Haya machungwa vipi?

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,886
2,766
Ukweli ni kwamba tangu nizaliwe hadi sasa naelekea utu uzima wenyewe sijawahi ona haya machungwa. Nachojua machungwa aidha yawe matamu au machachu, ila hayakosi maji. Sasa haya sijui ya wapi. Na ni mwaka jana na huu tu ndio nimeanza kuyaona.

Chungwa kwanza kubwa, halafu gumu, kuonyesha kabisa lina walakini. Nanunua machungwa matano na yote nakatakata na kuyatupa. Naambulia hapo vimajimaji kiasi, na nyama ya chungwa iliyobakia ni ngumu, mbichi na isiyo na maji. Yanatoka wapi? Kwa nini yanakuwa hivyo? Au nayo yanapepewa kama ndizi?

Yani tunapigwa kila kona. Tikiti, ndizi, sasa machungwa, mbogamboga. Kwa nini haya machungwa wasiyaache hadi msimu wake?

IMG_20240322_214322.jpg
 
Mimi niliacha kununua machungwa naona natupa tu pesa kununua machungwa nayokwenda yatupa.
Hakuna matunda siku hizi si embe,tikiti,nanasi
 
Ukweli ni kwamba tangu nizaliwe hadi sasa naelekea utu uzima wenyewe sijawahi ona haya machungwa. Nachojua machungwa aidha yawe matamu au machachu, ila hayakosi maji. Sasa haya sijui ya wapi. Na ni mwaka jana na huu tu ndio nimeanza kuyaona.

Chungwa kwanza kubwa, halafu gumu, kuonyesha kabisa lina walakini. Nanunua machungwa matano na yote nakatakata na kuyatupa. Naambulia hapo vimajimaji kiasi, na nyama ya chungwa iliyobakia ni ngumu, mbichi na isiyo na maji. Yanatoka wapi? Kwa nini yanakuwa hivyo? Au nayo yanapepewa kama ndizi?

Yani tunapigwa kila kona. Tikiti, ndizi, sasa machungwa, mbogamboga. Kwa nini haya machungwa wasiyaache hadi msimu wake?

View attachment 2942131
HAYO MACHUNGWA YANALIMWA BUZA HAYO
 
Kipindi ni mtoto Kuna shamba la mzee mmoja lilikua Lina mchungwa umezaa machungwa makubwa Yana rangi nzuri yanavutia lakini yapo tu watu hawayavuni mpaka yanadondoka chini mengi kweli
Nikawa najiuliza kwanini watu hawana habari nayo,siku Moja nimetoka shule Nina njaa na kiu nikasoma ramani nikaruka fensi kwa lengo la kuiba angalau matatu niishi,kweli bana nikaotea kama sita hivi
Nimeenda nimekaa chini ya mti Ninafurahia machungwa yangu
Kumenya Sasa!!

Chungwa sita zote ni sponchi kama vitenesi,niliulaani ule mti haikupita mwezi ukakaTwa
 
Kipindi ni mtoto Kuna shamba la mzee mmoja lilikua Lina mchungwa umezaa machungwa makubwa Yana rangi nzuri yanavutia lakini yapo tu watu hawayavuni mpaka yanadondoka chini mengi kweli
Nikawa najiuliza kwanini watu hawana habari nayo,siku Moja nimetoka shule Nina njaa na kiu nikasoma ramani nikaruka fensi kwa lengo la kuiba angalau matatu niishi,kweli bana nikaotea kama sita hivi
Nimeenda nimekaa chini ya mti Ninafurahia machungwa yangu
Kumenya Sasa!!

Chungwa sita zote ni sponchi kama vitenesi,niliulaani ule mti haikupita mwezi ukakaTwa
😅 Uliumia sana bila shaka
 
Sema wabongo kwenye kuzingatia ubora tulishashindwa, dar zinakuja kila aina ya takataka, mfano parachichi ilibidi niache tu kununua!
Duh nilijua ni m ndio huwa nashangaa parachichi za dar lazima liwe limeharibika sehemu..
Nilishaacha kabisa kununua pia.
 
Back
Top Bottom