Hebu tuiangalie nchi ya Ukraine katika kurunzi ya kiuchumi

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,783
UTANGULIZI
Mambo mengi sana yameongelewa, lakini kuna yaliyofichika nyuma ya pazia. Unapoangalia mgogoro wa Ukraine na kuuchambua hebu tujitahidi kuzingatia haya mambo muhimu yafuatayo. Tuzingatie umuhimu wa kiuchumi wa nchi ya Ukraine kwenye siasa za Urusi, Marekani na Ulaya. Hapa nazungumzia utajiri wa rasilimali ambao nchi ile inayo, halafu mwishoni pima mwenyewe:

NAFASI YA UKRAINE KIUCHUMI BARANI ULAYA NA DUNIANI:
1. Ukraine ndiyo taifa kubwa zaidi barani Ulaya (Ukiitoa Urusi)

2. Ukraine inauwezo wa kufanya kilimo (Agricultural Potential) chenye kulisha watu milioni 600, bara zima la Ulaya.

3. Ukraine ndiyo taifa la kwanza barani Ulaya kwa kuwa na madini mengi ya Uranium (Ukiitoa Urusi)

4. Ukraine ndiyo taifa la pili barani Ulaya kuwa na madini mengi ya Tinanium (Duniani ni taifa la 10)

5. Ukraine ndiyo taifa la pili duniani kuwa na madini mengi ya Mangenese (Explored Manganese Reserves)

6. Ukraine hadi kufika mwaka 2020 lilikuwa ni taifa la saba lenye madini mengi ya chuma (2022 Imegundulika ni la pili duniani)

7. Ukraine ni taifa la pili barani Ulaya kuwa na madini mengi ya Mercury.

8. Ukraine ni taifa la kumi na tatu duniani lenye gesi nyingi (Shale Gas Reserves).

9. Ukraine ni taifa la saba duniani kuwa na hifadhi kubwa ya makaa ya mawe.

10. Ukraine ni taifa la tano kuwa na watu wengi barani Ulaya (Watu milioni 44).

MUHIMU KUFAHAMU:
Nchi ya Ukraine ilitaka kujiunga na Umoja wa Ulaya miaka ya 2010's lakini Raisi Viktor Yanukovich alikataa na kusema kamba tatizo ni kukuza uchumi basi ataenda kuomba mkopo wa dola za kimarekani bilioni 15 (Bail-Out) kutoka Urusi. Jambo hili, mazingira makubwa ya rushwa, pamoja na kukataa kuiingiza Ukraine NATO vilipelekea maandamano makubwa mwaka 2014. Yanukovich aliponea chupuchupu kuuawawa hadi alipokuja kuokolewa na kukimbiziwa nchini Urusi ambako yuko uhamishoni mpaka leo hii.

Endapo nchi ya Ukraine itajiunga na Umoja wa Ulaya, ukizingatia ina rasilimali nyingi na nguvu kubwa sana kiviwanda na kiteknolojia, hasa vile vilivyoacha na jamhuri ya kisovieti basi Ulaya inaweza ikapata utajiri mkubwa sana. Ukraine ikifanikiwa kiuchumi na kujiunga na NATO: Je, nchi ya Urusi itakuwa kwenye nafasi ipi (Hapa jawabu sina kabisa)

Is Ukranian Crisis a symptom of resource curse?
 
Pato lao kitaifa likoje? Wana nguvu kiasi gani kwenye ujasusi wa kiuchumi?
Hawafanya vizuri kiuchumi, japo miaka ya 90 walikuwa ni moja ya taifa lenye viwanda vikubwa na teknolojia muhimu barani Ulaya. Rasilimali wanazo nyingi sana, ambapo kama wakijiunga na Umoja wa Ulaya wanaweza kufanya mambo makubwa sana.
 
Ukrain imezungukwa na majeshi ya Russia kote, sasaivi russia anapigana naye kwenye mitaa ya kiev lakini bado jamaa anaamini atawashinda. mtu ameshaingia nchini kwako mnapigania kwenye corridor za nyumba yako na nyumba yako ndio inadondoka kuta lkn unaamini utashinda?
 
Ukrain imezungukwa na majeshi ya Russia kote, sasaivi russia anapigana naye kwenye mitaa ya kiev lakini bado jamaa anaamini atawashinda. mtu ameshaingia nchini kwako mnapigania kwenye corridor za nyumba yako na nyumba yako ndio inadondoka kuta lkn unaamini utashinda?
Zelensky yuko kazini....kibaraka anapambania maslahi ya bwana zake NATO....wananchi wanaweza kumpa heshima ya URAIS kumbe ni KIKARAGOSI cha watu.....

