TIMING
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 31,197
- 18,227
Habari za mda huu wana MMU
Majira haya ya saa 4 usiku natoka kwa mupenzi ninaetarajia kumtia chuo (ndoa) aliniita nimpelekee hela ya kujikimu kwa matumizi.
Nimefika tumekaa barazani mara kapita mama yake alikua ameletewa ugoro akausifu kwa kua ni mwingi akasema enzi anasoma chuoni alikua akibeba na kuenda nao kupiga uraibu huko chuoni na baazi ya wanafunzi walikua wakimuomba na alikua akiwapatia ila ilikua ukiwazingua mara walie,wengine hujikojolea.
"Mama kumbe ushenzi uliuanza zamani" maneno hayo yamemtoka mtarajiwa wangu kumuambia mama ake mzazi tukiwa barazani mi sikupenda nikamfinya kidogo kumuonesha nimechukia na asirejee tena.
"Unanifinya namna hii kwani yule ni mama yako" kauli hii ilizidi kunichoma na kunifanya nichukie zaidi na kujenga masuali yasio na majibu kwa haraka.
Alinyanyuka mchumba wangu kuenda kuchukua chakula ili amletee mtoto ale pale nje aliponyanyuka yeye akaja dada yake kuja kunipa kapani na kunisalimia shemeji yake sikuona vibaya nikamsimulia kisa cha mdogo wake na kumtaka amkanye kwani yule ni mzee wake yapaswa kumuhishimu.
Basi hapo mapenzi yaligeuka yakawa uhasimu alipotuona tunaongea na dada yake yeye hakurudi tena pale akaa pembeni ili kumrizisha nikamuambia njoo tukae wote "Sina ten muda wa kukaa njee naenda kulala" hilo ndilo lililokua jibu lake.
Niliendelea kupiga stori na dada yake na kumuambia unaona majibu ya mdogo wako hayo jeee huko katika ndoa itakuaje " Shem tabia ni kama ngozi mvumilie tuuu" alinijibu
Nikamuita mupenzi aje nimuage niondoke " kama umechoka kutoa umbea nenda zako" mi nikaamua kuwasha usafiri wangu na kuondoka.
Niko njiani kuelekea home sms kibao
Ukikaa na malaya wako mi sitaki kuongelewa km mimi sikufai basi mchukuwe yeye tena namba yake nataka ufute ukome kunidiskasi na mpuuzi yule tabia yako hii sijapenda
Sms ziko kama 10 kapiga simu sijapokea kaengeza na nyengine sms za kulani
"Bby samahani zilikua ni hasira tuuu plz pokea simu yangu"
Mi mawazo yananipa nimwage manyanga hasa kwa vile nishagegeda sana maana naona huko katika ndoa kutakua ni sawa na uwanja wa fujo kwa staili hii
Wadau niambieni munaonaje hii hali?
jaalia imekutokea ww
vijana wa siku hizi mmekua kama vespa za unguja, injini strokes mbili tu.... we hadi unataka kuoa hujamjua mpenzio japo ABC??
haya kijana, naona afadhali ya maharage ya mbeya