Hekima inapoita: Mauaji ya Barlow yanahitaji kulaaniwa, kukataliwa na yanalia "haki"

Natamani kukuunga mkono Mkuu Mkandara, kwa matumaini kuwa ulitaka kusema tumefikishwa mahali pa kuchoka.

Nyongeza yangu ni hii: kwamba katika mazingira tuliyonayo sasa, pengine ni busara kuanza kujianda kwa vita ya wao kwa wao, kwa sababu vita si mbaya katika kila maana. Vita inaweza kuwa mapito ya jamii kuboresha nchi. Historia ya mataifa mengi inaonesha vita inao uwezo wa kuboresha nchi. Vita itaboresha Iraq, vita iliboresha Ujerumani, Vita iliboresha ufaransa. Vita iliboresha Marekani. Vita imeboresha Afrika ya Kusini.

Mawazo yaliyosababisha wewe kutoa mchango huu ninaoupatia nyongeza, kwangu yanafanana na mawazo ya mtu mwoga.

Now uwoga unayo nafasi katika kumlinda mtu, lakini mimi nionavyo, amani inayotokana na uwoga wa mmojawapo katika jamii si amani ya haki. Tunahitaji amani ambayo chimbuko lake ni heshima, na heshima katika jamii nyingi imejengwa kwa vita.
Mkuu wangu nimekusikia sana lakini sidhani kama kweli uko tayari kwa vita na kama wewe upo tayari sidhani kama nyuma yako kuna watu watakufuata. Watanzania vuvuzela sana, rutunasema sana lakini inapofikia swala la vita sidhani kama mko tayari isipokuwa kwa sababu za kipumbavu kama hizi.

Hoja yangu haihusu kabisa nidhamu ya woga na huo Uwoga unazungumzia wewe hauwezi kulingana na UPENDO maana neno hili linatoka moyoni na sii hisia bali kuelewa thamani ya UTU wako na mwenzako. Ni rahisi sana kusema binadamu wote sawa lakini pasipo mapenzi hata ukipigana vita basi vita hivyo havitakwisha. Ni rahisi pia kwako kusema Iraq, Marekani na Ujarumani zilipitia vita na hivyo kuboresha maisha yao lakini ulichoshindwa kuelewa ni kwamba UZALENDO wao ndio ulowasukuma kupigana vita dhidi ya kundi jingine, hawakutengana wala kupigana vita pasipo azma inayowajenga wao kwanza. Haya nambie sisi tutaingia vitani kupigana ili iweje?..

Hakuna Vita vya wenyewe vilivyoweza kuwajenga wananchi wake - HAKUNA isipokuwa kuwakwaza zaidi na zaidi na kuwagawa zaidi na zaidi maana nafisini hakuna UPENDO..Hivyo unaanza kufundishana kupendana kisha Uzalendo unalinda ngome zenu na Udugu hivyo hata adui akiingia mnakuwa tayari kujilinda. Tazama leo hii Hata Malawi wanatusimamia kidete kwa kifua mbele kabisa nna sii wao ntu hata Rwanda ya Kagame wanatuona ssi mazuzu na wala hajakosea maana kisha fahamu Tanzania ya Nyerere haipo tena. Kuna makundi makundi yanaypopingana yenyewe na wameisha poteza dira.. wapo wapo tu duniani wakisubiri kama Sii Mungu basi riziki yao itatoka kwa matajiri... wale wenye ndoto ya ONE DAY YES!
 
Kuna jambo moja la kuwekana sawa hapa. ‘Motive’ ya kuuawa Kamanda Barlow bado haijulikani kwa uhakika. Hoja ya MMM imejengeka kwenye assumption kwamba motive ya kifo chake ni chuki za raia dhidi ya polisi, au chuki za wahalifu dhidi ya polisi. Sijui MMM amejiridhisha vipi na kudhani hivyo – haswa ukizingatia mazingira ya kifo chake. Kwa nini Mzee Mwanakijiji hutaki pia kuangalia possibilities nyingine, kwa mfano, kwamba mwanamke anayehusishwa kwenye tukio hili pengine ndiye chanzo cha mauaji, au, pengine Kamanda alifananishwa na mtu mwingine, au ‘amehukumiwa kwa makosa yake mwenyewe’ (kama wewe mwenyewe MMM unavyotaka iwe) n.k.


