tulinganishe
 
Habari za jioni mabibi kwa mabwana,

Bila kupoteza wakati, hebu Leo tutembelee mkoa wa Iringa.

Kwa ufupi,

Jina iringa linatokana na neno lilinga, (which means fort) au boma kwa kiswahili. Mkoa wa Iringa una wilaya nne, ambazo ni Iringa Manispaa, Iringa Vijijini, Kilolo na Mufindi.

Katika elimu, mkoa wa Iringa una shule nyingi za sekondari (ni nyingi kuzitaja) na vyuo vikuu vitatu ambavyo ni;
Chuo kikuu cha Mkwawa
Chuo kikuu cha Iringa
Chuo kikuu cha Ruaha
Pamoja na taasisi nyingine za elimu ya juu zikiwemo chuo cha ustawi wa jamii na chuo cha mafunzo ya Ualimu cha Kleruu.

Shughuli za maendeleo, shughuli za maendeleo katika mkoa wa iringa ni kilimo, ufugaji, usindikaji na biashara.

Kilimo ndio inayochukua nafasi kubwa, hasa katika mazao ya nafaka, mbao, mazao ya biashara kama chai, mazao ya mbogamboga n.k. Bado kuna fursa nyingi hasa katika kilimo cha misitu ya mbao katika wilaya za Kilolo na Mufindi, ambazo hali ya hewa inafaa sana kwa makuzi ya misitu ya mbao. (Fursa hii vijana watanzania changamkieni)

Mpaka sasa mkoa wa Iringa una TV station moja (IMTV) na fm Radio Stations 7
Ambazo ni;
Trap Gang Radio
Ebony FM
Country FM
Nuru FM
Kibla ten FM
Furaha FM
Overcomers FM

Hivi karibuni Iringa imekuwa ni manispaa ya kuvutia sana kuanzia huduma za jamii (umeme, maji, afya na elimu), miundombinu, mazingira na ujenzi wa mji unaokuwa kwa kasi, hali hii pia imechochewa na kukamilika kwa ujenzi wa barabara ya lami inayounganisha Dodoma na iringa, ambapo kwa sasa Kanda ya Ziwa na kaskazini zimeunganishwa na nyanda za huu kusini na kupelekea kufunguka fursa zaidi za kibiashara.
Kwa sasa Iringa ni HUB.

Pamoja na mengine mengi.

Nihitimishe kwa kupongeza serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na pia hongera sana ndugu zangu wana Iringa, ongezeni juhudi.

Asanteni sana.

Iringa town,
View attachment 399626View attachment 399627

View attachment 399628View attachment 399629View attachment 399630

View attachment 399632

View attachment 399634

View attachment 399635

View attachment 399636

View attachment 399637View attachment 399638View attachment 399639View attachment 399640
Kuzuri sana kumbe! Nina hamu sana ya kutembelea Iringa, natumai mwaka huu hautoisha. Asante sana ndugu 'game over' kwa kutuletea huu uzi.
 
mwez wa nane nilikua iringa na ndugu zangu, jion tukafanya mtoko tukakata sana mitaa kumbe wao walikua wanatafuta sehem wapate bia zao. Baada ya kuzunguka bila mafanikio ndo wakauliza iringa hakuna bar? akili zao walitegemea ziwe kama,dar yaan viti viwe nje. wakamuuliza mama mmoja akawaambia mbona mmezipita nyingi tu na nyingine hii hapa. lol
 
Muungwana huongezea nyama kwenye mapungufu sio kuanza kuponda,kwa kweli namsifu mtoa uzi hata kwa picha alizoziweka tofauti na wewe uliyekaa kimya.Kwangi mimi ambaye sijafika imenisaidia kuona taswira fulani kama eneo ambalo liko livable.Hivyo vilivyosahaulika tujuze mkuu badala ya kumkashifu
nilitaka kujua mengi kuhusu mkoa huo nilivyoona Kichwa cha habari kumbe ndani hamna kitu zaidi ya mapichapicha tu.... nimemshauri mkuu akajipange upya atuletee full detail hii ni changamoto nimempa.
 
Safi kama Ulaya siku hizi nitarudi tena huko tangu mwaka 2000 sijafika the cool town Iringa
 
Nashukuru mkuu barbosa, yapo mengi ya kujivunia kuhusu iringa, binafsi nikizeeka nitarudi iringa,
To me This is the best town in Tz.
Picha zangu haziko vizuri ila kama unazo tuletee, ni faraja sana kuona picha za mji wa iringa.

Safi sana Mkuu. Nimejifunza kitu. Kiukweli sijawahi fika Iringa ila natamani nifike siku moja. Inshallah! By the way siyo urudi ukizeeka Mkuu..rudi ukiwa na nguvu uchangie maendeleo ya nyumbani.

Otherwise peace and love!
 
iringa poa sana. nimekaa kaa kidogo wakati huo nikiwa na timu ya watafiti kutoka IHI-DSM.
Babanusa hotel, pale town kati nimekula supu ya samaki na sambusa sana wakati huo nikijipa hifadhi Golf logde!!
 
Umenikumbusha mbali mkuu Frelimo ndo nilikua nakaa then Ilala niliandikishwa darasa la kwanza mwaka 1988 ila kabla ya kuanza shule dingi akapata uhamisho kurudi Dar
papo pouwa iringa siku izi lami tu mpaka mkimbizi,tumaini na flerimo
 
Back
Top Bottom