Hawa watu sasa wamekubali kuwa Corona imeisha?

Nimekwambia Daktari alimsifia JPM kwa kuwa na msimamo thabiti wa kutokuyumba na kufuata mkumbo.

Akasema jambo la kwanza kutokuweka lockdown, pili, kutoa watu hofu kwamba huu ugonjwa huenda tukawa nao mda mrefu au ukaja mwingine hatari kuliko huu lazima tujifunze namna na kuishi nao.

Tahadhari zilichukuliwa, shule zikafungwa, maeneo ya mikusanyiko, uvaaji wa barakoa, vitakasa mikono.

Kingine alichofanya ni kutilia shaka vipimo na kuagiza uchunguzi wa maabara ufanyike. Kitu ambacho alionekana kituko licha ya nchi zingine nazo kukiri kuna shida kwenye vipimo vya Corona.

Tukafungua shule na vyuo huku shughuli za uchumi zikiendelea, kumbuka hayo yote yamefanyika tukiwa tunashutumiwa kuficha taarifa na kusitisha kupima maambukizi mapya.

Rudia tena kuelewa, alichosifia ni kusimamia maamuzi yako akaenda mbali kwa kwamba yeye hata kama mtu anasimamia jambo lisilosahihi anaheshim msimamo. Yeye ni mtu wa Eritrea.

Shida yake na JPM ilikua kwenye kutokutoa taarifa za maambukizi mapya.

Mkuu Monk,

Kwanza nikupongeze kwa kujadili bila kuonyesha mihemko. Naheshimu sana hali hiyo hata kama sikubaliani na unayoyaandika hapa.


Umechambua kwa utaratibu, nami nitakujibu kwa utaratibu huo huo:

1. "Daktari alimsifia JPM kwa kuwa na msimamo thabiti wa kutokuyumba na kufuata mkumbo."
Hili sikubaliani naye na wewe. Ugonjwa huu ni mpya, haukujulikana athari zake zingekuwa zipi. Tahadhari iliyotakiwa kuchukuliwa ni kufuata taratibu zilizopo zinazotumika kwenye magonjwa ya milipuko, huku taratibu zikiendelea kuuelewa ugonjwa ulivyo.
Kiongozi atakuwa na "msimamo thabiti" toka wapi na yeye kujiamria tu kufanya vyake ambavyo hata zile taratibu za kawaida za magonjwa mengine yeye anaona upuuzi?

Swala si "kufuata mkumbo" ni swala la kufuata Taratibu zinazoeleweka katika kupambana na magonjwa ya aina hii. Ugonjwa ulipoanzia, China, walishaonyesha njia na kudhibiti kuenea kwa ugonjwa haraka katika jamii.

Hapa hata wewe unataka kujisahaulisha tu kwamba wakti huo waChina walikuwa wakiletwa hapa kwa ndege kama watalii. Huo ndio msimamo thabiti?

2. "...kutokuweka 'lockdown', kutoa watu hofu-------; lazima tujifunze namna ya kuishi nao."
Elimu ya aina ya ugonjwa huu aliitoa wapi wakati anafanya maamuzi hayo? China walichukua hatua, wakaudhibiti ugonjwa usisambae. Yeye aliona mfano huo kuwa haufai kwa vigezo vipi.

Hadi hii leo, hakuna anayejua kwa nini ugonjwa unaumiza na kusababisha vifo vingi maeneo mengine zaidi ya mengine. Daktari, wewe, au JPM mnaweza kueleza sababu zinazofanya iwe hivyo?

Dunia hii ya leo, ambapo taarifa zinasambaa kwa haraka, mtu atatoaje watu hofu huku ugonjwa ukisambaa duniani kote? Unatoa hofu watu huku ugonjwa huujui kabisa, huna dawa..., unatoa hofu watu kwa kukazania waende makanisani na misikitini na kujifukizia? Kuna sayansi gani hapa inayotoa ushahidi wa uhakika kuwatoa watu hofu.

"Ujifunze kuishi nao" huku huelewi ugonjwa upo vipi na wala hufanyi lolote la mhimu kuudhibiti usienee zaidi kwenye jamii? Unauachia uenee, na madhara yake ya baadae huyajui. Unakubali tu 'ujifunze kuishi nao."