Na kama tutakubaliana na MMM kwamba mauaji haya yametokea katika mazingira hayo anayoyaeleza yeye (ya visasi dhidi ya polisi, ‘collective punishment….), nadhani la muhimu zaidi kwa wananchi siyo kulaani mauaji hayo kwa nguvu zote kama anavyosema (japo ni sawa kufanya hivyo). Muhimu zaidi ni kutafakari kwa kina nini haswa kimetufikisha katika mazingira haya, na hatua gani za haraka za kuchukua (sisi wananchi wenyewe – tusitegemee serikali, kwani, as Hon Msigwa said it “problems cannot be solved by the same level of thinking that created them!’ ,
 
Kuna jambo moja la kuwekana sawa hapa. ‘Motive’ ya kuuawa Kamanda Barlow bado haijulikani kwa uhakika. Hoja ya MMM imejengeka kwenye assumption kwamba motive ya kifo chake ni chuki za raia dhidi ya polisi, au chuki za wahalifu dhidi ya polisi. Sijui MMM amejiridhisha vipi hadi kudhani hivyo – haswa ukizingatia mazingira ya kifo chake. Kwa nini Mzee Mwanakijiji hutaki pia kuangalia possibilities nyingine, kwa mfano, kwamba mwanamke anayehusishwa kwenye tukio hili pengine ndiye chanzo cha mauaji, au, pengine Kamanda alifananishwa na mtu mwingine, au ‘amehukumiwa kwa makosa yake mwenyewe’ (kama MMM anavyotaka iwe) n.k.


Na kama tutakubaliana na MMM kwamba mauaji haya yametokea katika mazingira hayo anayoyaeleza yeye (ya visasi dhidi ya polisi, ‘collective punishment….), nadhani la muhimu zaidi kwa wananchi siyo kulaani mauaji hayo kwa nguvu zote kama anavyosema (japo ni sawa kufanya hivyo). Muhimu zaidi ni kutafakari kwa kina nini haswa kimetufikisha katika mazingira haya, na hatua gani za haraka za kuchukua (sisi wananchi wenyewe – tusitegemee serikali, kwani, as Hon Msigwa said it “problems cannot be solved by the same level of thinking that creted them!’ ,
 
Kuna jambo moja la kuwekana sawa hapa. ‘Motive’ ya kuuawa Kamanda Barlow bado haijulikani kwa uhakika. Hoja ya MMM imejengeka kwenye assumption kwamba motive ya kifo chake ni chuki za raia dhidi ya polisi, au chuki za wahalifu dhidi ya polisi. Sijui MMM amejiridhisha vipi na kudhani hivyo – haswa ukizingatia mazingira ya kifo chake. Kwa nini Mzee Mwanakijiji hutaki pia kuangalia possibilities nyingine, kwa mfano, kwamba mwanamke anayehusishwa kwenye tukio hili pengine ndiye chanzo cha mauaji, au, pengine Kamanda alifananishwa na mtu mwingine, au ‘amehukumiwa kwa makosa yake mwenyewe’ (kama MMM anavyotaka iwe) n.k.

Na kama tutakubaliana na MMM kwamba mauaji haya yametokea katika mazingira hayo anayoyaeleza yeye (ya visasi dhidi ya polisi, ‘collective punishment….), nadhani la muhimu zaidi kwa wana nchi siyo kulaani mauaji hayo kwa nguvu zote kama anavyosema (japo ni sawa kufanya hivyo). Muhimu zaidi ni kutafakari kwa kina nini haswa kimetufikisha katika mazingira haya, na hatua gani za haraka za kuchukua (sisi wananchi wenyewe – tusitegemee serikali, kwani, as Hon Msigwa said it “problems cannot be solved by the same level of thinking that creted them!’ ,
 
Mzee Mwanakijiji,
na hivyo kosa la mtoto alokojolea Msahafu linaweza kabisa kuzua vita baina ya Waislaam na Wakristu,....
Mkuu nimelipenda bandiko lako kasoro hapo tuu!Je unamaanisha mtoto auwawe?Ama ni vigezoi gani vitakavyo justify kuchoma nyumba za ibada kwasababu ya mtoto huyo?Tolorence ni jambo la maana sana kwa dini zote.

Vita vikianza kwasababu hiyo,basi lazima kuwepo upande wa kukiri udhaifu!Na apande huo ni huo wenye kuleta vita ama vurugu!
 
