Jana 2.9.22 majira ya saa saba mchana police walikuwa wanakamata wapiga debe pale daraja la mto Ruaha, walimkimbiza mmoja akakimbilia uelekeo unakotokea mto, wakaenda naye walipofika mbele kukawa na watu wanaoga mtoni, walipoona mtu anapita anakimbia na nyuma yake wanakuja polisi, na wao wakatoka kwenye maji wakaungana naye mbio kuelekea upande wajuu huku wameacha nguo kando ya mto bila kujua aliyeko mbele anakimbizwa kwa kosa gani huku polisi wakizidi kuongezeka, sijui huko walikokimbilia waliishia wapi ila ilikuwa kama cenema