3. Kituko ni hiki "Shule zikafungwa" - Misikiti na makanisa yakafunguliwa?

4. Swala la vipimo ni aibu hata kuliweka hapa. Mtu aliyekwenda shule tena akasoma hadi Ph.D. na tena mwanasayansi. Kama hili nalo wewe mku 'Monk' unaona ni jambo la kujivunia lililofanywa na kiongozi wa nchi, basi sawa.
Hata kama vipimo vingekuwa na mashaka, ile njia iliyotumika ilionyesha ujinga wa hali ya juu sana kuwahi kutokea popote.

5. Huyo Daktari wako alisifia pia tulipositisha kufanya vipimo na kuficha taarifa za ugonjwa? Maana hata hili kwake litakuwa ni "kusimamia maamuzi na msimamo thabiti"? Huyo Daktari wako, umesema toka wapi, Eritrea, mwambie udaktari wake unaweza kuwa wa magumashi, na waajiri wake wakimtambua kuwa ni mtu wa aina hiyo, hata hiyo kazi ataipoteza.

6. Hapo mwisho, Daktari wako atakuwa anajichanganya (contradict) - kwa nini aone shida ya kutotoa takwimu kwa mtu ambaye anamsifia kuwa na msimamo, hafuati mkumbo wa wengine?

Mwisho: ninakuomba, ukiwasiliana tena na huyo Daktari wako, muulize kama COVID-19 imekwisha kabisa Tanzania kutokana na hatua zilizochukuliwa na JPM. Mpe mrejesho kwamba hapa corona haipo tena na hakuna watu waliopoteza maisha yao kutokana na gonjwa hilo.

Mwambie, tulicheza patapotea, tukabahatisha sana, sasa ni wakati wetu kujisifu kwa bahati yetu nzuri hiyo.. Sasa tunaweza kuuambia ulimwengu wote waje hapa kujifunza jinsi ya kushughulikia magonjwa ya aina hiyo pindi yakitokea tena huko mbeleni.
 
Wengi wa waliokufa walikuwa na comorbidities. Yaani hawakufa kwa sababu ya gonjwa moja tu. Walikuwa na magonjwa au gonjwa jingine. Wengine walikuwa na terminal illnesses.
Hujui unachoandika hapa.
Isingekuwepo corona, wagonjwa hao wengi wangekuwa bado ni hai.
 
Sio marekani tu kwenye vifo vingi.Ni nchi ni nyingi tu zina maelfu ya vifo.Tatizo lipo na usipopima utakuwa na vifo vichache.I dont see problem with USA government to provide incentives to hospitals with highest number of cases.Testing is one of the best preventive strategy.
South Afrika vifo 5000.Brazili vifo 70000.Italy vifo 35000.
Na kutopima au kutotaka kujua hakuuondoi ugonjwa.
 
Daktari mmoja wa WHO alisema haafiki kutokutoa taarifa za maambukizi ila anamsifu JPM kwa kuwa na msimamo. Akasema lockdown kwa nchi zetu haiwezi leta tija.

Akamalizia yeye anapenda sana mtu anayesimamia maamuzi yake na kutokuyumbishwa, akaenda mbali zaidi kwamba hata kama anachosimamia hakipo sahihi ila kwake ni ule msimamo wa mtu ana uheshim sana kuliko mtu anaebadilikabadilika.
What if ni msimamo wa kipumbavu na kijinga? Utaendelea kujipiga kifua kwamba una msimamo?
 
Sina uhakika sana, ila ngoja niulize.

Je, nchini Tanzania watu wanakufa kama nzi waliopuliziwa dawa ya kuua wadudu?

Maana kwa hivi sasa sioni tahadhari zozote zile zilizopendekezwa zikichukuliwa na watu nchini Tanzania....
Probably yes,Ila kwa kuwa serikali imeamua kuficha no one knows.Hata huko US tunapoambiwa wanakufa wa tu hadi 2000 a day haimanishi kila mtu na kila nyumba Kuna msiba
 
Mkuu Monk,

Kwanza nikupongeze kwa kujadili bila kuonyesha mihemko. Naheshimu sana hali hiyo hata kama sikubaliani na unayoyaandika hapa.