Nimeongea na the late comm Libe,amesema baada ya kufika na kutoa hesabu yake malaika alimpa asome coment zilioandikwa hapa na feisi buku.anasema aliumia sanana kulia kama mtoto akamuomba malaika amruhu japo tu kutoa record ya taarifa ya wote waliouhukumu kwa ukweli na uongo,his prayer has been granted and the recodr will relate only taarifa za uzinzi za watu waliomtuhu hapa tangu wazaliwe na wazinzi wao na mahali walipo pia rport hiyo itaambatanishwa na cd za uzinzi wa watu hao ambao itachezeshwa live hapa na feisi buku stay tune.soon itakuwepo hapa ili mrudi tene kuhukumu who did not deserve that style of death
 
Wakuu,
Niliwahi kusoma habari kuhusu mbunge mmoja kuwa mahututi, nikaona watu wanasema 'avute tu' tuchukue jimbo hilo.
Nilijiuliza hivi tumefika mahali tunapoteza utu kiasi hiki! Majibu niliyoyapata kichwani kwangu ni kuwa kuna kitu, hawa wanaosema si wendawazimu wana sababu hata kama si nzuri, lakini wanasababu.

Kwanza sikubaliani kabisa na falsafa ya visasi, kunyimana haki au kuondoka katika ubinadamu katika masuala yanayotuhusu. Nakubaliana na MM kuwa haki ni haki hata kama ni ya adui.

Badala ya kuwalaumu wale wanaoshangalia, inabidi tujiulize kwanini haya yanatokea.
Hawa wanaoshangilia hata kama hakuna moral authority ya kufanya hivyobado wanatoa mchango muhimu sana ambao si rahisi kuupata. Wanarahisisha kazi ya tafiti kwa sababu chuki wanaoyoonyesha katika uwazi wa namna hiyo haiwaelezei wao bali ni kielelezo kizuri cha jamii yetu na wapi tulipo.

Washangilaji wasipofanya hivyo watakuwa wanatenda uovu ule ule unaotendwa na jeshi la Polisi wa kufunika uchafu chini ya kapeti. Sihalalishi uovu, ninachojaribu kusema ni kile ninachokiona.

Jeshi la Polisi limekuwa jeshi la ajabu sana. Kifo cha Zona Morogoro kimefunikwa na jeshi hili na kuaminishwa kuwa alipigwa na kitu kizito. Jeshi la Polisi kwa kuwatumia akina Mwema, Chagonja, Kamuhanda, Advera wameficha ukweli kuhusu kifo cha kinyama cha Mwangosi. Wamejitahidi kutunga kila aina ya uongo kwa bahati mbaya kamera haisemi uongo.

Kifo kile ambacho ni kinyama sana kutokana na mazingira yake na jinsi kilivyoonekana dhahiri hakikupaswa kufunikwa na upuuzi wa lugha za Jeshi la Polisi. Wao kama Jeshi la Polisi wamesimama kidete kulindana si kama askari mmoja mmoja basli jeshi zima la Polisi.

Hawakujali haki ya Mwangosi kuishi, kutafuta riziki zake halali hata kama alikuwa adui yao.
Walichojali ni kulindana tena kwa maneno ya kuudhi yasiyo na utu wala heshima kwa binadamu!
Leo yamemkuta kamanda wa jeshi lile lile lililodhulumu haki ya Mwangosi, kwanini tuseme ni suala la mtu na si jeshi zima?

Hawa wanaoshangilia wanatusaidia kuikumbusha jamii kuwa hali tuliyo nayo ni mbaya!
Ndio njia yao ya kuonyesha hisia zao bila vurugu. Pengine nyoyoni mwao wanaungua zaidi ya kauli hiyo.

Wanafikisha ujumbe kuhusu jeshi letu kwa wenye dhamana.
Wakisema kwa maneno wanaishia kuundiwa kamati na tume za kuwapuuza kama za Jaji Ihema, Makunga na Nchimbi, hii ni njia yao ya kutoa ujumbe kuwa something is wrong in our society.

Tusiangalie kauli ya kushangilia, tuangalie kwanini tumefika hapa, akina nani wametufikisha hapa na wapi tunaelekea.
Kama Rais Kikwete hatashtuka na watu kushangilia msiba basi ni sikio la kufa lislilosikia dawa.

Tunachopaswa ni kumwambia Kikwete kuwa amelifikisha taifa katika hali ya watu kushangilia msiba!
Hata kama ataziba masikio, tumwambie'this is just a tip of ice' anatakiwa aliangalie jeshi la Polisi maana walinzi wa amani wanapoombewa misiba na kushangilia inapotokea basi hakuna amani.
 
