kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,310
- 12,607
Kwenye uchaguzi wa 2020 Ni vigumu kusema CCM itashindwa na chama cha upinzani, lakini Vyama vya upinzani vinaweza kupata viti vingi vya ubunge na udiwani kama watamwachia Mh. Membe awe mgombea pekee kwa niaba ya vyama vya upinzani kuliko wakimsimamisha mgombea mwingine akiwemo mh. Lissu.
Baba wa taifa alishawahi kusema kuwa mgombea atakayekuja kuiangusha CCM madarakani atatoka CCM.
Hesabu ni rahisi tu, wasioipenda CCM na wanaoipenda chadema wapo tayari kumchagua yeyote hata kama ni kiazi.
Mh. Membe kama akigombea ataungwa mkono pia na wana CCM wengi na mashuhuri ambao ni rafiki zake na wale ambao wanakerwa na jinsi CCM ilivyo na inavyoendeshwa kwenye awamu ya tano.
Hivyo basi Membe atapata kura za marafiki zake na wanaokerwa na mambo ndani ya awamu ya tano na atapata kura za wasioipenda CCM, wanaotaka mabadiliko na wanaoipenda chadema au ACT, au NCCR.
Shida pekee ya Membe ni ya kile kilichotokea kwa Lowassa na Sumaye kurudi tena CCM.
Kupanga ni kuchagua, maoni tyuu.
Baba wa taifa alishawahi kusema kuwa mgombea atakayekuja kuiangusha CCM madarakani atatoka CCM.
Hesabu ni rahisi tu, wasioipenda CCM na wanaoipenda chadema wapo tayari kumchagua yeyote hata kama ni kiazi.
Mh. Membe kama akigombea ataungwa mkono pia na wana CCM wengi na mashuhuri ambao ni rafiki zake na wale ambao wanakerwa na jinsi CCM ilivyo na inavyoendeshwa kwenye awamu ya tano.
Hivyo basi Membe atapata kura za marafiki zake na wanaokerwa na mambo ndani ya awamu ya tano na atapata kura za wasioipenda CCM, wanaotaka mabadiliko na wanaoipenda chadema au ACT, au NCCR.
Shida pekee ya Membe ni ya kile kilichotokea kwa Lowassa na Sumaye kurudi tena CCM.
Kupanga ni kuchagua, maoni tyuu.