Umechambua kwa utaratibu, nami nitakujibu kwa utaratibu huo huo:

1. "Daktari alimsifia JPM kwa kuwa na msimamo thabiti wa kutokuyumba na kufuata mkumbo."
Hili sikubaliani naye na wewe. Ugonjwa huu ni mpya, haukujulikana athari zake zingekuwa zipi. Tahadhari iliyotakiwa kuchukuliwa ni kufuata taratibu zilizopo zinazotumika kwenye magonjwa ya milipuko, huku taratibu zikiendelea kuuelewa ugonjwa ulivyo.
Kiongozi atakuwa na "msimamo thabiti" toka wapi na yeye kujiamria tu kufanya vyake ambavyo hata zile taratibu za kawaida za magonjwa mengine yeye anaona upuuzi?

Swala si "kufuata mkumbo" ni swala la kufuata Taratibu zinazoeleweka katika kupambana na magonjwa ya aina hii. Ugonjwa ulipoanzia, China, walishaonyesha njia na kudhibiti kuenea kwa ugonjwa haraka katika jamii.

Hapa hata wewe unataka kujisahaulisha tu kwamba wakti huo waChina walikuwa wakiletwa hapa kwa ndege kama watalii. Huo ndio msimamo thabiti?

2. "...kutokuweka 'lockdown', kutoa watu hofu-------; lazima tujifunze namna ya kuishi nao."
Elimu ya aina ya ugonjwa huu aliitoa wapi wakati anafanya maamuzi hayo? China walichukua hatua, wakaudhibiti ugonjwa usisambae. Yeye aliona mfano huo kuwa haufai kwa vigezo vipi.

Hadi hii leo, hakuna anayejua kwa nini ugonjwa unaumiza na kusababisha vifo vingi maeneo mengine zaidi ya mengine. Daktari, wewe, au JPM mnaweza kueleza sababu zinazofanya iwe hivyo?

Dunia hii ya leo, ambapo taarifa zinasambaa kwa haraka, mtu atatoaje watu hofu huku ugonjwa ukisambaa duniani kote? Unatoa hofu watu huku ugonjwa huujui kabisa, huna dawa..., unatoa hofu watu kwa kukazania waende makanisani na misikitini na kujifukizia? Kuna sayansi gani hapa inayotoa ushahidi wa uhakika kuwatoa watu hofu.

"Ujifunze kuishi nao" huku huelewi ugonjwa upo vipi na wala hufanyi lolote la mhimu kuudhibiti usienee zaidi kwenye jamii? Unauachia uenee, na madhara yake ya baadae huyajui. Unakubali tu 'ujifunze kuishi nao."

3. Kituko ni hiki "Shule zikafungwa" - Misikiti na makanisa yakafunguliwa?

4. Swala la vipimo ni aibu hata kuliweka hapa. Mtu aliyekwenda shule tena akasoma hadi Ph.D. na tena mwanasayansi. Kama hili nalo wewe mku 'Monk' unaona ni jambo la kujivunia lililofanywa na kiongozi wa nchi, basi sawa.
Hata kama vipimo vingekuwa na mashaka, ile njia iliyotumika ilionyesha ujinga wa hali ya juu sana kuwahi kutokea popote.

5. Huyo Daktari wako alisifia pia tulipositisha kufanya vipimo na kuficha taarifa za ugonjwa? Maana hata hili kwake litakuwa ni "kusimamia maamuzi na msimamo thabiti"? Huyo Daktari wako, umesema toka wapi, Eritrea, mwambie udaktari wake unaweza kuwa wa magumashi, na waajiri wake wakimtambua kuwa ni mtu wa aina hiyo, hata hiyo kazi ataipoteza.

6. Hapo mwisho, Daktari wako atakuwa anajichanganya (contradict) - kwa nini aone shida ya kutotoa takwimu kwa mtu ambaye anamsifia kuwa na msimamo, hafuati mkumbo wa wengine?

Mwisho: ninakuomba, ukiwasiliana tena na huyo Daktari wako, muulize kama COVID-19 imekwisha kabisa Tanzania kutokana na hatua zilizochukuliwa na JPM. Mpe mrejesho kwamba hapa corona haipo tena na hakuna watu waliopoteza maisha yao kutokana na gonjwa hilo.

Mwambie, tulicheza patapotea, tukabahatisha sana, sasa ni wakati wetu kujisifu kwa bahati yetu nzuri hiyo.. Sasa tunaweza kuuambia ulimwengu wote waje hapa kujifunza jinsi ya kushughulikia magonjwa ya aina hiyo pindi yakitokea tena huko mbeleni.