Yaani kwa kweli hapa tulipofikia panatia huzuni! Raia sasa haoni taabu kushangilia kifo cha polisi. Inavyoelekea ipo siku Mk,were atakufa na watu watashangilia. Naunga mkono hoja ya MM kwa 100%. Tufike mahali hekima ndo ituongoze zaidi kuliko ushabiki. Mr. Dhaifu anatakiwa kutumia kiti chake kulifumua hili gheshi vinginevyo visasi vitaendelea mpaka tukome! Kama leo RPC anauawa nini kitazuia kuuawa kwa IGP, WAZIRI n.k? Au hata DHAIFU mwenyewe? KIKWETE fanya mambo mkuu nchi iko pabaya hii!!
 
Imeandikwa "USIUE". Kila binadamu "ANA HAKI YA KUISHI." Mi nafikiri hizi ni nyakati za mwisho wa dunia kulingana na maandiko matakatifu amani itatoweka na mauaji yatazidi katika uso wa dunia na punde muyaonayo haya furahini make siku yakurudi kwake ikaribu.
 
Nimesema juzi kuwa ukosefu wa hekima ni janga kubwa la kitaifa kwa kweli nilimaanisha hilo. Tangu habari za mauaji ya Kamanda Barlow yalipotokea mwitikio wa watu wengi umekuwa ni kutokujali, kuhalalisha na hata kushangilia ni kama mtu kusema "akome". Wengi wanahalalisha hili kwa sababu wanaamini ujumbe umetumwa kwa polisi na kuwa polisi 'wanaua watu na sasa kimewarudia'. Kauli hizi ndizo zinazothibitisha ukosefu wa hii hekima.Tumeshuhudia kosa la mtoto mmoja kwenda kuhukumiwa makanisa na wakristu; leo kosa la Kamuhanda anahukumiwa Barlow? Leo hii kosa la askari mmoja wanalaumiwa jeshi zima kiasi kwamba leo chochote kitakachompata polisi tunafurahia?

Ni lazima tujifunze kuwa na hekima ya kutofautisha kitu kinachoitwa "collective punishment" kwamba tunaadhibu wote kwa kosa la mmoja. Labda ni kwa sababu tunaamini (bila kufikiria sana) kuwa "samaki mmoja akioza wameoza wote". Ukweli ni kuwa samaki mmoja akioza siyo wote wameoza!

Kamanda Barlow ahukumiwe kwa matendo yake mwenyewe na si matendo ya wengine. Je alikuwa ni kamanda mzuri kwa polisi, je alisimamia haki na utawala wa kisheria kwa kadiri ya uwezo wake (yaani pamoja na mapungufu yake kama alivyoshughulikia hili la koswakoswa la afisa)? Je kuwa dhaifu kiutendaji adhabu yake ni mauti?

Tuna tofauti gani basi na wale ambao wanaona mtu anapigwa na watu kwa sababu kadaiwa ni 'kibaka' na wao bila kuuliza wanachukua jiwe na kurusha au wanauliza "lete petroli" halafu wanaondoka zao huku nyuma mtu anatiwa kiberiti? Tuna tofauti gani na jamii isiyoerevuka ambayo haitaki kutafuta ukweli inaishi kwa imani na hisia tu?

Mauaji ya Barlow kama yalaivyokuwa mauaji ya Mwangosi na ya wananchi wengine wengi yanapaswa kulaaniwa na siyo kuhalalishwa, yanastahili kupingwa na siyo kutetewa na yanahitaji kukataliwa na siyo kuzoeleka.

Ni wazi kuna mapungufu ya kiutendaji na mambo mengi ambayo hayajibu maswali yetu ndio maana wengine tulitaka maafisa wa juu wa jeshi hilo wang'olewe kwa sababu wameligeuza kuwa ni jeshi la kisiasa sasa. Inapofika watu wanaona jeshi la polisi ni la CCM au lisilo na ule ukaribu wa zamani na wananchi basi ni hatari kwa sababu hawatalipa ushirikiano na wakipata nafasi ya kuwatendea polisi wanawatendea! Mwema, Chagonja na wengine wajuu wanapaswa kuondolewa ili mabadiliko ya kweli ya jeshi yaletwe na watu wenye uwezo. Inapofika watu hawaoni huruma ya mtu kupoteza maisha yake tumefika pabaya.

