Maryam Malya
Senior Member
- Nov 29, 2021
- 115
- 258
Na Mwl Udadis, Tarime
Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania ameingia katika rekodi ya viongozi wachache Duniani kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru. Naungana na wanazuoni kote Duniani kutoa pongezi za dhati kwake kwa kupewa heshima hii, tunaelewa kabisa kwamba heshima hii ni matokeo ya juhudi kubwa unayoifanya kuleta mageuzi ya kiuchumi nchini Tanzania.
Tangu alipoingia madarakani, Rais Samia Suluhu Hassan ameonesha kuwa kiongozi bora katika sehemu zote za utawala. Mafanikio yake katika uchumi, kijamii, utamaduni, na siasa si tu yamegeuza Tanzania, lakini pia yameleta athari chanya katika eneo la Afrika ya mashariki. Mfano katika uwekezaji kati ya mwaka 2021 hadi 2023 kituo cha uwekezaji kilisajili miradi 778 yenye thamani ya USD Bilioni 10.532 yenye uwezo wa kuzalisha ajira zipatazo 125,382.
Maendeleo ya Kiuchumi: Chini ya uongozi wa Rais Samia, uchumi wa Tanzania umeshuhudia ukuaji mkubwa na utulivu. Sera zake na juhudi zake zimevutia uwekezaji wa kigeni na kuunda mazingira yanayofaa kwa maendeleo ya kiuchumi. Amefanya kazi kwa bidii katika kukuza uchumi kwa kuzingatia sekta kama kilimo, uzalishaji, na teknolojia, hivyo kuongeza fursa za ajira na kuinua maisha ya Watanzania.
Maendeleo ya Kijamii: Rais Samia amedhihirisha dhamira yake ya dhati ya kuboresha maisha ya wananchi wake. Utawala wake umewekeza katika maeneo muhimu kama afya, elimu, na miundombinu. Katika Elimu tumeona vyumba vya madarasa zaidi ya Elfu 15,000 vikijengwa ndani ya mwaka mmoja, shule za kutosha, vibali vya ajira, mikopo kwa elimu ya juu na hata kwa wanafunzi wa diploma na bado amefuta tozo ya VRF kwa wanufaika wa mikopo.
Diplomasia ya Uchumi: Katika jukwaa la kimataifa, Rais Samia amekuwa ishara ya diplomasia na ushirikiano. Mbinu yake katika mahusiano ya kimataifa imeongeza hadhi ya Tanzania katika jumuiya ya kimataifa. Ameimarisha ushirikiano na nchi mbalimbali duniani na kuwa kinara katika masuala yanayolenga kujenga ustawi wa jamii endelevu maeneo kama vile usalama wa chakula ambapo Tanzania imekuwa mwenyeji wa mkutano wa AGRF 2023.
Tunapoisherehekea siku hii kubwa, pia tutambue kuwa heshima hii ni kumbukumbu ya uwezekano wa mabadiliko chanya ambayo viongozi wenye dhamira njema wanaweza kuleta kwa nchi zao na ulimwengu kwa ujumla. Mchango wa Rais Samia Suluhu Hassan utaendelea kuwa kioo kwa vizazi vijavyo. Sina mashaka kwamba utapewa Tuzo ya Amani ya Nobel siku zijazo.