Ahsante kwa pongezi japo sina uhakika endapo nna stahili.

Turudi kwenye mjadala mkuu, achana na hayo mazungumzo yetu na Daktari wa WHO, wewe binafsi nijibu haya maswali.

1. Ni kwa namna gani Tanzania imeathirika zaidi kwa Corona kwa maamuzi au namna ilivyokabiliana na Corona kulinganisha na nchi zingine zilizopambana na huo ugonjwa.

2. Ni nchi ipi kipekee imefanikiwa na ni yakutolewa mfano wa ilivyopambana na Corona.

3. Huu ugonjwa athari na maafa yake ni kama tulivyoambiwa awali?

4. Tanzania bado tuna vifo vya Corona kama inavyodaiwa na vyombo vya mataifa na mashirika mengine?

4. Ni kipi Magufuli hakupaswa kufanya au alitakiwa akifanye ili aonekane amepambana ipasavyo na Corona?

Mwisho, jaribu kunisoma tokea mwanzo kuna baadhi ya mambo, mengi tu natofautiana na mwamba, lakini kwenye hili zengwe la Corona namuunga mkono, na hii sasa sio Daktari wa WHO, hii ni mimi The Monk , yeye aliukubali msimamo na maamuzi thabiti.
 
What if ni msimamo wa kipumbavu na kijinga? Utaendelea kujipiga kifua kwamba una msimamo?

Jaribu kufuatilia kwa utulivu mjadala. Huyo sliyemsifia JPM yeye anachomsifia ni msimamo wake kwenye chochote, alilitambua hilo akaongezea hata kama unachokisimamia hakipo sahihi, huo ndio ulikua mtazamo wake.
 
1. Ni kwa namna gani Tanzania imeathirika zaidi kwa Corona kwa maamuzi au namna ilivyokabiliana na Corona kulinganisha na nchi zingine zilizopambana na huo ugonjwa.

Jibu si "namna Tanzania ilivyoathirika" kutokana na maamuzi, tatizo ni kufanya maamuzi bila ya kuwa na uelewa wa jambo unalolifanyia maamuzi.
Hii bahati nasibu yetu tuliyojaliwa hapa isiwe ndio ubingwa wetu wa kujisifia.

Mara zote, kiongozi mwenye busara, hawezi kuhatarisha maisha ya watu wake kwa kuweka mbele maslahi mengine, kama ya kiuchumi bila ya kuwa na ufahamu wa yatakayotokea mbeleni.

Sasa tunajisifu, hata hatujui bahati yetu (na kumbuka sio sisi tu, hata Burundi na kwingineko) na wao walicheza patapotea hivi hivi kama sisi.

Hadi sasa hatujui ni nini kilisababisha Corona yetu iwe tofauti na ile inayosumbua na kusababisha vifo vingi zaidi huko kwingine.

2. Ni nchi ipi kipekee imefanikiwa na ni yakutolewa mfano wa ilivyopambana na Corona.

Zipo nyingi.
Na hapa jirani yetu kabisa ni Rwanda. Sikubaliani, na sipendi kabisa mambo mengi ya huyo jamaa hapo Rwanda, lakini katika kupambana na COVID-19, Rwanda ni "Textbook" kwa wengine. Hakukata kona, amefanya tu yaliyotakiwa kwa taratibu zinazokubalika.

Kama Rwanda wataendelea na utaratibu kama huu na kuutumia katika nyanja nyingine, kwa hakika nchi hiyo itabadilika haraka sana kimaendeleo.

Hakuna njia za mkato, na huwezi kuvumbua tu taratibu zako kwa kuoteshwa au kuamka unavyojisikia na kuzitumia kuondoa tatizo. Fuata taratibu, na panapohitaji marekebisho kulingana na hali yako fanya. Lakini huwezi kukiuka taratibu zote na kujifanyia tu kivyako.

Hili ni tatizo kubwa sana na JPM kama hujagundua. Hataki kufuata taratibu, ndio maana mnasifia huko mnakokuita "kutofuata mkumbo."

3. Huu ugonjwa athari na maafa yake ni kama tulivyoambiwa awali?

Awali mliambiwa ni athari zipi?

Nyinyi awali mlijua athari hizo hazitakuwepo na ndio maana mkachukua maamuzi mliyofanya?

