Heshima kwa watu wanaokuzidi umri

Heshima kwa watu wanaokuzidi umri

i411

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2011
Posts
906
Reaction score
297
pg 28.jpg
Nimeona hii kwa blog ya jamii na wabongo wengi wakawa wanamponda dogo eti yeye hana nidhamu kwavile anaamukia wakubwa na mkono mmoja mfukoni. Nyie waungwana mwaonaje hili dogo kafanya kosa au kuendana na kazi yake yupo sawa kuwa relax.

Mimi naona kwavile dogo anakipaji sio kosa lake manake yeye anafanya tuu mazoezi na kuongeza kipaji chake alichopewa na muumba. Wakina siye ambao miguu imepinda ndo mambo ya heshima mbele sana. Kwawale walio wahi kuomba kazi wanajuu hili swala na wale walioenda kuomba kuoa mtoyo wa mtu wanaelewa somo. Lakini hii isiwe kigezo cha kulaumu watu wengine kama mnavyomuona dogo umri bado anamengi ya kujifunza na yeye yupo kwenye mambo ya kimichezo na watu kwenye hiyo kazi wanatakiwa wawe relax sio wa kupaparika.
 
ni ujinga kumsalimia mtu hasa rais wa nchi yako mkono mfukoni. jamani hata kama jk ametuharibia nchi bado ndiye rais wetu at least a general respect is needed.
huyu dogo ni b.w.e.g.e akili hamnazo.
 
Ya zamani sana hii,dogo nae ana ustaa wa kizamani.
 
dogo amechemka, JK ana age ya dingi yake, Anatakiwa amheshimu kama dingi,
 
kweli mkuu, na hata ukichukulia umri unamlinda! Ila kuna jamaa mmoja (simfahamu jina anaongeaga kwenye kipindi cha sport kizaazaa) nilimsikia siku moja akisema kuwa TZ tumekwama kimichezo pamoja na maeneo mengine sababu ya ukosefu wa elimu. Na alitolea hata mfano wa wanariadha na wechezaji wa Kenya, Uganda, Zambia nk wanavyoweza kufanikiwa kimaisha (career) sababu ya elimu.
Asiyejua elimu inakujaje katika picha hii ya dogo basi naye ni 'group' moja! Maskini kipaji anacho!!
ni ujinga kumsalimia mtu hasa rais wa nchi yako mkono mfukoni. jamani hata kama jk ametuharibia nchi bado ndiye rais wetu at least a general respect is needed.
huyu dogo ni b.w.e.g.e akili hamnazo.
 
Inawezekana mfukoni kaweka mirungi, naogopa isimdhalilishe kwa preside.
 
Inawezekana mfukoni kaweka mirungi, naogopa isimdhalilishe kwa preside.
...Dogo alinimaliza aliporudi kutoka UK kufanya majaribio Westham alishauriwa akirudi bongo apige menu kali na mazoezi sana awe na stamina ya kutosha then arudi tena...yeye akatafuta mchumba na kuoa!!...nadhani haithamini taaluma yake.
 
Huyo dogo ushamba tu ndio unamsumbua, hauwezi kusalimiana na mtu anayekuzidi umri ki namna hiyo, japokuwa Kikwete katufisadi lakini angalau angeonyesha heshima kidogo.
 
Malezi au ulimbukeni tu?

Dogo hana nidhamu kabisa plus uelewa wake ni mdogo sana. Hivi kweli rais wa nchi haji kama Mzee wa Rula ukimuita, hivyo hata kisaikolojia inamaana alishindwa kujiandaa. Ukienda mahakamani unajua kabisa sitakiwi kupiga kelele, hospitali unajua kabisa nitakutana kabisa na wagonjwa n. k. Kwa maoni yangu Ngasa kachemka.
 
Hana adabu kabisa tena hapa ni wakati wamekaribishwa ikulu
attachment.php
 
kwa maadili ya kitanzania, siyo nidhamu kumsalimia anayekuzidi umri kwa mkono mmoja. hata hivyo hii naiona kama backfire kwani jk alishawahi kumsalimia Jacob Zuma kwa mkono mmoja, mkono mwingine ukiwa mfukoni. all in all, it doesnt matter what level of education you have to behave well, morals and family background counts
 
Hii kitu ya wanamichezo kuvaa mitracksuit kwenda ikulu au bungeni uwa inanichefua sana hivi kweli vyama vya michezo vinashindwa kuwapa dress code ya kueleweka au ndio umaskini?
 
ni ujinga kumsalimia mtu hasa rais wa nchi yako mkono mfukoni. jamani hata kama jk ametuharibia nchi bado ndiye rais wetu at least a general respect is needed.
huyu dogo ni b.w.e.g.e akili hamnazo.

Ni kweli... lakini je rationale ya kutokuweka mikono mfukoni ni nini??
 
Back
Top Bottom