Hivi mauaji haya yana tofauti gani ya Pro. Mwaikusa? yana tofauti gani na mauaji ya yule Mwanasheria miaka michache iliyopita pale Dar; yana tofauti gani na mauaji wananchi kule Arusha, au Songea? Well.. tofauti ni namna tu lakini ni kuwa wote wamepoteza maisha katika mazingira ambayo hayakupaswa kutokea; ni mazingira ambayo yanahitaji kuchunguzwa na kuondolewa ili isije ikafika mahali huko mbeleni tukasikia Waziri auawa, Mwenyekiti wa Chama cha siasa apigwa risasi au Mbunge auawa au hata iwe yale yale ya Afisa auawa au mwananchii auawa akidhwaniwa ni jambazi!

Hekima inatuita tulaani mauaji haya, kuyapinga na kutaka juhudi zote za kuwaleta kwenye haki zifanyike pasi ya huruma au upendeleo au husuda. Hii haina maana watu tunaridhika na utendaji wea jeshi la polisi. Ushahidi ni mwingi mno kuwa jeshi letu linahitaji mabadilikko ya mfumo (structural reform) ili kulifanya liwe la kisasa zaidi, likijali watu na likiwa linaelewa tunu ya kanuni za demokrasia. Mahitaji ya mabadiliko hayo hayalalishi unyama dhidi ya polisi au raia. Na pamoja na hilo mabadiliko ya msingi yatokee ndani ya jeshi la polisi ili lionekane kweli linajali raia.

Binafsi ninalaani vikali mauaji ya kinyama ya kamanda wa polisi na kutaka haki itendeke kuhakikishwa wahusika wanakutana na mkkono wa sheria. Huwezi kupinga mauaji ya Mwangosi na kutaka haki itendeke halafu ushangilie mauaji ya Kamanda.

Haki ni haki hata ya adui yako ni haki. Mwangosi alikuwa na haki ya kuishi kama vile Barlow alivyokuwa nayo na kama mamia wengine walivyokuwa nayo na ambayo ilikatishwa kinyama. Tusivumilie mauaji ya aina hii kwani yana chochea visasi. Itakuwaje kama polisi nao katika kujihami wanaanza kuua kama mbwa na wananchi wanarudishia kisasi kama wana wazimu?

Litakuwa ni taifa la damu. Damu ambayo isipokataliwa itaendelea kutiririka kama kijito kisichokoma.

Mkuu ukweli ni kwamba kama wao wanashindwa kuthamini uhai wa watu wengine ni vipi na sisi tutathamini uhai wao.Imefikia hatu uhai wa mwananchi wa kawaida ni sawa na wa kifaranga cha kuku kiasi kwamba hata mtu akiuwawa na polisi hakuna linalofanyika.Watoto wanaachwa yatima kutokana na ukatili wa polisi alafu wao na viongozi wa nchi wanaendekeza kulindana tu.

Mkuu hivi unafikiri leo akifa yule kamuhanda ni wangapi watasherehekea kifo chake.Sina haja ya kuwa mnafiki wala kuficha ukweli kwamba mimi ni mmoja wa watu ambae hata leo akitangulia mbele ya haki sitajali lolote.

Tatizo kubwa la nchi yetu ni hii double standard ya watawala wetu.Maisha ya mtu maskini hayana thamani mbele ya watawala hawa ila ya wachache(vigogo,mafisadi n.k) ndio muhimu kwao.

Nakuhakikishia ya kuwa hata mabaya yakimkuta mkuu wa kaya leo hii wako wengi zaidi tu watafurahia kuliko hata ilivyo kwa huyu RPC.

Inasikitisha kila siku watu tunapiga kelele waliohusika na kifo cha Mwangosi pamoja na viongozi wa jeshi wawajibike lakini yeye ameweka pamba masikioni na kuvaa miwani ya mbao kanakwamba alieuwawa ni kifaranga cha kuku.
 
Mkuu wangu nimekusikia sana lakini sidhani kama kweli uko tayari kwa vita na kama wewe upo tayari sidhani kama nyuma yako kuna watu watakufuata. Watanzania vuvuzela sana, rutunasema sana lakini inapofikia swala la vita sidhani kama mko tayari isipokuwa kwa sababu za kipumbavu kama hizi.