4. Tanzania bado tuna vifo vya Corona kama inavyodaiwa na vyombo vya mataifa na mashirika mengine?

Je Tanzania hakuna vifo vya corona, hata kama havitokei kwa wingi kama huko kwingine?

Kutotaka kujua kuwa kuna vifo vinatkea ndio tuchukulie hakuna vifo? Na kama hakuna vifyo, mnajua kwa nini vifo havipo kama huko kwingine, au hili unaona halina maana yoyote?

4. Ni kipi Magufuli hakupaswa kufanya au alitakiwa akifanye ili aonekane amepambana ipasavyo na Corona?

Hakupaswa kuchezea kamali na maisha ya raia zake kwa maslahi ya kiuchumi kwa ugonjwa ambao hakujua matokeo yake yakoje.

Alipaswa, kwa uchache, asimame katika taratibu zote zinazotakiwa, na zinazofahamika na zimetumika katika magonjwa mengine ya milipuko.

Kuweka dharau ya kitu usichokuwa nacho ufahamu wowote sio jambo la kusifia hata kidogo.

Na kama hutaki kujua jinsi tulivyovamia mambo kwa pupa bila tahadhari yoyote. Ile dawa ya Madagascar ilikuwa ni kielelezo tosha cha ujinga tuliokuwa nao juu ya ugonjwa huu.
Mara nyingine tena ya kukuonyesha maamuzi ya ajabu sana kutoka kwa JPM.
 
Jibu si "namna Tanzania ilivyoathirika" kutokana na maamuzi, tatizo ni kufanya maamuzi bila ya kuwa na uelewa wa jambo unalolifanyia maamuzi.
Hii bahati nasibu yetu tuliyojaliwa hapa isiwe ndio ubingwa wetu wa kujisifia.

Mara zote, kiongozi mwenye busara, hawezi kuhatarisha maisha ya watu wake kwa kuweka mbele maslahi mengine, kama ya kiuchumi bila ya kuwa na ufahamu wa yatakayotokea mbeleni.

Sasa tunajisifu, hata hatujui bahati yetu (na kumbuka sio sisi tu, hata Burundi na kwingineko) na wao walicheza patapotea hivi hivi kama sisi.

Hadi sasa hatujui ni nini kilisababisha Corona yetu iwe tofauti na ile inayosumbua na kusababisha vifo vingi zaidi huko kwingine.



Zipo nyingi.
Na hapa jirani yetu kabisa ni Rwanda. Sikubaliani, na sipendi kabisa mambo mengi ya huyo jamaa hapo Rwanda, lakini katika kupambana na COVID-19, Rwanda ni "Textbook" kwa wengine. Hakukata kona, amefanya tu yaliyotakiwa kwa taratibu zinazokubalika.

Kama Rwanda wataendelea na utaratibu kama huu na kuutumia katika nyanja nyingine, kwa hakika nchi hiyo itabadilika haraka sana kimaendeleo.

Hakuna njia za mkato, na huwezi kuvumbua tu taratibu zako kwa kuoteshwa au kuamka unavyojisikia na kuzitumia kuondoa tatizo. Fuata taratibu, na panapohitaji marekebisho kulingana na hali yako fanya. Lakini huwezi kukiuka taratibu zote na kujifanyia tu kivyako.

Hili ni tatizo kubwa sana na JPM kama hujagundua. Hataki kufuata taratibu, ndio maana mnasifia huko mnakokuita "kutofuata mkumbo."



Awali mliambiwa ni athari zipi?

Nyinyi awali mlijua athari hizo hazitakuwepo na ndio maana mkachukua maamuzi mliyofanya?



Je Tanzania hakuna vifo vya corona, hata kama havitokei kwa wingi kama huko kwingine?

Kutotaka kujua kuwa kuna vifo vinatkea ndio tuchukulie hakuna vifo? Na kama hakuna vifyo, mnajua kwa nini vifo havipo kama huko kwingine, au hili unaona halina maana yoyote?



Hakupaswa kuchezea kamali na maisha ya raia zake kwa maslahi ya kiuchumi kwa ugonjwa ambao hakujua matokeo yake yakoje.

Alipaswa, kwa uchache, asimame katika taratibu zote zinazotakiwa, na zinazofahamika na zimetumika katika magonjwa mengine ya milipuko.

