Mida ya saa 12 jioni jamaa kahangaikia gari(daladala) hadi kapata. Kaingia ndani na 500 tu mfukoni halafu ndani wamebanana kiasi kwamba hata kunyanyua mkono wala kujikuna mtu hauwezi.Unaona bwana!
Konda kapita kaanza kudai nauli.Jamaa kaingiza mkono mfukoni, katoka na 10,000.Jamaa kashangaa wee lakini kamshukuru MUNGU kwa baraka hiyo.
KUMBE JAMAA KAINGIZA MKONO KWENYE MFUKO WA MTU MWINGINE!!!!:embarrassed:
Konda kamrudishia chenji yake jamaa bado anamshukuru MUNGU tu halafu akashuka haraka haraka kwenye kituo hata sio chake. Ile kujisachi jamaa kajikuta na jero lake lile lile!
KUMBE KWENYE KURUDISHA MFUKONI KARUDISHA KWENYE MFUKO WA MTU MWINGINE!!!