Hoja yangu haihusu kabisa nidhamu ya woga na huo Uwoga unazungumzia wewe hauwezi kulingana na UPENDO maana neno hili linatoka moyoni na sii hisia bali kuelewa thamani ya UTU wako na mwenzako. Ni rahisi sana kusema binadamu wote sawa lakini pasipo mapenzi hata ukipigana vita basi vita hivyo havitakwisha. Ni rahisi pia kwako kusema Iraq, Marekani na Ujarumani zilipitia vita na hivyo kuboresha maisha yao lakini ulichoshindwa kuelewa ni kwamba UZALENDO wao ndio ulowasukuma kupigana vita dhidi ya kundi jingine, hawakutengana wala kupigana vita pasipo azma inayowajenga wao kwanza. Haya nambie sisi tutaingia vitani kupigana ili iweje?..

Hakuna Vita vya wenyewe vilivyoweza kuwajenga wananchi wake - HAKUNA isipokuwa kuwakwaza zaidi na zaidi na kuwagawa zaidi na zaidi maana nafisini hakuna UPENDO..Hivyo unaanza kufundishana kupendana kisha Uzalendo unalinda ngome zenu na Udugu hivyo hata adui akiingia mnakuwa tayari kujilinda. Tazama leo hii Hata Malawi wanatusimamia kidete kwa kifua mbele kabisa nna sii wao ntu hata Rwanda ya Kagame wanatuona ssi mazuzu na wala hajakosea maana kisha fahamu Tanzania ya Nyerere haipo tena. Kuna makundi makundi yanaypopingana yenyewe na wameisha poteza dira.. wapo wapo tu duniani wakisubiri kama Sii Mungu basi riziki yao itatoka kwa matajiri... wale wenye ndoto ya ONE DAY YES!

Asante mkuu kwa hoja hii unayoileta. Nakubaliana nawe katika dhana ya Upendo, kwamba upendo una thamani zaidi kuliko vita. Hata hivyo, kuna mahala hoja yako inapokuwa legelege kidogo--pale unaposhindwa kutambua nafasi ya vita katika ukombozi wa jamii. Jamii nyingi duniani zikisukumwa hadi kwenye ukuta, na njia za kutokea pale ambazo ni za mazungumzo zikawa zinazibwa kwa sababu za kipumbavu kama uwongo wa mchana kweupe, mabavu, ama falsafa zisizokuwa na maslahi makuu kwa taifa, vita imekuwa ndiyo njia ya mwisho ya kutokea.

Umesema "Hakuna Vita vya wenyewe vilivyoweza kuwajenga wananchi wake." Mimi nasema kauli hii SI sahihi. Wamarekani walipigana vita vya wao kwa wao karne ya 18, kuunda taifa imara ambalo tunaliona leo. Leo hii wanaimba wimbo wao wa taifa "The Star Spangled banner" huku bendera yao ya nyota hamsini na moja nadhani, ikiwa juu, kwa kuwa watu katika taifa lile walichagua kulazimisha wapumbavu fulani kuziona facts sahihi kwa vita. Hili pia ni sahihi kwa mataifa yaliyo kusini mwa Afrika. Miaka ya nyuma tumeunga mkono vita Zimbabwe, RSA, Msumbiji, Namibia, Angola, na miaka ya karibuni katika visiwa fulani vya Indian Ocean kwa sababu ya dhana hii ninayoileta kwako. Vita si mbaya katika kila maana, hasa logic inapokuwa imeshindikana kabisa kama pale tunapoonekana kufikia sasa. Nakubaliana na wewe unaposema tumedharaulika sana katika miaka ya karibuni. Tunatia aibu katika jumuia ya mataifa. Kwa bahati mbaya hoja yako haijajitosheleza kuelezea tonajitoa kivipi katika nafasi hiyo ya aibu ambayo tumejifikisha?

Tumeingia katika mfumo wa vyama vingi tangu 1992. Wananchi wameonesha kuchukia utaratibu unaotumika sasa kuendesha nchi yetu kwa kutoa hisia zao katika njia nyingi sana, lakini hapaonekani nia thabiti ya kuruhusu mawazo mbadala kuendesha nchi. Sitaki kurudia maelezo ya udhaifu uliopo katika kuendesha nchi kwa sababu wengi wanayajua. Na wewe nina hakika utakuwa unajua habari za kushamiri kwa rushwa, mtindo wa kuendesha nchi kwa kuwaongopea wananchi, utaratibu wa kurithisha vijukuu katika kila nafasi muhimu ya uongozi bila kujali uwezo wa kiakili wa huyo mrithi unapolinganisha na watoto wengine katika nchi, and the list goes on and on. Wewe ndugu Mkandara, tuseme unaona dalili zozote za walio katika madaraka kutambua udhaifu wao na kupisha wenye mawazo tofauti kuendesha nchi? Nina hakika dalili hakuna.