Kuweka dharau ya kitu usichokuwa nacho ufahamu wowote sio jambo la kusifia hata kidogo.

Na kama hutaki kujua jinsi tulivyovamia mambo kwa pupa bila tahadhari yoyote. Ile dawa ya Madagascar ilikuwa ni kielelezo tosha cha ujinga tuliokuwa nao juu ya ugonjwa huu.
Mara nyingine tena ya kukuonyesha maamuzi ya ajabu sana kutoka kwa JPM.
Huyu jamaa ni hasara kwa nchi yetu.Na kwa ujinga wa kutokufuata taratibu na kujifanya ujuaji mwingi,mwaka huu akitekeleza budget yake hata kwa 20%atakuwa mwanaume,watu tu wajiandae kubeba maumivu yanayosababishwa na misimamo ya kijinga
 
Sio marekani tu kwenye vifo vingi.Ni nchi ni nyingi tu zina maelfu ya vifo.Tatizo lipo na usipopima utakuwa na vifo vichache.I dont see any problem with USA government to provide incentives to hospitals with highest number of cases.Testing is one of the best preventive strategy.
South Afrika vifo 5000.Brazili vifo 70000.Italy vifo 35000.
Vifo mbona vipo kila siku tu. Uongo?

Hebu tuwekee na idadi ya vifo kwenye hizo nchi ambavyo havikusababishwa na COVID-19.

Au tokea COVID ije hivyo vifo vingine vimejisitisha?

Hebu tuwekee basi hiyo idadi ili tuweze kulinganisha.

Na kuhusu serikali kutoa hela zaidi kwa spitali zinazoripoti hizo cases za Corona, ndiyo, kuna tatizo.

Tatizo lenyewe ni udanganyifu. Udanganyifu wa kuzidisha idadi ili zipate hela nyingi zaidi.

Na wanapodanganya kwa kuzidisha hizo idadi, wanakuwa wanapotosha hali halisi ilivyo na matokeo yake ni kuongeza taharuki kwenye jamii kwa kuifanya jamii iamini taarifa zisizo na usahihi.
 
Jibu si "namna Tanzania ilivyoathirika" kutokana na maamuzi, tatizo ni kufanya maamuzi bila ya kuwa na uelewa wa jambo unalolifanyia maamuzi.
Hii bahati nasibu yetu tuliyojaliwa hapa isiwe ndio ubingwa wetu wa kujisifia.

Mara zote, kiongozi mwenye busara, hawezi kuhatarisha maisha ya watu wake kwa kuweka mbele maslahi mengine, kama ya kiuchumi bila ya kuwa na ufahamu wa yatakayotokea mbeleni.

Sasa tunajisifu, hata hatujui bahati yetu (na kumbuka sio sisi tu, hata Burundi na kwingineko) na wao walicheza patapotea hivi hivi kama sisi.

Hadi sasa hatujui ni nini kilisababisha Corona yetu iwe tofauti na ile inayosumbua na kusababisha vifo vingi zaidi huko kwingine.



Zipo nyingi.
Na hapa jirani yetu kabisa ni Rwanda. Sikubaliani, na sipendi kabisa mambo mengi ya huyo jamaa hapo Rwanda, lakini katika kupambana na COVID-19, Rwanda ni "Textbook" kwa wengine. Hakukata kona, amefanya tu yaliyotakiwa kwa taratibu zinazokubalika.

Kama Rwanda wataendelea na utaratibu kama huu na kuutumia katika nyanja nyingine, kwa hakika nchi hiyo itabadilika haraka sana kimaendeleo.

Hakuna njia za mkato, na huwezi kuvumbua tu taratibu zako kwa kuoteshwa au kuamka unavyojisikia na kuzitumia kuondoa tatizo. Fuata taratibu, na panapohitaji marekebisho kulingana na hali yako fanya. Lakini huwezi kukiuka taratibu zote na kujifanyia tu kivyako.

Hili ni tatizo kubwa sana na JPM kama hujagundua. Hataki kufuata taratibu, ndio maana mnasifia huko mnakokuita "kutofuata mkumbo."



Awali mliambiwa ni athari zipi?

Nyinyi awali mlijua athari hizo hazitakuwepo na ndio maana mkachukua maamuzi mliyofanya?



Je Tanzania hakuna vifo vya corona, hata kama havitokei kwa wingi kama huko kwingine?

