Hii inatokea kwenyeBONGO MOVIES tu

Hii inatokea kwenyeBONGO MOVIES tu

Bujibuji Simba Nyamaume

Platinum Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
78,144
Reaction score
166,077
ni kwenye BONGO MOVIE pekee....leo naanza na 10.....

ni kwenye BONGO MOVIE pekee,flashback ya miaka 6 nyuma hafu unakuta wahusika wana simu za Iphone na Galaxy,laptop za Apple
........................
ni kwenye BONGO MOVIE pekee,maisha enzi za biashara za utumwa ama enzi za uchifu/utemi hafu unasikia maneno kama ''hamna noma'',''dili'',''mzuka''
......................
ni kwenye BONGO MOVIE pekee,mwanafunzi wa high level ama askari wa kiume kichwani ana wave,hafu ''timber'' na kidevuni ndevu
.....................
ni kwenye BONGO MOVIE,mtu anamfumania mwenzi wake na kuishia kuuliza ''mnafanya nini'' au ''whats happening here"
.....................
ni kwenye BONGO MOVIE pekee,watu wanamkimbiza mtu porini wanapita njia zilezile alizopita ''mbaya'' wao hata kama huyo mtu amewaacha umbali mrefu nyuma kiasi cha wao kutomuona kabisa mbele
..............
ni kwenye BONGO MOVIE,mtu akijificha ndani ya pori kubwa wanaomtafuta wanaenda ''straight'' alipojificha
.............
ni kwenye BONGO MOVIE,mtu anamkuta mtu njiani ana matatizo na yeye mwenye uwezo kumuomba ampe msaada huyo mwenye matatizo.
...........
ni kwenye BONGO MOVIE,mtu yupo sebuleni kwake anaangalia tv akiwa amevaa suti na chini ana viatu
...............
ni kwenye BONGO MOVIE pekee,jambazi gari analotumia kwenye ''matukio'' pasipo hata kubadilisha plate number ndilo analotumia katika shughuli zake za kawaida
................
ni kwenye BONGO MOVIE pekee,mtu anayefanya kazi ya uhudumu supermarket ama fresh graduate anakaa kwenye apartment ya maana
............
ni kwenye BONGO MOVIE pekee.......TUPIA YA KWAKO
ni kwenye BONGO MOVIE pekee........ITAENDELEA
 
Mtu yuko kijijini anachota maji kisimani kichwani ana weaving na amevaa hereni za gold
 
Ni kwenye bongo movie tu,mtu anaonyeshwa anatembea tu kwa nusu saa na kisha baada ya hapo unaambiwa "watch out for part 2"
 
Back
Top Bottom