Mimi sijahimiza watu kuanza vita kesho. Nimesema tujiandae kwa vita vya wao kwa wao kwa kuwa naamini linaweza kutokea kundi katika jamii likatumia vigezo nilivyovisema hapo juu kuingia katika vita--baridi au moto, lakini mazingira tuliyo nayo yanaruhusu vita kuanza. Tumaini pekee lililobakia kuzuia vita katika nchi yetu ni hii sirka ya uwoga katika jamii ya Tanzania, ambayo hata wewe Mkandara unaionesha hapa kwa hoja zako.

Ni nchi gani duniani watu wake wanaweza kukaa kimya bila kuchukua hatua za kivita wakati mauaji ya kisiasa yanafanywa na watu waliopo madarakani. Ni nchi gani itakaa katika utulivu wakati watu walio katika madaraka wanapora matokeo ya kura. Sioni kosa katika kutarajia vita. Je ni kweli kwamba watanzania wote ni waoga?
 
Mwanakijiji acha porojo mdau,,,,punguza perepeteee,,,unajifanya huyajuuui wanayotenda polisi????matukio mangapi wao wanayafanya na hayana manufaa kwa raia,,,,polis hata mmoja akiharibu amelichafua jeshi la polisi kwa namna yeyote ile,,,,ndo maana tukio hilohilo akifanya raia wa kawaida wala hakuna mshtuko mkubwa,,,,unaposema waje watendaji wenye kuweza kuliendesha jesh nje ya utash wa kisiasa inaonesha wewe unajiweka kando na yanayoendelea tanzania???hata alipokuja mwema watu wengi walidhan angeendesha jeshi kitaaluma,kwakuwa pia ni mwanasheria je yanayoendelea huyaoni???kwa sababu huyo mwema anateuliwa na mwanasiasa,,,,,kingine ni kwamba hakuna atakayeliweka sawa jeshi la polisi maana wote wanatoka humohumo,,,,polis ni wachafu tangu zama hizo,,,,vilevile chuki baina ya polisi na raia imesababishwa sana na POLISI WENYEWE,KWA KUDHAN KUWA WAO NI VIUMBE WENGINE,,,,,,,SASA BASI USIFIKIRI KWAMBA HAYA YATAISHA YATAENDELEA SANA TENA ZAID NA ZAIDI
 
Mkuu ukweli ni kwamba kama wao wanashindwa kuthamini uhai wa watu wengine ni vipi na sisi tutathamini uhai wao.Imefikia hatu uhai wa mwananchi wa kawaida ni sawa na wa kifaranga cha kuku kiasi kwamba hata mtu akiuwawa na polisi hakuna linalofanyika.Watoto wanaachwa yatima kutokana na ukatili wa polisi alafu wao na viongozi wa nchi wanaendekeza kulindana tu.

Mkuu hivi unafikiri leo akifa yule kamuhanda ni wangapi watasherehekea kifo chake.Sina haja ya kuwa mnafiki wala kuficha ukweli kwamba mimi ni mmoja wa watu ambae hata leo akitangulia mbele ya haki sitajali lolote.

Tatizo kubwa la nchi yetu ni hii double standard ya watawala wetu.Maisha ya mtu maskini hayana thamani mbele ya watawala hawa ila ya wachache(vigogo,mafisadi n.k) ndio muhimu kwao.

Nakuhakikishia ya kuwa hata mabaya yakimkuta mkuu wa kaya leo hii wako wengi zaidi tu watafurahia kuliko hata ilivyo kwa huyu RPC.

