MwanaFalsafa1
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 5,565
- 836
Mh ana dalili za kupewa tuzo za Mo Ibrahim? Kwa mujibu wa nani?
Who cares.
Kuna kila dalili kuwa, iwapo Rais JK ataendeleza Utawala Bora, Uwazi, Uwajibikaji na Haki kwa kila mtu, anaweza kutunukiwa tuzo mashuhuri ya MO IBRAHIM.
Hii itakuwa ni heshma kubwa kwa Tanzania.
Hata hivyo inasikitisha kuona kuwa CDM wanaendeleza vitendo visivyo vya kizalendo ambavyo vinaweza kusababisha tuzo hiyo ikaota mbawa.
Yafaa uongozi wa CDM utafakari suala hili kwa makini. Waelewe kuwa wanaweza kutoka mchango muhimu kuhakikisha kuwa Tanzania inapata tuzo hii ya heshma kwa mara ya kwanza. Akiipata JK, tutakuwa tumeipata wa-Tz wote.
Wakati mwingine ni muhimu kuweka ushabiki wa kichama pendeni na kulinda maslahi ya kitaifa.
Hiyo tuzo inaendana na madola lukuki ambayo kwa namna fulani yatakugusa - wewe na mimi.
Wewe Kishongo, zawadi ya MO si kwa viongozi walioshindwa kazi kama Kikwete. Ni kwa viongozi ambao wamefanya vyema kama akina Festus Mogaye rais wa zamani wa Botswana.
Wenye kujua vigezo vya utendaji bora ndio wanaompa hiyo tuzo.
Kama maoni yako ni kwamba 'ameshindwa kazi', wenzako wanaojua kupima viongozi kimataifa wana mtizamo tofauti.
Hana wa kushindana naye Africa kwa sasa, uwezekano mkubwa tuzo litakuja Tz 2016 kupitia JK.
hahaaa hakuna siku nimecheka duniani kama leo..Yaaani JK apewe tuzo ya MO IBRAHIM???? yaani akipewa JK basi na mugabe atapewa kwa kweli....Huyu huyu JK nayemjua kweli apewe tuzo ??mhh inawezekana lakini
Michango yako inaonesha hujui tuzo ya Mo Ibrahim ni kitu gani.
Hutahukumiwa kwa kukaa kimya... badala ya kujaza pumba kwenye jamvi.
Kama wewe ndiyo umetumwa kumpigia kampeni kwa lugha yako unamharibia.Peleka najisi uliyoshibishwa kwingine, si hapa.
Acha uwongo. Tuzo ya Mo Ibrahim haikuwepo enzi za Nyerere. Hata hivyo Nyerere alitunukiwa The Mahatma Gandhi Peace Prize among many others. Upo hapo? Hizo dalili anazotaja Kishongo ziko kwenye figment ya imaginations zake. Kwanza Salim Ahmed Salim kama mshirika kwenye bodi ya Mo Ibrahim hatakubali jina la Mkwere lipitishwe. Hajasahau ubaya aliomtendea 2005."Mtakatifu" mbona hajapewa hiyo?