Kutotaka kujua kuwa kuna vifo vinatkea ndio tuchukulie hakuna vifo? Na kama hakuna vifyo, mnajua kwa nini vifo havipo kama huko kwingine, au hili unaona halina maana yoyote?



Hakupaswa kuchezea kamali na maisha ya raia zake kwa maslahi ya kiuchumi kwa ugonjwa ambao hakujua matokeo yake yakoje.

Alipaswa, kwa uchache, asimame katika taratibu zote zinazotakiwa, na zinazofahamika na zimetumika katika magonjwa mengine ya milipuko.

Kuweka dharau ya kitu usichokuwa nacho ufahamu wowote sio jambo la kusifia hata kidogo.

Na kama hutaki kujua jinsi tulivyovamia mambo kwa pupa bila tahadhari yoyote. Ile dawa ya Madagascar ilikuwa ni kielelezo tosha cha ujinga tuliokuwa nao juu ya ugonjwa huu.
Mara nyingine tena ya kukuonyesha maamuzi ya ajabu sana kutoka kwa JPM.

Turahisishe mambo kwamba Tanzania tuna bahati.

Mkuu naomba kila mmoja abaki kusimamia anachokiamini kipo sahihi.

Tufanye bahati imekua upande wetu.
Kwenye hili la Corona acha kuongelea utaalam. Nchi zenye wataalam na kuzingatia yote zimebaki na maswali hadi sasa.

WHO umeona walivyokua wanabadilikabadilika kutoa miongozo?

Tofauti ya madhara ya Corona kati ya nchi zilizochukua hatua na ambazo hazikuchukua hatua haiwezi kufafanuliwa au kutolewa maelezo kitaalam.
 
Vifo mbona vipo kila siku tu. Uongo?

Hebu tuwekee na idadi ya vifo kwenye hizo nchi ambavyo havikusababishwa na COVID-19.

Au tokea COVID ije hivyo vifo vingine vimejisitisha?

Hebu tuwekee basi hiyo idadi ili tuweze kulinganisha.

Na kuhusu serikali kutoa hela zaidi kwa spitali zinazoripoti hizo cases za Corona, ndiyo, kuna tatizo.

Tatizo lenyewe ni udanganyifu. Udanganyifu wa kuzidisha idadi ili zipate hela nyingi zaidi.

Na wanapodanganya kwa kuzidisha hizo idadi, wanakuwa wanapotosha hali halisi ilivyo na matokeo yake ni kuongeza taharuki kwenye jamii kwa kuifanya jamii iamini taarifa zisizo na usahihi.
Not true.

Kumhudumia mgonjwa wa COVID-19 ni gharama.Wadonjwa wengine huwa wanahitaji ventilator kwa wastani wa siku mbili mpaka tatu lakini wagonjwa wa covid-19 hiitaji ventilotrs kwa wiki mbiii au zaidi.
Pia watoa huduma wa afya wapo katika hatari sana.Si vibaya wakapata posho.
Serikali ya USA kutoa ruzuku kwa hospitali zenye COVID nyingi ni sahihi.

Na nimesema hapo juu kuwa si Marekani tu yenye vifo vingi.Nchi nyingi zenye testing system nzuri zimeonyesha vifo ni vingi.
 
Huyu jamaa ni hasara kwa nchi yetu.Na kwa ujinga wa kutokufuata taratibu na kujifanya ujuaji mwingi,mwaka huu akitekeleza budget yake hata kwa 20%atakuwa mwanaume,watu tu wajiandae kubeba maumivu yanayosababishwa na misimamo ya kijinga
Hvi bado umejifungia ndani?
 
Huyu jamaa ni hasara kwa nchi yetu.Na kwa ujinga wa kutokufuata taratibu na kujifanya ujuaji mwingi,mwaka huu akitekeleza budget yake hata kwa 20%atakuwa mwanaume,watu tu wajiandae kubeba maumivu yanayosababishwa na misimamo ya kijinga
Mchague Membe iki awe faida kwa nchi yetu
 
Mchague Membe iki awe faida kwa nchi yetu
Nipo ndani mkuu,nimetuma proposal ya kufungua ofisi tarehe 6 August wenye shirika wanasema tuendelee kutelework.nipo ndani na mgeni yeyote anaenitembelea home anaishia getini
 
Back
Top Bottom