#Siempre JMT🙏
 
inadondoka kuta lkn unaamini utashinda?
Yawezekana bado kuna upenyo! Kwani spy master wa Ujerumani alitoroshwaje juzi kutoka Kiev. Dhana hii inashika kasi kwa sababu kitendo cha Germany kusema kitampa Ukraine 'ant tanks' silaha za kuangamiza vifaru kupitia uholanzi, inaonyesha bado kuna upenyeo ambao Russia hajaudhibiti nchini Ukraini
====
Kuhusu mada mezani, mambo yaliyoelezwa na mleta mada nadhani yanachangia pakubwa kwenye mgogoro
 
Yawezekana bado kuna upenyo! Kwani spy master wa Ujerumani alitoroshwaje juzi kutoka Kiev. Dhana hii inashika kasi kwa sababu kitendo cha Germany kusema kitampa Ukraine 'ant tanks' silaha za kuangamiza vifaru kupitia uholanzi, inaonyesha bado kuna upenyeo ambao Russia hajaudhibiti nchini Ukraini
mtu anakwambia atakupatia silaha ili upigane mwenyewe na upiganie nyumbani kwako, silaha ambazo ni dhaifu kuliko za jambazi aliyekuvamia, anayekupa silaha nyumbani kwake kuko salama ila kwako nyumba inazidi kumongónyoka, and you still believe anakusaidia? hata wakitoa silaha zote, unaamini ukrain itashindana na Russia?

Ni kwamba wanamtumia ukrain kama condom kupima uwezo wa Russia, wao wenyewe hawawezi kabisa kupigana naye, hata Ujerumani yenyewe haina uwezo kupigana na Russia, ni marekani tu ambayo inaweza kupigana na russia, na matokeo yake yatakuwa madhara kwa dunia nzima kiuchumi na kwa maafa.

Hizo nchi zote za ulaya zinategemea sana urusi kwa gas na oil, leo tu akitoboa kwa risasi bomba la gas toka ukrain kwenda ulaya wataanza kupikia kuni, au waanze kusafirisha gas toka nchi nyingine ambayo kwao itauzwa gharama sana.

kiuhalisia, hata ningekuwa mimi ni russia, ningeingia vitani kwasababu walichokuwa wanafanya nato ni dharau na kumpiga kidole cha machoni russia, wamemdharau kwa miaka mingi hadi wanataka kuingia chumbani kwa kuweka base pale ukrain? dharau gani hizo? hii vita wa kulaumiwa ni marekani na nato, ambao siku zote wanajali zaidi maslahi, na wanatumia pesa nyingi duniani kudhamini vita na kuliko kusaidia maisha ya wanadamu.
 
Zelensky yuko kazini....kibaraka anapambania maslahi ya bwana zake NATO....wananchi wanaweza kumpa heshima ya URAIS kumbe ni KIKARAGOSI cha watu.....

#Siempre JMT🙏
anatafuta heshima, wakati nchi inakuwa magofu, on the other way, kule Russia maisha yanaendelea kama kawaida. yeye raia wake wanakimbia nchi, hawazalishi, wanaumia na kufa. wamagharibi wamekaa pembeni wanamwangalia tu ili kuzipima silaha na uwezo wa urusi, wakimtumia yeye kama chambo, na yeye hajui hilo. katika dunia hii wazungu wa magharibi hawajawahi kumpenda mtu, wanapenda maslahi tu.
 
Screenshot_20220226-001338_Twitter.jpg
 
  • Thanks
Reactions: ffn
anatafuta heshima, wakati nchi inakuwa magofu, on the other way, kule Russia maisha yanaendelea kama kawaida. yeye raia wake wanakimbia nchi, hawazalishi, wanaumia na kufa. wamagharibi wamekaa pembeni wanamwangalia tu ili kuzipima silaha na uwezo wa urusi, wakimtumia yeye kama chambo, na yeye hajui hilo. katika dunia hii wazungu wa magharibi hawajawahi kumpenda mtu, wanapenda maslahi tu.
Hakika kamarada😍
 
ikiwa utaongea zaidi kuliko kusikiliza ..Utajinyima fursa nyingi za kujilimbikizia maarifa
mkuu wewe unaamini vita hii ni ya kiuchumi zaidi kwasababu ya maliasili zilizopo ukrain, though urusi yenyewe imeshasema inachohitaji ni kudistabilize uwezo kijeshi wa ukrain na kutoiruhusu kuwa na nuke. na hata hayo masuala ya maliasili, unafikiri urusi hazihitaji? ni kweli anazihitaji hasa kama angeweka purpet wake pale ili badala ya kunyonywa na wamagaribi azinyonye yeye. vyote vipo, ila suala la NATO kuweka base yake pale ndilo limemuogopesa sana urusi.
 
Ukrain imezungukwa na majeshi ya Russia kote, sasaivi russia anapigana naye kwenye mitaa ya kiev lakini bado jamaa anaamini atawashinda. mtu ameshaingia nchini kwako mnapigania kwenye corridor za nyumba yako na nyumba yako ndio inadondoka kuta lkn unaamini utashinda?
Acha taarabu una jua kuzungukwa pote wewe.russia wame target sehemu chache tu
281261584.jpg
 
Back
Top Bottom