Heri ya mwaka Mpya 2019

Heri ya mwaka Mpya 2019

Soma utamaduni wa kiyahudi.. siku mtoto anapozaliwa, siku anapotahiriwa... tarehe ya kuzaliwa inaandikwa lini... utapata majibu kwanini Xmas ni 25 Dec na isiwe tar 1.
Ni vema kutofautisha biblia na mila za kiyahudi. Kama ilivyo uislamu na uarabu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sherehe za Mwaka Mpya zimekuwapo kwa muda mrefu. Maandishi ya kale yaliyochongwa yaonyesha kwamba Wababiloni waliadhimisha sherehe hizo katika milenia ya tatu K.W.K. Walifanya sherehe kuu ya mwaka mpya katikati ya mwezi wa Machi. Kitabu cha The World Book Encyclopedia chasema kwamba “wakati huo mungu Marduki aliamua mambo ya mwakauliofuata.” Sherehe za mwaka mpya za Wababiloni ziliendelea kwa siku 11 na zilitia ndani maandamano, kutolewa kwa sadaka, na ibada ya kuomba mvua na mazao.

Mwaka mpya wa Waroma ulianza pia mwezi wa Machi katika kipindi fulani. Lakini mnamo mwaka wa 46 K.W.K., Maliki Juliasi Kaisari aliamua uanze Januari mosi. Hapo mbeleni Januari mosi ilikuwa siku ya Janus mungu wa mianzo na mwaka wa 46 siku hiyo ikawa pia siku ya kwanza ya mwaka wa Waroma. Tarehe hiyo ilibadilika lakini sherehe haikubadilika. Kitabu cha marejeo cha Cyclopedia cha McClintock na Strong kinasema kwamba katika Januari mosi watu “walijiingiza katika sherehe zenye fujo na ulevi, na ushirikina mbalimbali wa kipagani.”

Hata leo, sherehe za Mwaka Mpya zatia ndani ushirikina mbalimbali. Kwa mfano, katika maeneo kadhaa ya Amerika Kusini, wengi hukaribisha Mwaka Mpya huku wakisimama kwa mguu wao wa kulia tu. Wengine hupiga mbiu na kufyatua fataki. Watu wa Jamhuri ya Cheki wana desturi ya kula dengu wakati wa Mkesha wa MwakaMpya, lakini siku hiyo Waslovakia huweka fedha au magamba ya samaki chini ya kitambaa cha meza. Desturi kama hizo ambazo hufanywa ili kukinga bahati mbaya na kuhakikisha ufanisi huendeleza imani ya kale kwamba mambo yatakayokuja huamuliwa siku ya kwanza ya mwaka.

Maoni ya Biblia

Biblia yashauri Wakristo ‘wajiendeshe kwa adabu, si katika sherehe zenye makelele ya ulevi.’* (Waroma 13:12-14; Wagalatia 5:19-21;1 Petro 4:3) Wakristo hawashiriki katika sherehe za Mwaka Mpya kwa sababu mara nyingi sherehe hizo ndizo zenye ulevi na mambo mengine ya kupita kiasi yanayokatazwa na Biblia

Kwa wanaotoka Moshi wanajua mwisho wa mwaka huwa 70%wanenda kufanya nini?
Achilia kufahamiana, kusalimia,kujuana vizuri,kurefresh akili n.k
Una sababu nzuri ya kusherehekea? Iweke hapa.
Chanzo chake umekiona?
Je ni agizo kwenye biblia?
SIJAONA KATIKA SIKUKUU HII ILA ULEVI NA UZINZI ULIOKITHIRI
 
Uko sahihi kwa upande uliouona haraka, mtu hunena kiujazacho moyo wake, mimi nili-target recipients mbali mbali basi.

we have readers- friends all over the world. Relax.

Vipi Kichina na Kigiriki pia huvijui?
 
Tunatakia heri ya mwaka mpya, wala sio show off za kibongo, na kujua lugha sio sifa kama washamba wanavyofikiria ni kujua tu lugha wala sio akili nyingi wala sio ubilionea wala sio uheshimiwa; lugha ni lugha tu hata motto miaka 2-3 au 4 anaongea kutegemea na alipozaliwa na aliyemzaa
 
Soma utamaduni wa kiyahudi.. siku mtoto anapozaliwa, siku anapotahiriwa... tarehe ya kuzaliwa inaandikwa lini... utapata majibu kwanini Xmas ni 25 Dec na isiwe tar 1.
Ni vema kutofautisha biblia na mila za kiyahudi. Kama ilivyo uislamu na uarabu

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijakupata.... kwaio unaishi kwa utamaduni upi?? Wa kikristo au kienyeji?
 