Inasikitisha kila siku watu tunapiga kelele waliohusika na kifo cha Mwangosi pamoja na viongozi wa jeshi wawajibike lakini yeye ameweka pamba masikioni na kuvaa miwani ya mbao kanakwamba alieuwawa ni kifaranga cha kuku.

kuna matukio kibao,,,,yanayoonyesha kuwa polis wanawaonea raia,,,,tunaona wanapoingia kutuliza vurugu vyuo vikuu,,,wanawadhalilisha sana wasichana,,,,kuwashikashika masir-buri yao na manyonyo yao,,,,,,,,,
 
Nakubaliana kabisa na Mwanakijiji na makala yake nzuri.Amejaribu kuwaelewesha wale ambao wanaamini kuwa kifo cha kamanda kama lipizo kwa Polisi ,kwangu naamini kifo chochote kinaweza kufanywa/kutekelezwa kwa makusudi na genge la watu wasiojali utu na thamani ya mtu au kwa mipango ya mungu.Nasikitika sana kuona baadhi ya watu wanaoshangilia kifo cha kamanda,mi nadhani si busara na wanatakiwa watafakari kwamba hivi wao watakuwa wanasikia tu vifo vya wenzao?kwamba wao hawatakufa?iwe vifo vya kawaida au kifo kama kilicho mpata kamanda Barlow?Kila mmoja ataonja mauti.Tuache ushabiki kwenye mambo ya vifo.
 
.Bwana Kama wewe ungehesabu maovu yetu, nani angesimama, nani angesimama, nani angesimama mbele yako....
 
Jamii iliyopoteza Uvumilivu [Lost tolerance=self destruction]

Rais wangu Kikwete amka ufanyie kazi aina hii ya maisha la sivyo tunakoelekea ni kubaya saaaana siksiliza wtz wanataka nini acha siasa kidogo, uliza utaalamu uko wapi ktk hili

Zuia wakati una uwezo wa kuizuia, ipo siku inakuja kutamani lakini utakuwa umechelewa

Angalia watu wanavyouwana (Tarime kule Nyamongo, Mikutano ya CHADEMA, Majeshi kule Kilombelo, Ulimboka, Mwangosi, na sasa Kamanda wetu Barlow na Makanisa Kuchomwa si zanzibar bali karibu na IKULU "Mbagala"

Jamii inafundishwa na vyombo vya usalama kupoteza uvumilivu (Lost tolerance and self damage)
 
Mkuu MMM,

Rules of the game ndio zimepelekea faulo nyingi hata kwenye jambo la utu/uhai kama hili. Wao (polisi) badala ya kusitkitka au kutoa taarifa zenye kuonesha wanajali au kuthamini uhai wa raia wanapokufa mara nyingi wamekuwa wanafanya "dhihaka" kwa matamko yao mepesi tena yenye udanganyifu na ghiliba lukuki.

HATA HIVYO nakubali rai yako, kwamba hakuna uhalali wa kufurahia kifo cha Barlow. Kama jamii ni lazima tuchore mstari/mpaka ktk mambo kama haya.

TWO WRONGS NEVER MAKE ONE RIGHT
uhalali upo wakufurahia kifo cha Barlow kwani wao wakituua wanafurahi na kutudhihaki kwanini tuliandamana kwani hukumu ya maandamano ni kifo?waonje kwanza machungu ya mauti ndio wajue na sisi tunaumia.
 
Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya udhaifu wa " Amiri Jeshi Mkuu na Mkuu wa Majeshi yote ya Ulinzi "na Usalama". Na huyu si mwingine bali ni Mkuu wetu wa Nchi.

Sitegemei mabadiliko ya kweli bila ukomo wa huu utawala DHAIFU.
 
Jeshi hili la polisi ndugu MM unategemea mapya gani tokea kwao, nakuhakikishia ndani ya Saa 24 utasikia raia wasiokuwa na hatia wamekamatwa wakihusishwa na mauaji ya Liberatus , double standard ya Hali ya juu, labda wewe hukai tanzania hulifahamu jeshi la polisi, Mimi kwa dhamira yangu ya wazi nasema to hell, nimeridhika na kilichotokea .

Hii ni signature yako. mbona kama haviendani? au nawe ni kigeugeu?

They wiil disqualify you for the little weaknesses you have and they will never glorify you for the great strength you have shown, Phd- Houston Texas July 23, 2012
 
uhalali upo wakufurahia kifo cha Barlow kwani wao wakituua wanafurahi na kutudhihaki kwanini tuliandamana kwani hukumu ya maandamano ni kifo?waonje kwanza machungu ya mauti ndio wajue na sisi tunaumia.

Ukiulizwa Barlow ameua nani na wapi utasema? kwa nini makosa ya KAMUHANDA, ANDENGENYE akiwa ARUSHA, Shilogile wa Moro abebeshwe kamanda Barlow?
 
Back
Top Bottom