mdukuzi
JF-Expert Member
- Jan 4, 2014
- 16,461
- 37,213
Pamoja na mapungufu yake Magufuli alikuwa na sifa moja, akikupenda na kukuamini utakula mema ya nchi na atakulinda, hakuwa kigeugeu ila akikuchukia imekula kwako.
Hakuwa mnafiki kujifanya anakupenda wakati hakupendi,
Marafiki zake walimpenda kwa hilo walijiaminisha kuwa atawalinda milele kwa lolote ambalo lingetokea wakasahau maandiko matakatifu kuwa amelaaniwa amtumainiaye mwanadamu.
Mmoja kati ya marafiki wa Magufuli alikuwa bwana Mfugale. Kiasili huyu bwana hakuwa fisadi, alikuwa mtu msafi ndio maana Magufuli alimpenda.
Mara kadhaa aliomba kustaafu ila alikataliwa na Magufuli maana kama nguvu alikuwa nazo na bado Taifa lilihitaji msaada wake.
Tatizo likaja ni kuwa Magufuli alifanya Tanroads kama kampuni yake kupatia humo akatengeneza madili mengi sana na akaipa kazi zisizokuwa za kwake kiasili, mfano usimamiaji na ununuzi wa mitambo ya kiwanda cha sukari Mkulazi cha mkoani Morogoro. Hii kazi ilipaswa kusimamiwa na TAMESA ila ikaagiea Tanroads waifanye, bilioni 68 zikapotea kimiujiza.
Pili uwanja wa ndege wa Chato uliotakiwa kusimamiwa na mamlaka ya viwanja vya ndege nchini jukumu hilo akapewa Tanroads ya Mfugale.
Bajeti ya awali ya uwanja ilikuwa sh bilioni 17.79 lakini mpaka uwanja unakamilika ilitumika bilioni 52.32 mara tatu ya bajeti, kiasi cha zaidi ya bilioni 34.
Nani angethubutu kuhoji matumizi hayo mbele ya John Pompeo.
Miezi michache baada ya Magufuli kufariki ndio mamlaka husika zikaanza kuimulika na kuomba ufafanuzi wa matumizi ya Tanroads.
Madudu yaliyoibuliwa huko ni mengi sana, yalikuwa yanaenda kuharibu heshima ya mzee Mfugale aliyoijenga kwa miaka mingi.
Siku chache kabla ya Mfugale kufariki iligundulika kuwa Tanroads ilifanya malipo mara mbili kwa kampuni fulani ya ujenzi kwa kazi moja yaani double payment.
Mzee wa watu akaingia kwenye sonona akajilaumu bora angestaafu mapema akalea wajukuu kuliko kuingia kwenye kashfa ambazo alikuwa tu akipokea maelekezo toka kwa mwendazake.
Sonona inaua akafa kwa presha na masikitiko moyoni
RIP Mfugale
Hakuwa mnafiki kujifanya anakupenda wakati hakupendi,
Marafiki zake walimpenda kwa hilo walijiaminisha kuwa atawalinda milele kwa lolote ambalo lingetokea wakasahau maandiko matakatifu kuwa amelaaniwa amtumainiaye mwanadamu.
Mmoja kati ya marafiki wa Magufuli alikuwa bwana Mfugale. Kiasili huyu bwana hakuwa fisadi, alikuwa mtu msafi ndio maana Magufuli alimpenda.
Mara kadhaa aliomba kustaafu ila alikataliwa na Magufuli maana kama nguvu alikuwa nazo na bado Taifa lilihitaji msaada wake.
Tatizo likaja ni kuwa Magufuli alifanya Tanroads kama kampuni yake kupatia humo akatengeneza madili mengi sana na akaipa kazi zisizokuwa za kwake kiasili, mfano usimamiaji na ununuzi wa mitambo ya kiwanda cha sukari Mkulazi cha mkoani Morogoro. Hii kazi ilipaswa kusimamiwa na TAMESA ila ikaagiea Tanroads waifanye, bilioni 68 zikapotea kimiujiza.
Pili uwanja wa ndege wa Chato uliotakiwa kusimamiwa na mamlaka ya viwanja vya ndege nchini jukumu hilo akapewa Tanroads ya Mfugale.
Bajeti ya awali ya uwanja ilikuwa sh bilioni 17.79 lakini mpaka uwanja unakamilika ilitumika bilioni 52.32 mara tatu ya bajeti, kiasi cha zaidi ya bilioni 34.
Nani angethubutu kuhoji matumizi hayo mbele ya John Pompeo.
Miezi michache baada ya Magufuli kufariki ndio mamlaka husika zikaanza kuimulika na kuomba ufafanuzi wa matumizi ya Tanroads.
Madudu yaliyoibuliwa huko ni mengi sana, yalikuwa yanaenda kuharibu heshima ya mzee Mfugale aliyoijenga kwa miaka mingi.
Siku chache kabla ya Mfugale kufariki iligundulika kuwa Tanroads ilifanya malipo mara mbili kwa kampuni fulani ya ujenzi kwa kazi moja yaani double payment.
Mzee wa watu akaingia kwenye sonona akajilaumu bora angestaafu mapema akalea wajukuu kuliko kuingia kwenye kashfa ambazo alikuwa tu akipokea maelekezo toka kwa mwendazake.
Sonona inaua akafa kwa presha na masikitiko moyoni
RIP Mfugale