Hello wana JF nimeona nianzishe uzi huu hapa ili tukutane tutakiane heri ya mwaka mpya na kupeana jumbe mbali mbali za mafanikio kwa mwaka unaokuja na kuendelea.

Mtakie heri ya mwaka mpya member yoyote hapa na kama una ujumbe wowote wa heri mwachie hapa.

Ujumbe wangu kwenu wana JF wenzangu, kwanza kabisa kwa wale tuliokwaruzana au mliokwaruzana hapa na pale ndani na nje ya JF ningewaomba mmalize tofauti zenu tuanze mwaka mpya afresh, washwalihi wanasema yaliyopita si ndwele tugange yajayo.

Mwaka 2019 uwe wa tofauti kwetu, tuwe positive na kudumsha amani na upendo ndani na nje ya JF. Tusichukiane humu au kudharauliana maana huwezi kujua mtu unaegombana nae humu kesho au keshokutwa mtakutana nae wapi na anaweza kuwa na msaada gani kwako. kutofautiana kupo ila tusicatch feelings mpaka ifikie hatua ya kujenga uadui.

Tuishi kama familia moja ambayo lengo letu lakukutana hapa ni kuburudika, kupashana habari, kuelimika, kujamiiana na masuala mengine mengi mengi ya muhimu katka maisha yetu ya kila siku.

Kikubwa tujue tu kuwa kila mtu ana mapungufu yake na hakuna aliekamilika lakini tukiwa na upendo na umoja hata haya mapungufu yetu yatakuwa hayaonekani kwa wengine.


Niwatakie heri ya mwaka mpya wakuu.

new year.jpg
best-wallpaper-happy-new-year-2019_104729734.jpg
 
dunia imedanganywa na ikadanganyika eti huu ni mwaka 2018!!!
 
Ukitaka kujua mwisho wa ubaya ni aibu ni pale unapodhani ukimweka mwenzio ndani siku zitasimama au maisha hayatoendelea.

Mlisema wakalie krismas segerea wakala na wapo salama.

Mkasherekea wakae ndani hadi mwaka mpya na wamevumilia na Sasa 2019 hii hapa.

Natumai ipo siku mtawaona wakitoka uraiani na watawakuta amjapiga hatua kwa lolote badala yake kila mtakapowaona au mtakapokuwa mkitafakari kuhusu wao mtaumia na kudhoofika kimwili.

Nitake kuwatakia mwaka mpya mwema na ukawe mwaka wa kumshinda mtesi wetu kwa kuutafuta Uhuru uliotekwa na watu wachache wasiokuwa na hofu ya Mungu mioyoni mwako.

Kama Kuna kuzaliwa Basi Kuna kifo na Kama Kuna madaraka pia Kuna kustaafu,Kuna kutawala na mwisho ukatawaliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kisa kuna watu wanalewa & kufanya dhambi tele ndio wewe usifurahi kuuona mwaka mwingine??

basi tusisheherekee lolote ka vipi
 
Kama kichwa habari kinavyojieleza. Naomba mwenye ufahamu anisaidie
Unakuta mtu hadi anafunga duka eti anaenda mkesha wa Xmass au mwaka mpya. Wakati watu ndio wanafanya biashara mda huo. Kisa mchugaji au padre ameagiza watu wakakeshe hadi saa sita.
Hivi najiuliza tu. Ni wapi kwenye maandiko yameandika juu ya kusubiri Xmass au mwaka mpya usiku wa kuamkia tarehe ya tukio.. lakini isitoshe ni kwamba tarehe 25. 12. SIO siku ya kuzaliwa Yesu.
Ndio natambua kabisa kwamba ni vema kumshukuru Mungu kwa ajili ya mwaka mpya au Xmass lakini sio kiwango cha kuacha kazi, mme, mke au familia kwa ujumla. Kisa mkesha
Nijuavyo mimi. Kila mtu anakazi yake na anapenda kazi yake iwe na mafanikio.. hivyo viongozi wa dini kusisitiza kwenda kwa ajiri ya sikukuu hizi ni vizuri tutambue na wao wapo kazini hivyo wanalazimika kutumia maneno ya Aina zote hadi ya kukufanya kuona kazi yako haina thamani zaidi ya kwenda mkeshani.. na ujuwe uwepo wako ndio mafanikio ya kazi yake lakini hajui maslahi yako yameshindikana au umesitisha.
Kwa mwenye kujua maana ya mikesha hii atuambie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom